Huawei kurusha satelaiti mbili za 6G mwezi Julai

Sam Gidori

Senior Member
Sep 7, 2020
165
414
shutterstock_1559934065-e1607673218292.jpg

Kampuni ya Teknolojia ya Huawei inatarajiwa kurusha satelaiti mbili angani mwezi Julai, 2021 ikilenga kuingia katika teknolojia ya intaneti ya 6G.

Kampuni hiyo ya China imekuwa mstari wa mbele duniani kuboresha kasi ya upatikanaji wa mtandao wa intanet, hii ikiwa ni mara ya pili kurusha satelaiti angani kwa lengo la kujaribisha teknolojia hiyo.

Teknolojia ya 6G inatarajiwa kuwa na kasi mara 100 ya ile ya 5G. Kwa wastani, mtandao wa 5G una kasi ya juu zaidi ya Gigabits 20 kwa sekunde (Gbps) na kasi ya wastani ya 100+ Megabits kwa sekunde (Mbps).

Kampuni hiyo inatarajiwa kuzindua rasmi mtandao huo pamoja na kuweka miundombinu ya mtandao wa 6G ifikapo mwaka 2030. Huawei inatarajiwa pia kutoa maelezo kuieleza dunia teknolojia ya 6G ni nini hasa.

Hii inakuja wakati China ikijitutumua katika matumizi ya mtandao wa 5G, ikitajwa kuwa na watumiaji milioni 202 mwishoni mwa mwaka jana, idadi hiyo ikitarajiwa kuongezeka kufikia watumiaji milioni 822 ifikapo mwaka 2025.

Kwa sasa, Korea Kusini ndio nchi inayoongoza kwa matumizi ya mtandao wa 5G, ikiwa na asilimia 67 ya watumiaji wa mtandao huo, Marekani ikiwa na asilimia 55 na Japan ina asilimia 50. Asilimia 3 tu ya simu za mkononi duniani ndio zimeunganishwa na teknolojia ya 5G, nchi za bara la Asia zikiwa kileleni.

Wakati dunia ipo mbioni kwenda teknolojia ya 6G, Afrika bado inapambana na teknolojia ya 3G! Ripoti ya Mtandao wa Uchambuzi wa Teknolojia wa GSMA unasema kuwa takriban asilimia 51 ya simu za mkononi barani Afrika zimeunganishwa na teknolojia ya 3G.

Ingawa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara zimeanza kujiongeza kufikia teknolojia ya 5G, teknolojia ya 3G bado itaendelea kutawala katika nchi hizo kwa kipindi kirefu mbeleni. Mapema mwezi Aprili, Kenya ilikuwa nchi ya pili barani Afrika kujiunga na teknolojia hiyo baada ya Afrika Kusini, ikitajwa GSMA kuwa “hatua kubwa kwa Afrika kuelekea dunia ya 5G.”

Chanzo: Insidetelecom
 
1. kwanza 6G haitoki kwenye satelite, ni kama unasema Huawei katengeneza Baiskeli za kwenda zanzibari, satelite ni mfumo mwengine wenye speed ndogo na ping kubwa, tayari 4g ipo faster kushinda hata low orbit satelite sembuse 6G?

2. 6G ni standard, haijulikani itakuwa vipi mpaka makampuni yakae yaitengeneze, huwezi sema sasa hivi kampuni ina tengeneza 6G.
 
1. kwanza 6G haitoki kwenye satelite, ni kama unasema Huawei katengeneza Baiskeli za kwenda zanzibari, satelite ni mfumo mwengine wenye speed ndogo na ping kubwa, tayari 4g ipo faster kushinda hata low orbit satelite sembuse 6G?

