"How Europe Underdeveloped Africa," By Walter Rodney!

"How Europe Underdeveloped Africa," By Walter Rodney!

...Katika eneo la Mashariki ya Kati, kuna nchi mbili ambazo, kama zina maendeleo ya kiuchumi au kufanikiwa kijamii, ni kutokana na misaada na namna walivyoitumia. Nchi hizo ni Israel na Jordan.

...Inakadiriwa kuwa, mpaka kufikia mwaka 2008, msaada wa Marekani kifedha kwa Israel, ulikuwa USD 114 Bn.

...Nadhani, issue kubwa hapa ni jinsi ambavyo misaada inatumika. Je, fedha hizi hufika au hufanya kazi zilizolengwa? Je, ubadhirifu kwenye miradi inayofadhiliwa kwa fedha hizi ni wa kiasi gani na unadhibitiwa vipi? Je, miradi hii inafaida kwa jamii na nchi?

...Aidha tukumbuke kuwa, misaada si lazima iwe ya fedha. Inaweza kuwa ya kujifunza utaalamu fulani, kupewa teknolojia fulani, n.k.

...Wanaofurahia kusitishwa kwa misaada hii na wale wanaobeza, hawajui kitu kuhusu misaada, au wanaongozwa na ushabiki wa kisiasa. Watakaoathirika ni wananchi waliokuwa wakifaidika na miradi ya afya, elimu, maji na umeme, ambayo kwa namna moja ama nyingine haikuweza kufadhiliwa na Serikali.

...Misaada, iwe ya aina yeyote ile, ikitumiwa vizuri huleta maendeleo kwa jamii na kuchangia kukua kwa uchumi.

Mkuu, hivii katika akili za kawaida Israel unailinganisha na Tanzania? Nashindwa kuamini moja kwa moja kusema kwamba Israel imeendelea kwa asilimia kadhaa za msaada wa Mmarekani, yawezekana Mmarekani ndiye alieyeendelea kwa expense ya Israel. Kwa nini nasema hivyo? Israel na waisrael ambao wengi wao ni wayahudi ni watu waliobarikiwa sana vipaji katika Nyanja tofautitofauti ikiwa ni pamoja na kijeshi, kisayansi na hata kisiasa. Kama huwa unafuatilia vizuri, marekani hadi kuitwa superpower katika anga la kijeshi na kivita ni juhudi za Myahudi. Mfano, Albert Einstein aligundua bomu muhimu kabisa katika historia ya Marekani ambalo ndilo lililotumika kuipiga Hiroshima tarehe 6 August 1945 na siku tatu baadaye bomu lingine la aina hiyohiyo lililotengenezwa na mtaalamu huyohuyo ndilo pia likatumika kuipiga Nagasaki. Ni baadhi ya silaha ambazo ziliipa jina kubwa Marekani ambazo ni juhudi za Kiyahudi. Hali kadhalika kuna wataalamu kibao wa kiyahudi katika afya na idara zingine za Marekani, pamoja na usalama wa Taifa pia, yaani CIA na FBI.

Mkuu, pia umesema kwamba, msaada si lazima uwe wa kifedha, bali unaweza kuwa wa kitaalamu ikiwa ni pamoja na kupewa teknolojia Fulani. Kama ni hivyo, hata Afrika basi ina mchango na msaada mkubwa kwa Marekani. Inasadikika kuwa, kuna wataalamu wengi kutoka Ethiopia na Botswana, na hizi zote ni nchi za kiafrika, sasa je, na sisi tusitishe misaada kwa Marekani? Najua jibu hapa ni kwaba hatutaweza kwa maana huko wataalamu wetu wanalipwa shavu zuri kuliko katika nchi zao. Sasa kumbe na hata sisi tungekuwa tunawalipa vizuri wataalamu wetu na kuwathamini, basi nafikiri wangebaki na kama wangebaki, basi naamini wangeliendeleza Taifa. Lakini je, kuwalipa vizuri na kuwathamini inatosha kuwa-brainwash wasikimbie? wanahitaji pia kuwa katika utawala bora wenye demokrasia ili wafurahie maisha yao kwenye nchi yao. Haya, kila leo tunasikia na kuona madaktari wanaandamana kudai waongezwe mishahara, na baadhi yao wanaoonekana ni spokenmen hutolewa meno bila ganzi, je watakuwa na hamu ya kukaa nchini kwao? Go back in memory kwa alichokipata Dr Ulimboka, nafikiri kama wewe ni mzalendo mkuu, ungetoa hadi machozi kwa walichomfanyia.

