How Air Tanzania Should be Restructured

How Air Tanzania Should be Restructured

Wakuu, majuzi kuna jama zangu walifiwa na mama yao Mzazi.. wakatoka London UK kwenda kumzika mama yao..
Walipofika Dar wakati maiti imeshatangulia Home walikuta hakuna usafiri wa kwenda Mwanza na booking ilitakiwa wasubiri siku mbili palle Dar.. Kwa sababu ilikuwa muhimu wafike *UK ndogo - mapema kumzika mama yao walikodisha gari wakaendesha usiku kucha..Hii sifa ya Precision hata nashindwa kuielewa unless tunapima mzani wa maendelo kimaskini..

Huwa nacheka sana baadhi ya viongozi wanaposema ati - kwa standard yetu Uwanja wa Dar na Kili unatosha kabisa! - Kwa standard yetu sijui kitu fulani kinatosha!.. haya maneno ya standard yetu yametoka wapi?.. Hivi kweli maskini ana standard fulani ktk Quality ya kitu yaani maskini hata akivaa kandambili ni bora kuliko kutovaa kiatu kabisa ndivyo tunavyopima maendeleo yetu au tunatazama umuhimu wa viatu kulingana na matumizi yake sio na quality ni kipimo cha juu kabisa ambacho ndicho tunakilenga..Hakuna mtu aliyesema tuvae kiatu size kubwa au ndogo ya umbo la miguu yetu kuwa ndio maendeleo lakini Bongo neno hili linatumika sana ktk kupima maendeleo yetu..Nawaomba kizazi hiki muwe makini sana na maelezo ya viongozi wetu hasa tunapotaka kulijenga Taifa letu maanake inaonyesha wazi kuwa hawa viongozi wetu sio tu wamepitwa na wakati (makuzi yao hawakuvaa viatu) bali hawana nia njema na Tanzania..

Mimi nasema hivi hakuna standard kwa maskini wala Tajiri.. chakula chenye nutrition kinatakiwa kwa kila mtu uwe maskini au Tajiri, tofauti inaweza kuwa mapishi tu lakini hata siku moja sikubaliani na viongozi wanapo set goals kwa sababu ya umaskini wetu kuwa vinatosha..wameuza madini yetu, mali zetu kwa bei mbuzi ati kwa sababu sisi ni maskini, hivyo pato lake ni size yetu..
Sikubaliani hata siku moja na kutumia Umaskini kuwa ni unyonge isipokuwa Umaskini utumike kama kitu kinachotupa uchungu na hasira wa adha zitokanazo na umaskini hivyo kutusukuma kutumia maneno kama nguvu, ari na kasimpya ktk kuhakikisha tunatoka ktk Umaskini..Hatuwei kutoka kwenye umaskini ikiwa kila tunalofikiria ni kuua ATCL kwa sababu tu nchi za Magharibi wangefanya hivyo.. Hawa sio maji yetu hata kidogo.. Hapa Canada kuna mashrika ya ndege yasiyopungua 20, majuzi tu niliona habari kuhusu Marekani wakizungumzia security - kulikuwa na ndege zaidi ya 35,000 hewani within the same time na wakasema hiyo ni kawaida kabisa hesabu hufikia hadi 75,000..

Pundamilia)7,
Mkuu huku niliko ticket zinauzwa na Agencies, mashirika yote ya ndege ofisi zao nenda Airport!.. na ticket zao ghali kuliko Agencies kwa sababu kila Agencies hununua ticket za ndege ni Adnace hivyo mashirika kama BA. KLM na kadhalika tayari wameisha jua average ya mauzo mwaka 2009..
Ni sawa na card za simu, mashirika kama Tigo yanakuwa yameisha uza zile card wenyewe wanaziita Voucher kwa walanguzi hata kabla hazijatumika.. Hata ujenzi wa nyumba huku ujenzi wa Condo huanza tu baada ya 3/4 ya vyumba vimeisha uzwa (mortgage) hivyo kwa lugha nyingine fedha yetu ndio zinajenga hilo highrise building!.. Mkuu ni dunia ya ushindani ATCL wanatakiwa kukata matumizi kabisa hao wafanyakazi mikoani hawatakiwi kabisa zaidi ya watu wawili Airport kwa ajili ya ticket check up!..Bomoa kabisa management yote hakuna tena wanasiasa ndani pengine mtu kama Mwapachu ambaye aliweza kuibeba ATC wakati iko ktk chart awe Mwenyekiti wa board.. Si unajua tena Tanzania bila watu fulani fulani kuwepo ndani hatuwezi kabisa kufganya kitu..Kubebana ni moja ya Utamaduni wetu..
 
..

Pundamilia)7,
Mkuu huku niliko ticket zinauzwa na Agencies, mashirika yote ya ndege ofisi zao nenda Airport!.. na ticket zao ghali kuliko Agencies kwa sababu kila Agencies hununua ticket za ndege ni Adnace hivyo mashirika kama BA. KLM na kadhalika tayari wameisha jua average ya mauzo mwaka 2009..
Ni sawa na card za simu, mashirika kama Tigo yanakuwa yameisha uza zile card wenyewe wanaziita Voucher kwa walanguzi hata kabla hazijatumika.. Hata ujenzi wa nyumba huku ujenzi wa Condo huanza tu baada ya 3/4 ya vyumba vimeisha uzwa (mortgage) hivyo kwa lugha nyingine fedha yetu ndio zinajenga hilo highrise building!.. Mkuu ni dunia ya ushindani ATCL wanatakiwa kukata matumizi kabisa hao wafanyakazi mikoani hawatakiwi kabisa zaidi ya watu wawili Airport kwa ajili ya ticket check up!..

