Mparee2
JF-Expert Member
- Sep 2, 2012
- 2,591
- 4,279
Kimsingi mtoto aliyefaulu vizuri aende Form six ila wale wenye pass za kati na chini wapitie hivyo vyuo vingine.Kwa Sasa Kuna ushawishi mkubwa wa serikali eti wanaomaliza kidato Cha nne hakuna maana ya kwenda A level bali vyuo tu.
Ni hivi ndugu zangu huwezi kuwa na thinking capacities kwa ku abandon A level kwa kuona form four inatosha. Tunajenga kizazi Cha kufikiria ajira tu bila uwezo wowote.
Mfano huwezi sema eti unafanana na na mtu aliyesoma PCM akaenda kusoma electronics na wewe uliyesoma form four tu ukaenda kusoma DIT electronics haiwezekani.
Kwanza form four hasomi differentiation, integration Wala complex namba. Sasa huo huo uwezo wa kuanalyse mambo makubwa anautoa wapi?
Elimu ya Form SIX hujengea mtoto uwezo wa kujiamini, kusimamia maamuzi yake na kuweza kujisimamia kwa umri wake. Ukitaka ujue tofauti uliza ma HR wanao wafanyia Interview ya kazi watakuambia tofauti....