Mkuu, huwa naamini sana katika nadharia za kifalsafa na ni kwa namna gani wazee wa zamani waliendelea. Mfano, mwanafalsafa Goran Hyden (1943) yeye anaamini, "...development is a result of human efforts...". Lazima kwa namna moja ama nyingine utakubaliana na mimi kuwa, nchi yoyote huendelea kwa juhudi za watu wake wenyewe. Sasa je, ni watu wa aina gani? Ni raia wa kawaida na viongozi kwa pamoja Hyden ndio anaowazungumzia. Raia tunao na tena ni wavumilivu na wachapa kazi wanaofanya kazi kama recruits, lakini viongozi hatuna.

Nakuwa optimist sana kwa falsafa ya hapa kazi tu ya Bw. Magufuli hasa kwa kiburi alichokionesha kwa Mmarekani na umarekani wake na misaada yake ya kinafiki, sasa ifike hatua, nasi tuombwe misaada. Nilifuatilia vizuri sana wakati alipokuja Obama. Katika hotuba ya kumkaribisha, the then Tanzanian President, the so-called Mzee, His Excellency Dr Kikwete, alikuwa anainyenyekea sana misaada na kuiomba iendelee, yaani hadi aibu.

Tanzania tunaweza, kikubwa tunatakiwa tuwe wazalendo.
 
Hawajui watendalo indeed.Nilisoma kitabu hiki mara ya kwanza 1974.Oh,kilibadilisha mtazamo wangu kuhusu nchi za magharibi na misaada yao kabisa.Sidhani kama vijana wa kileo wameshawahi hata kukisoma kitabu hiki let alone kukisikia.Ndio maana hawaoni ubaya wa misaada ya wanyonyaji hawa waliojificha kwenye jina la wafadhili.Siku hizi wanaitwa partners of develoment!What a shame.Hawa sio partners ni adui zetu.

You can call them whatever the name you feel it fits. Maadui, wanafiki, wahujumu na kadhalika, lakini ukweli unabaki palepale kwamba, Bwana Walter yeye nadhani hoja yake kwa sasa katika nchi za Afrika zilizo chini ya Sahara si tena za kuzungumzia ukoloni wala ukoloni mambo leo kuhusisha na umaskini wake.

Mkuu, binafsi huwa naamni kabisa, kwanza kitendo tu cha kujua kuwa huu ni ukoloni mambo leo, basi tayari ushajitambua. Sasa kama ushajitambua, kwa nini sasa usipige vita huo ukoloni mambo leo? Au unataka kuuambiwa umma wa jamiiforums kuwa waafrika hawajajua mambo haya? Tunao wataalamu kibao wanaolifahamu hili, kwa hiyo inatosha kabisa kujikwamua.

Bado naitetea sana nadharia ya Prof. Nurkse kuwa, we are poor because we are poor.
 
View attachment 333820

Ukisoma kitabu hiki utajua namna Ulaya ilivyoididimiza Afrika!
Na bahati mbaya mpango huo bado haujaisha!
Tunaoshabikia misaada hatujui tutendalo!

View attachment 333824

Mkuu hapo unaongelea miaka zaidi ya 50 iliyopita.

Jiulize, JE MFANO TANZANIA KATIKA MIAKA HAMSINI BADO WAZUNGU WAMEIDIDIMIZA AU NI WATANZANIA NDIO WANAIDIDIMIZA TANZANIA????

Mtakumbuka mengi sana baada ya MCC kuondoa misaada yake.

Kipanya na MCC.jpg
 
Nakuwa optimist sana kwa falsafa ya hapa kazi tu ya Bw. Magufuli hasa kwa kiburi alichokionesha kwa Mmarekani na umarekani wake na misaada yake ya kinafiki, sasa ifike hatua, nasi tuombwe misaada. Nilifuatilia vizuri sana wakati alipokuja Obama. Katika hotuba ya kumkaribisha, the then Tanzanian President, the so-called Mzee, His Excellency Dr Kikwete, alikuwa anainyenyekea sana misaada na kuiomba iendelee, yaani hadi aibu.

Tanzania tunaweza, kikubwa tunatakiwa tuwe wazalendo.

Mkuu unaongea kisiasa mno. Angalia katika Google ni nchi ngapi ambazo zinafadhiriwa na MCC na wana uwezo kuliko wewe Tanzania.

Achana na ushabiki wa kisiasa hujui muda huu viongozi wa serikali wamechanganyikiwa vipi kuhusu MCC. Tanzania bado ni nchi changa hatuwezi kujikwamua katika kipindi kifupi hivi. Tuwe wakweli sometimes!!!!!!!!!!!!
 
View attachment 333820

Ukisoma kitabu hiki utajua namna Ulaya ilivyoididimiza Afrika!
Na bahati mbaya mpango huo bado haujaisha!
Tunaoshabikia misaada hatujui tutendalo!