Mkuu Mkandara,

Maelezo yangu juu ya namna gani ATCL watauza tiketi zao nilisema kuwa hilo ni suala la kimkakati tu kwetu sisi tunaweza kuliongelea by the way, lakini sioni kama ni issue kubwa sana. Lakini hata hivyo hebu fikiria kama Air Canada ingekuwa na ofisi ya kuuza tiketi hapo Toronto kama zilivyo pale ATC House au Tancot House, nani angelikwenda kununua tiketi? Kwa kifupi ni watu wachache mno kama siyo hakuna. Ni kwani ninasema hivi, katika nchi ambazo zimekwisha piga hatua kubwa katika maendeleo ya kiuchumi wana miundo-mbinu mizuri ya kuweza kuuza tiketi. leo ninaamini wewe ukitaka tiketi ya kwenda popote unanunua kutoka nyumbani kwako kwa kutumia mtandao wa internet. hebu niambie ni watu wangapi hapa nyumbani wanaaccess na internet mbali na kuwapo kwa miundo-mbinu itakayoweza kufanya biashara ya kukata tiketi iwe kama katika nchi zilizoendelea?
Mazingira ya mahali unapofanyia biashara ndiyo panaweza ku-determine nini cha kufanya.
Kwa mfano katika mazingira ya kwetu hapa Tanzania uuzaji wa tiketi unafanyika kwa njia ya mashirika yenyewe kuuza tiketi zao. Siyo ATCL pekee ndiyo wanaofanya hivyo
British Airways wanauza tiketi pale Movenpick
KLM & Kenya Airways wanauza tiketi pale Peugeot House
Air India hapo opp ya KLM & Kenya Airways
Emirates walikuwa na ofisi pale Haidery Plaza
Ethiopian Airlines hapo TDFL Bldg. etc,etc.




Bomoa kabisa management yote hakuna tena wanasiasa ndani pengine mtu kama Mwapachu ambaye aliweza kuibeba ATC wakati iko ktk chart awe Mwenyekiti wa board.. Si unajua tena Tanzania bila watu fulani fulani kuwepo ndani hatuwezi kabisa kufganya kitu..Kubebana ni moja ya Utamaduni wetu..

Hili la kumpa Mzee Mwapachu uenyekiti naomba nilirudie, kwa maoni yangu sioni ubaya wowote wa kumpa huyu Mzee uenyekiti wa Bodi ya ATCL. Lakini watanzania tupo millioni kadhaa, kazi yake tuliiona huko nyuma, nafikiri ni wakati mwafaka kwake yeye kuachwa apumzike na kuwaacha watu wengine waoneshe uwezo wao pia.


-------------------------------------------------------------
 
Kweli maneno yako mkuu, kuhusu ticket mkuu wangu kulingana na mazingira yetu tumebanwa kutumia mashirika mama.. lakini hata hivyo mbona zipo agencies kibao zinakata tickets? tumeasha anza kufanya hivyo kwa mnini tusihakikishe mpango huo unawezekana kabisa..Tukianza na shirika letu wenyewe pamoja na Precision Air..
Kuhusiana na Mwapachu mkuu wangu tunahitaji bado watu walioweza kufanikisha watupe busara zinazoambatana na biashara hii. Shirika la ndege ni biashara ngumu sana, ngumu kuliko usafiri wa aina yoyote ile hivyo inputs ni muhimu sana sio lazima awe active ktk kuendesha shughuli za shirika. Anaweza kuwa mwenyekiti tu wa board na CEO (nafasi moja) akatoka hata nje, kuna wakati tukubali kujifunza ili kufanikisha kitu fulani..experience ni muhimu sana kuliko elimu ktk utawala wakati mwingine..
 
Za10,
Inasikitisha kwelikweli..... mambo ya ad hoc siku zote hayawezi kuleta manufaa wala kuwa sustainable......
unazungumzia miaka ya nyuma... halafu kama ni kuwa na state- of -the -art airport Addis, its a recent development licha ya kwamba ET ina zaidi ya miaka 100 toka iazishwe na bado inadunda.Mimi nimejaribu kuangalia hata viwanja vyetu vya ndege... utaona kabisa hakuna sense of planning for the future..DIA ilivyojengwa in the early 80s ndio imebakia hivyohivyo na inazidi kuminywaminywa kwa kuongezewa ugly structures kila kukicha... vijibadana na vikontena kila mahali...( na wahusika kila leo unawasikia wanasafiri nje ya nchi kwenda kujifunza..sijui wanajifunza nini na wanakuja ku apply vipi!)..

Angalia uwanja wa Zanzibar..hapo tena ni shughuli! Kinachoshangaza ni kwamba pamoja na kusikia kuna mipango ya kuupanua.... kuna watu wanajenga tena si ujenzi mdogo..karibu kabisa na airport...hii maana yake sijui ni nini.... au ndo mbinu za kuja kudai compensation hefty?
Anyway coming back to our national carrier.... may be a divine intervention will salvage the situation.Tusubiri tuone.

