Hukumu ya Zombe: Aachiwa!

Hukumu ya Zombe: Aachiwa!

Updated by Invisible:

Watuhumiwa wote wameachiwa hawana hatia!


Hii ndio Tanzania, kuna watu miongoni mwetu watakula wali hadi wanakufa; kuna watu watakula ukoko hadi wanakufa na kuna watu watakula matandu hadi wanakufa.

Mwenye nacho ataongezewa daima dumu na asiekuwa nacho ataendelea kunyang'anywa hata kile kidogo alichokipata.

Kisingizio tunaambiwa ushahidi uliotolewa hauna nguvu za kuwatia hatiani moja kwa moja, ndio yale yale "... marehemu alikuwa ndio mwenye makosa...". Hatujajua hukumu imesemaje kuhusu wale ndugu zetu waliouawa. Je, WALIKUWA NI MAJAMBAZI???

Ila tukumbuke UBAYA WOTE HULIPWA HAPA HAPA DUNIANI, na watalipwa, watalipwa, watalipwa kwa waliyoyachuma kwa mikono yao kabla hawajarudishwa kaburini wakiwa hawana kauli.
 
Impact ya hii kesi itakuwa mbaya sana kwa jamii, kwanza polisi wataendelea kuua kadri wanavyoona inawafaa. Kumbuka baada ya kuwaua hawa, wameua vijana 2 Arusha, 1 (dereva taxi) Ubungo Dar, wa 2 Mbeya (Tunduma na Kyela). Sasa wanaelekea wapi?

Kwa upande wa wananchi, hii inajenga hoja ya kummaliza mhalifu bila kusubiri polisi.

Kuna kipindi nilikwenda Mbeya, nikasimuliwa kwamba ukikamatwa unaiba nchini Zambia na ikajulikana wewe ni Mtz basi wanakuua mara moja bila kusubiri polisi, kwakuwa utashinda kesi ikipelekwa mahakamani.
 
Kwa mtaji huu akina Chenge, Jitu Patel, Mramba, etc wote wataishia hivi hivi
 
Hahaha...

- Ni mapenzi ya Mungu
- Hatuna jinsi, imeshakuwa tu
- Sasa mimi nifanyeje?
- Wakubwa washaamua bwana...
- Mungu atatusaidia tuu...

We acha tu!


HAKUNA MATATA
MAMBO POWA
TAMBARARE

unalala, unaamka siku zinaenda, hatujiandikshi kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, hatupigi kura tunazeeka tunaexpire wengine watakuja, hatuwaambii haki zao wanakuja na maneno mengine misleading and misguided yanayotukuza unyonge

Usipime
shwari
fresh
waaaa
and the days go on
 
Maskini Nchi yangu .Feleshi alikuwa kwenye panel hii baadaye akaja akawa DPP .Leo anashindwa kesi Mahakamani akiwa kwenye Tume ile na leo DPP damu ya mnyonge imemwagika .Hapa nadhani kuna siasa na CCM wataandhibiwa tu .
 
Jamani kwa nini hatuachii mahakama ifanye kazi yake?? ninyi humu kwani ni mahakimu au majaji?? kujua sana sheria sio maana yake kukosoa kila hukumu itakayotolewa mahakamani, wewe hata kama ukiwa profesa wa sheria but ukiwa mahakamani lazima ukubali maamuzi ya mahakama otherwise kuna mahakama ya rufaa ambayo kazi yake ni kusikiliza na kutoa hukum upya kesi iliyotolewa maamuzi mahakama kuu.
Tuache kubwabwaja hapa, tunaipotosha jamii kabisa, coz siku hiz kila mtu anajua kama JF ni one of the reliable source of information kwa vyombo vya habari vya kibongo. Watakuja kuandika huko kama JF watu wamesema kwamba zombe kapendelewa!!
Naomba kuwasilisha
 
Sina cha kusema zaidi ya kukili wazi kuwa sheria imechukua mkondo wake.

Upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha mashitaka yao.

lakini kuna nafasi kama upande wa mashitaka haujarithika na hukumu basi wana haki kisheria kkata rufaa
 
Jamani kwa nini hatuachii mahakama ifanye kazi yake?? ninyi humu kwani ni mahakimu au majaji?? kujua sana sheria sio maana yake kukosoa kila hukumu itakayotolewa mahakamani, wewe hata kama ukiwa profesa wa sheria but ukiwa mahakamani lazima ukubali maamuzi ya mahakama otherwise kuna mahakama ya rufaa ambayo kazi yake ni kusikiliza na kutoa hukum upya kesi iliyotolewa maamuzi mahakama kuu.
Tuache kubwabwaja hapa, tunaipotosha jamii kabisa, coz siku hiz kila mtu anajua kama JF ni one of the reliable source of information kwa vyombo vya habari vya kibongo. Watakuja kuandika huko kama JF watu wamesema kwamba zombe kapendelewa!!
Naomba kuwasilisha


Umeingia kwa kazi maalumu ama ndiyo wafuasi wa Zombe ? Inakuaingia akili kweli wale jamaa hawana hatia ? OK wao hawana hatia na je wale walio uawa Jaji kasemaje ?
 
