Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

Baada ya siku ngapi nawe utaanza tesa watu? -Ooooh umeme umekatika, wakuu laptop yangu haina charge. .. Niko Dodoma Area D wadau wa huku tuonane. .. Wakuu leo lazima niweke mzigo wote,... Wakuu leo nimechoka sana...na bla bla kibao..etc
 
Baada ya siku ngapi nawe utaanza tesa watu? -Ooooh umeme umekatika, wakuu laptop yangu haina charge. .. Niko Dodoma Area D wadau wa huku tuonane. .. Wakuu leo lazima niweke mzigo wote,... Wakuu leo nimechoka sana...na bla bla kibao..etc
Ila shunie anajitajidi kumaliza story hana arosto kali kama za hao wengine bruno the fisherman haieleweki makaburi yasokua na hatia tangu mwaka jana had leo shunie anajitahidi sana sana
 
Baada ya siku ngapi nawe utaanza tesa watu? -Ooooh umeme umekatika, wakuu laptop yangu haina charge. .. Niko Dodoma Area D wadau wa huku tuonane. .. Wakuu leo lazima niweke mzigo wote,... Wakuu leo nimechoka sana...na bla bla kibao..etc

Shunie hanaga hayo mambo utakua unamkosea.. Fuatilia stori anazoleta humu, wadau wake tunamfahamu..
 
Ila shunie anajitajidi kumaliza story hana arosto kali kama za hao wengine bruno the fisherman haieleweki makaburi yasokua na hatia tangu mwaka jana had leo shunie anajitahidi sana sana
Shunie hanaga hayo mambo utakua unamkosea.. Fuatilia stori anazoleta humu, wadau wake tunamfahamu..
Watu waliozoea arosto hao
 
SEHEMU YA 06...

“Sasa wewe nakuachia nenda kawaeleze ndugu zako kuwa hapa ni moto wa kuotea mbali! Mimi ndiye malkia wa msitu huu! Jeshi langu si mchezo nitawamaliza! Ondokaaaa upesi!” Aliongea kwa ukali bibi Nyanjige na Lupilya ulinyanyuka na kukimbia kuelekea porini akiwa uchi wa mnyama kila alikopita alikuta miili ya watu ikiwa imelala chini bila nyama! Na Nzige walikuwa kila mahali lakini hawakumgusa amri aliyoitoa bibi ilionekana kusambazwa kila mahali.

“Mh! Huyu bibi si mchezo ni heri upambane na dunia nzima lakini si yeye!” Alisema meja Lupilya Baada ya kutembea kwa nusu saa hivi aliikuta helkopta imeegeshwa watu wengi walikuwa pembeni yake wakiwa mifupa mitupu, aliwaruka na kuingia ndani ya helkopta, mifupa mingine ya watu wawili ilikuwemo ndani ya helkopta hiyo.

“Hii acha niondoke nayo ili wakaelewe vizuri nitakachokuwa nawaeleza, maana ninajua itakuwa si rahisi kuamini yaliyotokea! Huyu bibi si mchezo jamani!” Alisema meja jenerali Lupilya akiwasha ndege ili aondoke.
 
SEHEMU YA 07...

Kwa muda wa miezi kama mitatu ya mwisho kabla Nyanjige hajaondoka Uingereza alikoishi kwa miaka 30 kurudi nyumbani Tanzania, alipoteza kabisa mawasiliano na mama yake na alishindwa kuelewa ni kitu gani kilimpata mpaka akawa kimya kiasi hicho kwani kwa kawaida alipokea barua moja kila mwezi kutoka kwa mama yake lakini kwa miezi mitatu mfululizo yote hakupata taarifa yoyote juu ya hali ya mama yake.

Ni jambo hilo ndilo lilifanya Nyanjige aamue kuondoka Uingereza mapema kabla ya muda aliopanga, lilimtia wasiwasi mwingi sana moyoni mwake na kumpa kumbukumbu nyingi sana juu ya mama yake na alitaka kuwa naye wakati huo.

Katika miaka yote 30 ambayo Nyanjige aliishi nchini Uingereza akisoma na hatimaye kufanya kazi ni mara mbili tu aliwahi kuonana na mama yake na mara ya mwisho ilikuwa miaka kumi kabla ya kufikiria kurudi Tanzania.

