Huu wimbo wa "katiba mpya" ni manufaa ya Wanasiasa na Wanaharakati zaidi kuliko Wananchi

May Day

JF-Expert Member
May 18, 2018
6,162
8,820
Siku za hivi karibuni kumezuka Wanasiasa na Wanaharakati wanaohanikiza kupatikana kwa katiba mpya, huku wakijaribu kuiaminisha jamii ya Watanzania kwamba kupatikana kwake ndio itakuwa mwisho wa Matatizo ya nchi hii.

Kwa muda wote ninajaribu kuwasikiliza mmoja baada ya Mwingine na bado sioni ni kiasi gani nashawishika kuona kwamba kuna ukweli unaojitosheleza, ningetamani kusikia hoja nzito zinazonithibitishia kuwa kama Nchi basi tumekuwa tunakwamishwa na mambo haya au yale, na kwamba tukipata katiba mpya basi kila kitu kitakuwa sawa. Zaidi naona kama mengi wanayojaribu kuyapigania ni ya kisiasa na madaraka zaidi kuliko matatizo halisi ya kila siku ya Wananchi.

Nijuacho mimi ni kuwa Mwanasiasa anaishi kwa siasa, hivyo kuanzisha jambo la kuwafanya waonekane wapo kazini kwao ni namna nzuri ya kuweka tiki kwenye kalenda zao kwamba tar hii walikuwa Makambako, tarehe ile Kahama, iliyofuata Namtumbo n.k na hivyo kujiongezea CV, na hata kipato maana tayari watakuwa na namna ya kuwaonesha Wahisani/Wafadhili kuwa wapo busy.

Watajitahidi kuwashawishi Wananchi ili wawaunge mkono bila kujali ya kuwa tofauti na wao Wananchi hawana wa kuwafidia muda wao maana wao kwa wakati huo wapo kazini ili hali Wananchi wataacha shughuli zao za siku kuhudhuria mikutano hiyo, yaani kama ni Muuza chipsi, Kinyozi, Fundi wa kuchomelea, Mama Lishe n.k watatakiwa kufunga ofisi zao wakawasikilize Watu ambao wao wapo kazini.

Natamani nimsikie aliyekuwa Mbunge kwenye jimbo ninakoishi la Arusha Mjini, kwa muda wote aliokuwa kiongozi wa Jimbo aseme ni nini kilimkwamisha kutekeleza aliyokuwa anaahidi kwa kukwazwa na katiba iliyopo.

Mbunge huyu ni juzi tu ametoka kupokea mamilioni ya pesa kama mafao, hivi ni kiasi gani ametenga kwa waliokuwa wapiga kura wake kwa vipindi vyote hapa jimboni kuwasadia hili na lile kwenye shughuli zao?, au pia amekwamishwa na katiba iliyopo?. kumuona tena ni mpaka 2025 aje kupambana kutafuta fursa nyingine ya kurudi Bungeni.

Hivi ni Vijana/kina Mama wangapi wamewahi kupata msaada 'support' wa kiujuzi au mtaji ili waanzishe Viwanda vyao Vidogo Vidogo?, walipieni Vijana mafunzo ya Sido pale Ungalimitedi? natamani nioneshwe Wapiga Kura walionufaika kupitia Kiongozi wao na kama hakuna naomba Kiongozi aniambie ni kwa namna gani katiba iliyopo imemkwamisha.

Hivi isingekuwa zaidi Kwa Kiongozi anayejinadi kuwatetea na kuwajali sana Wananchi wake kuja na madai yawayo yote yale huku tayari akiwa na mamia ya Watu nyuma yake wanaomiliki viwanda/miradi/mashamba kwa muongozo/usimamizi/ushauri wake? au hata hilo wanakwamishwa na katiba iliyopo?.

Ninachojua mimi ni kuwa Mbunge wetu alikuwa anajiangalia yeye na familia yake kwanza na sio Wapiga kura/Wananchi.... Sasa leo wakitaka kutuambia kuwa inatakiwa katiba mpya ndio ibadili roho za Wanasiasa ni usanii wa kisiasa tu.

Na hebu hata Wananchi wa maeneo mengine nao wafanye tathmini ya mabadiliko waliyoyapata tangu wawashawishike kuwachagua Wabunge wao...Walinganishe hali ya Mbunge kabla ya kupata Ubunge na baada ya kupata Ubunge, ni nani amenufaika...ni yeye ay wao?....aulizwe Msigwa, aulizwe Sugu, aulizwe Mnyika, aulizwe Bulaya n.k.

Huenda ni kweli kuna umuhimu wa katiba mpya lakini si kweli kwamba wanasaiasa wanafanya hivyo kwa manufaa ya Wananchi bali ni kwa faida yao kwanza.

Na kama inabidi kufanya hizo harakati zao basi zifanyike bila kuathiri muda wa Wananchi?. Yaani Wananchi waachwe wajitafutie riziki zao za siku hadi siku huku na Wanasiasa wakipambania hilo wanalofikiri lina manufaa kwa nchi?.

Mimi kama Mwananchi kama kipo ninachotamani kukiona basi ni namna ya kuwawajibisha Wabunge/Wawakilishi wetu, walau kila Mwaka tuwe na mkutano tuwahoji ni mangapi ametimiza kati ya aliyoayaahidi...na maksi zikiwa chache basi apoteze sifa ya kuendelea kuwa Mbunge....hivi jambo kama hili halitekelezeki kwa kurekebisha tu kifungu bila kuhitaji mchakato mreeefu wa katiba mpya?.
 
Iyo katiba mbovu ndio inayofanya unapata mbunge ambaye hawajibiki kwako mwananchi, ndio inayokuletea mbunge asiyejua majukumu yake kukutetea mpiga kura wake kwa kuhakikisha budget inayopitishwa inajibu changamoto za maisha yako, katiba mpya ndio saidia kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili pesa hiyo ipelekwe kwenye miradi ya maendeleo ie kupunguza nafasi za uteuzi/za kisiasa mfano hatuna sababu ya kuwa na wabunge mawaziri wakati kazi zao zinafanywa na makatibu wakuu, maRC, maDC ambao majukumu yao yanaingiliana na maDED. Pia itaongeza uwajibikaji na ushieikishwaji mfano mahakama kuwajibika kutoa haki kwa kufuata sheria sio kufuata matakwa ya aliyemteua
 
Wananchi ndio waathirika wa katiba mbovu.
Ni sawa ila basi Wananchi wasitumike kama chambo.

Maana tatizo la Wanasiasa wanapotaka la kwao Wananchi tunawekwa kati kati .
 
Siku za hivi karibuni kumezuka Wanasiasa na Wanaharakati wanaohanikiza kupatikana kwa katiba mpya, huku wakijaribu kuiaminisha jamii ya Watanzania kwamba kupatikana kwake ndio itakuwa mwisho wa Matatizo ya nchi hii.

Kwa muda wote ninajaribu kuwasikiliza mmoja baada ya Mwingine na bado sioni ni kiasi gani nashawishika kuona kwamba kuna pointi, ningetamani kusikia hoja zinazonithibitishia kuwa kama Nchi basi tumekuwa tunakwamishwa na mambo haya au yale, na kwamba tukipata katiba mpya basi kila kitu kitakuwa sawa. Mengi wanayojaribu kuyataja ni ya kisiasa na madaraka zaidi kuliko matatizo halisi ya kila siku ya Wananchi.

Nijuacho mimi ni kuwa Mwanasiasa anaishi kwa siasa, hivyo kuanzisha jambo la kuwafanya waonekane wapo kazini kwao ni namna nzuri ya kuweka tiki kwenye kalenda zao kwamba tar hii walikuwa Makambako, tarehe ile Kahama, iliyofuata Namtumbo n.k na hivyo kujiongezea CV, na hata kipato maana tayari watakuwa na namna ya kuwaonesha Wahisani/Wafadhili kuwa wapo busy.

Watajitahidi kuwashawishi Wananchi ili wawaunge mkono bila kujali ya kuwa tofauti na wao Wananchi hawana wa kuwafidia muda wao maana wao kwa wakati huo wapo kazini ili hali Wananchi wataacha shughuli zao za siku kuhudhuria mikutano hiyo, yaani kama ni Muuza chipsi, Kinyozi, Fundi wa kuchomelea, Mama Lishe n.k watatakiwa kufunga ofisi zao wakawasikilize Watu ambao wao wapo kazini.

Natamani nimsikie aliyekuwa Mbunge kwenye jimbo ninakoishi la Arusha Mjini, kwa muda wote aliokuwa kiongozi wa Jimbo aseme ni nini kilimkwamisha kutekeleza aliyokuwa anaahidi kwa kukwazwa na katiba iliyopo.

Mbunge huyu ni juzi tu ametoka kupokea mamilioni ya pesa kama mafao, hivi ni kiasi gani ametenga kwa waliokuwa wapiga kura wake kwa vipindi vyote hapa jimboni kuwasadia hili na lile kwenye shughuli zao?, au pia amekwamishwa na katiba iliyopo?. kumuona tena ni mpaka 2025 aje kupambana kutafuta fursa nyingine ya kurudi Bungeni.

Hivi ni Vijana/kina Mama wangapi wamewahi kupata msaada 'support' yake kuanzisha Viwanda Vidogo, au kuwasaidia kulipia yale mafunzo mafupi yanayoendeshwa na Sido pale Ungalimitedi? nioneshwe huyu na yule hizi shughuli zao zina mkono wa aliyekuwa Mh Mbunge, au hata hilo nalo linasubiri katiba mpya?

Hivi isingekuwa zaidi Kwa Kiongozi anayejinadi kuwatetea na kuwajali sana Wananchi kuja na madai yawayo yote yale huku tayari akiwa na walau Watu 100 nyuma yake wanaomiliki viwanda/miradi/mashamba kwa muongozo/usimamizi/ushauri wake? hata hilo kakwamishwa na katiba iliyopo?.

Ninachojua mimi ni kuwa Mbunge wetu alikuwa anajiangalia yeye na familia yake kwanza na sio Wapiga kura/Wananchi. Sasa leo wakitaka kutuambia kuwa inatakiwa katiba mpya ndio abadili roho yake ya "mimi na familia kwanza" si rahisi kuelewa.

Na hata Wananchi wa maeneo mengine nao Wajiulize, kwa Msigwa, Sugu, Mnyika na hata wale wa CCM wasioshabikia katiba mpya.

Huenda ni kweli kuna umuhimu wa katiba mpya lakini si kweli kwamba wanasaiasa wanafanya hivyo kwa manufaa ya Wananchi bali ni kwa faida yao kwanza.

Hivi haiwezekani wafanye hayo bila kuwasumbua Wananchi?. Yaani Wananchi waachwe wajitafutie riziki zao na Wanasiasa tafuteni riziki zenu....mmoja asimkwamishe mwingine, au la Wanasiasa wawe wanawafidia Wahudhuriaji walioacha shughuli zao kama wao walivyo kazini.

Mimi kama Mwananchi kama kipo ninachotamani kukiona basi ni namna ya kuwawajibisha Wabunge/Wawakilishi wetu, walau kila Mwaka tuwe na mkutano tuwahoji ni mangapi ametimiza kati ya aliyoayaahidi...na maksi zikiwa chache basi apoteze sifa ya kuwa Mbunge....hivi hili halitekelezeki kw kurekebisha tu mahali bila kuhitaji katiba mpya?.
Maandishi mengi AKILI KISODA
 
Wanasiasa wanatabia za kuambaa na matukio...
Huwa siwaamini Wanasiasa kabisa, awe ni Mpinzani au anayetawala....wote watakwambia ni kwa maslahi ya Wananchi.

Alie nje anamlazimisha waliyemaarakani aweke mazingira na yeye siku moja aingie madarakani huku aliye madarakani anafanya kila linalowezekana asije akapoteza madaraka.
 
Siku za hivi karibuni kumezuka Wanasiasa na Wanaharakati wanaohanikiza kupatikana kwa katiba mpya, huku wakijaribu kuiaminisha jamii ya Watanzania kwamba kupatikana kwake ndio itakuwa mwisho wa Matatizo ya nchi hii.

Kwa muda wote ninajaribu kuwasikiliza mmoja baada ya Mwingine na bado sioni ni kiasi gani nashawishika kuona kwamba kuna pointi, ningetamani kusikia hoja zinazonithibitishia kuwa kama Nchi basi tumekuwa tunakwamishwa na mambo haya au yale, na kwamba tukipata katiba mpya basi kila kitu kitakuwa sawa. Mengi wanayojaribu kuyataja ni ya kisiasa na madaraka zaidi kuliko matatizo halisi ya kila siku ya Wananchi.

Nijuacho mimi ni kuwa Mwanasiasa anaishi kwa siasa, hivyo kuanzisha jambo la kuwafanya waonekane wapo kazini kwao ni namna nzuri ya kuweka tiki kwenye kalenda zao kwamba tar hii walikuwa Makambako, tarehe ile Kahama, iliyofuata Namtumbo n.k na hivyo kujiongezea CV, na hata kipato maana tayari watakuwa na namna ya kuwaonesha Wahisani/Wafadhili kuwa wapo busy.

Watajitahidi kuwashawishi Wananchi ili wawaunge mkono bila kujali ya kuwa tofauti na wao Wananchi hawana wa kuwafidia muda wao maana wao kwa wakati huo wapo kazini ili hali Wananchi wataacha shughuli zao za siku kuhudhuria mikutano hiyo, yaani kama ni Muuza chipsi, Kinyozi, Fundi wa kuchomelea, Mama Lishe n.k watatakiwa kufunga ofisi zao wakawasikilize Watu ambao wao wapo kazini.

Natamani nimsikie aliyekuwa Mbunge kwenye jimbo ninakoishi la Arusha Mjini, kwa muda wote aliokuwa kiongozi wa Jimbo aseme ni nini kilimkwamisha kutekeleza aliyokuwa anaahidi kwa kukwazwa na katiba iliyopo.

Mbunge huyu ni juzi tu ametoka kupokea mamilioni ya pesa kama mafao, hivi ni kiasi gani ametenga kwa waliokuwa wapiga kura wake kwa vipindi vyote hapa jimboni kuwasadia hili na lile kwenye shughuli zao?, au pia amekwamishwa na katiba iliyopo?. kumuona tena ni mpaka 2025 aje kupambana kutafuta fursa nyingine ya kurudi Bungeni.

Hivi ni Vijana/kina Mama wangapi wamewahi kupata msaada 'support' yake kuanzisha Viwanda Vidogo, au kuwasaidia kulipia yale mafunzo mafupi yanayoendeshwa na Sido pale Ungalimitedi? nioneshwe huyu na yule hizi shughuli zao zina mkono wa aliyekuwa Mh Mbunge, au hata hilo nalo linasubiri katiba mpya?

Hivi isingekuwa zaidi Kwa Kiongozi anayejinadi kuwatetea na kuwajali sana Wananchi kuja na madai yawayo yote yale huku tayari akiwa na walau Watu 100 nyuma yake wanaomiliki viwanda/miradi/mashamba kwa muongozo/usimamizi/ushauri wake? hata hilo kakwamishwa na katiba iliyopo?.

Ninachojua mimi ni kuwa Mbunge wetu alikuwa anajiangalia yeye na familia yake kwanza na sio Wapiga kura/Wananchi. Sasa leo wakitaka kutuambia kuwa inatakiwa katiba mpya ndio abadili roho yake ya "mimi na familia kwanza" si rahisi kuelewa.

Na hata Wananchi wa maeneo mengine nao Wajiulize, kwa Msigwa, Sugu, Mnyika na hata wale wa CCM wasioshabikia katiba mpya.

Huenda ni kweli kuna umuhimu wa katiba mpya lakini si kweli kwamba wanasaiasa wanafanya hivyo kwa manufaa ya Wananchi bali ni kwa faida yao kwanza.

Hivi haiwezekani wafanye hayo bila kuwasumbua Wananchi?. Yaani Wananchi waachwe wajitafutie riziki zao na Wanasiasa tafuteni riziki zenu....mmoja asimkwamishe mwingine, au la Wanasiasa wawe wanawafidia Wahudhuriaji walioacha shughuli zao kama wao walivyo kazini.

Mimi kama Mwananchi kama kipo ninachotamani kukiona basi ni namna ya kuwawajibisha Wabunge/Wawakilishi wetu, walau kila Mwaka tuwe na mkutano tuwahoji ni mangapi ametimiza kati ya aliyoayaahidi...na maksi zikiwa chache basi apoteze sifa ya kuwa Mbunge....hivi hili halitekelezeki kw kurekebisha tu mahali bila kuhitaji katiba mpya?.
Suala la Katiba Mpya limepoteza radha yake baada ya CDM kulivalia njuga kwa kile knachoonekana ajenda za kusaka madaraka. Suala hili halichukui sura ya kitaifa na wananchi wa kawaida wasio na vyama inaonekana kama fasheni.
 
Ni sawa ila basi Wananchi wasitumike kama chambo.

Maana tatizo la Wanasiasa wanapotaka la kwao Wananchi tunawekwa kati kati .
Wananchi ndio uumia pindi maamuzi yanapokuwa mabovu ya viongozi.
Katiba mbovu ndo imeleta kina sabaya
 
Wananchi ndio uumia pindi maamuzi yanapokuwa mabovu ya viongozi.
Katiba mbovu ndo imeleta kina sabaya
Hayo yalikuwa mapendekezo ya aliyekuwa madarakani sioni katiba ingemzuia vipi.

Kwa huku Afrika hizi Katiba iwe mbaya iwe nzuri bado kutekekezwa kwake kutategemea hisani ya aliyeko madarakani....akiona kipande kinachomkera kwenye hiyo katiba anaongea na chama chake wanakiondoa au kukibadilisha ili kimfae yeye....ona kina Museven.

Hata huko Vyama vya upinzani Katiba zinafuata Kiongozi Mkuu/Mwenye Chama anataka nini, sio Chadema, Cuf, Nccr, Tlp, Act, ni yaleyale tu....ndio maana naona haya ni maigizo na kutafuta cha kuwaweka bize tu.
 
Mleta mada Wala sijasoma mada yako. Kichwa Cha habari tu kimenifanya nitie maoni yangu.

Itakuwa hujui muunganiko uliopo Kati ya katiba na siasa halafu pia hujui uhusiano wa siasa na maisha.

Maisha yanaathiriwa moja kwa moja na siasa. Halafu siasa inaathiriwa na katiba.

Mfano katiba inaweza kubadili mfumo wa siasa kuwa wa kifalme vyama vyote vya siasa vikaondoka.

Na viongozi (wanasiasa) wanaweza kukataza bodaboda kuwa chombo cha usafirishaji abiria, bodaboda nchi nzima wakapoteza ulaji wao.

Katiba! Katiba! Katiba! Haturudi nyuma daima mbele.
 
Siku za hivi karibuni kumezuka Wanasiasa na Wanaharakati wanaohanikiza kupatikana kwa katiba mpya, huku wakijaribu kuiaminisha jamii ya Watanzania kwamba kupatikana kwake ndio itakuwa mwisho wa Matatizo ya nchi hii.

Kwa muda wote ninajaribu kuwasikiliza mmoja baada ya Mwingine na bado sioni ni kiasi gani nashawishika kuona kwamba kuna ukweli unaojitosheleza, ningetamani kusikia hoja nzito zinazonithibitishia kuwa kama Nchi basi tumekuwa tunakwamishwa na mambo haya au yale, na kwamba tukipata katiba mpya basi kila kitu kitakuwa sawa. Zaidi naona kama mengi wanayojaribu kuyapigania ni ya kisiasa na madaraka zaidi kuliko matatizo halisi ya kila siku ya Wananchi.

Nijuacho mimi ni kuwa Mwanasiasa anaishi kwa siasa, hivyo kuanzisha jambo la kuwafanya waonekane wapo kazini kwao ni namna nzuri ya kuweka tiki kwenye kalenda zao kwamba tar hii walikuwa Makambako, tarehe ile Kahama, iliyofuata Namtumbo n.k na hivyo kujiongezea CV, na hata kipato maana tayari watakuwa na namna ya kuwaonesha Wahisani/Wafadhili kuwa wapo busy.

Watajitahidi kuwashawishi Wananchi ili wawaunge mkono bila kujali ya kuwa tofauti na wao Wananchi hawana wa kuwafidia muda wao maana wao kwa wakati huo wapo kazini ili hali Wananchi wataacha shughuli zao za siku kuhudhuria mikutano hiyo, yaani kama ni Muuza chipsi, Kinyozi, Fundi wa kuchomelea, Mama Lishe n.k watatakiwa kufunga ofisi zao wakawasikilize Watu ambao wao wapo kazini.

Natamani nimsikie aliyekuwa Mbunge kwenye jimbo ninakoishi la Arusha Mjini, kwa muda wote aliokuwa kiongozi wa Jimbo aseme ni nini kilimkwamisha kutekeleza aliyokuwa anaahidi kwa kukwazwa na katiba iliyopo.

Mbunge huyu ni juzi tu ametoka kupokea mamilioni ya pesa kama mafao, hivi ni kiasi gani ametenga kwa waliokuwa wapiga kura wake kwa vipindi vyote hapa jimboni kuwasadia hili na lile kwenye shughuli zao?, au pia amekwamishwa na katiba iliyopo?. kumuona tena ni mpaka 2025 aje kupambana kutafuta fursa nyingine ya kurudi Bungeni.

Hivi ni Vijana/kina Mama wangapi wamewahi kupata msaada 'support' wa kiujuzi au mtaji ili waanzishe Viwanda vyao Vidogo Vidogo?, walipieni Vijana mafunzo ya Sido pale Ungalimitedi? natamani nioneshwe Wapiga Kura walionufaika kupitia Kiongozi wao na kama hakuna naomba Kiongozi aniambie ni kwa namna gani katiba iliyopo imemkwamisha.

Hivi isingekuwa zaidi Kwa Kiongozi anayejinadi kuwatetea na kuwajali sana Wananchi wake kuja na madai yawayo yote yale huku tayari akiwa na mamia ya Watu nyuma yake wanaomiliki viwanda/miradi/mashamba kwa muongozo/usimamizi/ushauri wake? au hata hilo wanakwamishwa na katiba iliyopo?.

Ninachojua mimi ni kuwa Mbunge wetu alikuwa anajiangalia yeye na familia yake kwanza na sio Wapiga kura/Wananchi.... Sasa leo wakitaka kutuambia kuwa inatakiwa katiba mpya ndio ibadili roho za Wanasiasa ni usanii wa kisiasa tu.

Na hebu hata Wananchi wa maeneo mengine nao wafanye tathmini ya mabadiliko waliyoyapata tangu wawashawishike kuwachagua Wabunge wao...Walinganishe hali ya Mbunge kabla ya kupata Ubunge na baada ya kupata Ubunge, ni nani amenufaika...ni yeye ay wao?....aulizwe Msigwa, aulizwe Sugu, aulizwe Mnyika, aulizwe Bulaya n.k.

Huenda ni kweli kuna umuhimu wa katiba mpya lakini si kweli kwamba wanasaiasa wanafanya hivyo kwa manufaa ya Wananchi bali ni kwa faida yao kwanza.

Na kama inabidi kufanya hizo harakati zao basi zifanyike bila kuathiri muda wa Wananchi?. Yaani Wananchi waachwe wajitafutie riziki zao za siku hadi siku huku na Wanasiasa wakipambania hilo wanalofikiri lina manufaa kwa nchi?.

Mimi kama Mwananchi kama kipo ninachotamani kukiona basi ni namna ya kuwawajibisha Wabunge/Wawakilishi wetu, walau kila Mwaka tuwe na mkutano tuwahoji ni mangapi ametimiza kati ya aliyoayaahidi...na maksi zikiwa chache basi apoteze sifa ya kuendelea kuwa Mbunge....hivi jambo kama hili halitekelezeki kwa kurekebisha tu kifungu bila kuhitaji mchakato mreeefu wa katiba mpya?.
Kuwa gizani si lazima uwe kipofu.
 
