Huyu mdudu ana maana gani?

Huyu mdudu ana maana gani?

ngoja wachina waje waongee nae uenda ana ujumbe kwa familia yako kama msiba au njaa na kutumbuliwa usimuue maana wametoweka sana siku hizi wacha wazaliane uenda wakavutia watalii toka China
 
Mantis in English Kwa Kiswahili simjui huyu ni mdudu kama wadudu wengine ana Wanakuwaga na rang ya kijan Na wengne Rang ya gold hawana Baraka Yoyote sema kama unaweza shadow karate ukifanya na yeye anakugezea
 
Nimeamk asubuhi nikakuta huyu mdudu yupo kwenye mawe jirani na mlango.... Nikiwa katika harakati za kutaka kumuua akatokea mwenyeji wa huku nilipo akadai huyo mdudu ni wa baraka nisimuue, hakuishia hapo akaongezea kuwa huyo mdudu ana akili kuliko binadamu na wachina wanaongeaga nao kwa ishara.

Kuna yeyote anajua kuhusiani na huyo mdudu atueleze.
View attachment 654917
Mfuge uje uwauzie wachina.
 
Acheni imani potofu kuna maelfu ya aina za wadudu kwaiyo sio kila mdudu unamjua au ushawai kumuona uyo ni mdudu Kama wadudu wengine tu
Wabongo bhana wepesi wa kuhusisha vitu na ushirikina

Sasa akimuona, Walking stick ataenda kwa mganga

b95f853f775e3d9bdc103a4bef44e899.jpg
 
sasa mkuu ulitaka kupoteza uhai wake kwa kosa gani, kua kiumbe hai ni ukatili
 
Nimeamk asubuhi nikakuta huyu mdudu yupo kwenye mawe jirani na mlango.... Nikiwa katika harakati za kutaka kumuua akatokea mwenyeji wa huku nilipo akadai huyo mdudu ni wa baraka nisimuue, hakuishia hapo akaongezea kuwa huyo mdudu ana akili kuliko binadamu na wachina wanaongeaga nao kwa ishara.

Kuna yeyote anajua kuhusiani na huyo mdudu atueleze.
View attachment 654917
ungekuwa una soma yoga na elimu ya kisayansi asili ya kibinadamu.ungepata kujua.mshana jr hatakuja
 
Ni watulivu sana, hawana papara!!! tulikuwa tunawaita Gonga Chungu.
Hakuna mtoto alipenda kuwaua kwa sababu tuliamini ukimuua glass au chungu chenu kitavunjika....
 
Ekishondwa kwa lugha ya wahaya wenyewe tunasema ishara mbaya hata kama ukimkuta ndan ya nyumba mtoe haraka huwa anaashiria mabaya
 
kiingereza= mantis
kiswahili= Vunja jungu
kisukuma= Chamba Ndenho
 
aah wapi hao wadudu nimewaua kama mia hivi kipindi bado nakua na hamna cha baraka wala nini, ni wadudu tu kama wadudu wengine ila tangu nimekua nimejua kua sio busara kuua kitu kisicho na madhara kwa binadamu ivo nawaachaga tu.
 
Ni ishara ya Uongozi mzuri (bora) uliopo Madarakani, maana katika Utawala huu ndio tumeshuhudia Tetemeko (Kagera) kukamatwa (kupatwa) kwa Jua na sasa Mdudu huyo wa Ajabu...!

Waite watu wa Mali Asili wakamuhifadhi kama moja ya kivutio nchini..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom