Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

SEHEMU YA 11...

Nyanjige akiwa amepandisha hasira kupita kiasi alirudi nyumbani kwao huku akilia, hakuwa na la kufanya kwani hakufahamu ndugu hata mmoja nchini Tanzania wazazi wake walitokea Kongo miaka mingi walipofika Mwanza walichukua majina ya Kisukuma na kujifunza kabila hiyo wakaonekana Wasukuma wakati walikuwa Wabembe kutoka Zaire.

Ndugu pekee aliyekuwa nae pale alikuwa ni dereva aliyemleta kutoka mjini huyo ndiye aliyemtegemea kumpa kila aina ya msaada!
“Siki...li...za ka...ka mimi nime..pa..twa na ma..tati..zo nafi..kiri ume..ona, hivi una...weza kunisaidia vipi?’
“Kwa tatizo gani?”
“Nataka kuzika mifupa ya mama yangu!”
“Hilo tu lisikumbue dada yangu nitakusaidia mimi ni binadamu kama wewe!”

“Nisaidie nitakulipa kiasi chochote cha pesa!”
Dereva alirudi nyuma na kufungua buti la gari na kutoa jembe na koleo ambavyo alitembea navyo wakati wa mvua kumsaidia kila anapozama katika tope! Baada ya kuvichukua alivua shati lake na kukunja suruali.

“Ni wapi tuchimbe kaburi dada?”
“Chimba tu hapa hapa mbele!” Alijibu Nyanjige akilia machozi kwa uchungu, moyo wake uliuma sana na hasira ilimkaba kooni aliamini asilimia mia kuwa mama yake hakuwa mchawi ila aliponzwa na macho mekundu sababu ya moshi wa miaka mingi nyumbani kwa gavana.
“Haiwezekani ni lazima nilipe kisasi kwa wananchi wa kijiji hiki hawawezi kumuua mama yangu mpendwa kinyama namna hii wanastahili adhabu tena adhabu ya kuchukua maisha yao!” Aliwaza Nyanjige huku akiendelea kulia machozi na dereva akiendelea kuchimba kaburi.

Masaa mawili baadaye shimo lilikuwa tayari na dereva alimpa Nyanjige taarifa hiyo na wote wawili wakaingia hadi ndani ambako Nyanjige alibeba mwili wa mama yake uliokuwa mifupa tupu katika mikono yake na kuanza kutembea hadi nje! Baadhi ya mifupa ilikatika na kudondoka chini akalazimika kurudi kuiokota ndipo shimo likafunikwa!
 
SEHEMU YA 12...

Yalikuwa mazishi ya watu wawili tu!Katika maisha yake yote Nyanjige hakuwahi kuumia moyo kama siku hiyo, walipomaliza mazishi hayo tayari ilikuwa saa sita ya usiku na dereva aliomba ruhusa ya kuondoka lakini Nyanjige alikataa na kuahidi angemlipa pesa za siku zote ambazo angekaa naye.

Kwa usiku mzima Nyanjige alilia akimlilia mama yake, moyo wake ulijaa kisasi alitaka kulipa kisasi kwa unyama aliofanyiwa mama yake! Asubuhi siku iliyofuata waliondoka hadi mjini Mwanza kwenye maduka ya madawa ya mifugo ambako Nyanjige alinunua sumu ya kuulia wadudu aina ya DDT bila dereva kugundua kilichonunuliwa na wote wawili walirejea tena hadi kijijini Usagara!

Jioni Nyanjige alizunguka kijijini bila kuongea na mtu yeyote akijaribu kutafuta ni wapi kilipokuwa kisima ambacho wanakijiji walitumia kwa maji ya kunywa, alipogundua mahali kilipokuwa alirudi nyumbani na usiku wa siku hiyo dereva akiwa usingizini alitoka na kutembea hadi kwenye kisima akaimiminina sumu yote kwenye maji.

Usiku huohuo alitoroka na dereva wake kuelekea Kigoma kupitia kibondo, Kasulu hadi Kigoma mjini ambako alimlipa dereva kiasi cha shilingi laki tano na kuagana nae! Ni siku hiyo hiyo aliyoingia Kigoma ndiyo siku aliyovuka na boti hadi mji wa Kalemi nchini Kongo ambako alipanda basi lililompeleka moja kwa moja hadi Kinshasa ambako alijitambulisha kama mtafiti wa wanyama na kuruhusiwa kuishi porini.