Mm naomba tupige kura wananchi wote kama tunahitaji katiba mpya
Ingawa ukiiweka moja kwa moja kwa picha hiyo utawahanganya tu watu na matokeo hayatakuwa na uhalisia.

Labda Watu wadadavuliwe waweze kupima ni mangapi yanakosekana kwa kutumia katiba iliyopo na mangapi yatapatikana ikipatikana katiba mpya...wakiweka tofauti kwenye mizani basi wataamua kihalali.
 
Siku za hivi karibuni kumezuka Wanasiasa na Wanaharakati wanaohanikiza kupatikana kwa katiba mpya, huku wakijaribu kuiaminisha jamii ya Watanzania kwamba kupatikana kwake ndio itakuwa mwisho wa Matatizo ya nchi hii.

Kwa muda wote ninajaribu kuwasikiliza mmoja baada ya Mwingine na bado sioni ni kiasi gani nashawishika kuona kwamba kuna ukweli unaojitosheleza, ningetamani kusikia hoja nzito zinazonithibitishia kuwa kama Nchi basi tumekuwa tunakwamishwa na mambo haya au yale, na kwamba tukipata katiba mpya basi kila kitu kitakuwa sawa. Zaidi naona kama mengi wanayojaribu kuyapigania ni ya kisiasa na madaraka zaidi kuliko matatizo halisi ya kila siku ya Wananchi.

Nijuacho mimi ni kuwa Mwanasiasa anaishi kwa siasa, hivyo kuanzisha jambo la kuwafanya waonekane wapo kazini kwao ni namna nzuri ya kuweka tiki kwenye kalenda zao kwamba tar hii walikuwa Makambako, tarehe ile Kahama, iliyofuata Namtumbo n.k na hivyo kujiongezea CV, na hata kipato maana tayari watakuwa na namna ya kuwaonesha Wahisani/Wafadhili kuwa wapo busy.

Watajitahidi kuwashawishi Wananchi ili wawaunge mkono bila kujali ya kuwa tofauti na wao Wananchi hawana wa kuwafidia muda wao maana wao kwa wakati huo wapo kazini ili hali Wananchi wataacha shughuli zao za siku kuhudhuria mikutano hiyo, yaani kama ni Muuza chipsi, Kinyozi, Fundi wa kuchomelea, Mama Lishe n.k watatakiwa kufunga ofisi zao wakawasikilize Watu ambao wao wapo kazini.

Natamani nimsikie aliyekuwa Mbunge kwenye jimbo ninakoishi la Arusha Mjini, kwa muda wote aliokuwa kiongozi wa Jimbo aseme ni nini kilimkwamisha kutekeleza aliyokuwa anaahidi kwa kukwazwa na katiba iliyopo.

Mbunge huyu ni juzi tu ametoka kupokea mamilioni ya pesa kama mafao, hivi ni kiasi gani ametenga kwa waliokuwa wapiga kura wake kwa vipindi vyote hapa jimboni kuwasadia hili na lile kwenye shughuli zao?, au pia amekwamishwa na katiba iliyopo?. kumuona tena ni mpaka 2025 aje kupambana kutafuta fursa nyingine ya kurudi Bungeni.

Hivi ni Vijana/kina Mama wangapi wamewahi kupata msaada 'support' wa kiujuzi au mtaji ili waanzishe Viwanda vyao Vidogo Vidogo?, walipieni Vijana mafunzo ya Sido pale Ungalimitedi? natamani nioneshwe Wapiga Kura walionufaika kupitia Kiongozi wao na kama hakuna naomba Kiongozi aniambie ni kwa namna gani katiba iliyopo imemkwamisha.

Hivi isingekuwa zaidi Kwa Kiongozi anayejinadi kuwatetea na kuwajali sana Wananchi wake kuja na madai yawayo yote yale huku tayari akiwa na mamia ya Watu nyuma yake wanaomiliki viwanda/miradi/mashamba kwa muongozo/usimamizi/ushauri wake? au hata hilo wanakwamishwa na katiba iliyopo?.