2. 6G ni standard, haijulikani itakuwa vipi mpaka makampuni yakae yaitengeneze, huwezi sema sasa hivi kampuni ina tengeneza 6G.
Si bora Angesema Xiomi ungemsaport😂😂😂
 
Si bora Angesema Xiomi ungemsaport😂😂😂
Xiaomi hayupo kwenye biashara ya telecom,

Website za Tech nyingi zimekuwa matarumbeta ya kusambazia propaganda. Mtafute mtu yoyote mwenye basic kidogo tu za mambo ya network anajua satelite ipo slow kiasi gani,

Elon Musk Ana trend sana na internet yake ya satelite pamoja na kufanya wonders alichoambulia kwenye starlink ni ping ya Around 30ms, na download speed around 40 mpaka 50mbps. Hivi vyote unapata kwenye mitandao yote ya 4g hapa Tz
starlink-tests-980x785.jpg


Then anatokea mtu anasema wamepeleka 6G kwenye satelite? Tayari unaona hapa unapigwa kamba ya nguvu
 
Acha bas bro star link wanatumia sattelite na bael speed yao iko faster comlare to hyo 4g yako unayl ongelewa kama ulifundishwa darasan haimaanishi dunia itaabk kama ilivyo andikwa kaanagalia mfano neurolink project zake zipoje utakuja gundua ukimwambia mtu atabisha kulinga na alivyo kalilishwa
1. kwanza 6G haitoki kwenye satelite, ni kama unasema Huawei katengeneza Baiskeli za kwenda zanzibari, satelite ni mfumo mwengine wenye speed ndogo na ping kubwa, tayari 4g ipo faster kushinda hata low orbit satelite sembuse 6G?

2. 6G ni standard, haijulikani itakuwa vipi mpaka makampuni yakae yaitengeneze, huwezi sema sasa hivi kampuni ina tengenezac
 
Acha bas bro star link wanatumia sattelite na bael speed yao iko faster comlare to hyo 4g yako unayl ongelewa kama ulifundishwa darasan haimaanishi dunia itaabk kama ilivyo andikwa kaanagalia mfano neurolink project zake zipoje utakuja gundua ukimwambia mtu atabisha kulinga na alivyo kalilishwa
Unaweza tetea hoja yako kwa ushahidi? Mfano ukaleta speed test ya starlink ikiipita 4g ya Tanzania?

Voda kwangu hapa ping ni 17ms
Screenshot_20210501-201036.png


Nakuruhusu unaweza Google pia starlink ikiwa na ping ndogo zaidi?

Starlink ipo faster against satelite wenzake, mpinzani wake kwa sasa ni 3g, ila inaitwa na 4g na 5g ndio kabisa hata haifananishiki.
 
1. kwanza 6G haitoki kwenye satelite, ni kama unasema Huawei katengeneza Baiskeli za kwenda zanzibari, satelite ni mfumo mwengine wenye speed ndogo na ping kubwa, tayari 4g ipo faster kushinda hata low orbit satelite sembuse 6G?

2. 6G ni standard, haijulikani itakuwa vipi mpaka makampuni yakae yaitengeneze, huwezi sema sasa hivi kampuni ina tengeneza 6G.
Mkuu SpaceX anasambaza hundreds of Starlink Sat ktk low earth orbit na speed ipo vizuri pengine ni over hiyo 4g ulosema!

Kuna kitu gani hapo ambacho pengine labda sijakielewa vizuri?
 
Mkuu SpaceX anasambaza hundreds of Starlink Sat ktk low earth orbit na speed ipo vizuri pengine ni over hiyo 4g ulosema!

Kuna kitu gani hapo ambacho pengine labda sijakielewa vizuri?
Lete ushahidi wa hio speed mkuu, nimetoa yangu latency ni 17ms na ni huku Tanzania mwisho Wa Dunia,

Nchi kama za Scandinavia, Korea, Japan etc 4g theoretically inazidi 1gbs na wanayo pata user average inazidi 100mbps, mfano korea mwezi wa tatu ni around 170mbps (according to ookla), na starlink average ni 50 mpaka 80 (hao hao Ookla),

Na kikubwa kabisa ni ping, ping za 30ms tulikuwa tunazipata tangu Enzi za 3g, kwenye 4g ikashuka chini 20ms na 5g ni single digit chini ya 10. Fiber hizi za kina Zuku ni 1ms ama 2ms tu, ilichofikia starlink ni between hio 3g na 4g bado haijafika level za 4g

Inachoaifiwa ni kwamba ina speed kuliko satelite nyengine itafaidisha watu wa vijijini, ila watu walio mjini na wenye access ya mobile data ama fiber haiwahusu.
 
