Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

basi nahisi hapo njian watapita kune mbuga ya wanyama af bibi atafanya yake...mara paaap miluzi...mapolisi wote watakufa
 
SEHEMUU YA 73

Msafara uliingia jijini Dar es salaam masaa sita baadaye na kwenda moja moja hadi makao makuu ambako mbiu ilipigwa wanajeshi wote wakakusanyika na bibi Nyanjige kukabidhiwa kwa mkuu wa majeshi .

Nawapongezeni sana kwa kumkamata bibi huyu lakini napenda kuwaeleza kuwa suala hili hivi sasa halikuwa mikononi mwetu tena inabidi tulipeleke mikononi mwa sheria , pigeni simu polisi waje wamchukue ni lazima ashtakiwe kwa mauaji mshenzi mkubwa huyu” Alifoka mkuu wa majeshi .

Simu ilipigwa na dakika ishirini baadaye polisi walifika na kumchukua bibi Nyanjige moja kwa moja hadi kituo cha polisi ambako alitoa maelezo kisha kutupwa mahabusu !” muda wote alichekelea wala hakuonyesha kuwa na wasiwsi wowote . jambo hilo liliwashangaza watu wengi sana ukilinganisha na kosa la mauaji ya halaiki alilokuwa akishtakiwa nalo .

Siku mbili baadae alichukuliwa na kupelekwa gerezani keko ambako aliendelea kusota wakati polisi wakiendelea kukamilisha upelelezi wao , kila mwezi alipelekwa mahakamani mara moja ambako alisomewa shitaka la mauaji na kurudishwa tena mahabusu ! kila siku ya kesi yake idadi kubwa ya watu walijaa mahakamani lengo lao ikiwa ni kumuona bibi Nyanjigebibi aliyeushangaza ulimwengu kesi yake iliwavutia watu wengi sana jijini Dar es salaam.

Polisi walijitahidi kukusanya kila aina ya ushahidi ili kumtia hatiani bibi Nyanjige lakini walishindwa kuupata ushahidi kwa sababu ilikuwa si rahisi kuthibitisha mbele ya mahakama kuwa ni yeye aliyewaamuru wanyama na wadudu kuwashambulia wanajeshi na kuwaua . kesi pekee iliyoonekena kuwa na nguvu ni ya mauaji ya watu karibu mia na hamsini waliokunywa maji kisima ambamo bibi Nyanjige angeweza kushinda katika kesi zote ingawa ni kweli alifanya mauaji kwa kuwaamrisha wanyama .
 
SEHEMU YA 74

Ni kutokuwepo kwa ushahidi wa kutosha ndiko kulifanya bibi Nyanjige asote mahabusu kwa karibu miezi therasini na sita ! Mwezi therasini na saba ulipoingia ghafla alianza kuugua ugonjwa wa ngozi , kikohozi na homa kali ! Walijaribu kumtibu katika hospitali iliyokuwepo gerezani bila mafanikio yoyote hali yake ilizidi kuwa mbaya hata mahakamani wakawa hawampeleki .

Miezi miwili baada ya kuugua hali yake ilikuwa mbaya zaidi homa ilizidi kupanda madaktari walifikiri homa ya matumbo lakini hata walipompa dawa za ugonjwa huo bado hazikumsaidia ! Alizidi kuzidiwa ndipo walipoamua kumpeleka hospitali ya Tifa ya Muhimbili ambako alipikelewa na kulazwa .

Alipofanyiwa vipimo aligundulika kuwa na kimeta alioupata sababu ya kuishi na wanyama porini kwa muda mrefu , alipewa dawa za ugonjwa huo ambazo alizitumia kwa muda wa mwezi mzima lakini bado hali yake haikutengemaa , homa ilizidi kuendelea kuwepo ! Madaktari walizidi kuchanganyikiwa na kushindwa juelewa ni nini kingefenyika kumsaidia .

Kikohozi kilizidi kupamba moto , alikohoa usaha nyakati za usiku pia alitoka jasho jingi mwilini . Alipoteza sehemu kubwa ya uzito wa mwili wake hilo lilifanya madaktari wafikirie kifua kikuu na kuamua kumpima makohozi ! .

Majibu yalipotoka yalionyesha kweli alikuwa na ugonjwa wa kifua kikuu na kulazimu aanzishwe matibabu ! lakini hata baada ya matibabu ! ya kifua kikuu kumalizika bado hali yake ilikuwa mbaya mno! Hakuwa hata na uwezo wa kunyanyuka kitandani ambako halilala akiwa amepigwa pingu yake mikono .