Alijua aliyoyaacha nyuma yake yalikuwa makubwa na kweli watu mia moja na hamsini walikunywa maji ya kisimani asubuhi ya siku aliyomwaga sumu walikufa! Uchunguzi ulipofanyika sumu aina ya DDT iligundulika katika maji na kila mwanakijiji alikua na uhakika sumu hiyo ilimwaga katika kisima na Nyanjige na kutoroka ni hapo ndipo msako kumsaka ulipoanza.
 
SEHEMU YA 13...

Askari aliyenusirika msituni Kungoni:
“Jamani huko hali ni mbaya kupita kiasi, jeshi lote mlilonipa limemalizika kuna mbung’o na Nzige wa hatari sijapata kuona, wanakula miili ya watu kama mchezo! Watu wote mlionipa wameliwa na kubaki mifupa tupu! Njooni muone mfano wake huku kwenye helkopta!” Alisema Meja Jenerali Lupilya na kuwachukua wakuu wa majeshi hadi kwenye helkopta aliyowasili nayo! Kila mtu alishika mdomo kwa mshangao jinsi wanajeshi wawili walivyoliwa nyama za mwili wao.

“Waliofanya hivi ni mbung’o na nzige?”
“Ndiyo na vijana wote niliokwenda nao wapo kama unavyoiona hii mifupa!”
“Du! Na wewe umeokoka vipi?” Mkuu wa majeshi aliuliza.
“Huyo bibi kanihurumia tu kwa sababu niliongea Kisukuma!”
“Anaongea Kisukuma?”
“Ndiyo tena vizuri tu! Ila jeshi lake si mchezo ni la wanyama na wadudu tupu na wote wanamtii anaishi peke yake msituni, mlishawahi kuona binadamu anazuia Nzige kula kitu?”

“Hapana!”
“Basi mie nimeona kwa macho yangu nzige walikuwa wanile lakini bibi huyo alipofanya “Psyiiiiii” nzige wote wakatulia!”
Siku hiyo hiyo kikao kilikaa na kuamriwa kuwa jeshi jingine lenye askari 10,000/= lipelekwe haraka msituni kwa mapigano mengine makali zaidi ili kuhakikisha bibi Nyanjige anakamatwa na kurejeshwa nchini Tanzania kwa mashtaka ya mauaji ya halaiki ya watu na Lupilya alitakiwa tena kuliongoza jeshi hilo.

Wakuu wa majeshi walishangaa kumwona Meja Jenerali Lupilya akivua magwanda yake pamoja na silaha akakabidhi kwa mkuu wa majeshi akawa ameacha jeshi! Kujiuzuru kwa Lupilya kuliwafanya wengi waamini jeshi la bibi Nyanjige hakuwa mchezo.

“Jamani mimi naona ni heri muombe msaada umoja wa Mataifa nina hakika nyie wote mnaokwenda hamtarudi hapa Tanzania!” Alishauri Lupilya lakini hakuna mtu aliyesikiliza, siku hiyo hiyo alifukuzwa kambini na mkuu wa majeshi aliamua kuongoza kikosi hicho kwenda Kongo kupitia Kigoma kushuhudia mwenyewe! Alisomea mambo ya jeshi nchini Cuba na Israel hivyo alikuwa na uhakika wa kupata ushindi dhidi ya jeshi la wadudu na wanyama wa bibi Nyanjige.
 
SEHEMU YA 14

...Msituni:
Tembo zaidi ya elfu tano walikusanyika kumzunguka bibi Nyanjige! Mbung’o pamoja na Nzige wasio na idadi walizunguka angani na kufanya eneo hilo liwe na kivuli ingawa ilikuwa ni hali ya jua kali! Ulikuwa ni kama mkutano wa hadhara wa wanyama na wadudu na bibi Nyanjige alikuwa akiwasiliana na wadudu na wanyama wote katika lugha zao akiwatahadharisha juu ya uvamizi mwingine na kuwaomba wakae tayari.