1. kwanza 6G haitoki kwenye satelite, ni kama unasema Huawei katengeneza Baiskeli za kwenda zanzibari, satelite ni mfumo mwengine wenye speed ndogo na ping kubwa, tayari 4g ipo faster kushinda hata low orbit satelite sembuse 6G?

2. 6G ni standard, haijulikani itakuwa vipi mpaka makampuni yakae yaitengeneze, huwezi sema sasa hivi kampuni ina tengeneza 6G.
Mkuu,

Hakuna kinachoshindikana with Technology, wala usishangae.

Ukiangalia drivers za 5G, kimsingi kuna some research topics ambazo haziko kwenye scope of 5G na wataalamu wana zi consider Kama 6G.
Kitu kama Terahertz (THz) ni Mfano Mzuri.
5G standards ambazo zinaendelea.kuwa developed kwa sasa zime focus kwenye Matumizi ya spectrum below 52.5 GHz.
Spectrum 114 GHz kwenye Road map ya 3GPP 5G Release, ni Relaeses 18–21 au za Mbele.
Spectrum juu ya 114 GHz haijakuwa assigned kwa any release.

Kimsingi Matumizi ya Frequencies 140 GHz and above for cellular communications yako out of scope ya 5G.

Hizi ndio zinaitwa Terahertz (THz) frequencies.

Zina unique properties za kuwezesha applications mpya na za kuvutia , for example adding sensing to wireless networks.

Research kwenye hili bado ziko kweny early phases, hardware zinazotakiwa kuwezesha kuileta THz commercially bado sana, in terms of chips, Mfano kwa sasa Qualcom ni one of the leading 5G Chips Manufacturers.

Researchers, especially kwenye institutions kama HUAWEI and Acdemic Labs zitawezesha (THz) hili with time.

Usishangae
 
Mkuu,

Hakuna kinachoshindikana with Technology, wala usishangae.

Ukiangalia drivers za 5G, kimsingi kuna some research topics ambazo haziko kwenye scope of 5G na wataalamu wana zi consider Kama 6G.
Kitu kama Terahertz (THz) ni Mfano Mzuri.
5G standards ambazo zinaendelea.kuwa developed kwa sasa zime focus kwenye Matumizi ya spectrum below 52.5 GHz.
Spectrum 114 GHz kwenye Road map ya 3GPP 5G Release, ni Relaeses 18–21 au za Mbele.
Spectrum juu ya 114 GHz haijakuwa assigned kwa any release.

Kimsingi Matumizi ya Frequencies 140 GHz and above for cellular communications yako out of scope ya 5G.

Hizi ndio zinaitwa Terahertz (THz) frequencies.

Zina unique properties za kuwezesha applications mpya na za kuvutia , for example adding sensing to wireless networks.

Research kwenye hili bado ziko kweny early phases, hardware zinazotakiwa kuwezesha kuileta THz commercially bado sana, in terms of chips, Mfano kwa sasa Qualcom ni one of the leading 5G Chips Manufacturers.

Researchers, especially kwenye institutions kama HUAWEI and Acdemic Labs zitawezesha (THz) hili with time.

Usishangae
Nani kakaa akasema Thz ni 6G? Matumizi ya binadamu 2030 yatakua ni yapi? Hivi vitu sipangi mimi na wewe ama Huawei mwenyewe Bali ni kundi la makampuni, serikali, wadau muhimu etc bila ushahidi siwezi kuelewa, hasa dunia hii ya leo iliojaa propaganda na uongo.