‘Jamani tu mtibu vipi huyu bibi? ”
“Hata mim nashindwa kuelewa kila dawa tumeshampa lakini bado haisaidii !” “Sasa tufanye nini?
“Hivi ESR yake ilikuwa ngapi ?” “Mara ya mwisho ilikuwa sitini !”
"sitini?" "Ndiyo!"
 
SEHEMU YA 75

Hiyo iko juu sana na inaonyesha wazi kuna tatizo ! unaonaje tungempima Elisa test uone kama ana ukimwi maana dalili zote ni za ukimwi !” Nakuunga mkono daktari yalikuwa ni maongezi kati ya madaktari wawili waliomshughulikia bibi Nyanjige kwa karibu zaidi walifikia uamuzi huo na siku iliyofuata alicchukuliwa damu kwa ajiri ya kipimo cha ukimwi !

Hakuna aliyekuwa tayari kuamini majibu yalipotoka kuwa bibi Nyanjige alikuwa na virusi vya ukimwi vilivyokuwa vikitishia uhai wake .
Niliupata wapi jamani ugonjwa huu ? Bibi Nyanjige alijiuliza baada ya daktari aliyekuwa akimpa ushauri nasaha kumueleza wazi juu ya afya yake alishindwa kuelewa lakini alipotuliza akili vizuri aligundua ni wapi aliupata ugonjwa huo.

Ni siku ile ya ajali ya basi nakumbuka kuna damu ya majeruhi niliyekuwa nikimvuta magwanda ya jeshi na kumvalisha nguo zangu iligusa kwenye kidonda changu nafikiri ni siku hiyo nilipoambukizwa ! Aliwaza bibi Nyanjige .
Mwisho wa maisha yake aliuona u karibu kupita kiasi alijua wakati wowote ule angeweza kuaga dunia ! Kila alipofikiria roho za watu waliokufa kwa sababu yake aliogopa sababu yake alijua wazi hukumu kubwa ilikuwa ikimsubiri .

Eee Mungu nisamehe shetani alinidanganya nikaua watu wasio na hatia ! alilia bibi Nyanjige kwa uchungu.
Septemba 23 1998 ushahidi wote ulikamilika , ilidhibitika wazi mbele ya mahakama kuwa bibi Nyanjige alitia sumu kisimani na kuwaua wananchi 150 wa kijiji cha Usagara mkoani Mwanza !

Ingawa hapakuwa na ushahidi wa kutosha juu ya wanajeshi zaidi ya 7000 waliokufa nchini Congo na katika mbuga ya wanyama Mikumi baada ya kushambuliwa na wanyama jaji alimtia bibi Nyanjige hatiani .
 
SEHEMUU YA 76

Kitanda chake kilizungukwa na watu wapatao kumi , kati yao alikuwepo jaji maarufu jijini Dar es salaam kwa kutoa hukumu za vifo , alikuwa jaji mwanamke asiye na huruma hata kidogo naalikuwa miongoni mwa watu waliochukizwa sana na kitendo alichofanya bibi Nyanjige .

Huyu alikuwa jaji Angela Ngaiza ilikuwa ni siku ya hukumu ya bibi Nyanjige ingawa alionekana kuwa katiak hatua za mwisho kabisa za uhai wake , alikuwa amekonda mno na aliangalia macho yake huku na kule bila matumaini .

Nyanjiige !” jaji aliita “Na..am mhe .shi..miwa jaji ” aliitika bibi Nyanjige kwa taabu.
Mahakama inakutia hatiani kwa kosa la mauaji ya watu 150 waliokufa baada ya wewe kuweka sumu kwenye kisima cha maji huko Usagara ushahidi uliopatikana kutoka kwa wwatu mbalimbali akiwemo mtu aliyenunua sumu hiyo kutoka dukani kwake na majibu ya vipimo vya maji ya kisima uliofanywa na madaktari uonanyesha wazi ulifanya mauaji hayo na kwa sababu hiyo basi kabla ya kukuhukumu naomba ujitete !

Hakimu alisema akimwangalia kitandani .
Sina la kujitetea !” Kwa sababu hiyo ninakuhukumu kifo cha kunyongwa !” Jaji alisema bila ya huruma
Jaji naomba nikukumbushe kitu kimoja kuwa huwezi kuhukumu maiti !
Huwezi kuhukumu mtu aliyekufa tayari !

Mimi ni kama mait….! Bibi Nyanjige hajamalizia sentesi yake , shingo yake ikaanguka pembeni na hasema kitu tena ! Daktari alipompima aliguandua tayari alishaaga dunia .
Afadhali !” Jaji alisema kwa sauti ya chini

Mwisho.... Asanteni kwa kufatilia simulizi hii ya kusisimua

Tukutane hapa tena kwenye simulizi nyingine nzuri ya kusisimua Dunia haina usawa
 
Back
Top Bottom