Hii hukumu ya Bihalamulo nadhani imebadilishwa, kwani hakuna sababu za kuichelewesha namna hii. Huenda jaji alikuwa ametupilia mbali madai ya walalamikaji, sasa ameambiwa atakiona cha mtema kuni iwapo naye ataendeleza wimbi hilo la kuiangusha CCM, ama alikuwa ametoa hukumu ya ki-Arusha-Arusha lakini baada ya kugundua kuwa majaji wenzake wanatoa hukumu za tofauti akaamua naye abadili kwendana na sawa na majaji wenzake. Uamuzi wowote utakaotolewa leo unaweza kuwa umefikiwa katika hizi dakika za mwisho mwisho tu.