Si kwamba JPM hashauriki kabisa, ila ana whims sana, ana summary executions sana, na mambo mengine akishayachukulia politically kubadilika ni vigumu.
Hata huko kwenye Barrick, we could have done a lot better than that with a better strategy. Hiyo USD 300 million ni kama hela ya kumdanganya mtoto kwa pipi ili uchukue jumba lake la urithi.
Hiyo setup ya Twiga siwezi kushangaa nikiambiwa ina legal technicalities ambazo zinatu disadvantage. Yani ikawa kama vile Barrick wananunua insurance ya kutupiga halafu tusiwashitaki kwa sababu kampuni na sisi tumo.
Maendeleo yanataka uongozi ulio na commitment ya kupata feedback ya watu.
Sasa rais anazuia mikutano ya siasa, ambayo watu wanaelezea grievances zao. Hii ni feedback channel. Atawezaje kujifanyia self evaluation na kufanya mambo yawe bora zaidi?
Haya ya mikutano ya siasa tuwaachie wanasiasa na masharti walopeana.
Mkuu, JK baada ya tume ya Bomani walikaa na wawekezaji wa madini wakaja na mrahaba toka 3% mpaka 4%.
JPM na Prof. Kabudi na wengineo kwenye timu ya negotiations wamekaa na Barick na kutoka na USD 300mil, plus 16% shareholding kwenye new company, kuleta makao makuu ya Twiga Company Mwanza, kuwa sehemu ya board na management, kupata 50/50 economic benefits baada ya kuondoa "operation costs na taxes".
Nadhani (kama sijashau). Kuwa na refineries hapa bongo.
Kwa mambo haya sio haba. Kama BWM na JK kwa miaka yao walishindwa. Sidhani kama hakufanya due diligence. Ila kama tunadhani vinginevyo, atakaepokea kijiti basi ataanzia hapo.
Tukirudi kwenye agri-investment, I still see the big boss has not been whole informed on how much we could earn.
Fikiria jirani Kenya...export earnings from cut flowers hit approximately 113.2 billion Kenyan shillings (1.1 billion U.S. dollars), which was a 38 percent increase from the previous year....Aprox 2.5 Tril TZS za maua tu
In 2016, horticulture earnings stood at a record high of Sh101.5 billion, contributing 1.44 per cent of the country’s GDP.
www.businessdailyafrica.com
Kenya part ya nchi ni jangwa. Mazingira ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Manyara, Nyanda za juu; kwa ukubwa wa eneo kama tukiwekeza we could make more money kuliko Kenya au basi sawia na Kenya.
Airport za Kenya wana cold-room za horticultural exports. Kwa manunuzi ya ndege ni mwanzo mzuri bila shaka agenda ya uwekezaji kama itapata mtoa mada mzuri, kuna haja ya kuwa na cargo flight kwa ajili ya horticultural products pia.
Bado nina imani na huyu mzee. Suala ni namna gani ya kumfikia na kumpa depth ya what could be earned kwenye various agro outputs