WoS:

Kila siku namwambia Bob Mkandara kuwa MwenyeMungu hakucheza bahati nasibu kuumba ulimwengu. Kusubiri Divine intervention wakati wenzetu wana systematize shughuli zao ni sawa na kucheza Bahati nasibu.

Kinachotakiwa ni ku-systematize shughuli za shirika hilo. Wapo wanaotaka hilo shirika lijiunge na mashirika mengine. Hiyo ni sawa lakini sio lazima.

Cha muhimu ni kutafuta kundi la wateja na baadaye shirika kutengeneza model inayo-cater wateja hao. Wachukua mfano wa mnywaji wa Bia na Chibuku. Hizo zote ni pombe lakini zina-cater wasikilizaji tofauti. Ukiongeza bei ya Chibuku, mnywaji atakwenda kwenye komola, chimpumu, gongo au ulanzi. Mnywaji wa bia, ukiongeza bei atakachofanya ni kuifuata bei mpya au kupunguza unywaji.

Kwa mfano kuna wafanya biashara wa kitanzania wanaotaka kufanya usafiri wa haraka kati ya Mwanza na DSM, Kigoma na Mwanza. Mtwara na DSM.


Hiyo ya kusubiri divine intervention ndio inasababisha ndugu zetu pamoja na kujua kusoma na kuandika kuanza kuua Albinos.
 
Hili la kumpa Mzee Mwapachu uenyekiti naomba nilirudie, kwa maoni yangu sioni ubaya wowote wa kumpa huyu Mzee uenyekiti wa Bodi ya ATCL. Lakini watanzania tupo millioni kadhaa, kazi yake tuliiona huko nyuma, nafikiri ni wakati mwafaka kwake yeye kuachwa apumzike na kuwaacha watu wengine waoneshe uwezo wao pia.

Punda:

Excellence ina-rithishwa. Sababu kubwa ya kushindwa kwa sekta nyingi Tanzania ni kuwa viongozi walifanya kazi kisiasa na kushindwa kuanzisha excellence ambayo vizazi vipya ingechukua.

Mfano Ethiopia Airline alitegemea management ya waMarekani toka ianzishwe kwenye 1940s. Na Kiongozi wa juu muEthiopia kuchua nafasi ya juu alifanya hivyo nadhani kwenye 1971. Na huyu jamaa alikuwa ni Insider, kwa maana kuwa alianza na rank ya urubani mpaka kufikia juu kabisa.

Ninapobeba mabox uwa tuna mikutano na inatolewa historia ya pioneers wetu ambayo inakufanya wewe uwe ndani ya list.
 
Punda:

Excellence ina-rithishwa. Sababu kubwa ya kushindwa kwa sekta nyingi Tanzania ni kuwa viongozi walifanya kazi kisiasa na kushindwa kuanzisha excellence ambayo vizazi vipya ingechukua.

Mfano Ethiopia Airline alitegemea management ya waMarekani toka ianzishwe kwenye 1940s. Na Kiongozi wa juu muEthiopia kuchua nafasi ya juu alifanya hivyo nadhani kwenye 1971. Na huyu jamaa alikuwa ni Insider, kwa maana kuwa alianza na rank ya urubani mpaka kufikia juu kabisa.

Ninapobeba mabox uwa tuna mikutano na inatolewa historia ya pioneers wetu ambayo inakufanya wewe uwe ndani ya list.

Zakumi,

Basically from my experience, nimeona Tanzania kama taifa limepata hasara kubwa kwa kutokuwa na mpango mahsusi kabisa wa kuwa-groom vijana katika maeneo mbalimbali. Wengi wa vijana ambao wamefanya vizuri katika maeneo yao na ku-raise wengi wao ilitokana na juhudi zao binafsi au msaada wa kundi fulani la watu wachache. Tumekuwa tunashuhudia grooming up za viongozi wa kisiasa zikipewa kipaumbele zaidi lakini siyo viongozi watakao manage uchumi wetu. As a result tunapata bora viongozi katika mashirika na taasisi zetu au inafika wakati tunalazimika kuanza upya kusaka namna ya kujikwamua. Ni vema tukageuka na kuwa na sera endelevu juu ya jambo hili na mengineyo ili kuongeza kasi ya maendeleo ya nchi hii.
Nikirejea kwenye hili la ATCL, kwa muda mrefu sana baada ya ATC kutangazwa kama moja ya mashirika yanayobinafsi kupitia PSRC, maamuzi yake mengi makubwa yalikuwa ni lazima yaidhinishwe na PSRC. Kwa maana hiyo kulikuwa na Management, Board na Commission (PSRC) katika ngazi ya kufanya maamuzi. ATC haikutakiwa kufanya shughuli zozote za maendeleo bila ya idhini ya tume ya Rais PSRC. Jambo hili liliidumaza ATC kwa sababu Tume ya Rais haikuwa inaiangalia ATC kama chombo kinachotakiwa kujiendesha kibiashara. Maamuzi ya Tume yaliathiri kukuwa kwa mipango ya maendeleo ikiwemo kuto kutoa mafunzo yatakiwayo kwa ajili ya utekelezaji wa succession plan. Kwa kipindi kirefu ATC haikuweza kuwaingiza kwenye Aviation system wahitimu waliotoka katika vyuo vyetu vikuu. Mara ya mwisho kufanyika jambo hili ilikuwa ni wakati wa uongozi wa Mzee Mwapachu ambapo ali-recruit wahitimu kadhaa kwenye maeneo mbalimbali ndani ya ATC.
Leo hii tunapojadiliana hapa, ATCL inayo sera ya job succession lakini haitekelezwi kwa sababu moja kubwa uwezo mzima wa kiutendaji, nobody anayekumbuka kufanya hayo. Leo hii bila ya kufanya mabadiliko ya muhimu, nobody will be attracted to join ATCL kwani it is hard to predict what will be next.
 