Mfano nakupa, 5G ililenga mambo haya walipoeka standard kwa mara ya kwanza
1. Kuongeza capacity, hasa kwenye majiji makubwa kwenye watu wengi na vifaa vingi vitakavyotumia 5g
2. For the first time network yake ikawa sio mobile first ika target magari ya kujiendesha yenyewe, mitambo na viwanda, IOT etc
3. Ping ndogo ili kufanikisha ya juu mfano machine za hospital, Gari za kujiendesha zenyewe etc
4. Speed kubwa ya internet etc

Makampuni kama Huawei, Nokia, Ericson, Qualcomm etc wakawa wanatengeneza 5g kutokana na Guidelines hizo hapo juu.

Kunaweza kukatokea kitu 6g kikawa kitu chengine kabisa, na watu wengi mna Angalia speed tu, tuna matatizo makubwa kuliko speed.

Mfano 5g ina speed zaidi 1Gbps, je nani humu jukwaani Ana simu ambayo inazidi hiyo speed? Pengine hakuna ama wawili watatu, same kwa pc, hivyo unaona speed sio priority sana

Ila ping? Kila mtu a nahitaji, capacity? Wote tu nahitaji ukiwa sehemu ina watu wengi speed ina drop kuliko maelezo,

Mfano kwangu mimi wakigundua backbone nzuri let's say ma exabyte ya data yanapita waka fanya mobile data iwe unlimited usilipie vifurushi ni much better, ningependa 6g ifocus huko kuliko.

Mkuu conclusion 6g haina standard, kuna vision tu, mpaka wakae waamue 6g ni nini.
 
Nani kakaa akasema Thz ni 6G? Matumizi ya binadamu 2030 yatakua ni yapi? Hivi vitu sipangi mimi na wewe ama Huawei mwenyewe Bali ni kundi la makampuni, serikali, wadau muhimu etc bila ushahidi siwezi kuelewa, hasa dunia hii ya leo iliojaa propaganda na uongo.

Mfano nakupa, 5G ililenga mambo haya walipoeka standard kwa mara ya kwanza
1. Kuongeza capacity, hasa kwenye majiji makubwa kwenye watu wengi na vifaa vingi vitakavyotumia 5g
2. For the first time network yake ikawa sio mobile first ika target magari ya kujiendesha yenyewe, mitambo na viwanda, IOT etc
3. Ping ndogo ili kufanikisha ya juu mfano machine za hospital, Gari za kujiendesha zenyewe etc
4. Speed kubwa ya internet etc

Makampuni kama Huawei, Nokia, Ericson, Qualcomm etc wakawa wanatengeneza 5g kutokana na Guidelines hizo hapo juu.

Kunaweza kukatokea kitu 6g kikawa kitu chengine kabisa, na watu wengi mna Angalia speed tu, tuna matatizo makubwa kuliko speed.

Mfano 5g ina speed zaidi 1Gbps, je nani humu jukwaani Ana simu ambayo inazidi hiyo speed? Pengine hakuna ama wawili watatu, same kwa pc, hivyo unaona speed sio priority sana

Ila ping? Kila mtu a nahitaji, capacity? Wote tu nahitaji ukiwa sehemu ina watu wengi speed ina drop kuliko maelezo,

Mfano kwangu mimi wakigundua backbone nzuri let's say ma exabyte ya data yanapita waka fanya mobile data iwe unlimited usilipie vifurushi ni much better, ningependa 6g ifocus huko kuliko.

Mkuu conclusion 6g haina standard, kuna vision tu, mpaka wakae waamue 6g ni nini.
Jua even before 3GPP hawajaja na 5G standards the so called washikadau, am talking about Vendors, tayari walishakuja na Model / Proposal zao za 5G na nyingi zikawa adopted na 3GPP kama 5G release / Standard kwa Road Map.
Unataka nikupe shule ya why / drivers for 5G ?

Maana umeandika Ngonjera kibao.

