Watanzania bana, sasa mnadhani wapi haki itapatikana?
Dah, Mahakama Kuu haiwezi kufanya kosa, mashtaka yalikuwa dhaifu na mtuhumiwa sasa anarajea mtaani kukabiliana na vyombo vya habari vilivyomchafua jina... Kaazi kwelikweli
Lakini si aliyeua ni Koplo Saad ambaye hayupo? Vyombo vya habari na wamiliki wake wakae mkao wa kuanza kulumbana na Zombe kwa kudaiwa fidia
labda ije evidence mpya. Ama sivyo wanasema inakuwa double jeapardy.je anaweza kukamatwa tena ? na kushitakiwa upya ?
mahakama inafanya kazi kutokana na ushahidi unaoletwa mbele yake na wala si kwa kusoma magazeti na hisia!
Hivi mlitaka iweje? Kama Zombe hakuua na ushahidi hautoshelezi, mnataka ahukumiwe kwa sheria ipi? Mashtaka ni dhaifu wakuu!
Angalia hata nilichogusia kuhusiana na kesi ya kina Mramba... Kesi hiyo pia inaelekea ni dhaifu tu!
Kesi ya kina Mramba: Serikali itashindwa!
Inaweza ikawa inawauma wengi lakini sheria ni msumeno...
Tatizo sio woga mazee,bali nakushangaa tu jinsi unavyowahsauri watu walioko Dar waingie mtaani wafnaye vurugu kudai haki kisha wapigwe virungu na polisi(kama siyo risasi) wakamatwe na kufunguliwa mashtaka kisha wahukumiwe ilhali wewe uko mikoani/majuu unakula tu BATA...Haiwezekani aiseeHaki inadaiwa kivyoyote wewe, hata kumuua jaji Masati....kumbuka watu wamepoteza ndugu zao kwa ulafi wa Zombe, na ni dhahiri bado tunaletewa za kuleta. Acha woga, mafisadi hawana msalie mtume.
Ukweli huo ulionekana hata wakati wa utoaji ushahidi,mashahidi karibu wote ushahidi wao ulikuwa ni wa hisia zaidi kuliko ukweli husika,Binafsi niliamini Zombe angeachiwa kutokana na ushahidi dhaifu uliotolewa.
Tufikie mahala tuwe tunaangalia mwenendo wa kesi na si kushangaa hukumu,kulikuwa na mapungufu mengi mno kwa mashahidi wa mashitaka wakitoa ushahidi dhaifu mno uliotanguliwa na jazba bila kuangalia uzito wa kesi ya mauaji.Binafsi ningeshangaa kama JUDGE angeweza kutoa hukumu kwa kuangalia mazingira ya nje ya mwenendo wa kesi na si ushahidi na mwenendo mzima wa kesi...
Pia hili ni fundisho kwa vyombo vyetu vya habari kwa namna ambavyo vinaweza kupotosha sheria,naamini kama JUDGE angekuwa dhaifu angeweza toa hukumu ili kufurahisha jamii na si kwa kuangalia mwenendo wa kesi na ushahidi,Kwa kweli JUDGE amekuwa objective.nilifuatilia kwa makini kesi ya Zombe na kwa kiasi kikubwa ushahidi kwenye kesi ya kuua ulikuwa ni dhaifu mno,kwa kiasi kikubwa kesi ilikuwa ni ya kisiasa zaidi.
Hi ni changamoto kwa wanahabari kuipitia hukumu ya JUDGE na kuangalia namna alivyofikia hitimisho na madhaifu atayoonyesha kwenye marejeo ya ushahidi na mwenendo mzima wa kesi kwa ajili ya kuinua upeo wetu wanahabari kwenye habari zinazohusu mambo mazito kama haya ya mauaji ya kukusudiwa yatendwayo na baadhi ya maaskari wetu.
Mbele ya Jaji Salum Massatti anayeisikiliza kesi hiyo, Bageni alidai kuwa Zombe alimweleza kuwa walisoma na Jaji Kipenka darasa moja katika Shule ya Sekondari Songea na kwamba ameahidi kuwasaidia katika suala la mauaji hayo.
"Mshitakiwa wa kwanza aliniambia kuwa Jaji Kipenka ni "classmate" wake... walisoma naye darasa moja Songea Boys na kwamba wamewasiliana na amemwambia kuwa tupeleke taarifa iliyorekebishwa ili awasaidie vijana wetu," alidai Bageni wakati akijibu maswali kutoka kwa wakili wa serikali, Angaza Mwipopo.
Bageni alidai kutokana na ushauri huo wa Zombe waliamua kuibadili taarifa waliyoipeleka kwenye tume hiyo, tofauti na taarifa waliyoiandaa ambayo ilipelekwa katika kitengo cha uhalifu, maarufu kama 99.