Kweli maneno yako mkuu, kuhusu ticket mkuu wangu kulingana na mazingira yetu tumebanwa kutumia mashirika mama.. lakini hata hivyo mbona zipo agencies kibao zinakata tickets? tumeasha anza kufanya hivyo kwa mnini tusihakikishe mpango huo unawezekana kabisa..Tukianza na shirika letu wenyewe pamoja na Precision Air..
Kuhusiana na Mwapachu mkuu wangu tunahitaji bado watu walioweza kufanikisha watupe busara zinazoambatana na biashara hii. Shirika la ndege ni biashara ngumu sana, ngumu kuliko usafiri wa aina yoyote ile hivyo inputs ni muhimu sana sio lazima awe active ktk kuendesha shughuli za shirika. Anaweza kuwa mwenyekiti tu wa board na CEO (nafasi moja) akatoka hata nje, kuna wakati tukubali kujifunza ili kufanikisha kitu fulani..experience ni muhimu sana kuliko elimu ktk utawala wakati mwingine..

Hawa maajenti wa kuuza tiketi ni sehemu tu ya kimkakati lakini in future hawa jamaa watapungua sana kwani hata biashara wanavyofanya sasa itabidi wabadilike. mauzo mengi yatafanywa na wale agents watakaokuwa na uwezo mubwa wa kifedha wa kuwekeza kati miundo mbinu ya internet. Kwa mfano hapo zamani ulikuwa kama unataka kusafiri na ATC ukikata tiketi kwa agent unapata tiketi halisi ya ATC, baadae ulipoanza mfumo wa Bank Settlement Plan ambapo zinatumika universal tiketi kwa wasafirishaji wote, baadhi ya maajenti hawakuweza kuingia huko ama kwa kukosa sifa au kutoweza kuweka deposit gurantee katika benki. Halikadhalika tukifika katika hatua ya total paperless tickets nadhani wataendelea kupungua zaidi.
Kwangu mimi naona Mwapachu can do more than kuwa mwenyekiti wa board. Ninafikiri kuwa anaweza kuwa katika Presidential advisory capacity ambapo ataweza kumshauri Rais au serikali zaidi ya mambo ya ndege. Kwa mfano katika sakata zilizojitokeza ndani ya ATCL tangu SAA iliponunua hisa, mahujaji, ukodishaji wa ndege na hadi hili la kusimamishwa kuruka, nina hakika kama huyu Mzee na wazee wenzake wengine wangeombwa kumshauri Rais nadhani tungekuwa tunaongea mambo mengine sasa hivi.
Lakini hata ningependa kutoa changamoto kwa vyombo vyetu vya habari vipige hatua walau moja mbele kwa kutafuta maoni tofauti kutoka kwa wataalam mbalimbali hasa pale kunapokuwa na burning issue. Kwa mfano, katika matatizo ya ATCL tungependa kusikia wataalam mbalimbali wa aviation, uchumi nk wanasema nini juu ya kadhia iliyoikuta ATCL. Kwa kufanya hivyo kuna wapa nafasi wananchi wa kawaida kujua walau kwa kiasi fulani ni nini labda mbadala wa hali iliyokuwepo. Kwa kufanya hivyo pia huongeza wigo wa majadiliano baina ya wananchi kwa wananchi. Hii njia is more effective katika kutoa elimu ya umma kwa wananchi.
Nitakupa mfano mmoja japokuwa ninatoka kidogo nje ya mada, mara nyingi tumekuwa tukilalamika ni jinsi gani wananchi wataelimishwa juu ya kutumia haki zao katika kupiga kura bila ya kushawishiwa visivyo au ni namna gani elimu kwa wananchi itatolewa ili watambue haki zao ni zipi na hawastahili kutoa rushwa.
Sasa vyombo vyetu vingi vya habari vimegeuka kuwa ni kama vile vyombo vya kimagharibi ambavyo vinaandika yale ambayo wanayataka wasomaji wayasome na si yale ambayo wananchi au wasomaji wanatakiwa kuyasoma.
Ninamalizia kwa kusema kuwa mabadiliko katika nchi yetu si kwenye siasa na uchumi kama ambavyo wengi wanafikiria hivyo bali pia vyombo vya habari inabidi vibadilike viwatumikie wananchi zaidi kuliko vinavyofanya sasa hivi.
 
Pundamilia,
maneno yako msumari mkuu wangu hapa kula zako 5..

