Hukumu ya Zombe: Aachiwa!

Hukumu ya Zombe: Aachiwa!

hii nji imeshauzwa wenye nazo na wenye madaraka ndio walio juu ya sheria
 
Sheria wakuu imefanya kazi yake watu mtapinga lakini Jaji ndo huyo mwamuzi wa mwisho.
 
tunasubiri updates!.....................

Updates ni kwamba Zombe na wenzake wote nane wameachiwa huru kwa kukutwa hawakuwa na makosa waliyoshitakiwa nayo.Kama hilo ni kweli mustakabali wa wale waliouawa msitu wa pande unakuwa vipi?
 
Updated by Invisible:

Watuhumiwa wote wameachiwa hawana hatia!

It is true. Nimesikia kwa Radio Tanzania, kipindi cha harakati kuwa Zombe na wenzake wameachiwa na JAJI MASATI amesema waliohusika watafutwe waletwe kwa mashitaka lakini sio hawa. Ajabuuu
 
Watanzania bana, sasa mnadhani wapi haki itapatikana?

Dah, Mahakama Kuu haiwezi kufanya kosa, mashtaka yalikuwa dhaifu na mtuhumiwa sasa anarajea mtaani kukabiliana na vyombo vya habari vilivyomchafua jina... Kaazi kwelikweli
Well said mkuu,tatizo watu tuna kawaidam ya kukimbilia kumllamikia/kumhukumu Jaji/Hakimu badala ya kuangalia udhaifu wa mashtaka yenyewe(ikiwa ni pamoja na ushahidi dahifu),kwa hali ilivyokuwa ilikuwa si kitu cha ajabu kwa Abdallah Zombe na wenzake kuachiwa huru.Cha msingi tusubiri tu upande wa mashtaka(serikali) utasema nini/utachukua hatua gani juu ya hukumu hii....
 
Anynews from High court?

Updated by Invisible:

Watuhumiwa wote wameachiwa hawana hatia!

Kwa maana hiyo wale wafanyabiashara wa madini walijiuwa wenyewe! Si shangai wananchi wanapoamua kuuwa vibaka mtaani, bado kidogo wataanza shughulikia fisadi.
 
Basi EPA, Richmond kina Mramba hakuna kesi hapo.

Liyumba atakuwa huru muda si mrefu
 
hii nji imeshauzwa wenye nazo na wenye madaraka ndio walio juu ya sheria
Hivi mlitaka iweje? Kama Zombe hakuua na ushahidi hautoshelezi, mnataka ahukumiwe kwa sheria ipi? Mashtaka ni dhaifu wakuu!

Angalia hata nilichogusia kuhusiana na kesi ya kina Mramba... Kesi hiyo pia inaelekea ni dhaifu tu!

Kesi ya kina Mramba: Serikali itashindwa!

Inaweza ikawa inawauma wengi lakini sheria ni msumeno...
 
Acha kuwaingiza mkenge wenzio wewe,waingie mtaani kufanya nini????,haki haidaiwiw hivyo aiseee

Haki inadaiwa kivyoyote wewe, hata kumuua jaji Masati....kumbuka watu wamepoteza ndugu zao kwa ulafi wa Zombe, na ni dhahiri bado tunaletewa za kuleta. Acha woga, mafisadi hawana msalie mtume.
 
Zamani nilikuwa nuikisikia kuwa sheria ni msumeno nilikuwa najua kuwa inakata kotekote...
Kumbe nilikuwa nakosea kabisa...
Maana halisi ni kwamba sheria inayumbayumba kama msumeno
 
Poleni wadau wote mliokuwa mnafuatilia kwa makini kesi hii..pole na kwangu pia kwa sa babu nimejikuta naumia bila kutegemea!!!
Tanzania oyeeeeeee....!
m out!
 
Tanzania has lost its map, it has no clue to where it is heading. The leader is even more confused than the followers.
 
Lakini si aliyeua ni Koplo Saad ambaye hayupo? Vyombo vya habari na wamiliki wake wakae mkao wa kuanza kulumbana na Zombe kwa kudaiwa fidia

Kweli mkuu.
Lakini kwa nini jaji Masati aliahirisha kesi hadi Koplo Lema akafariki? Kwani kesi ingepelekwa Muhimbili asingetoa ushahidi wake?
Kwa ushahiri uliotolewa mahakamani ni kweli Zombe na wenzake hawakuonekana na hatia. Hivi kwa mwendo huu itakuwa kosa kuamini kwamba kazi ya kutengeneza ushahidi labda ilimhusisha na jaji mwenyewe?
 
Sasa wale waliokuwa wanamvimbia macho itakuwaje ? na je atarudi kazini kweli ? akirudi si ndio ataua sana, hii kazi kama habari ndio hizi bac wataua sana maana wanajua mwisho wa siku wapo nje na kulipa kisasi kama kawa
 
Zombe huyo nje na wenzake!!!!. Wote wametolewa kwa mlango wa nyuma kwa magari mawili ya polisi landcriser p/up wakiwa wanashangilia kama mashabiki wa mpira waliopanda p/up. Huku magari matatu ya polisi na silaha kali wakiwalinda. Kote kulikuwa kumemwagwa askari kanzu nje na ndani, magari ya FFU na gari la maji washawasha!!!Kwa mtizamo wa kiundani huo tangu asubuhi ule ulinzi ualiashiria mamamuzi ya kuwachukiza wananchi.

Wenye vyombo vya habari jiandaeni kwa kesi za fidia, serikali jiandae kwa fidia!!!
Je sasa, ni nani aliwaua wale wazalendo?? Je ni mtu mmoja Saadat aliweza kuwabeba wote na kuwapeleka pande bila msaada na kuwalipua??? Jamani sijaelewa hizi mnazosema sheria!!! Ila kuna jambo, subirini na yule mzee Mahenge atajibu, tena kwa kishindo, aliapa!!!!! Msiniulize atajibu kivipi, ila atajibu.
 
mmh! hii kali sana, hata yule aliyekiri kuona mauaji yakifanyika na kwamba yeye ndo alibeba maiti kupeleka mhimbili na hakutoa taarifa popote mpaka alipobanwa selo naye yupo huru!
 
Wadau atakayebahatika kupata copy ya hukumu tunaomba awasilishe! Inawezekana waliokuwa karibu na mahakama wamerekodi hukumu (audio) si vibaya wakaiweka tukapata nafasi ya kusikiliza yaliyojili
 
Back
Top Bottom