Mkuu, haujatuambia ni hoja gani Walter alizozi-allocate kwenye kitabu chake hicho tajwa hapo juu, imekuwa kama wewe mwenyewe haujakipitia, ila tu ni kwa sababu title yake ni sawa na wazo lako, basi ukaona kina-fit.
Katika nadharia yake ya Ki-bourgeoisie (Vicious Circle of Poverty), Prof. Ragnar Nurkse anasema, "a society is poor because is poor." anaendelea kusema, "...it is poor because it lacks savings and consumption..."
Hapa tumeona maneno mawili ambayo Prof. anayatumia katika nadharia yake, yaani "savings" na consumption. Katika tafsiri yake ya haya maneno, Prof. Nurkse katika savings anamaanisha investment, tena uwekezaji wa ndani. Yaani kama Tanzania basi iwasogeze karibu na kuwatia moyo ma-tycoon kama kina Mengi, Bakhresa na wengine kwa nia njema na si kwa kuwavuta kwa malengo yao binafsi.
Neno la pili ni consumption, ambapo Prof. anamaanisha Markets, na yenyewe iwe ya ndani. Sasa kutengeneza soko la ndani ni kuruhusu watu wazaliane na ikiwezekana na kuwa-award wanaozaa kama kumbikumbi.
Kwa kifupi Prof. yeye, katika mtazamo wa kusema kwamba ukoloni, ambao ndio hoja kubwa ya Walter Rodney, ndiyo sababu kubwa ya waafrika kuwa maskini. Ukoloni umeshaisha siku nyingi, sasa swali la kujiuliza kwa nini bado tu maskini?
Nadharia ya Prof. Nurkse, binafsi huwa nakubaliana nayo japo wengi huwa wanaipinga, lakini kiuhalisi ni hoja yenye tija sana. Sasa hebu tuangalie uhalisia wa nadharia yake kwa mazingira ya Afrika, hasa Tanzania.
SAVINGS: Nchi kama nchi lazima iimarishe pato la ndani ili kuweza kujifanyia mambo yake bila interaction yoyote. Mfano JPM alipoingia Ikulu, nilifurahi sana eti kusema miezi miwili tu serikali yake imekusanya trillion 4, binafsi nilitarajia sasa nchi hii inaenda kuwa super tajiri ndani ya awamu moja tu ya JPM. Nurkse yeye ni perismist na misaada ya nje, maana inaifanya serikali kuingiliwa kisiasa.
MARKET: sasa watu kama hawazaliani, soko tunalipataje? Wakati waafrika tunashangilia uzazi wa mpango na tukiona gari limeandikwa VACECTOMY tunaruhusu wake zetu walikimbilie
Waafrika hatufikirii!!!!!!!!!