Wanyama na wadudu waliomchukulia bibi Nyanjige kama Malkia wao waliahidi kutoruhusu mtu yeyote amdhuru labda wote wawe wamemalizika! Lugha ya wadudu na wanyama aliojifunza ilimsaidia sana kuwasilina sana kuwasiliana na wanajeshi wake.Baada tu ya mkutano huo Tembo, Nzige na Mbung’o wote walisambaa na kuanza ulinzi msituni. ****************

Meli zipatazo ishirini kubwa zikiwa zimebeba askari pamoja na vifaa mbalimbali vya kivita zilikuwa safarini kuelekea Kongo! Ndege zaidi ya hamsini ziliruka moja baada ya nyingine kutoka uwanja wa ndege wa Kigoma kwenda Kongo, helkopta zilizojazwa madawa ya kuua wadudu zilikuwa hewani zikielekea msituni kwa lengo la kuwaua Nzige na mbung’o wote kabla ya kumkamata bibi Nyanjige!

Kulikuwa na kila dalili kuwa isingechukua masaa hata mawili kabla msitu huo haujafutwa katika uso wa dunia Tembo wote wakiwa wameteketezwa kwa makombora!

Askari wote walifurahia vita hiyo na walikuwa na uhakika wa kumkamata bibi Nyanjige na kumrudisha Tanzania akiwa maiti au hai! Vifo vya wenzao zaidi ya 5000 viliwatia hasira kali sana na walitaka kulipiza kisasi!

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 15

...Asubuhi ya siku hiyo msitu ulikuwa kimya kabisa, ni ndege tu waliopiga kelele wanyama wengine walikuwa kimya! Tembo wengi walikusanyika katikati ya msitu wakiwa wameiweka nyumba ya bibi Nyanjige katikati kuhakikisha usalama wake.

Ndege aina ya Tai ambao idadi yao ilikuwa si rahisi kuifahamu walionekana wakiruka angani, walikuwa tayari kwa hatari yoyote ambayo ingetokea na walikuwa na ufahamu kuwa wakati wowote msitu ungeweza kuvamiwa tena.

Kwa amri waliyopewa na bibi Nyanjige kama wangevamiwa Tembo na nzige wangeendelea na vita vya nchi kavu na ndege aina ya Tai, Kunguru na mwewe wangeendelea na vita vya angani wakipambana na na ndege zilizotegemewa kuuvamia msitu. Hali ya vita ilinukia kila mahali,kilichokuwa kikisubiriwa wakati huo ni kuwasili kwa maadui.

Masaa machache baadaye miungurumo wa ndege za kivita ilisikika angani upande wa mashariki, bibi Nyanjige aliponyanyua uso wake kuangalia angani aliziona ndege kumi zikipita na alipozisoma kwenye mabawa yake aliliona neno TAN na zilikuwa na nembo ya Twiga nyuma yake alijua ndege hizo zilikuwa ni za jeshi la Tanzania.

Bila kuchelewa alipiga mluzi kwa sauti ya juu ili kuashiria kuwa sasa mambo yalikuwa tayari na palepale makundi yote ya ndege waliokuwa wakizunguka angani walizizingira ndege zote tatu na kuziweka katikati kisha wakaanza kutoboa vioo vya ndege hizo kwa mbele na kuingia hadi ndani ambako walianza kuwashambulia marubani kabla hawajafanya jambo lolote.

Ndege walifanya hivyo kwa ndege ya kivita moja baada ya nyingine hatimaye ndege zote kumi zilianguka chini na kulipuka! Mamia ya ndege pia walilipuliwa na moto.
*
*

Bibi Nyanjige aliyekuwa bado yu katikati ya kundi kubwa la tembo alishuhudia mashambulizi ya ndege wake na kuhisi ushindi! Lakini ghafla alishtuka alipoona helkopta tano zikiruka kutoka upande mwingine wa msitu na vitu kama mipira ya maji ilichungulia kutoka ndani ya helkopta hizo, alijua tayari vita nyingine ilikuwa imefika.
 
Naona shigongo kakumwagia vitu vyake!..hongera shunie!
 
Back
Top Bottom