View attachment 333824
hivi vitu tumevisoma sana t6angu mashuleni.......
leo ndo watu tunayajua
ok,.....misaada sio issue mbona msaada wa japan tumechukua kwanini tusiache kote ndgu???
minaonA serikali yangu haijajipanga bado
 
View attachment 333820

Ukisoma kitabu hiki utajua namna Ulaya ilivyoididimiza Afrika!
Na bahati mbaya mpango huo bado haujaisha!
Tunaoshabikia misaada hatujui tutendalo!

View attachment 333824
hakuna taifa litakalotusaidia bila lenyew kuwa linafaidika pia, si marekan si watu wa ulaya wala wachina....shida hapa ni kwamba pengine masharti yanayotolewa na europe na hawa america yanakuwa yanatishia chama kama demokrasia au uhuru wa kujieleza yanakuwa yanatishia baadhi ya watawala kubaki madarakan ndo mana viongozi wa africa hapa tunakuwa wakali sana..ndo mana nchi zetu nying za zinaipenda china kwakuwa yeye hufuata interest zake tu habari za mnafungana mnapigana ye hana habari nazo.............
 
Mkuu, kuna watu wanashabikia ujinga wakidhani kufanya hivyo watapata faida yoyote!
Matatizo mengine ya kwetu wenyewe kutolipa kodi kusaini mikataba isiyo na tija kwa taifa
 
Mkuu, hivii katika akili za kawaida Israel unailinganisha na Tanzania? Nashindwa kuamini moja kwa moja kusema kwamba Israel imeendelea kwa asilimia kadhaa za msaada wa Mmarekani, yawezekana Mmarekani ndiye alieyeendelea kwa expense ya Israel. Kwa nini nasema hivyo? Israel na waisrael ambao wengi wao ni wayahudi ni watu waliobarikiwa sana vipaji katika Nyanja tofautitofauti ikiwa ni pamoja na kijeshi, kisayansi na hata kisiasa. Kama huwa unafuatilia vizuri, marekani hadi kuitwa superpower katika anga la kijeshi na kivita ni juhudi za Myahudi. Mfano, Albert Einstein aligundua bomu muhimu kabisa katika historia ya Marekani ambalo ndilo lililotumika kuipiga Hiroshima tarehe 6 August 1945 na siku tatu baadaye bomu lingine la aina hiyohiyo lililotengenezwa na mtaalamu huyohuyo ndilo pia likatumika kuipiga Nagasaki. Ni baadhi ya silaha ambazo ziliipa jina kubwa Marekani ambazo ni juhudi za Kiyahudi. Hali kadhalika kuna wataalamu kibao wa kiyahudi katika afya na idara zingine za Marekani, pamoja na usalama wa Taifa pia, yaani CIA na FBI.
...Nadhani hapa tafsiri ya neno msaada au maana yake, ndio itagomba.

...Unasema wamebarikiwa vipaji. Wapo hata waTanzania waliobarikiwa vipaji, ila hawawezi fika mbali kwa kuwa hawana fedha wala hawajapata mazingira ya kuvitumia ipasavyo vipaji hivyo. Uwezeshwaji ni muhimu. Ndio maana wakitoka nje, wanang'aa.


...Unaamini kwamba Einstein single handedly ali deliver the atomic bomb? Actually yeye hakugundua hilo bomu, bali alishawishi -kwa kumwandikia barua Roosevelt- uundwaji wake, ili Nazi Germany wasiweze kulitumia -kama wangeweza kulitengeneza- na kushinda vita. Wajerumani walikuwa wa kwanza kutenganisha atom, na wakaanza utafiti wa kutengeneza silaha.

...Nadhani unafahamu The Manhattan Project, iliyoongozwa na Oppenheimer, wakati huo. Einstein aliishia kwenye E=mc2, na si namna ya kutengeneza bomu. Waliotengeneza "Little Boy" na "Fat Man" ni watu wengine.

...Umuhimu wa fedha kwenye mradi unaweza kuuona kwa kutafiti fedha iliyotumika kwenye mchakato mzima. At that time hamna nchi iliyokuwa na uwezo wa kukusanya resources kama ilivyofanya Marekani.


...Ndio nailinganisha na Tanzania linapokuja suala la kutegemea au kutotegemea misaada, wana mambo mengi ya kufanya, hawana hela. Nimeitaja na Jordan hapo!