Kuna kitu nilitaka kukiongezea tu kuhusu Watu na Mazingira..mtanisamehe natoka nje ya mada kwa sababu inauma sana kusikia ATCL inatarajia kuruka hivi karibuni na hakuna mabadiliko yoyote zaidi kuwa bailed out, with no string attached to it!..ATCL bado ni shirika la serikali hivyo siasa juu ya biashara kama kawa... imefunika!

Unajua mkuu wangu sisi waafrika na hasa Watanzania tuna kasoro moja kubwa sana ya URITHI..
Sisi ni watu ambao urithi tunauchukulia kama vile ni radhi ya mzazi kiasi kwamba mzazi anaweza kwenda kaburini hakumrithisha mtu au kumrithisha mtu wa nje kabisa maadam tu awakomoe watoto na ule msomo Na wewe tafuta za kwako!..
Wazee wetu hata kuandika Urithi (Will) hawataki kwa sababu sio mila yetu na pia kwao will ndio kwanza kutabiriana mauti.
Hivyo utamkuta mzee ana mali, tuseme tajiri kwa kuagiza vipuri toka nje lakini contact zote anazo yeye mwenyewe, mwanaye wa kumzaa hajui baba yake anaunganisha vipi biashara zake zaidi ya kukaa dukani kuuza mali zile..Ukimuuliza mzee jibu utakalo pewa ni bora usingeuliza..Kikubwa wanachoweza kusema ni kujisifia jinsi wao walivyoweza kufika pale walipofika kuwa wame suffer kichenzi.. Now, jiulize wali suffer kwa ajili gani hakuna zaidi ya maisha yao wenyewe as individual..hivyo vita yake kupata mafanikio inaishia pale yeye alipokuwa tajiri..Bila wao kufahamu au wasijali kitu kuwa at the end of their life, wakisha kufa mali zao hupotea na pengine ndugu, marafiki na jamaa kugombania mali zile kama pilau la msibani.

Ni ktk mtazamo kama huu nimeona hata Uongozi wa nchi zetu umekuwa ktk mila na desturi kama hizi. Kuna fundo la kimeo kati ya wazazi (viongozi) wetu ambalo sifahamu limetokana na kitu gani.. sijui kama ni roho ya kwa Nini!...au pengine umaskini wa hali na mali ndio umechangia zaidi..
Kuna watu hunambia pengine Tanzania tulipata Uhuru haraka sana kabla hatujawa na wataalam wa kutosha kuweza kuendesha mali zetu lakini binafsi sidhani kuwa hii ni sababu ya msingi... Kwani walimu wetu walitakiwa kuwa wazazi wetu wenyewe sio Mkoloni..
Tazama nchi kama South Afrika, Zimbabwe, Msumbiji na nchi nyingine zilizotawaliwa kwa muda mrefu bado kunamatatizo makubwa ya Utawala wa mtu mweusi unaposhika nchi..hawa wenzetu wametawaliwa zaidi ya miaka 500 lakini ngozi nyeusi ilipokamata tu chumi za nchi hizo zimeyumba au kuporomoka...
Sasa hujiuliza ingetuchukua sisi miaka mingapi chini ya Ukoloni ili sisi tufikie uwezo mkubwa wa kitaalam na nidhamu ya kazi na kuwa responsible..Jibu la haraka ni kwamba hata kama ingechukua karne 1000, tusingeweza kitu kwa sababu Uhuru wetu ni sawa na mtumwa aliyeachiwa huru ghafla bila kujiandaa na dunia ya nje, hivyo haijalishi ni miaka mingapi mtumwa huyo alikuwa katika Utumwa iwe mwaka au karne nzima isipokuwa transition ya mtumwa huyo ndiyo Muhimu sana katika kumwezesha mtumwa huyo kuhimili ya dunia hiyo anayokwenda...

Ni imani yangu kuwa Wamarekani weusi pamoja na kwamba wamechukua miaka mingi kufika uhuru waliokuwa nao leo au niseme hapa walipo lakini kuna kheri nyingi zimetokana na slow transition ya haki zao hatua kwa hatua.. Kwanza Uhuru wa US, kisha utumwa, ukafuata ubagulizi wa rangi -social integration..wakapigania haki za msingi kama elimu, afya, usafiri, makazi na all human rights ambazo kwa nguvu ya kutafuta haki hizo waliweza kupandikiza fikra na urithi wa wazazi wao.
Fikra toka kila hatua ya mapambanoo yao...Toka Du Bois, Fredrick Douglas hadi kina MLK, Malcom X, Kunta Kinte ni historia ambazo zimekuwa honoured na passed through generations hadi leo hii wana viongozi kama Obama..Every step forward kulikuwa na hatua in stages tofauti na sisi tulipotaka Uhuru tu tukapewa kama yule mtumwa..Hivyo aidha hatukujua tufanye nini na Uhuru huo ama ndio yale yale ambayo mimi husema kuwa ni Sinia la Pilau siku ya Kisomo (Hitma).. nikiwa na maana watu wenye njaa ukiwawekea sinia la Pilau pamoja na kwamba siku hiyo ni ya huzuni kubwa ya kufiwa (Hitma) utashangaa watakavyo weza gombania matonge na hakuna utaratibu wowote ule unaoweza kutumika kuwapunguza kazi hawa watu...Pale kila mtu na mzigo wake..

