Nashukuru sana mh Robot kwa kunipa nafasi hii ya kunikaribisha hapa jamvini ili nijitambulishe kwa wanajamvi wengine ambao ndio wenyeji wangu.Nikiwa mgeni kwenye safu hii naomba mwongozo wenu ambao kwangu nina hakika utakuwa wenye weledi kwa sababu mara zote "ugeni si kitu chema"Nawaomba munipokee kwa moyo mkunjufu ili tushirikiane katika kulisukuma gurudumu hili la
kuelimisha kwani nielewavyo mimi Tanzania itajengwa na wote wenye moyo na italiwa na wale wenye
meno.Asanteni sana.
ccm acheni maigizo , hivi mlisikia wapi kwamba nyoka akijivua gamba ataitwa mnyooo? wehu nyie, ukweli ni kwamba atakuwa nyoka yule yule, badala ya kuwafukuza chamani watu kama rostam, chenge na lowasa mnatuletea maigizo ya mchana kweupe.
Kweli CCM imejivua gamba nakua Nyoka mkali zaidi,Kama mtunza hazina wa CCM alikuwa waziri wa fedha akatolewa na wizi wa EPA na hasa Kagoda Agriculture sitaraji uchaguzi ujao kuacha kuibiwa zaidi ya maelezo.Nachofikiria wataiba wapi tena!? Kwa kuanzia Pension Fund zote,Ujenzi mkubwa unofanywa na serikali,Bank zilizo chini ya serikali,TRA kupitia misamaha na mingine mingi (Poleni Watanzania).
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.