Humprey Polepole, yupo Channel ten sasa hivi

Humprey Polepole, yupo Channel ten sasa hivi

Makongoro Charles.

Kwa vile ni mchambuzi mzuri wa mambo ya kisiasa nilitegemea lazima aseme Charles Makongoro Nyerere ndo turufu pekee kwa CCM kama kweli wanataka kuendelea kukamata dola
 
Akichambua Baadhi Ya Watangaza Nia Ndani Ya Ccm Kijana Huyu Mwenye Waledi Mkubwa Pia Aliwataka Makamba Na Mwigulu Kujipika Kwanza Waive Mana Bado Ni Wabichii Pia Aliongeza Kuwa Sitta Na Wasira Hawafai Kabisa Kupewa Ridhaa Mana Waliyakanyaga Maoni Ya Wananchi Kwenye Rasimu Ya Warioba

Chanzo Chanel Ten

MADA MOTO
 
Kwa vile ni mchambuzi mzuri wa mambo ya kisiasa nilitegemea lazima aseme Charles Makongoro Nyerere ndo turufu pekee kwa CCM kama kweli wanataka kuendelea kukamata dola
Makongoro ametulia.
 
Kuna namna tunaweza kuona video ya hicho kipindi online?
 
Kwa vile ni mchambuzi mzuri wa mambo ya kisiasa nilitegemea lazima aseme Charles Makongoro Nyerere ndo turufu pekee kwa CCM kama kweli wanataka kuendelea kukamata dola

mako hajawahi onja mchuzi wa pweza hatuwezi jua kama ni mlafi au la, bora lowasa tukikosa sana basi dr.mahiga,
 
Hatimaye Mwanaharakati na aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Jaji Warioba ilikuwa na kazi ya kukusanya maoni ya rasimu ya Katiba Mpya Humphrey Polepole Jana wakati akiongea na Kituo cha Channel Ten alisema kuwa ni kada wa CCM wakati amekuwa akisema kwa muda mrefu kuwa si Mwanachama wa Chama chochote cha siasa hapa nchini....
 
Jana Humphrey Polepole alidai kuwa umri wa akina January na Mwigulu siyo mzuri kwa nafasi kuiongoza nchi tena akamkosoa Wassira kuwa alikataa rasimu ya wananchi hivyo hafai nikamwelewa.

Sasa nikajiuliza hiyo rasimu ambayo yeye alishiriki kuiandika nayo sio umri ni huo huo? Inakuaje anapinga umri wakati ni haki yao ya msingi na yeye alisaidia kuuweka kwenye rasimu mpya ambayo anadai Wassira aliikataa?

Maoni kuwa hata yeye anaikataa hiyo rasimu?
 
Thubutu. Nimesikia na Mrisho Mpoto analitaka hilo Jimbo kazi ipo watamuweza Genius John John Mnyika?
 
Mkuu hayo ni maoni yake kwamba jamaa bado Vijana sana na hawana uzoefu wa kutosha japokuwa katiba inawaruhusu. Katoa mfano wa akina NKurunziza na Joseph Kabila kung'ang'ania madaraka japokuwa sio kigezo kwani wapo marais wazee wengi wanang'ang'ania madaraka hapo siungani naye. Aseme tu hawajakomaa kuwa ma Rais watanzania hawajawaona vya kutosha kama wana sifa hizo maana wanamiaka mitano tu kwenye madaraka ya ubunge na uwaziri sijui kama wana miaka hata mitatu bado sana
 
Waryoba mnamkubali ingwa ni CCM, Shibuda hamumkubali ingawa ni CDM.

Kwanini mnamponda Polepole? Wanafiki.

hivi ndo ww ulikuwaga unscheza mpira ktk gazet la sani? hata post yako imesadifu jina la kobelo mzee wa waluwalu.
 
mako hajawahi onja mchuzi wa pweza hatuwezi jua kama ni mlafi au la, bora lowasa tukikosa sana basi dr.mahiga,

Mmmh haya bana kila mtu na mtazamo wake. Ila mwenzio siko kishabiki zaidi ndo maana naona kwa ccm Makongoro ndo anafaa, nje ya ccm ni Dr. Slaaa
 
Polepole haeleweki,umri wa miaka 40 kashrk kupendekeza,mara hana chama leo n ccm. Mbona anajichanganya? Tatizo la kuwa muongo alafu unakuwa msahaulifu,kosa kweli. Mchambuzi daima hutakiwi uoneshe itikadi yako.
 
Its just cantergerous as how the elections are concerned.hope mwandosya becomes the fifth President
 
Back
Top Bottom