"How Europe Underdeveloped Africa," By Walter Rodney!

"How Europe Underdeveloped Africa," By Walter Rodney!

Huu ni ujinga wa hali ya juu kulialia kuwa wazungu wa ulaya wamechangia uduni wetu wakati leo ni miaka zaidi ya hamsini tangu tuwe huru.

Idadi ya miaka aliyokaa mkoloni wa kiingereza hapa tanzania haizidi miaka 35 na mjerumani ni miaka kama 30. kwa maana hiyo miaka tuliyokuwa huru ni mingi kuliko miaka tuliyotawaliwa na wote wajerumani na waingereza.

Mbona tumeshindwa kujiletea hayo maendeleo? Itapita miaka elfu halafu bado watu kama nyie mtakuja na hizi ngonjera zenu hapa kama kasuku
 
Haaa haaa waTanzania ni kati ya watu wahovyo wanaishi katika sayari hii ambayo sidhani kama watamudu kuendelea kuwepo miaka 50 ijayo iwapo hawatabadilika.Baada ya kuboronga na kuizika demokrasia kule Zanzibar tunakuja na vitabu tulivyotumia kwaajili ya kufaulu mitihani na kupata mivyeti isiyokuwa na faida kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
 
Tusitfute sababu hata kama ameandika, tuna miaka mingapi toka tumepata uhuru, inamaana tutaishi maisha kuzilaumu nchi za Ulaya, siasa mbovu, ubinafsi, na tamaa za viongozi wa Afrika kumetufanya tusiendelee.
 
Unafurahia nchi kuingia kwenye misukosuko.

Kapimwe akili.
Mkuu hiyo source yahuo msuko suko siunajua lakini? Nadhani ungekuwa mzalendo wakweli ungewashauri watawala wetu wasifanye hayo yaliyopelekea tufike hapo kwenye huo unaoita msuko suko.
 
wameendelea kwa misaada?
...Katika eneo la Mashariki ya Kati, kuna nchi mbili ambazo, kama zina maendeleo ya kiuchumi au kufanikiwa kijamii, ni kutokana na misaada na namna walivyoitumia. Nchi hizo ni Israel na Jordan.

...Inakadiriwa kuwa, mpaka kufikia mwaka 2008, msaada wa Marekani kifedha kwa Israel, ulikuwa USD 114 Bn.

...Nadhani, issue kubwa hapa ni jinsi ambavyo misaada inatumika. Je, fedha hizi hufika au hufanya kazi zilizolengwa? Je, ubadhirifu kwenye miradi inayofadhiliwa kwa fedha hizi ni wa kiasi gani na unadhibitiwa vipi? Je, miradi hii inafaida kwa jamii na nchi?

...Aidha tukumbuke kuwa, misaada si lazima iwe ya fedha. Inaweza kuwa ya kujifunza utaalamu fulani, kupewa teknolojia fulani, n.k.

...Wanaofurahia kusitishwa kwa misaada hii na wale wanaobeza, hawajui kitu kuhusu misaada, au wanaongozwa na ushabiki wa kisiasa. Watakaoathirika ni wananchi waliokuwa wakifaidika na miradi ya afya, elimu, maji na umeme, ambayo kwa namna moja ama nyingine haikuweza kufadhiliwa na Serikali.

...Misaada, iwe ya aina yeyote ile, ikitumiwa vizuri huleta maendeleo kwa jamii na kuchangia kukua kwa uchumi.
 
SAVINGS: Nchi kama nchi lazima iimarishe pato la ndani ili kuweza kujifanyia mambo yake bila interaction yoyote. Mfano JPM alipoingia Ikulu, nilifurahi sana eti kusema miezi miwili tu serikali yake imekusanya trillion 4, binafsi nilitarajia sasa nchi hii inaenda kuwa super tajiri ndani ya awamu moja tu ya JPM. Nurkse yeye ni perismist na misaada ya nje, maana inaifanya serikali kuingiliwa kisiasa.
...Nadhani, ulimaanisha intervention.

...Sidhani kama tuna uchumi wa kukusanya Tshs 4 Tn kwa miezi miwili, labda 3. Tunaweza kusanya hiyo, tukilazimisha, ila tutaua shughuli za uzalishaji na uwekezaji, hatimae tutapoteza zaidi mapato.

...Una matarajio makubwa sana, ndugu. Ni kitu kinawezekana, lakini, it will take time, long time.

sasa watu kama hawazaliani, soko tunalipataje? Wakati waafrika tunashangilia uzazi wa mpango na tukiona gari limeandikwa VACECTOMY tunaruhusu wake zetu walikimbilie.
...Soko si lazima liwe na ndani. Tujifunze jinsi Japan, Singapore, Taiwan, n.k. walivyoweza kujenga uchumi wao kwa kuuza katika masoko ya nje. We need to invest in people.

