Huu ufa kwenye hii ndoa unazibika?

Huu ufa kwenye hii ndoa unazibika?

Sijui kama nimekuelewa vizuri! Inaonekana ulimsaliti harafu mkasuluhishwa yakaisha.
Sasa kama ulimsaliti huko nyuma harafu mkasuluhishwa yakaisha,kwake yeye moyoni hayakuisha! Hata ungemnunulia nini au kumpa fedha kiasi gani.
Lifahamu hili ukimsaliti Mwanamke akagundua huwa hasahau kabisa na hawezi kukuamini hata siku moja,kama wapo ni Wachache.
Kwa mfano hapo unasema Unasafiri ndiyo kabisa.
Changamoto kama ninyi ni Waislamu nadhani mrudi kwa Wazee tena,vinginevyo talaka unaachia.
Kama sikuelewa hivyo niwie radhi.
 
Kuna kitu unakificha,huweki wazi.Huko kupelekana kwa wazazi na hizo case, tatizo lilikua nini??Umempiga tukio gani binti wa watu mpaka anataka kuondoka.


Kuna issue kama hii ya kwako, binti analazimisha kusepa lkn hatoi sababu, vikao vyote - hasemi sababu.
Ikafika muda mpaka paroko.kaingilia kati - bado hali tete.Siku na siku wameitwa kwa paroko, binti karopoka - jamaa amekua akimlazimisha na kumsisitiza wafanye kinyume na maumbile. Kikao chote kimya, binti na yule jamaa wakaaga, wakaondoka kwenda nyumbani - Na ndoa ikaendelea na lile swala likaishia hapohapo..bila hata ushauri wa mtu.
 
Furaha haipo tena wakuu nimedaiwa talaka na mke wangu usiku wa kuamkia leo, mimi mke bado namuhitaji. Chanzo cha yote(tatizo) ni mimi haihusiani na usaliti na tulishakaa vikao na familia tukayamaliza lkn mara zote toka hapo haijawahi kuisha wiki bila kununiana furaha siku 3 nne zillizobaki ni sintofahamu pamoja na kuwa anatimiza majukumu yake yote kama mke.

Usiku wa kuamkia leo baada ya kuniomba talaka yake alimpigia mama yake simu by 7 kasoro usiku kumueleza kuwa hana furaha tena! mama alikuwa na hamu ya kujua nini tatizo lkn binti alisisitiza siioni ndoa yangu tena na kukata simu ila kabla ya kukata alimuahidi kesho ntakuambia kila kitu.

Kwa hili sikuwa na namna sababu nilisharuhusu simu kupigwa japo baada ya kupiga simu nilimuomba usizungumze chochote na mama yako kuhusu hili wewe utajua namna ya kuongea ili kutuliza hali na ameniitikia kwa kunielewa, lkn sijui kichwani anawaza nini!

Nilimuahidi mimi pia nitazungumza na mama yake, jambo jingine nimemuomba nimuache peke yake kwanza nisafiri ili angalau upatikane muda wa utulivu kwanza lkn sio kumpa talaka.
Kuna maisha baada ya talaka mkuu.

Mpe anachotaka. Kulazimisha mapenzi ni kitu kibaya sana.
 
Furaha haipo tena wakuu nimedaiwa talaka na mke wangu usiku wa kuamkia leo, mimi mke bado namuhitaji. Chanzo cha yote(tatizo) ni mimi haihusiani na usaliti na tulishakaa vikao na familia tukayamaliza lkn mara zote toka hapo haijawahi kuisha wiki bila kununiana furaha siku 3 nne zillizobaki ni sintofahamu pamoja na kuwa anatimiza majukumu yake yote kama mke.

Usiku wa kuamkia leo baada ya kuniomba talaka yake alimpigia mama yake simu by 7 kasoro usiku kumueleza kuwa hana furaha tena! mama alikuwa na hamu ya kujua nini tatizo lkn binti alisisitiza siioni ndoa yangu tena na kukata simu ila kabla ya kukata alimuahidi kesho ntakuambia kila kitu.

Kwa hili sikuwa na namna sababu nilisharuhusu simu kupigwa japo baada ya kupiga simu nilimuomba usizungumze chochote na mama yako kuhusu hili wewe utajua namna ya kuongea ili kutuliza hali na ameniitikia kwa kunielewa, lkn sijui kichwani anawaza nini!

Nilimuahidi mimi pia nitazungumza na mama yake, jambo jingine nimemuomba nimuache peke yake kwanza nisafiri ili angalau upatikane muda wa utulivu kwanza lkn sio kumpa talaka.
Kuwa mwanaume babu. Piga chini. Kwani akifa unafanyaje? Jitahd kuruhusu kukubali jambo likifika wakat wake kaka
 
Uko sahihi kwa asilia mia mkuu
Fuata moyo wako mkuu. Kama moyo umegoma kumuachia usimuache. Ndoa nyingi unazoziona zipo hadi uzeeni zilipitia changamoto hata kufikia kutamani kuachana. Walitatua tofauti zao maisha yakaendelea.

