How Air Tanzania Should be Restructured

How Air Tanzania Should be Restructured

Pundamilia07,
Mkuu yote sawa...nimepiga simu ofisi ya British Airways hapa wamenambia ticket wana issue ONLY to Dar - Tanzania..siwezi kufikishwa Mwanza kwa sababu hakuna member wa timu yao anayekwenda huko...
Kwa maelezo zaidi kuhusiana na connection kanambia wanaweza tu kunisafirisha ikiwa kuna mashirika ambayo ni franchise yao, ni codeshare partners wao pia kikubwa zaidi ni member wa network ya ushirikiano (Airlines Allience) ambayo shirika linatakiwa kuwa member au subsidiary wake kunifikisha Mwanza..Sasa sielewi kinachoendelea kama kanifunga kamba sijui lakini majibu yake ndio hayo siwezi kupata ticket moja hadi Mwanza - Tanzania.

Ni wazi kabisa hayo maelezo sahihi kwani nilichoandika ndiyo sahihi na wala hakihitaji nyongeza. Lakini pia inategemea jibu ulilolipata lilitokana na swali gani ulilouliza. Anyway let me give you benefit of doubt kwamba BA hawezi kukata ticket kwa sector ya Mwanza kwasababu ATCL imesimamishwa uanachama wa IATA, lakini pia siyo sababu kubwa sana ya kufanya abiria asifike Mwanza, kwani katika reservation system Precision Air mwanachama wa IATA anakwenda Mwanza. Kama nilivyosema hapo juu kuwa majibu hutegemea na swali lilivyoulizwa.


Mkuu, hizo hesabu za asilimia 70 ya wasafiri wa ndege kwenda nje unafikira nimetunga!..Hata hivyo haiusiani kabisa na ATCL isipokuwa ni hesabu ambayo nimeipata toka chombo cha serikali hivyo siwezi kuiweka kama unavyodai kwa sababu sikuipata toka site fulani..
Nachokuomba chukulia kuwa ni kweli

Takwimu ni kitu muhimu sana hasa pale tunapojenga hoja. Kama nilivyoandika hapo awali kwa vile source ya data hizo ni 'unknown' siweza kuzikata wala kuzikubali.


na jaribu kuangalia jinsi gani ATCL inaweza kufanya kazi zaidi kwa kushirikiana na mashirka kama Emirates kwa sababu nilizoandika mwanzoni..USHIRIKIANO . Iwe kwa kununua hisa, iwe kwa Ubia, iwe kujiunga na Allience yote kwangu ni sawa maadam tunaweza kusafirisha abiria wetu toka Mwanza< Bukoba moja kwa moja kwenda nje with a connection Dar au Kili..

Mkuu wangu Mashirika yote makubwa duniani mbali na ku run international flights yana mashirika madogo yanayo run ndani ya nchi zao iwe Uingereza, France, Japan au America na kuna ushirikiano kmkubwa kati ya shirika mama (International) pamoja na hilo la ndani (Local).. huwezi kuchukua Air Canada kuja Toronto au Vancouver ukaunganisha na shirika lolote la ndani ati maadam kuna ndege inakwenda huko..


Ushauri wangu juu ya hili ni kuwa ukombozi wa ATCL hautategemea kujiunga na mashirika makubwa, kinachotakiwa hapa ni ATCL isafishe nyumba yake na kujenga uwezo kwanza wa soko la ndani na Region kabla haijajiingiza kwenye International market. Wakiweza kufanya vema kwenye soko la ndani na Region then watakuwa attractive kiasi cha kuweza kuwavuta washirika wakubwa kufanya nao biashara. Ikiwa ATCL haijimudu katika soko la ndani sitegemei kama mashirika makubwa uliyoyataja yatakuwa na haja ya kufanya kazi na ATCL. Nafasi ya ATCL kufanya vizuri ndani na Region ipo kubwa sana japokuwa Kenya Airways atampa upinzani usoepukika kwa kutumia tool yake aliyoiweka ndani ya nchi yetu yaani Precision Air.