Jamani kwa nini hatuachii mahakama ifanye kazi yake?? ninyi humu kwani ni mahakimu au majaji?? kujua sana sheria sio maana yake kukosoa kila hukumu itakayotolewa mahakamani, wewe hata kama ukiwa profesa wa sheria but ukiwa mahakamani lazima ukubali maamuzi ya mahakama otherwise kuna mahakama ya rufaa ambayo kazi yake ni kusikiliza na kutoa hukum upya kesi iliyotolewa maamuzi mahakama kuu.
Tuache kubwabwaja hapa, tunaipotosha jamii kabisa, coz siku hiz kila mtu anajua kama JF ni one of the reliable source of information kwa vyombo vya habari vya kibongo. Watakuja kuandika huko kama JF watu wamesema kwamba zombe kapendelewa!!
Naomba kuwasilisha

Sawa, mahakamani kwa jaji Masati hawana hati, na kwetu wananchi je?
 
Zombe alipokamatwa alikuwa tayari amepangiwa kituo kipya cha kazi na alikuwa ni RPC Rukwa. Sasa itabidi RPC wa sasa kule Rukwa aondolewe ili Zombe arudi kazini mara moja. Huyo aliyepo sasa atapangiwa kazi nyingine.
 
Hivi wananchi pia tunaweza kumuingiza mtu hatiani?? Nilikua sijui!!


Leo una hoji haya kwa kuwa una furaha kuna siku yatakufika utarudi hapa hapa JF kulalama .Mtu mwenye akili timamu hawezi kuelewa kesi nzima inakuwa watu wote wanakuwa hawana hatia hakika hata kama ni sheria na mkondo .Ila nakupa angalizio yatakufika si siku nyingi na uwe mkweli uje JF useme.Endelea kufurahia pamoja na Zombe .
 
Kesi ya Zombe na hata zile za EPA na za akina Mramba ni viini macho tu. CCM wanatupiga changa la macho.
 
Haki imetendeka hata kama ni mwarobaini. Tatizo ni jinsi ya kuandaa mashitaka.
 
Leo una hoji haya kwa kuwa una furaha kuna siku yatakufika utarudi hapa hapa JF kulalama .Mtu mwenye akili timamu hawezi kuelewa kesi nzima inakuwa watu wote wanakuwa hawana hatia hakika hata kama ni sheria na mkondo .Ila nakupa angalizio yatakufika si siku nyingi na uwe mkweli uje JF useme.Endelea kufurahia pamoja na Zombe .

Mi nimetoa maoni yangu kuhusu hukumu ya leo, kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni, nadhani hat wewe pia una uhuru wa kufanya hivyo, sasa tena mbona umeanza vitisho?? Au na wewe una undugu na marehemu wale wa mahenge??
 
Jamani mwenye nakala ya hukumu atuwekee hapa tuichambue!!

Kama kweli wameshindwa kuwa na hatia... basi tunataka kuona haki ya wafiwa inapatikana kwa namna moja au nyingine...

Kwa nini jeshi la polisi lisishtakiwe kwa corporate manslughter kama hakuna ushahidi wa kutosha? Kama sheria ya corporate manslaughter haipo Tanzania basi huu ndio wakati muafaka wa kuileta...

Pia tulete sheria ya double jeopardy ili kama ikiwezekana hao jamaa ambao walikuwa wanadaiwa kuwauwa raia wema waje warudishe tena kujubu wajibu wao katika kukamatwa kwa wafanyabiashara waliouwawa...
Pia naona ni wakati muafaka wa timu nzima ya adminstration ya jeshi ijiudhuru kuanzia masha na mwema na wengine wote waliohusika kwa namna moja au nyingine...yote haya katika jina la haki itendeke...

Yawezekana sasa Zombe akawageuzia kibao ili wampe fidia...
Ni uchungu sana na hawa prosecution wetu wanaokwenda mahakamani kwa hearsay evidence... nao pia inafaa wajiudhuru kwa kushidwa kutoa haki ipasavyo... ije team nyingine ya ma-prosecution na ku-review evidence zote na kesi ianze upya... mapungufu yote yaliyojitokeza yazibwe...
Ni haya tu wakuu
 
Au na wewe una undugu na marehemu wale wa mahenge??
Duuh, kumbe hapa hadi uwe na undugu!? Hebu nikae pembeni mimi nisiye ndugu wa Zombe, marehemu, Jaji Masati na mwendesha mashtaka !!!
 
Jamani mmesoma hukumu ya jaji ? Umekosekana ushahidi wa kumtia hatiani zombe.
Tunaomba hukumu tuisome ndiyo tuhukumu. Vinginevyo inaonekan sisi ni watu wa kuropoka bila kuwa na ushahidi.
Kama watu makini ilitakiwa hukumu ya zombe iwepo hapa ndio tuweke comments.
 
haki imetendeka hata kama ni mwarobaini. Tatizo ni jinsi ya kuandaa mashitaka.
waendesha mashitaka wanalipwa laki tatu na hawana vitendea kazi wataweza kuendesha kesi kama hizi?
 
Jamani mmesoma hukumu ya jaji ? Umekosekana ushahidi wa kumtia hatiani zombe.
Tunaomba hukumu tuisome ndiyo tuhukumu. Vinginevyo inaonekan sisi ni watu wa kuropoka bila kuwa na ushahidi.
Kama watu makini ilitakiwa hukumu ya zombe iwepo hapa ndio tuweke comments.

Jamani Zombe ilikuwa ni rahisi kutoka, lakini hawa akina Bageni wanao sema waliua watu Sinza posta, ndo namshangaa Jaji na mahakama yake. kweli mnyonge hana haki, tunaweza kuzalisha suicide bombers.
 
Back
Top Bottom