Ni kweli inawezekana kwamba Zombe hana hatia. Lakini mambo kama haya ambapo jamii inaona wazi kabisa kwamba kuna uwalakini mkubwa halafu Mahakama inapindisha hukumu au inazingatia ushahidi ambao hauna uzito ili kufikia malengo wanayoyataka then hii ndio inawafanya watu kukosa imani na vyombo vya serikali.
Kwa hali hii wananchi wengi wataendelea kuvunjika moyo, kukata tamaa na kuendelea kukerwa na Serikali yao yote kwa ujumla.
Kila chombo cha serikali kwa sasa kinanyooshewa kidole kwa kuwa Dhaifu. Bunge kwa kushindwa kuwatetea wananchi pamoja na wabunge kujilimbikizia mali na kuonekana kutowajali wananchi, Serikali kwa kuwa mbali na wananchi na kufungia macho maovu makubwa kwenye jamii na Mahakama kuwa sehemu ya kuhalalisha uovu.
Inakatisha tamaa zaidi kuona kwamba mambo makubwa kabisa na yenye mustakabali wa kitaifa huchukuliwa kirahisi rahisi au hupindishwa wakati mambo madogo hukemewa na kuchukuliwa hatua kubwa ya kuyakomesha kabisa. Kwa hali hii itakua ni vigumu sana kukomesha Mob Justice (kuchukua sheria mikononi).
Hukumu ya Zombe is a big scandal, shame and mockery of the Justice system in our country but a tainted corruption and grave recklessness, lack of profesionalism, ignorance of the Attorney General Office, investigation and Police Department.
Jaji Salum Massati wa Mahakama ya Rufani Tanzania, anayesikiliza kesi ya mauaji inayomkabili aliyekuwa Kaimu Kamanda na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar Salaam, Abdallah Zombe na wenzake tisa, amehoji kama kweli marehemu walikufa wakati wakipambana na polisi, kwa nini majereha waliyopata yanafanana.
Alisema kinachomtia shaka ni matokeo ya uchunguzi wa miili ya marehemu (postmoterm) kuonyesha kuwa marehemu wote wanne walipigwa risasi maeneo yanayofanana kisogoni, kinyume na maelezo kwamba kulikuwa na kurushiana risasi kati ya watuhumiwa na polisi.
Jaji Massati alielezea wasiwasi wake huo jana mara, baada ya mshitakiwa wa pili katika kesi hiyo, Christopher Bageni, kuhojiwa na wakili wake, mawakili wa upande wa mashitaka na wazee wawili wa baraza.
Jaji alisema majibu ya uchunguzi huo yanaonyesha kuwa marehemu wote walipigwa risasi kisogoni sehemu zinazofana hivyo alihoji kama kulikuwa na mapambano baina yao na polisi kama inavyodaiwa na Zombe na wenzake, iweje sehemu zilizopita risasi katika miili ya marehemu zifanane.
Jaji Massati anayeisikiliza kesi hiyo ya mauaji katika Mahakama Kuu ya Tanzania, alisema inaonyesha kuwa risasi zile zilipigwa moja kwa moja na si upande wa kati wa mashambulizi yanayosemekana yalikuwepo baina ya polisi na wafanyabiashara hao.
Ni kweli inawezekana kwamba Zombe hana hatia. Lakini mambo kama haya ambapo jamii inaona wazi kabisa kwamba kuna uwalakini mkubwa halafu Mahakama inapindisha hukumu au inazingatia ushahidi ambao hauna uzito ili kufikia malengo wanayoyataka then hii ndio inawafanya watu kukosa imani na vyombo vya serikali.
Kwa hali hii wananchi wengi wataendelea kuvunjika moyo, kukata tamaa na kuendelea kukerwa na Serikali yao yote kwa ujumla.
Kila chombo cha serikali kwa sasa kinanyooshewa kidole kwa kuwa Dhaifu. Bunge kwa kushindwa kuwatetea wananchi pamoja na wabunge kujilimbikizia mali na kuonekana kutowajali wananchi, Serikali kwa kuwa mbali na wananchi na kufungia macho maovu makubwa kwenye jamii na Mahakama kuwa sehemu ya kuhalalisha uovu.
Inakatisha tamaa zaidi kuona kwamba mambo makubwa kabisa na yenye mustakabali wa kitaifa huchukuliwa kirahisi rahisi au hupindishwa wakati mambo madogo hukemewa na kuchukuliwa hatua kubwa ya kuyakomesha kabisa. Kwa hali hii itakua ni vigumu sana kukomesha Mob Justice (kuchukua sheria mikononi).
Hukumu ya Zombe is a big scandal, shame and mockery of the Justice system in our country but a tainted corruption and grave recklessness, lack of profesionalism, ignorance of the Attorney General Office, investigation and Police Department.