...Tunaweza zaliana ikawa shida! Watu watakufa njaa, na watoto hawatasoma. Matokeo yake, umasikini zaidi.

...Kwa hali ilivyo, unafikiri ingekuwaje kama tungekuwa watu 70 Mn? Huduma za jamii zisingeweza kustahimili.
 
Walioididimiza na wanaoendelea kuididimiza Afrika ni Waafrika wenyewe.

Tuache kuwasingizia wengine!

Huwezi ku-underestimate madhara ya ukoloni, SAP policies, foreign aid, na utandawazi (hasa kwenye kipengele cha soko huria) kwa muafrika. Ndio kuna sababu za ndani ila za nje pia ndio Mzizi wa matatizo yetu yaliyo mengi.
Ni mzungu tu tena asiye na fikra huru na Yule anayelinda maslahi ya tabaka tawala la nchi yake anayeweza kuandika ulichoandika.
Ni kweli waafrika tuna sehemu yetu kwenye kusababisha matatizo yetu ila mzungu hawezi kukwepa lawama hizi.
 
Watanzania tuache kuwaonea wivu nchi zilizoendelea. Sizitaki mbichi hizi haitakaa itusaidie. Tu maskini kwa kuwa hatutumii ipasavyo raslimali zetu kama vile maliasili, watu tulio nao kwenye taifa. Vijana wanazurura, wanavuta unga na bangi, hawafayi kazi za uzalishaji japo wana nguvu. Technology hatuna ya kubadilisha tulivyo navyo kuwa mali. Tunawasingizia wazungu kwa umaskini tulio nao. Kuna mikoa ambayo wazungu hawakufika kabisa je ni matajiri? Walishatuachia nchi miaka 55 iliyopita. Tena nadiriki kusema wasingekuja wazungu nchi hii tungekuwa na hali mbaya kama wahazabe.
Nakubaliana na baadhi ya uliyosema lakini hakuna suala la kuwaonea wivu wazungu. Lililopo tunapaswa kuwanyanyapaa kwa mbinu zao chafu za kutaka kuendelea kutunyonya. Historia inatudhihirishia hila za Wazungu tangu walivyoanza kuja barani mwetu hadi Leo. Walikuja wakaanza kutuibia rasulimali zetu na kwenda kujenga nchi zao kwa Mali zetu. Tulipowastukia na kuanza harakati za kudai Uhuru waliondoka kwa shingo upande. Kwa kuwa walishatusoma ujuha wetu wa kutaka tuwe kama wao tuishi maisha ambayo hayalingani na hali halisi ya nchi zetu ambazo bado hazijaendelea wameweza kututeka na kutufanya tuendelee kuwa tegemezi kwao. Wakati huo huo wao wakiendeleza kutunyonya kwa mlango wa nyuma wa uwekezaji, soko huria na misaada yenye masharti. Imefika mahali wapo Watanzania ama Waafrika kwa ujumla wanaoamini hatuwezi kuishi bila misaada ama bila kuwasikiliza na kuwakubalia kila wasemalo kana kwamba sisi wenyewe hatuna uwezo na akili za kupanga mambo yenye manufaa kwetu. Akitokea kiongozi mwenye mawazo mazuri ya kimaendeleo badala ya kukubali kumsaidia ili taifa lisonge mbele tunaanza kutafuta kumkwamisha kwa maneno na vitendo. Ndio maana tukaambiwa Miafrika ndivyo tulivyo!
 
Ama kweli Waafrika tuna shida sana kama si laana katika kufikiri.
 
Nakubaliana na baadhi ya uliyosema lakini hakuna suala la kuwaonea wivu wazungu. Lililopo tunapaswa kuwanyanyapaa kwa mbinu zao chafu za kutaka kuendelea kutunyonya. Historia inatudhihirishia hila za Wazungu tangu walivyoanza kuja barani mwetu hadi Leo. Walikuja wakaanza kutuibia rasulimali zetu na kwenda kujenga nchi zao kwa Mali zetu. Tulipowastukia na kuanza harakati za kudai Uhuru waliondoka kwa shingo upande. Kwa kuwa walishatusoma ujuha wetu wa kutaka tuwe kama wao tuishi maisha ambayo hayalingani na hali halisi ya nchi zetu ambazo bado hazijaendelea wameweza kututeka na kutufanya tuendelee kuwa tegemezi kwao. Wakati huo huo wao wakiendeleza kutunyonya kwa mlango wa nyuma wa uwekezaji, soko huria na misaada yenye masharti. Imefika mahali wapo Watanzania ama Waafrika kwa ujumla wanaoamini hatuwezi kuishi bila misaada ama bila kuwasikiliza na kuwakubalia kila wasemalo kana kwamba sisi wenyewe hatuna uwezo na akili za kupanga mambo yenye manufaa kwetu. Akitokea kiongozi mwenye mawazo mazuri ya kimaendeleo badala ya kukubali kumsaidia ili taifa lisonge mbele tunaanza kutafuta kumkwamisha kwa maneno na vitendo. Ndio maana tukaambiwa Miafrika ndivyo tulivyo!
OK OK Ethiopia haikutawaliwa na wakoloni, mbona ni miongoni kwa nchi maskini duniani? Wahazabe wa kule manyara na Singida hawa kumuona mzungu kabisa wana maendeleo gani?
 
