Huu sio ubinadamu kabisa

Kuna siku nimekaa na Manzi paper ya Civil procedure kumbe bhana kachora kwenye ACt mara msimamizi huyu hapa duh ilikuwa balaa Manzi afu alikua mjamzito hapo hapo akafukuzwa chuo na kujifungua juu mtot akafariki duh sitakuja kusahau
 
Hiy
Watu tulikuwa tunaiba booklete inajazwa kila kitu, unaingia nayo, ile unayoepewa unaipiga chini unaanza tumia uliyo ingia nayoo... then unaomba booklet ingine unapanga sasa majibu vizuri πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… shule raha sanaaa
Hiyo technique imemfukuzisha dogo mmoja hapo hapo MUST mwaka juzi.
 
Ongea na dean of students hiyo issue inaweza pata Msaada Maana kuingia na simu ni kosa so ubinadamu unabidi kutumikishana zaidi
Sheria bila busara ni ukandamizaji.
Hata mtu akiuua huwa wanaangalia km mtu alikusudia au ilikuwa ni bahati mbaya.
 
Dogo amevunja sheria na hana wa kumlaumu.
Kama msamaha tunamuombea apewe kwa huruma tu.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] khaaaah wee.
Sasa wee pesa ulikua nazo, wasiokua nazo je? Watatoa wapi za kuhonga.
 
Sheria ni katili sana.
 
Sema tu ni wewe Ili usaidiwe..

anyway, Mimi ni lecturer hapo MUST na Ndie niliekukamata na simu.. umeona uje huku jeiefu ukidhani sipo? Hili suala nakuhakikishia ntalivalia njuga hadi ufukuzwe chuo
Hivi mnajisikiagaje ku comment ujinga?
 
Watu tulikuwa tunaiba booklete inajazwa kila kitu, unaingia nayo, ile unayoepewa unaipiga chini unaanza tumia uliyo ingia nayoo... then unaomba booklet ingine unapanga sasa majibu vizuri πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… shule raha sanaaa
Yaani wewe hapo unaona ni sifa kubwa kuibia na kupata cheti au degree usiyostahili. Wakijuwa wakakunyag'anya hiyo degree utawatangazia ubaya mpaka motoni. Yaani unajisifu kuibia. Ndiyo maana wale wanaoiba serkalini na mashirika ya taifa na kujenga mahekalu husifiwa na wale wanaofanya kazi kwa uaminifu hutukanwa kama wajinga wasiokuwa na akili. Hii ndiyo TZ yetu. Ninyi ndiyo wahusika katika kushusha hadhi ya elimu ya TZ. Ndiyo ninyi mliyopata degree za civil engineering kwa michongo na kuibia mkawa mnasimamia majengo yaliyopkuja kuporopomoka kwa sababu vyeti mlivipata pasipo kupita mitihani kihalali. Lakini sasa mnajisifu na mnataka Wataqnzania wengine wapitie njia zenu. HATA AIBU HAMNA.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] khaaaah wee.
Sasa wee pesa ulikua nazo, wasiokua nazo je? Watatoa wapi za kuhonga.
Waroge, mbona wagaganga mashuhuri wengi, msimamizi anakuwa akuoni unachofanyaπŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…
 
Kipindi nipo law school of Tanzania, Kuna jamaa mmoja aliwahi kuingia na sheria ambayo haikutajwa kwenye instructions. Camera ikammulika. Alidisco
 
Kikubwa nilimaliza salama na G.P.A swaaafi, na kazi zangu ni nzuri sana nazofanya yani zina quality πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… elimu ya darasani sio kipimo cha ubora au ubaya wa kazi, kuna ambao hawajasoma wapo smart sana kwenye miradi kwa uzoefu kuliko G.P.A temboo.. banaaa wews fanya linalowezekana kikubwa umalize upewe cheti chako kazi utajifunza mtihani, elimu ya Tz ilisha vurugwaaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…