Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

SEHEMU YA 46...

Usiku huo kwa bibi Nyanjige hakutaka uwe usiku wa bure, alitaka kuutumia kwa kazi katika zungukazunguka yake bila kutiliwa mashaka alifanikiwa kufika mahali yalipofichwa mabomu na silaha nyingine za kijeshi, alianza kusomba mabomu taratibu na kuyatega sehemu mbalimbali za kambi bila kugundulika, aliyaseti yote yalipuke baada ya masaa mawili.

“Hii ndiyo kiboko yao lazima niwamalize hawa watu, nataka siku moja niingie katika kitabu cha orodha ya watu maarufu duniani na huu ni wakati wa mimi kuondoka niwaachie kasheshe yao” Alisema bibi Nyanjige huku akitabasamu.
Aliondoka kama anakwenda kukojoa na kutokomea porini akijua baada ya masaa mawili kambi lingegeuka tanuru la moto na mamia ya wanajeshi wangegeuka mkaa au matofali ya kuchoma.

Masaa mawili kama alivyopanga akiwa katikati ya pori aliona moto mkubwa ukiwaka nyuma yake! Akajua tayari kazi yake imekamilika. **************
Maaskari walizinduliwa na milipuko ya mabomu na kuanza kukimbia huku na kule wakijaribu kuokoa maisha yao! Haikuwa rahisi hata kidogo kwani wengi walilipuliwa na kuwaka kwa moto! Mahema yaliwaka kwa moto na wengi wa wapiganaji walikufa ndani ya mahema yao!

Mpaka hali inatulia masaa matatu baadaye tayari wanajeshi 150 walikuwa chini wakiwa maiti! Kamanda alinusurika na alizidi kusikitika na kushindwa kuelewa ni kitu gani kilikuwa kikiendelea alianza kuhisi kulikuwa na vibaraka wa bibi Nyanjige kati yao, hakufikiri hata kidogo kuwa bibi Nyanjige ndiye aliyeifanya kazi hiyo kama kikulacho ki nguoni mwako. ***********

Kulipokucha asubuhi bibi Nyanjige alikuwa katika kijiji cha Kiambali mkoani Tanga, kijiji hiki kilikaliwa na watu wa jamii ya Kimasai peke yao! Kwa magwanda aliyokuwa nayo alijua ni lazima angewatia wasiwasi na wangetaka kumwona sura yake jambo ambalo kwa hakika lingesumbua.

Hakutaka kujitokeza mchana alichofanya ni kujificha kichakani mchaka kutwa, usiku ulipoingia aliyavua magwanda yake na kuanza kutembea taratibu kuingia kijijini.
 
SEHEMU YA 47...

Mtu wa kwanza kukutana naye alikuwa mlevi akitoka kilabuni, mtu huyo alishtuka sana kuona mwanamke yu uchi.
“We iko nani?”
“Mimi?” “Ndiyo!”
“Bibi Nyanj….!” Alitaka kutaja jina lake lakini alipokumbuka kuwa alikuwa akitafutwa na tayari jina lake lilikuwa maarufu midomoni mwa Watanzania alisita kulimalizia.

“Uuuuuuuuuuwiiiiiiii, saidia, jamani saidia! Mchawi! Mchawi huyu hapa!” Alipiga kelele mzee huyo, alikuwa ndiye mwenye nyumba zilizokuwa jirani na eneo hilo aliendelea kupiga kelele kwa muda mrefu hatimaye watu wengi walijitokeza wakiwa na silaha zao mikononi, wengine mapanga, mikuki na mawe..

Wananchi wa kijiji hicho walichukia wachawi hivyo walianza kumshambulia bibi Nyanjige kwa mawe na marungu na wengine walimrushia hata mikuki yao, alianguka chini huku akilia.

“Jamani mie siyo mchawi!” Alisema lakini hakuna aliyemsikiliza watu walizidi kumshambulia kila mtu akiamini bibi Nyanjige alikuwa mwanga!

Je, nini kitaendelea?
 
hivi huyo bibi hali? hanywi hata maji?
Unataka mpaka anapofika kwenye vimito na madimbwi na kunywa Maji na kula matunda pori tuwe tunaambiwa? Mi aliniacha hoi pale alipoingia store ya mabomu kirahisi na kuiba mabomu na kuyatega na yakawamaliza karibia wote....vitani hakuna sehemu inalindwa kama sehemu ya kutunzia silaha....sasa sijui alipenyaje?
 
Unataka mpaka anapofika kwenye vimito na madimbwi na kunywa Maji na kula matunda pori tuwe tunaambiwa? Mi aliniacha hoi pale alipoingia store ya mabomu kirahisi na kuiba mabomu na kuyatega na yakawamaliza karibia wote....vitani hakuna sehemu inalindwa kama sehemu ya kutunzia silaha....sasa sijui alipenyaje?
hahaha jamani wangetuambia hata sehemu moja basi alipokula mana naona mwanzo mwisho ni mikiki mikiki tu....
 
Back
Top Bottom