Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 153,008
- 453,976
SEHEMU YA 01...
Ingawa ilikuwa mchana hali katika msitu wa Kungoni nchini Kongo ilikuwa ya kiza nene! Mawingu yalitanda angani. Ni asubuhi ya siku hiyo tu ilinyesha mvua kubwa tena ya mawe na kusababisha baridi kubwa! Wanyama wengi walijikunyata sababu ya kulowa.
Milio ya ndege na wanyama mbalimbali ilisikika kila pembe ya msitu huo uliokuwa kilometa kama 520 kutoka Jiji la Kinshansa, ulikuwa ni msitu wenye tembo wengi kuliko msitu mingine yote barani Afrika na uliwavutia watalii wengi lakini waliogopa kuutembelea sababu tembo wa msitu huo waliua watalii.
Kila mtu aliamini hakuna mtu aliyeishi katika msitu huo jambo ambalo halikuwa sahihi hata kidogo, kwani mtu mmoja tena bibi kizee mwenye umri wa miaka 80 aliishi katika msitu huo kwa miaka mingi.
Alikuwa ameishi katika msitu huo kwa muda wa miaka isiyopungua thelathini akifanya utafiti wa maisha ya tembo na wanyama wengine kama ndege, Nzige na Mbungo! Alipofika Kongo kwa mara ya kwanza alikuwa na umri wa miaka 30, aliingia nchini humo akitokea Tanzania.
Kinshansa chini ya Patrice Lumumba ilimpokea mwanamke huyo kama mtafiti wa wanyama bila kudadisi sana kilichomfanya aondoke Tanzania na kumpa kibali cha kwenda kuishi msituni Kungoni.
Ni bibi huyo pekee aliyeishi katika msitu huo akizungukwa na wanyama wengi wao wakiwa ni tembo! Aliishi na wanyama hao kwa miaka thelathini mpaka wanyama wote wakamwona ni kama mnyama mwenzao, aliijua lugha za tembo, nzige, mbung’o na ndege mbalimbali! na kuwasiliana nao kama binadamu.
Kulipokuwa na hatari aliitambua kwa kuwasikiliza tembo, nzige, mbung’o na ndege! Alipohitaji kitu chochote porini alitoa mlio fulani mdomoni mwake na Tembo wote walikuja na aliwaagiza kufanya kitu chochote alichotaka! Kifupi wanyama wote walimwona kama malkia wao!
Itaendelea.
Ingawa ilikuwa mchana hali katika msitu wa Kungoni nchini Kongo ilikuwa ya kiza nene! Mawingu yalitanda angani. Ni asubuhi ya siku hiyo tu ilinyesha mvua kubwa tena ya mawe na kusababisha baridi kubwa! Wanyama wengi walijikunyata sababu ya kulowa.
Milio ya ndege na wanyama mbalimbali ilisikika kila pembe ya msitu huo uliokuwa kilometa kama 520 kutoka Jiji la Kinshansa, ulikuwa ni msitu wenye tembo wengi kuliko msitu mingine yote barani Afrika na uliwavutia watalii wengi lakini waliogopa kuutembelea sababu tembo wa msitu huo waliua watalii.
Kila mtu aliamini hakuna mtu aliyeishi katika msitu huo jambo ambalo halikuwa sahihi hata kidogo, kwani mtu mmoja tena bibi kizee mwenye umri wa miaka 80 aliishi katika msitu huo kwa miaka mingi.
Alikuwa ameishi katika msitu huo kwa muda wa miaka isiyopungua thelathini akifanya utafiti wa maisha ya tembo na wanyama wengine kama ndege, Nzige na Mbungo! Alipofika Kongo kwa mara ya kwanza alikuwa na umri wa miaka 30, aliingia nchini humo akitokea Tanzania.
Kinshansa chini ya Patrice Lumumba ilimpokea mwanamke huyo kama mtafiti wa wanyama bila kudadisi sana kilichomfanya aondoke Tanzania na kumpa kibali cha kwenda kuishi msituni Kungoni.
Ni bibi huyo pekee aliyeishi katika msitu huo akizungukwa na wanyama wengi wao wakiwa ni tembo! Aliishi na wanyama hao kwa miaka thelathini mpaka wanyama wote wakamwona ni kama mnyama mwenzao, aliijua lugha za tembo, nzige, mbung’o na ndege mbalimbali! na kuwasiliana nao kama binadamu.
Kulipokuwa na hatari aliitambua kwa kuwasikiliza tembo, nzige, mbung’o na ndege! Alipohitaji kitu chochote porini alitoa mlio fulani mdomoni mwake na Tembo wote walikuja na aliwaagiza kufanya kitu chochote alichotaka! Kifupi wanyama wote walimwona kama malkia wao!
Itaendelea.