“I have got to go home! Tanzania is my country!Tanzania is my home! My people are in Tanzania not here in the UK! I have to go and serve my own people rather than serving Britains(Ni lazima nirudi nyumbani, Tanzania ndiyo Taifa langu, Tanzania ndiyo nyumbani kwetu, Tanzania ndiyo asili yangu, watu wangu wako huko ni lazima niende kuwatumikia wao kuliko kuendelea kuwatumikia waingereza) Alisema Nyanjige akiwa mwenye mawazo mengi.

Alikuwa mwanamke mzuri sana lakini katika miaka yote aliyoishi Uingereza hakujaliwa kupata mtoto wala mchumba wa kumuoa! Si kwamba sura yake ilikuwa mbaya mno la hasha! Bali hakuwa na bahati ya kuolewa na hiyo ilitokana na shughuli nyingi alizokuwa nazo! Nyanjige alitamani sana kuwa na mtoto lakini haikuwa hivyo.

Kabla ya kuondoka nchini Uingereza alimnunulia mama yake zawadi nyingi za nguo za Kiingereza, alitaka mama yake apendeze na kuwa tishio mtaani kwao na ikiwezekana hata mkoa mzima wa Mwanza na vitongoji vyake wamfahamu!
 
SEHEMU YA 08...

Siku ya kuondoka London ndiyo ilikuwa siku ya furaha zaidi katika maisha yake, alipanda ndege ya shirika la ndege la Alliance Airlines iliyoondoka London kuja Dar es Salaam kupitia Paris, Uturuki, Misri, Ethiopia, Nairobi na hatimaye kuingia Dar es Salaam. Safari hiyo ilimchukua masaa zaidi ya ishirini na nne, wakati anaingia Dar es Salaam saa nne ya asubuhi alikuwa amechoka kupita kiasi lakini hakutaka kulala Dar es salaam kabisa na kuamua kuunganisha siku hiyo hiyo kuelekea Mwanza ambako aliwasili saa 10 jioni.

Alikuwa na hamu kubwa ya kuonana na mama yake hivyo alikodisha teksi kutoka uwanja wa ndege ambao upo kama kilometa nane kutoka Mwanza mjini hadi kijijini kwao Usagara kilometa kama sabini kutoka Mwanza mjini, ambako mama yake aliishi baada ya kustaafu kazi ya upishi nyumbani kwa gavana.

Iliwachukua zaidi ya masaa mawili kufika kijijini Usagara, sababu ya ubovu wa barabara uliokuwepo mjini Mwanza. Alishangazwa na hali aliyoikuta nyumbani kwa mama yake, nyumba ya mama ilikuwa imebomoka na kuanguka upande mmoja, nyasi ziliota hadi mlangoni mwa nyumba hiyo iliyojengwa kwa udongo! Mlango ulikuwa wazi na ilikuwa rahisi sana kufikiri watu walioishi katika nyumba hiyo walihama miezi michache kabla.

Hali hiyo iliufanya moyo wa Nyanjige upige kwa nguvu na kasi ya ajabu alihisi kuna tatizo lilitokea ambalo hakuwa na habari nalo! Hakutaka kuteremsha mizigo yake ndani ya gari na kuamua kuusukuma mlango na kuingia hadi ndani ya nyumba ya mama yake ambako alianza kuita jina la mama yake lakini hakuitikiwa hatimaye aliamua kusukuma mlango wa chumbani na kukuta umefungwa kwa komeo kutoka ndani, alijua kwa hakika ndani kulikuwa na mtu!
 
SEHEMU YA 09...

“Mama! Mama! Mama!”Aliendelea kuita lakini hali ndani ya nyumba ilikuwa kimya! Baada ya kuita sana hatimaye ilibidi amwite dereva ajaribu kumsaidia kuuvunja mlango wa chumbani ili waigie na kuangalia! Alipokuja dereva walifanikiwa kuuvunja mlango na kuingia hadi ndani! Ingawa giza lilikuwa halijaingia chumba hicho kilikuwa kiza tupu na ilikuwa si rahisi kuona kitu chochote kilichokuwemo ndani.

“Dereva una tochi?’
“Tochi dada sina ila nina kiberiti!”
“Basi nisaidie hicho hicho kiberiti nataka kuangalia humu ndani!”
“Kwani kuna nini dada?”
“Mama yangu aliishi hapa lakini dalili zilizopo zinanitisha sijui kahama?Sijui yupo wapi? Naomba hicho kiberiti nijaribu kuangalia vizuri humu chumbani!”