Umegundua makosa yako rekebisha. Usiharibu pesa yake. Kukupa pesa ili ununue uwanja anakuheshimisha wengine wengi wananunua vijawanja na asset zingine kwa pesa za mwanaume wanajulisha kaka zao mume anakuwa hana taarifa yoyote. Mwanamke akikuzidi pesa lazima uwe smart tumia pesa yako kwa ajili ya mambo yako ila usiharibu pesa anazokupa kwa kukuamini. Pombe na kupiga pesa umeharibu. Hata ungekuwa wewe umempa pesa atunze za kununua uwanja akatumbua na mashoga zake ungefukuza siku hiyohiyo.

Umeharibu rekebisha panapovuja. Weka wazi haitajirudia na usirudie.
 
Nyie ndio mnakunywaga sumu mkiqchwa. Hii dunia upo peke yako babu
Bwashee tuliza kichwa. Tunazungumzia ndoa ya mtu sio yako. Kuna wanaume wakifuata ushauri kama huo wako ndio unawapoteza kabisa. Hatufanani.

Hivi ingekuwa wewe umetuma pesa kwa mkeo anunue uwanja akazipiga kwa kunywea pombe ungemfanya nini? Halafu anakuazima pesa ili akanywe wewe ungemvumilia. Kwa vyovyote vile ungefukuza siku hiyohiyo. Kijana kamtibua wife ushauri wenu mnapoteza
 
Shida hasa ilikuwa pombe kiasi sikuwa nazingatia familia na hapo alikuwa mkoa mwingine kikazi hii ilileta shida kiasi hta nikashindwa kuheshimu amana zake sababu kunq wakati alipata eneo shamba nimnunulie na alinitumia milioni moja lkn sikuitimiza hii ahadi na ulitokea mzozo wa kudai talaka pia lkn tulikaa na familia tukamaliza hili kwa kuahidi kumrejeshea kiasi chake.Wakati huo mimi ni misheni town tu yy ni mujiriwa familia ikashauri itabidi ukaungane na mwenzio pmj nilikubalina na wazo hili nikajichukulia hakiba yangu kwanza nikamlipa kiasi chake nikabaki km na m hv ukiondoa maswala ya nauli na mahitaj mengine nikabakiwa km na laki 7 hivi so toka nimefika huku ni mwezi wa 4 sasa vtu havijaenda vile inavyotakiwa au ilivyopngwa.
Wiki iliyopita Kuna kiasi chake km 200000 hiv niliichukua na kumuahidi ntamrejeshea jna lkn sikutimiza hii ahadi, mara ghafla naona usiku vilio nauliza nini tatzo majibu ndio km hayo
Pole sana mkuu , ni bora impatient talaka yake .
Huyo mwanamke hakupendi wala hataki kuishi na wewe ndio maana hataki hata kuzaa na wewe .
Achana nae asije akakuwekea sumu akuondoe kwenye maisha yake kwa nguvu.
Huyo mwanamke ameona huna pesa wanawake wengi wa kizazi hiki wanajali sana pesa kulipo mapenzi hata kwenye ndoa.
Embu jipange vizuri upate kipato cha uhakika ndio uoe tena .
Mwanamke akikuzidi kipato halafu na wewe usiwe na kipato cha uhakika ni shida sana.
Dah ila hongera yaani mke wako anakupa hela yake kabisa aisee una bahati sana , wanawake wa sikuhizi kumpatia mume wake pesa sio kawaida wengi wao wamezoea kupokea tu
 
Mganga alikushauri Nini ukatenda ukijua mke hatajua???😅, pole sana. Hapo hakuna ndoa....mwanamke anapokasilika ni zaidi ya Simba umkutapo porini...kuwa makini mruhusu aende hata kama unamuhitaji kwa kiasi kikubwa. Tusije kukupoteza....mwanamke ataamua mwenyewe kama akuombe arudi au iwe jumla ......lakini usilazimishe, ogopa sana mwanamke anayekufanyia Kila kitu....akasilike aombe kitu alafu ukaze fuvu...tutakuzika😄😄
 
Kwa level aliyofikia ukiendelea kumlazimisha mwendo utaumaliza, kuwa makini hawa viumbe ni hatari mno
 
Kumbe tatizo ni wewe halafu sisi tunamlaumu Binti wa watu,
Mkeo kaona hawezi kufanya maisha na mtu aliyetawaliwa na ulevi na kusahau majukumu yake na future ya maisha yake/Maisha yenu,

Kwa kesi hii nipo upande wa mkeo coz siamini kama umebadilika,
Mpe talaka Binti wa watu kisha wewe tafuta mlevi mwenzako umuoe,mtaendana vizuri sana,siku zingine mtakua mnaamua tu kama mlale Kilabuni au mrudi home.
Mi naona tatizo mwamba hana pesa, Wala sio ulevi. Meanamke hawezi vumilia mtu hana pesa.
 
Nikiwaambia kwamba mwanaume ndo anahitaji ndoa kuliko mwanamke mnabisha. Ona sasa
Huyu mtoa post inaelekea ni mwanaume mzembe , anatuzalilisha sisi wanaume hivi kweli unaanzaje kumkopa mke wako pesa ?
Halafu tena usimlipe? Unaanzaje kupiga kibiriti pesa aliyokupa wife ukanunulie kiwanja.
Dah yaani hii dunia ina mambo sana kweli kuishi kwingi ni kuona na kusikia mengi
 
Back
Top Bottom