Mkuu, pia umesema kwamba, msaada si lazima uwe wa kifedha, bali unaweza kuwa wa kitaalamu ikiwa ni pamoja na kupewa teknolojia Fulani. Kama ni hivyo, hata Afrika basi ina mchango na msaada mkubwa kwa Marekani. Inasadikika kuwa, kuna wataalamu wengi kutoka Ethiopia na Botswana, na hizi zote ni nchi za kiafrika, sasa je, na sisi tusitishe misaada kwa Marekani? Najua jibu hapa ni kwaba hatutaweza kwa maana huko wataalamu wetu wanalipwa shavu zuri kuliko katika nchi zao. Sasa kumbe na hata sisi tungekuwa tunawalipa vizuri wataalamu wetu na kuwathamini, basi nafikiri wangebaki na kama wangebaki, basi naamini wangeliendeleza Taifa. Lakini je, kuwalipa vizuri na kuwathamini inatosha kuwa-brainwash wasikimbie? wanahitaji pia kuwa katika utawala bora wenye demokrasia ili wafurahie maisha yao kwenye nchi yao. Haya, kila leo tunasikia na kuona madaktari wanaandamana kudai waongezwe mishahara, na baadhi yao wanaoonekana ni spokenmen hutolewa meno bila ganzi, je watakuwa na hamu ya kukaa nchini kwao? Go back in memory kwa alichokipata Dr Ulimboka, nafikiri kama wewe ni mzalendo mkuu, ungetoa hadi machozi kwa walichomfanyia.
...Naona tafsiri yako ya neno msaada ni tafauti na ile inayofahamika, au ambayo iko kwenye hoja.


...Mazingira bora ya kazi, motisha, na uongozi bora, ni vitu vya muhimu katika kubakiza top talent. Ku-brainwash wasikimbie? Maana yake wawe ma zombie? Maana kama mazingira hayafai, mtu makini atakuwa wa kwanza kutafuta fulsa sehemu nyingine.

...Nakubaliana nawe!

Mkuu, huwa naamini sana katika nadharia za kifalsafa na ni kwa namna gani wazee wa zamani waliendelea. Mfano, mwanafalsafa Goran Hyden (1943) yeye anaamini, "...development is a result of human efforts...". Lazima kwa namna moja ama nyingine utakubaliana na mimi kuwa, nchi yoyote huendelea kwa juhudi za watu wake wenyewe. Sasa je, ni watu wa aina gani? Ni raia wa kawaida na viongozi kwa pamoja Hyden ndio anaowazungumzia. Raia tunao na tena ni wavumilivu na wachapa kazi wanaofanya kazi kama recruits, lakini viongozi hatuna.
...Tuko pamoja!


...Viongozi hutokana na hao "raia wavumilivu na wachapakazi" maana hawatoki sehemu tafauti bali miongoni mwao. Kwamba, raia ni wachapakazi? Sina uhakika, ila najua ni wavumilivu. Mwembe hauzai nazi!

Nakuwa optimist sana kwa falsafa ya hapa kazi tu ya Bw. Magufuli hasa kwa kiburi alichokionesha kwa Mmarekani na umarekani wake na misaada yake ya kinafiki, sasa ifike hatua, nasi tuombwe misaada. Nilifuatilia vizuri sana wakati alipokuja Obama. Katika hotuba ya kumkaribisha, the then Tanzanian President, the so-called Mzee, His Excellency Dr Kikwete, alikuwa anainyenyekea sana misaada na kuiomba iendelee, yaani hadi aibu.
..."hapa ni kazi tu" si falsafa, ni msemo maarufu.

Tanzania tunaweza, kikubwa tunatakiwa tuwe wazalendo.
...Tafsiri rasmi ya uzalendo ni patriotism. Tatizo lililopo kwenye uzalendo/patriotism ni pale ambapo wananchi hawaoni kama Serikali inawajali, kusimamia na kulinda maslahi yao. Hapa kuna kundi kubwa halitakuwa na uzalendo, maana hawaiungi mkono Serikali.

...Uzalendo/patriotism hujengwa kwa Serikali kutanguliza maslahi ya wananchi mbele. Marekani husema siku zote, kwamba, mMarekani haachwi nyuma popote pale alipo duniani, na atalindwa. Kitu hiki huchangia kujenga uzalendo.

...Nadhani neno uzalendo limekuwa likitumika ndivyo sivyo. Mzalendo ni mtu anayeunga mkono -kwa kupikwa awe hivyo na kwa tabia- mambo ya Serikali. Askari -polisi, jeshi, mgambo, n.k.- ni mfano mzuri wa mzalendo.

...Tunahitaji watu bora, siasa safi, na fedha. Haya ndio yatapelekea uwepo wa uzalendo/utaifa.
 
Danganyikeni ninyi sio mimi. Tumekuwa wavivu na wezi halafu tunazingizia watu wengine. Vitabu kama hivyo vinamfanya mwafrika azidi kudumaa kimawazo badala ya kusonga mbele. Kuna mataifa kama waisrael walipata shuruba isiyosemekana na leo wana maendeleo ije kuwa sisi?
Mkuu shikamoo!
 
Back
Top Bottom