SEHEMUU YA 76
Kitanda chake kilizungukwa na watu wapatao kumi , kati yao alikuwepo jaji maarufu jijini Dar es salaam kwa kutoa hukumu za vifo , alikuwa jaji mwanamke asiye na huruma hata kidogo naalikuwa miongoni mwa watu waliochukizwa sana na kitendo alichofanya bibi Nyanjige .
Huyu alikuwa jaji Angela Ngaiza ilikuwa ni siku ya hukumu ya bibi Nyanjige ingawa alionekana kuwa katiak hatua za mwisho kabisa za uhai wake , alikuwa amekonda mno na aliangalia macho yake huku na kule bila matumaini .
Nyanjiige !” jaji aliita “Na..am mhe .shi..miwa jaji ” aliitika bibi Nyanjige kwa taabu.
Mahakama inakutia hatiani kwa kosa la mauaji ya watu 150 waliokufa baada ya wewe kuweka sumu kwenye kisima cha maji huko Usagara ushahidi uliopatikana kutoka kwa wwatu mbalimbali akiwemo mtu aliyenunua sumu hiyo kutoka dukani kwake na majibu ya vipimo vya maji ya kisima uliofanywa na madaktari uonanyesha wazi ulifanya mauaji hayo na kwa sababu hiyo basi kabla ya kukuhukumu naomba ujitete !
Hakimu alisema akimwangalia kitandani .
Sina la kujitetea !” Kwa sababu hiyo ninakuhukumu kifo cha kunyongwa !” Jaji alisema bila ya huruma
Jaji naomba nikukumbushe kitu kimoja kuwa huwezi kuhukumu maiti !
Huwezi kuhukumu mtu aliyekufa tayari !
Mimi ni kama mait….! Bibi Nyanjige hajamalizia sentesi yake , shingo yake ikaanguka pembeni na hasema kitu tena ! Daktari alipompima aliguandua tayari alishaaga dunia .
Afadhali !” Jaji alisema kwa sauti ya chini
Mwisho.... Asanteni kwa kufatilia simulizi hii ya kusisimua
Tukutane hapa tena kwenye simulizi nyingine nzuri ya kusisimua
Dunia haina usawa