Huwezi ku-underestimate madhara ya ukoloni, SAP policies, foreign aid, na utandawazi (hasa kwenye kipengele cha soko huria) kwa muafrika. Ndio kuna sababu za ndani ila za nje pia ndio Mzizi wa matatizo yetu yaliyo mengi.

Sikubaliani kabisa na hivyo visingizio vyako. Ni visingizio vya watu wasio na maono wala weledi wowote ule.

Mbaya zaidi, ni visingizio vya watu wenye hulka ya ufisadi.

Tupo hapa tulipo kwa sababu ya ubovu na uozo wa CCM.

Leo hii kila kukicha tunasikia habari za wafanyakazi hewa waliokuwa wakilipwa mishahara.

Swali ibuka hapo ni je, hao wafanyakazi hewa wamekuwepo kwa muda gani? Kiasi gani cha pesa kimeteketekea kwa ajili yao tu?

Kiini cha matatizo yetu ni utawala bora. Kitu ambacho hatuna.

Ni rahisi sana kutupia lawama watu wengine na kuwanyooshea vidole kuwa wao ndo sababu kubwa ya matatizo yetu kuliko kukabiliana na ukweli na kukiri kuwa sisi wenyewe ndo chanzo cha matatizo yetu.

Kwa hiyo nakuelewa kabisa. Ni asili ya binadamu kukana uwajibikaji wake ikija kwenye mambo mabaya.

Ni mzungu tu tena asiye na fikra huru na Yule anayelinda maslahi ya tabaka tawala la nchi yake anayeweza kuandika ulichoandika.

Unaonyesha ulivyo na wigo wa fikra finyu na duni! Eti ni mzungu tu tena asiye na fikra huru ndo anaweza kuandika kama nilivyoandika.

Teh teh teh...ukiwa mtu mwenye fikra duni lazima uwaze hivyo.

Ni kweli waafrika tuna sehemu yetu kwenye kusababisha matatizo yetu ila mzungu hawezi kukwepa lawama hizi.

CCM ndo haiwezi kukwepa lawama za hali tuliyonayo. Ni CCM mwanzo mwisho.
 
View attachment 333820

Ukisoma kitabu hiki utajua namna Ulaya ilivyoididimiza Afrika!
Na bahati mbaya mpango huo bado haujaisha!
Tunaoshabikia misaada hatujui tutendalo!

View attachment 333824
Wengi vijana ni wa miaka ya tisini.
Ni wavivu wa kujua history.
Walter Romney, wakoloni walimua baada ya kuwapa ukweli.
Vijana acheni ushabki bila kuelewa mambo.
Wahisani hawa kama wanavyojiita hawana kheri na watu weusi zaidi ya kutugandamiza Kwa kisingizio cha neno Democracy
Libya imesambaa na inaendelea kuporwa kwa kisingizio cha kuleta democracy.
Divide and rule.
Neno ningelijua huja baadae.
 
ukimaliza kuswoma hapo kamsome Mohamed Babu katika African socialism or socialist Africa,ndo ujue nyie vijana wa ccm huwa hamna akili timamu hamjui mnaamini nini
so.jpg
 
Hawajui watendalo indeed.Nilisoma kitabu hiki mara ya kwanza 1974.Oh,kilibadilisha mtazamo wangu kuhusu nchi za magharibi na misaada yao kabisa.Sidhani kama vijana wa kileo wameshawahi hata kukisoma kitabu hiki let alone kukisikia.Ndio maana hawaoni ubaya wa misaada ya wanyonyaji hawa waliojificha kwenye jina la wafadhili.Siku hizi wanaitwa partners of develoment!What a shame.Hawa sio partners ni adui zetu.
View attachment 333820

Ukisoma kitabu hiki utajua namna Ulaya ilivyoididimiza Afrika!
Na bahati mbaya mpango huo bado haujaisha!
Tunaoshabikia misaada hatujui tutendalo!

View attachment 333824
 
Back
Top Bottom