FYI vendors huwaga hawangoji 3GPP waje na Standards ndio wao waanze Development, Never, watu wako lab na wame invest kwenye R&D kufikiria Mambo ya 2050.
Actually 3GPP Composition yake ime include Vendors, CSP, na Reputable Acadrmic Institutions Ulimwenguni hapa.

Hakuna Mahala nimesema THz ni 6G, ila ikiwa adopted kwenye Matumizi ya Cellular Communications itakuwa ni Next Generation.
Sasa ukitaka unaweza kusema what G will follow after 5G ni 7G na sio 6G its up to you.

Tunafundishana, ukiwa Mjuaji utakosa Mengi.

Unauliza ni Nani hapa Jukwaani ana simu yenye Speed ya 1G, childishly questions, ndio Maana nikataka kukupa shule ya Drivers, Why 5G.

FYI hizo Generations, developments zinafocus zaidi kwenye Acess / Air Interface.
Unapoleta Habari ya Backbone sijui nini ambayo Fiber optic ilishamaliza hilo tatizo Miaka Kadhaa iliyopita nakushangaa.
 
Jua even before 3GPP hawajaja na 5G standards the so called washikadau, am talking about Vendors, tayari walishakuja na Model / Proposal zao za 5G na nyingi zikawa adopted na 3GPP kama 5G release / Standard kwa Road Map.
Unataka nikupe shule ya why / drivers for 5G ?
nipe nimeangalia comment yako nzima sijaona mahala ulipotoa hipo shule
Maana umeandika Ngonjera kibao.

FYI vendors huwaga hawangoji 3GPP waje na Standards ndio wao waanze Development, Never, watu wako lab na wame invest kwenye R&D kufikiria Mambo ya 2050.
Actually 3GPP Composition yake ime include Vendors, CSP, na Reputable Acadrmic Institutions Ulimwenguni hapa.
nafahamu hili, lakini kuna kukubaliwa na kukataliwa, kipindi wanadevelop haikuitwa 5g, ilipokubaliwa tech huisika ndio ikaitwa 5g, hio satelite hadi ikubaliwe ndio itaitwa 6g, as of now sio 6g. unafkiri hakuna tech zilizokataliwa na sasa hivi sio 5g?
Hakuna Mahala nimesema THz ni 6G, ila ikiwa adopted kwenye Matumizi ya Cellular Communications itakuwa ni Next Generation.
Sasa ukitaka unaweza kusema what G will follow after 5G ni 7G na sio 6G its up to you.

Tunafundishana, ukiwa Mjuaji utakosa Mengi.
Unauliza ni Nani hapa Jukwaani ana simu yenye Speed ya 1G, childishly questions, ndio Maana nikataka kukupa shule ya Drivers, Why 5G.
sijajua mkuu una elimu gani ya computer, ila as long as hakuna storage inayomatch speed ya internet ina maana hio internet ni useless
mfano speed ya internet ni 8gbs, na wewe una hdd ikikazana sana ni 320mbps (40MBPS) hio internet haikusaidii, sababu write speed ya storage yako ni ndogo.
FYI hizo Generations, developments zinafocus zaidi kwenye Acess / Air Interface.
Unapoleta Habari ya Backbone sijui nini ambayo Fiber optic ilishamaliza hilo tatizo Miaka Kadhaa iliyopita nakushangaa.
Air ni kutoka isp kuja kwenye kifaa chako, unafikiri isp anaitoaje toka kwake na kupeleka kwenye mikonga mikuu baharini? unafikiri inaenda kwa Air pia. kunakuwa na core routers na infrastructure ambazo mimi na wewe hatuzioni kwa macho kila siku zinazoconnect na zile waya za baharini.

last time nimeona Nokia wamebreak record ya core router ilikuwa 550GBPS source hapa

most isp bado wanachezea kwenye 100GBPS, kwa speed ya 5G hao si watu 100 tu wakitumia kwa pamoja wanajaza capacity ya network? ikiwa hio 100gbps hapo ni watu 8 tu wanajaza, kwa style hio isp atakupa unlimited? watu wachache wanaweza fanya net ikawa slow.

