EL ELYON
JF-Expert Member
- Jan 2, 2013
- 1,563
- 1,886
Nina rafiki yangu mmoja tumeshakuwa kama ndugu maana tulikutana a level mpaka chuo kikuu tuko wote na kitaa tupo wote. Sasa alioa mke wake sasa ni miaka 3 wako kwenye ndoa halali kabisa. Mkewe ni mnyaturu, shida inayojitokeza yule mkewe pia anafanya kazi.
Tatizo ni kwamba yule mwanamke anaishi na mumewe kama vile bado hana familia yaani bado yuko tu kwao kwa baba na mama. Kwani hata kile kidogo anachopata karibia chote anatuma kwao na si kwamba kwao kuna maisha magumu kivile hapana.
Sasa inampa shida sana mumewe kwani anasema kwasasa wana familia ukizingatia wana mtoto tayari ilipaswa mkewe washirikiane kuendelea kuijenga familia yao kwa asilimia kubwa sana. Kingine kule kwao na mwanamke ni kama vile wao bado wanataka kuendelea kummiliki mtoto wao kama vile hana familia wala hajaolewa.
Sasa wakuu nini maana ya kuoana na kuanzsha familia kama mmoja anakuwa kama bado kimwili yuko na wewe lakini kiuhalisia hajatoka kwao maana hata wazazi wetu baba na mama hawa nao kila mmoja alitoka kwao ukoo tofauti familia tofauti wakaanzsha familia ndio wakatuzaa sisi
Ushauri wenu tafadhari.....
NB: wanyaturu inasemekana ni watamu sana
Tatizo ni kwamba yule mwanamke anaishi na mumewe kama vile bado hana familia yaani bado yuko tu kwao kwa baba na mama. Kwani hata kile kidogo anachopata karibia chote anatuma kwao na si kwamba kwao kuna maisha magumu kivile hapana.
Sasa inampa shida sana mumewe kwani anasema kwasasa wana familia ukizingatia wana mtoto tayari ilipaswa mkewe washirikiane kuendelea kuijenga familia yao kwa asilimia kubwa sana. Kingine kule kwao na mwanamke ni kama vile wao bado wanataka kuendelea kummiliki mtoto wao kama vile hana familia wala hajaolewa.
Sasa wakuu nini maana ya kuoana na kuanzsha familia kama mmoja anakuwa kama bado kimwili yuko na wewe lakini kiuhalisia hajatoka kwao maana hata wazazi wetu baba na mama hawa nao kila mmoja alitoka kwao ukoo tofauti familia tofauti wakaanzsha familia ndio wakatuzaa sisi
Ushauri wenu tafadhari.....
NB: wanyaturu inasemekana ni watamu sana