Hukumu ya Zombe: Aachiwa!

Hukumu ya Zombe: Aachiwa!

Wakuu muhimu ni kwamba ushahidi ulijitosheleza? Tuache kuhukumu kwa kutumia magazeti na kutanguliwa na hisia zetu.
 
My god we are going to die all of us kwa hali hii dunia imekwisha iliyobaki tusubiri kiama tuuuuuuuuuuuuuuuuuuu
 
Hiyo ndio bongo nyumbani jamani.....tufanyeje sasa......kwetunikwetu tuuu! Ile kesi kama Zombe angepatikana na hatia ingekuwa miujiza....haiwezekani polisi wafanikishe upelelezi makini ili kumfunga kiongozi wao....wakati wanajua mambo hayo siku zote yanafanyika.
 
Last edited:
Kesi inawezekana ilijawa na jazba za kisiasa na kukurupuka yote yanawezekana hatia au sio hatia, ila kinachoonekana wengi hawana imani na judiciary system na hii ni hatari sana. Je wapi tupaamini. Mimi mwenyewe siamini mahakama za ikulu na mazingaombwe. Yote yanawezekana.
 
Lakini si aliyeua ni Koplo Saad ambaye hayupo? Vyombo vya habari na wamiliki wake wakae mkao wa kuanza kulumbana na Zombe kwa kudaiwa fidia
 
Wakuu muhimu ni kwamba ushahidi ulijitosheleza? Tuache kuhukumu kwa kutumia magazeti na kutanguliwa na hisia zetu.

Ushahidi?!!! Nngoja ukifika ahera koplo Lema atakueleza ushaidi unavyopotezwa na maporisi kwa juhudi kubwa.
 
Kuna haja ya watanzania kujichukuliwa sheria mkononi, maana kwenye vyombo vya sheria haki haitendeki. Siwezi kuamini kama p
 
okkk now i get image in ma head why koplo lema alikuwa shahidi muhimu sana katika kesi hii na wakamuondoa!
 
BREKING NYUUUZZZ:zombe na wenzake waachiwa huru

Kitendawili kilichotegwa takriban miaka mitatu iliyopita na aliyekuwa mkuu wa upelelezi wa jeshi la polisi,Mkoa wa dar es salaam (ACP) Abdallah Zombe na wenzake wanane wameachiwa huru sasa hivi katika mahakama kuu ya Tanzania.

source-Michuzi
 
Watu tumekaa presha juu juu kumbe mtu mwenyewe kaachiwa.Asilimia kubwa ya wanajamii humu ndani vichwani tulijua kama sio kunyongwa basi kasamehewa sana maisha matokeo yake TAFAUTI
 
Mwendesha mashtaka should do something otherwise ajiuzulu. maana yake hapa inaonyesha uwezo mdogo katika ofisi yake
 
okkk now i get image in ma head why koplo lema alikuwa shahidi muhimu sana katika kesi hii na wakamuondoa!

bado mkubwa picha nyingine nyingi tu utazipata kichwani zinakuja!
Chenge nae yuko huru hata kabla ya hukumu,sawa wananchi?!
Watanzania watakuwa hawana tena imani na mahakama...
 
***BREAKING NEWS: Watuhumiwa wote kesi ya ZOMBE waachiliwa huru!!!***


Monday, 17 August 2009 12:26

Hukumu iliyosomwa na JAJI Salum Masati iliyochukua takribani masaa sita, leo katika Mahakama Kuu ya Tanzania imewaachia huru watuhumiwa wote saba katika kesi ya mauji ya wafanya biashara wa madini na dereva taksi mmoja, iliyokua ikiwakibili aliyekuwa Afisa upelelezi wa mkoa wa Dar es Salam Abdallah Zombe na wenzake.

Zombe na wenzake walikuwa wanatuhumiwa kwa kosa la kufanya mauaji kwa kukusudia Sabinus Chigumbi, maarufu kama Jongo na ndugu yake Ephrahim Chigumbi na Mathias Lunkombe ambao ni wafanyabiashara wa Mahenge. Mwingine ni dereva teksi wa Manzese jijini Dar es salaam, Juma Ndugu.

Akisoma hukumu hiyo JAJI Masati amesema kuwa hakuna ushahidi wa moja kwa moja unaonesha kuwa watuhumiwa hao walihusika katika kufanya mauaji ya wafanyabiashara hao. Hivyo Mahakama haikuweza kuwatia hatiani.

Watu wengi wali waliokuwepo Mahakamani wameonesha kutoridhishwa na hukumu hiyo, hali ambayo inabakisha kitendawili juu ya hatima ya maisha ya waliokua watuhumiwa katika kesi hiyo wakiwa uraiani.
 
Back
Top Bottom