Ninachojua mimi ni kuwa Mbunge wetu alikuwa anajiangalia yeye na familia yake kwanza na sio Wapiga kura/Wananchi.... Sasa leo wakitaka kutuambia kuwa inatakiwa katiba mpya ndio ibadili roho za Wanasiasa ni usanii wa kisiasa tu.

Na hebu hata Wananchi wa maeneo mengine nao wafanye tathmini ya mabadiliko waliyoyapata tangu wawashawishike kuwachagua Wabunge wao...Walinganishe hali ya Mbunge kabla ya kupata Ubunge na baada ya kupata Ubunge, ni nani amenufaika...ni yeye ay wao?....aulizwe Msigwa, aulizwe Sugu, aulizwe Mnyika, aulizwe Bulaya n.k.

Huenda ni kweli kuna umuhimu wa katiba mpya lakini si kweli kwamba wanasaiasa wanafanya hivyo kwa manufaa ya Wananchi bali ni kwa faida yao kwanza.

Na kama inabidi kufanya hizo harakati zao basi zifanyike bila kuathiri muda wa Wananchi?. Yaani Wananchi waachwe wajitafutie riziki zao za siku hadi siku huku na Wanasiasa wakipambania hilo wanalofikiri lina manufaa kwa nchi?.

Mimi kama Mwananchi kama kipo ninachotamani kukiona basi ni namna ya kuwawajibisha Wabunge/Wawakilishi wetu, walau kila Mwaka tuwe na mkutano tuwahoji ni mangapi ametimiza kati ya aliyoayaahidi...na maksi zikiwa chache basi apoteze sifa ya kuendelea kuwa Mbunge....hivi jambo kama hili halitekelezeki kwa kurekebisha tu kifungu bila kuhitaji mchakato mreeefu wa katiba mpya?.
Wanapropaganda wa CCM mmepata mstari shawishi wa kupinga mabadiliko ya katiba. Yaani mmepania kutenganisha maslahi ya wananchi na ya wanasiasa hasa wa upinzani kwa vile mmejua kuwa Watanzania wengi hata waliosoma hawana uelewa wa haya mambo. Hii yote ni ili wananchi waendelee kuishi chini ya kivuli muflisi cha CCM kama chama dola kisichohojiwa wala kuwajibishwa kwa utendaji mbovu, ukandamizaji haki na ufisadi.

Ni mjinga pekee anayeweza kukubaliana na hoja ya kuwa katiba bora HAINA uhusiano na uchumi/maendeleo.

Ndio muendelezo wa ujinga mwingi uliopandikizwa kwamba: "siasa haitakiwi kabisa kwenye masuala ya maendeleo" na "maendeleo hayana chama wala itikadi"!

Kwa kifupi bila marekebisho ya katiba tuliyo nayo, Watanzania watakuwa wameamua kuendelea "kupigwa" na magenge yanayomiliki CCM kwa zamu. It's their funeral.
 
Hayo yalikuwa mapendekezo ya aliyekuwa madarakani sioni katiba ingemzuia vipi.

Kwa huku Afrika hizi Katiba iwe mbaya iwe nzuri bado kutekekezwa kwake kutategemea hisani ya aliyeko madarakani....akiona kipande kinachomkera kwenye hiyo katiba anaongea na chama chake wanakiondoa au kukibadilisha ili kimfae yeye....ona kina Museven.

Hata huko Vyama vya upinzani Katiba zinafuata Kiongozi Mkuu/Mwenye Chama anataka nini, sio Chadema, Cuf, Nccr, Tlp, Act, ni yaleyale tu....ndio maana naona haya ni maigizo na kutafuta cha kuwaweka bize tu.
True Hakuna kiongozi yeyeto aliyepo madarakani akajua umuhimu wa katiba mpya ni hadi atakapokuwa nje ya madaraka
 
Naomba kujua hii katiba mpya inayopigiwa upatu, ni nani mnufaika mkubwa?

Kama ni mwananchi je kipato cha mwananchi kitaongezeka? Huduma za afya ,elimu,maji,umeme,usafiri vitaboreshwandani ya katiba mpya?

Upande wa CHADEMA wananufaikaje kwenye siasa?

CCM itanufaikaje?
 
Back
Top Bottom