Hii ndiyo hofu yangu kubwa sana na taifa letu, sio tu kwa kuitazama ATCL bali utawala mzima wa nchi yetu(zetu)..Hatuna role model, watu kama Nyerere leo hii tayari tumekwisha watafutia mabaya yao. Kina Mkwawa, Mirambo, Mangi Sina na wengineo, hawa wote tuna taarifa nyingi za mabaya yao kuliko mazuri kuhusu historia za maisha yao, fikra zao na kadhalika.. Yote mazuri yamekuwa kuwa flushed na tutabishana sisi wenyewe utafikiri hatuna akili..matokeo yake leo hii hatuna wa kumtazama kama mfano bora isipokuwa Western World (wazungu) na mashujaa wake..
Mashujaa tuliokuwa nao (wanaotambulika) ni watu waliopanda mlima sijui Mt. Kilimanjaro, kukimbiza mwenge, waliotembea kwa miguu kuunga mkono Azimio la Arusha na mengine mengi ambayo kusema kweli hayamsaidii mrithi Mdanganyika aliyezaliwa ktk Umaskini. Haimuingii akilini huo Mlima au mwnge utaweza vipi kuondoa njaa yake ama kumpa tumaini la kesho kuwa mbora kati ya wabora..

Mkuu wangu inasikitisha sana, na hasa pale napoona kuna uwezekano mkubwa wa nchi yetu kwenda mbele lakini tunarudi nyuma kwa sababu We have no history, no one or nothing to look up to!..except Abroad..Na utamaduni wetu umekuwa kikwazo cha maendeleo yetu na yawezekana kabisa adui mkubwa wa maendeleio ya Mtanzania ni Mtanzania mwenyewe..Yaani Umaskini ndio adui mkubwa wa Umaskini..

Siasa za kuokoteza na kupachika kama viraka ndizo zimekuwa muundo wa fikra za Mdanganyika..It's about Mtumwa na Nyapala na kila maamuzi ya kitaifa utaona ni vitu ambavyo zinakuwa forced to the society.. Leo, Mama Clinton ameapishwa lakini umeona cha moto amekipata kutokana na Mumewe kuwa na NGO yake..Hakuapishwa bila kupitiwa na baraza la nchi hiyo..Sisi ndio kwanza mtu akichaguliwa na rais basi kapita na he become untouchables the very first day!..

I hope, Kikwete ataweza kuyasikia maoni yako na pengine kujaribu mwongozo mpya wa Taifa letu.. na wananchi wenyewe kujielemisha zaidi ktk ujenzi wa Taifa letu kwa kuelewa mapungufu yetu.. Badala ya kwenda kujifunza kuendesha baiskeli (Elimu yetu) tujifunze kutengeneza baiskeli..hata tukianza na zile spokes au baiskeli inayorudi nyuma..Kwa sababu nimechoka na elimu zetu tunapojisifia kuendesha baiskeli, jambo ambalo kusema kweli sio elimu isipokuwa ni mazoea tu..
 
Mkuu Mkandara,
Hii posting yako ya mwisho japokuwa imekwenda nje ya mada kama ambavyo ulivyoanza kwa kutanabahisha, imenibidi niirudie mara kadhaa ili ujumbe unikae vizuri. Ni makala nzuri ambayo imelenga kabisa kwenye fikra zangu nilizozijenga kutokana na hali halisi ya nchi yetu hasa nikiangalia historia nzima kabla na baada ya uhuru. Kama ambavyo niliandika huko nyuma kuwa siwalaumu wale waliopewa nyadhifa kipindi cha nyuma hasa pale mara baada ya kupata uhuru kwani hatukuwa na budi kuendesha nchi yetu wenyewe kwa hali yeyote. Kwa hiyo basi yeyote aliyeonekana atamudu kazi alipewa wakati mwingine bila ya kujali kama ana uwezo wa kitaaluma kwenye eneo alilokabidhiwa kufanya kazi au la.

Matatizo ya Tanzania hayawezi kutatuliwa na viongozi au kundi fulani la watu, matatizo yetu yatatatuliwa na sisi wenyewe. Kadri tunavyoona kuwa hali ya matatizo ya mtanzania yanavyoongezeka, maana yake ni kwamba hatuyakabili matatizo yetu, tunayaacha yaendelee kukua huku tukibweteka kwamba kuna mtu atakuja kututatulia shida zetu. Mimi siamini kuwa tukisha chagua viongozi labda wabunge na Rais basi kazi yetu imekwisha, la hasha, hawa waheshimiwa tunatakiwa kuwatumia kuhakikisha kazi zao wanazozifanya zinaendana na yale ambayo sisi tunataka. Ifike wakati hawa waheshimiwa waelewe kuwa misperformance yao maana yake ni kutokurudi kwenye ofisi wanazozishikilia. Ninasema hivi kwa maana halisi kuwa sisi wananchi tunawajibika moja kwa moja na matatizo ya nchi yetu na wala si viongozi (pekee yao). Tunaona mambo yanakwenda ndivyo sivyo hatuchukui hatua zipasazo badala yake tunarusha lawama tu kwa watu ambao wanajua fika udhaifu wetu kwamba hatuwachukulii hatua zozote.