Dereva aliingiza mkono wake mfukoni na kutoa kiberiti na kumkabidhi Nyanjige, alipokiwasha tu kwa mwanga mdogo uliokuwepo aliweza kukiona kitanda cha mama yake na kukisogelea, juu kulitandikwa shuka jeupe lakini hapakuonekana kuwa na kitu chochote chini ya shuka hilo cha kufanya afikirie mama yake alikuwa kitandani amelala!

Alikibeza kitanda na kuendelea kukagua sehemu mbalimbali za chumba huku akiwasha njiti nyingine ya kiberiti kila moja ilipozimika.
Alizunguka chumba kizima bila kuona kitu, akahamia chumba kilichokuwa kimebomoka upande huko nako pia hakuona kitu chochote! Nyanjige alizidi kuchanganyikiwa, ghafla wakati akirudi kwenye chumba cha mama yake aliona kitu kama karatasi chini ya kitanda aliinama na kuiokota, akaikunjua vizuri na kuanza kuisoma.

“Ng’wanone Nyanjige, nene nalisatu no! Ubusatu wenubu ndibona bukunibulaga! Bale bizile banhu bunisola bahayaga angu ndi nogi nakabulagaga bana babo! Aho banisola Bunitwala Kwibanza Lya sungusungu, bunitula mpaga nudeda getegete, Nushoka kukaya nalagula giti kanegene! I hali yane ya bubi no natumanaga nulu ukunisanga nali mhola! Aliyu mhayo untale ukonisanga nachile ng’wanone nalibona atiho nu munho wakunijeka leka nikundikile shuka ulagasanga maguhwa gani habulili wenubu! Nacha ng’wanone wikate mhola.
 
SEHEMU YA 10...

Nini.
Noko!
Barua hiyo iliandikwa kwa kisukuma lakini ilimaanisha maneno yafuatayo:
“Mwanangu Nyanjige, mimi naumwa sana na ugonjwa huu naona utaniua! Walikuja hapa watu wakanichukua hadi kwenye kikao cha sungusungu wakidai eti mimi ni mchawi, wakanipiga mpaka nikaja hapa nyumbani natambaa kama mtoto! Hali yangu ni mbaya mno mwanangu sijui kama utanikuta hai ukirudi lakini kikubwa najua utanikuta nimekufa na ninaona hakuna mtu wa kunizika hivyo najifunika shuka utaikuta mifupa yangu chini ya shuka hili hapa hapa kitandani, nakufa mwanangu naomba ubaki salama!
Mimi,
Mamayo!

Nyanjige alimaliza barua hiyo mwili wake ukiwa umekufa ganzi alitembea taratibu kuelekea kitandani na alipofunua shuka ilikuwa ni mifupa ya mama yake ikiwa chini ya shuka! Alishindwa kuvumilia akanguka chini na kuzirai! Dereva kuona hivyo alimbeba na kumtoa hadi nje na kuchukua maji yaliyokuwemo kwenye galoni ndani ya gari lake na kummwagia usoni na mwilini! Haikuchukua muda mrefu akazinduka na kuanza kulia machozi. Pamoja na kilio hicho hakuna hata jirani mmoja aliyejitokeza kuja kumsaidia au kuuliza ni kitu gani kilitokea Nyanjige na dereva walishangaa.

Baada ya kitu kama masaa mawili hivi bila kuona jirani akitokeza Nyanjige aliamua kwenda nyumba ya jirani kuulizia lakini alipofika watu wote walikimbilia ndani na kufunga milango ya nyumba zao na wengine kuongea naye kupitia dirishani.

“Nyanjige nitwa kwambilija, aliyo ikaya ying’we ituligije konguno na bulogi (Nyanjige tungekusaidia lakini familia yenu imetengwa na kijiji sababu ya uchawi)
“Hata kama mmenitenga ndiyo mnaweza mkamwacha mtu akafa mpaka kuwa mifupa? Huu ni unyama ni lazima niwaonyeshe nimechukia kiasi gani!

Isitoshe mama yangu hakuwa mchawi au mlimwita mchawi kwa sababu ya macho kuwa mekundu?Mmesahau kuwa alikuwa mpishi wa gavana?”
“Kwa kweli sio sisi ni serikali ya kijiji iliyoamua hivyo, hata sisi tumesikitika mno!” Alisema mama mmoja kupitia dirishani.

Itaendelea.
 
Back
Top Bottom