SEHEMU YA 47...
Mtu wa kwanza kukutana naye alikuwa mlevi akitoka kilabuni, mtu huyo alishtuka sana kuona mwanamke yu uchi.
“We iko nani?”
“Mimi?” “Ndiyo!”
“Bibi Nyanj….!” Alitaka kutaja jina lake lakini alipokumbuka kuwa alikuwa akitafutwa na tayari jina lake lilikuwa maarufu midomoni mwa Watanzania alisita kulimalizia.
“Uuuuuuuuuuwiiiiiiii, saidia, jamani saidia! Mchawi! Mchawi huyu hapa!” Alipiga kelele mzee huyo, alikuwa ndiye mwenye nyumba zilizokuwa jirani na eneo hilo aliendelea kupiga kelele kwa muda mrefu hatimaye watu wengi walijitokeza wakiwa na silaha zao mikononi, wengine mapanga, mikuki na mawe..
Wananchi wa kijiji hicho walichukia wachawi hivyo walianza kumshambulia bibi Nyanjige kwa mawe na marungu na wengine walimrushia hata mikuki yao, alianguka chini huku akilia.
“Jamani mie siyo mchawi!” Alisema lakini hakuna aliyemsikiliza watu walizidi kumshambulia kila mtu akiamini bibi Nyanjige alikuwa mwanga!
Je, nini kitaendelea?