Mimi siku zote nimekuwa na mawazo kwamba wananchi katika grass root levels waweze kujenga communities zao (non-political communities) ambazo zita-focus kwenye kushughulia kwanza yale matatizo yaliyowazunguka. Kwa kufanya hivyo itakuwa ni rahisi kupanua wigo wa shughuli za kijamii katika society zetu hatimaye kujenga uwezo ambao utasimamia kazi za wanasiasa katika kutumikia nchi. Nadhani kama communities zitakuwa na nguvu ya kutosha nina hakika kuwa viongozi wa kweli wakuwatumikia wananchi watajulikana na kutoka huko.

Mimi sifurahishwi hata kidogo na mfumo wetu wa siasa hasa wanasiasa wetu kwa jinsi ambavyo wanatumia muda mwingi kujinufaisha kiuchumi na kisiasa bila ya kujali kuwa wajibu wao kwa jamii ni nini. Nimewahi kukutana na viongozi mbalimbali ikiwemo baadhi ya wabunge na wanasiasa wa upinzani. Jambo ambalo nimeliona kuwa ni common kwa wengi wao ni kuwa hawako in touch na matatizo ya wananchi sana zaidi ya kuwa wanaangalia ni jambo gani afanye ili 'wapiga kura wasimpigie kelele' au jambo litakalompa credit ya kisiasa machoni mwa watu. Pia wengi wao unapoji-engage kwenye mazungumzo yanayoongelea matatizo ya kawaida kwenye jamii wengi wao huwa hawako aware kabisa au huona kuwa hilo jambo ni dogo na pengine halina umuhimu kwao. Sasa haya yote yanafanyika just because hakuna watu au mfumo wa kuwa-push hawa waheshimiwa waweze kufanya kazi kwa ufanisi.

Mimi ninashauri watanzania mbalimbali popote walipo wajaribu kuongelea ni kwa jinsi gani wananchi wataweza kujijengea uwezo wa kutatua matatizo yao. Siamini mbinu za kupandikiza chuki miongoni mwa wananchi au kuwagawa kwa namna yeyote ile kama ni njia mwafaka ya kutatua matatizo yetu zaidi ya kupandikiza chuki ambayo hatujui itaota mizizi kwa kiasi gani.

Hili la ATCL kusema kweli sitaacha kuliongelea pale itakapobidi kwa sababu ninaona kuwa ni wajibu wangu kufanya hivyo kwa manufaa ya watanzania wote, LAKINI, kwa vile nina heshimu serikali iliyoko madarakani, na ninamheshimu Rais, I do also respect his decision on ATCL in anticipation that amesikia what we said kwa muda wote tulipotoa maoni yetu mbalimbali. I believe maamuzi yake yamezingatia maoni yetu pia hata kama kuna pale tunapoona kuwa yametofautiana na ya kwetu. Lakini kubwa zaidi I bank on Mh Rais alichokifanya ni sehemu tu ya kutatua matatizo ya ATCL, ninategemea tutamwona akiendelea kutatua au kurekebisha matatizo mengine yaliyobaki ndani ya ATCL.
 
Last edited:
great news
Atcl reshuffle
NEW DIRECTOR OF OPERATION --JOSEPH IBANDA
CFO:::Eliasaphew kukabidhi ofisi jumatatu
MSHAURI WA CEO ---MARK MANJI OUT
WENGI KUBADILISHWA JUMATATU...., HABARI HII NIMEISIKIA HUKU MABOXIN LEO MCHANA JAMANI MWENYE NEWS ZAIDI ATULETEE TUCHAMBUE...ILA MI NASHAURI HAWA WASIACHWE WAPELEKWE ""THE HAGUE"" kwa hakimu MWAKANJILE....nafikiri hatuitaji ushaidi wakati kila kitu kipo open....

Atakaebaki tuna uhakika atakuwa na adabu kama si NUSU basi NZIMA

POLEN NA TUNAWATAKIA KILA LA KHERI ATCL KURUKA
 
1. Government buy shares in Precision, (luckily going into stock market) plus other TZ coys eg coastal travel, community airlines
2. Dissolve ATC
3. Make ATC assets available to the New National Airline

This is by far the most feasible solution to ATC malaise
 
kwako mwanakijiji,
ATCL haijapata faida yeyote for the past 10 years ni nani leo hii atakakubali kuwekeza pesa yake kwenye kampuni yenye track record kama hiyo na mengi ya madeni yake ni fraud ambayo asilimia kubwa zimesababishwa na wakubwa haohao. ni serikali ya watu wasiojuwa uchumi kama JK ndio wanaoweza kutumbikiza pesa za walipa kodi ndani ya ATCL, JK mwenyewe ukimwambia atoe pesa yake ya mfukoni awekeze ndani ya ATCL jibu lake litakuwa ni BIG NO, Anatoa pesa kwa ATCL kwa sababu ni pesa za walipa kodi na si za kwake kumbuka ni raisi sana ku take risk na pesa za wengine na si zakwako mwenyewe. kampuni. ATCL IS WORTHLESS ukilinganisha madeni na thamani yake na ndio maana TZ ikarudishiwa kwa thamani ya dola moja. hakuna mtu atayekubali kununua kitu ambacho ni worthless.
nini kifanyike,

