Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,081
- 464,063
- Thread starter
- #281
SEHEMU YA 65
Alikumbuka kwamba ni kweli walitakiwa kumfikisha mtu yule mbele ya Wakuu wa Majeshi akiwa hai na sio vinginevyo. Japokuwa bibi yule anatisha kutokana na historia za mauaji makubwa na mazito ambayo ameyafanya, lakini kumfikisha kwa wakuu akiwa amekufa, ni matusi kwa mwanajeshi mwenye cheo kama yeye. Kumpeleka mtuhumiwa tena mwanamke kizee akiwa amekufa mbele ya wakuu? Atajielezaje? Kwamba ametusumbua sana? Msumbufu mwenyewe mwanamke!!? Tena kizee? Haikumuingia akilini.
Mwili wa bibi Nyanjige ulikuwa kama umekufa ganzi. Maumivu yalikuwa makubwa na akajikuta akianza kukata tamaa kutoka mikononi mwa watu wale. Hakujua wakati kama ule anahitaji kutumia mbinu ya namna gani kumuokoa. Suala la kufa, halikuwa na mjadala, alitambua kwamba ni lazima ndani ya siku chache zijazo atakuwa amekufa, lakini mateso atakayoyapata yatakuwa mabaya zaidi ya kifo!
Msaidizi wa Mkuu wa Majeshi akarudi kutoka nyuma ya gari alikokuwa ameegemea akiwa tayari na suluhisho. “Hebu muingize kwenye gari”. Dereva akamtazama katika hali ya kutoelewa, lakini Mkuu alishaingia kwenye gari na kufunga mlango wake. Dereva akatekeleza hilo, alimbeba na kumwingiza kwenye kiti cha nyuma, akazunguka na kuingia kwenye kiti cha mbele, akawasha gari.
“Wapi Mkuu?”
“Twende Hospitali.”
* * * * * * *
Umati wa watu ulikuwa umejazana nje ya Hospitali ya mkoa kutaka kumwona Bibi Nyanjige, mwanamke aliyevuma nchi nzima kutokana na vitendo vya mauaji ya kushangaza. Watu walitaka kuhakikisha kwamba ni kweli mwanamke anayelisumbua jeshi la nchi ni mtu mzima kwa kiasi kinachozungumzwa?
Wengi walihisi kwamba huenda mwanamke huyo akawa ni mtu wa makamo au kijana na sio mtu mzima sana kama inavyotangazwa kwa sababu kutokana na kiwango cha matatizo anayoyasababisha, inakuwa vigumu kuamini kwamba kikongwe kama hicho kinaweza kufanya yote hayo.
Polisi walikuwa na kazi ya ziada kujaribu kusuma sukuma wananchi waliokuwa wakilisogelea lango la hospitali ambako Bibi Nyanjige alikuwa ameingizwa.
Alikumbuka kwamba ni kweli walitakiwa kumfikisha mtu yule mbele ya Wakuu wa Majeshi akiwa hai na sio vinginevyo. Japokuwa bibi yule anatisha kutokana na historia za mauaji makubwa na mazito ambayo ameyafanya, lakini kumfikisha kwa wakuu akiwa amekufa, ni matusi kwa mwanajeshi mwenye cheo kama yeye. Kumpeleka mtuhumiwa tena mwanamke kizee akiwa amekufa mbele ya wakuu? Atajielezaje? Kwamba ametusumbua sana? Msumbufu mwenyewe mwanamke!!? Tena kizee? Haikumuingia akilini.
Mwili wa bibi Nyanjige ulikuwa kama umekufa ganzi. Maumivu yalikuwa makubwa na akajikuta akianza kukata tamaa kutoka mikononi mwa watu wale. Hakujua wakati kama ule anahitaji kutumia mbinu ya namna gani kumuokoa. Suala la kufa, halikuwa na mjadala, alitambua kwamba ni lazima ndani ya siku chache zijazo atakuwa amekufa, lakini mateso atakayoyapata yatakuwa mabaya zaidi ya kifo!
Msaidizi wa Mkuu wa Majeshi akarudi kutoka nyuma ya gari alikokuwa ameegemea akiwa tayari na suluhisho. “Hebu muingize kwenye gari”. Dereva akamtazama katika hali ya kutoelewa, lakini Mkuu alishaingia kwenye gari na kufunga mlango wake. Dereva akatekeleza hilo, alimbeba na kumwingiza kwenye kiti cha nyuma, akazunguka na kuingia kwenye kiti cha mbele, akawasha gari.
“Wapi Mkuu?”
“Twende Hospitali.”
* * * * * * *
Umati wa watu ulikuwa umejazana nje ya Hospitali ya mkoa kutaka kumwona Bibi Nyanjige, mwanamke aliyevuma nchi nzima kutokana na vitendo vya mauaji ya kushangaza. Watu walitaka kuhakikisha kwamba ni kweli mwanamke anayelisumbua jeshi la nchi ni mtu mzima kwa kiasi kinachozungumzwa?
Wengi walihisi kwamba huenda mwanamke huyo akawa ni mtu wa makamo au kijana na sio mtu mzima sana kama inavyotangazwa kwa sababu kutokana na kiwango cha matatizo anayoyasababisha, inakuwa vigumu kuamini kwamba kikongwe kama hicho kinaweza kufanya yote hayo.
Polisi walikuwa na kazi ya ziada kujaribu kusuma sukuma wananchi waliokuwa wakilisogelea lango la hospitali ambako Bibi Nyanjige alikuwa ameingizwa.