then assume kumetokea breakthrough na hizo backbone badala ya GBPS zitoe petabyte kadhaa ama exa kwa vifaa vyetu hivi huoni kila nyumba itakuwa na internet nafuu yenye speed?
 
nipe nimeangalia comment yako nzima sijaona mahala ulipotoa hipo shule

nafahamu hili, lakini kuna kukubaliwa na kukataliwa, kipindi wanadevelop haikuitwa 5g, ilipokubaliwa tech huisika ndio ikaitwa 5g, hio satelite hadi ikubaliwe ndio itaitwa 6g, as of now sio 6g. unafkiri hakuna tech zilizokataliwa na sasa hivi sio 5g?


sijajua mkuu una elimu gani ya computer, ila as long as hakuna storage inayomatch speed ya internet ina maana hio internet ni useless
mfano speed ya internet ni 8gbs, na wewe una hdd ikikazana sana ni 320mbps (40MBPS) hio internet haikusaidii, sababu write speed ya storage yako ni ndogo.

Air ni kutoka isp kuja kwenye kifaa chako, unafikiri isp anaitoaje toka kwake na kupeleka kwenye mikonga mikuu baharini? unafikiri inaenda kwa Air pia. kunakuwa na core routers na infrastructure ambazo mimi na wewe hatuzioni kwa macho kila siku zinazoconnect na zile waya za baharini.

last time nimeona Nokia wamebreak record ya core router ilikuwa 550GBPS source hapa

most isp bado wanachezea kwenye 100GBPS, kwa speed ya 5G hao si watu 100 tu wakitumia kwa pamoja wanajaza capacity ya network? ikiwa hio 100gbps hapo ni watu 8 tu wanajaza, kwa style hio isp atakupa unlimited? watu wachache wanaweza fanya net ikawa slow.

then assume kumetokea breakthrough na hizo backbone badala ya GBPS zitoe petabyte kadhaa ama exa kwa vifaa vyetu hivi huoni kila nyumba itakuwa na internet nafuu yenye speed?
Nani kasema Satelite ni 6G ?
 
nipe nimeangalia comment yako nzima sijaona mahala ulipotoa hipo shule

nafahamu hili, lakini kuna kukubaliwa na kukataliwa, kipindi wanadevelop haikuitwa 5g, ilipokubaliwa tech huisika ndio ikaitwa 5g, hio satelite hadi ikubaliwe ndio itaitwa 6g, as of now sio 6g. unafkiri hakuna tech zilizokataliwa na sasa hivi sio 5g?


sijajua mkuu una elimu gani ya computer, ila as long as hakuna storage inayomatch speed ya internet ina maana hio internet ni useless
mfano speed ya internet ni 8gbs, na wewe una hdd ikikazana sana ni 320mbps (40MBPS) hio internet haikusaidii, sababu write speed ya storage yako ni ndogo.

Air ni kutoka isp kuja kwenye kifaa chako, unafikiri isp anaitoaje toka kwake na kupeleka kwenye mikonga mikuu baharini? unafikiri inaenda kwa Air pia. kunakuwa na core routers na infrastructure ambazo mimi na wewe hatuzioni kwa macho kila siku zinazoconnect na zile waya za baharini.

last time nimeona Nokia wamebreak record ya core router ilikuwa 550GBPS source hapa

most isp bado wanachezea kwenye 100GBPS, kwa speed ya 5G hao si watu 100 tu wakitumia kwa pamoja wanajaza capacity ya network? ikiwa hio 100gbps hapo ni watu 8 tu wanajaza, kwa style hio isp atakupa unlimited? watu wachache wanaweza fanya net ikawa slow.

then assume kumetokea breakthrough na hizo backbone badala ya GBPS zitoe petabyte kadhaa ama exa kwa vifaa vyetu hivi huoni kila nyumba itakuwa na internet nafuu yenye speed?
Dah, Hujaelewa Air Interface ?
 
Back
Top Bottom