1. serikali ijitoe na kuchukua deni lote na kuwashugulikia wahusika wote wa ubadhirifu kurudisha pesa zao.
2. watu binafsi wauziwe shirika baada ya kufutiwa deni na kupewa tax exemption ya miaka 10 based on profit kuwaacha wachukue nafasi.
3. likianza kutengeneza faida wataweza kuhuza shea zao kirahisi kwa maana watu wananunua shea kwa sababu kubwa nayo ni dividend.
4. wahusika wasikubali shea zozote za serikali unless serikali ikubali kuwa haitakuwa na influence yeyote ktk kutoa maamuzi ili kuepusha siasa kuendesha kampuni kama wanavyofanya hivi sasa.
 
kwako mwanakijiji,
ATCL haijapata faida yeyote for the past 10 years ni nani leo hii atakakubali kuwekeza pesa yake kwenye kampuni yenye track record kama hiyo na mengi ya madeni yake ni fraud ambayo asilimia kubwa zimesababishwa na wakubwa haohao. ni serikali ya watu wasiojuwa uchumi kama JK ndio wanaoweza kutumbikiza pesa za walipa kodi ndani ya ATCL, JK mwenyewe ukimwambia atoe pesa yake ya mfukoni awekeze ndani ya ATCL jibu lake litakuwa ni BIG NO, Anatoa pesa kwa ATCL kwa sababu ni pesa za walipa kodi na si za kwake kumbuka ni raisi sana ku take risk na pesa za wengine na si zakwako mwenyewe. kampuni. ATCL IS WORTHLESS ukilinganisha madeni na thamani yake na ndio maana TZ ikarudishiwa kwa thamani ya dola moja. hakuna mtu atayekubali kununua kitu ambacho ni worthless.
nini kifanyike,

1. serikali ijitoe na kuchukua deni lote na kuwashugulikia wahusika wote wa ubadhirifu kurudisha pesa zao.
2. watu binafsi wauziwe shirika baada ya kufutiwa deni na kupewa tax exemption ya miaka 10 based on profit kuwaacha wachukue nafasi.
3. likianza kutengeneza faida wataweza kuhuza shea zao kirahisi kwa maana watu wananunua shea kwa sababu kubwa nayo ni dividend.
4. wahusika wasikubali shea zozote za serikali unless serikali ikubali kuwa haitakuwa na influence yeyote ktk kutoa maamuzi ili kuepusha siasa kuendesha kampuni kama wanavyofanya hivi sasa.
 
Im with you. No way the Government can compete in the airline industry, no way!!

Let us revisit the structure of major airlines in aviation industry in the world. I will sight few examples for the purpose of this discussion. KLM, BA,EMIRATE,AA,ETHIPIA, are perceived by many as state owned cooperation. The matter of fact, these are private owned companies which have been given the status of National flag bearers.The states owned coop,which I could call '' owned by nobody'' cannot compete in this era of free market and globalization. Even those countries which still believe in state ownership, are facing the difficult times to run the business effectively.
Point no. 1-12 [refer original post] are not the real problems facing the ATCL. Those are the measures supposed to be taken to make the already functional airline more profitable.
The problem with ATCL is not capital, as we have seen times and again, our government has injected billions of dollars, in the end the capital is flushed in the toilet by the elites best known as Board members and CEO's. In a rotten country like ours, the managerial position is not based on technical know how rather technical know who! All positions are appointed by the president, no wonder this is an opportunity for the retiree to make up for the last.
In this context, categorically I would say,the main problem facing the ATCL is Management. In order to have effective management team the ATCL should be privatized and share floated to the public and Investors, the likes of Kenya Airline. The independent Management will pave a way to fix all problems facing the ATCL.
Remember the CEO's of all major airlines are hired through a serious vetting process regardless of their nationality or ethnicity. The candidate must prove beyond doubt their ability to run the airline with proven track record,unlike our shoddy system which allows President to appoint the unqualified individuals failed many organizations in the past. It is not too late to borrow the leaf from others, Kenya Airways so as to speak.
''Management! Management! Management!''
 
Mawazo ni mazuri,lakini bado ni jukumu la mliki yaani serikali kufanya maamuzi sahihi kwa muda sahihi,vinginevyo itakuwa ni gharama kuifufua au kuiuza kwa aina yoyote.Shirika lina madeni makubwa mno,ndege zake ni za zamani mno,na ni ndogo kufanya international freights.Tatizo jingine linaendeshwa kwa mazoea tu,sio kwa ushindani wa kibiashara.ATC its not economy viable alimvutii mwelekezaji yeyote makini,sana ni zile njia ambazo ATC inazitumia tu.Ni kulitangaza mufirisi likaundwa shirika jipya kwa mtaji mpya,Serikali ,wanahisa wazalendo,na waelekezaji kutoka mashirika mengine ya ndege.Ni jukumu la serikali kuboresha miundo mbinu ya viwanja vyetu,zima moto, paramedical sevices, vyombo vya kuongoza safari za ndege,umeme wa uhakika, kwa kiwango cha mataifa.Tusione vyaelea vinaudwa na watu makini.
 
Huwa najiuliza sana iweje kufufuka kwa ATCL kumekuwa kero kwa baadhi yetu?
 
Back
Top Bottom