Hata hivyo, tumeongea vya kutosha na ushauri wangu kwa serikali yetu ni kuliokoa shirika hili lakini badala ya kuliwekea regulations, wakati umefika sisi tuondoe hizo regulations ambazo hazihusiani kabisa na Policies zaidi ya kuwepo mkono wa serikali ndani ya Uongozi wa chombo hicho..ATCL iwe huru (public private company) na viongozi wake WAPYA wapewe nguvu ya kuwa Responsible na Accountable..

Mimi pamoja na kuwa siyo msemaji wa serikali, lakini nia kubwa ya serikali ni kuona kuwa katika nchi hii ATCL inaendelea kuwa mhimili mkubwa au muhimu katika kuendeleza sekta ya anga. Kwa hiyo basi kitendo chochote cha serikali kuiwacha ATCL isiweze kuendelea na shughuli zake ni sawasawa na kujitega yenyewe.
Serikali inataka kuwa na Airline ambayo itakuwa profitable na ikibidi hapo mbeleni serikali ibakize hisa chache tu na kuwacha sehemu nyingine imilikiwe na strategic partners na umma kwa ujumla. Endapo ATCL itakuwa katika misingi mizuri ni wazi kabisa faida zitokanazo na uwepo wake ni nyingi na zenye manufaa kwa taifa kuanzia employment, utaalam kwenye sekta hiyo, kodi za serikali nk.
Serikali kama mwenye hisa 100% ni wazi ndiye mwenye kauli ya mwisho na hatima ya ATCL kwa hiyo kama ilivyo kwa mwenye mali yeyote ana uamuzi wa kufanya lile ambalo anaona lina manufaa kwake. Haitakuwa rahisi na sawia kuikataza serikali isiisimamie ATCL ilhali yenyewe ndiyo mmiliki wake na inataratibu zake za kuendesha mambo yake. Kama imeamua kuunda tume, basi hayo ndiyo matakwa yake, cha msingi ni kuangalia hii tume imeagizwa nini. Kwa maoni yangu binafsi terms of reference za tume ni sahihi na tume kuwepo pia ni sahihi. Ni vizuri tupate kujua inside ya matatizo ya ATCL zaidi ya haya ambayo tunayajua, tuvute subira tutoe maoni yetu na nina hakika tume inayaona na kuyapima kwa uzito wake kwa maana na wao pia katika utendaji wao wanasikiliza public reactions.


Mengi nilikwisha andika huko nyuma ni jinsi gani ninaona inafaa kufanyika juu ya kuiunda ATCL mpya mnaweza kurudia kusoma na kuchangia pale mnapoona inafaa.

Bottom line ni kuwa ATCL ijengwe na kuendeshwa katika misingi ya biashara ilivyo sasa na wala si katika hali ya kufikirika.

For more information unaweza kunipata katika pundamilia@rocketmail.com
---------------------------------------------------------------------
 
Last edited:
Hapana mkuu wangu haikuhusiana na ATCL kusimamishwa hata kidogo.. Kama ingewezekana basi Precision wanakwenda Mwanza angenambia wanaweza kunipa ticket from TO - London - Dar -Mwanza na kurudi - Kweli nataka kusafiri na niliposoma maelezo yako ilikuwa kama umeniamsha!..

Ni mazungumzo ya muda mrefu nimeongea naye na kanambia UPO ushirikiano mkubwa sana baina na mashirika ya ndege na ndio maana unaona connection zinajulikana hata nje..ndege na flight zinapangwa kutokana na abiria wanaotegemewa na kadhalika pia tukumbuke kuwa kila ndege ina nauli zake wakitumia hata fedha local hivyo ni lazima kuwepo na makubaliano kabla hujabeba/ kusubiri ndege au abiria wa mtu..Anyway story ndefu ya nini wakati swala ni ATCL..

Mifano hiyo yote ya ushirikiano kanipa kutokana na maswali yangu.. Mkuu unajua nikisha simama ktk ubishi na hata nimekutumia wewe kumwambia mbona nimeambiwa inawezekana!..jibu la mwisho haiwezekani isipokuwa naweza kwenda hadi Dar na schedule wanayo lakini hawezi kunihakikishia usafiri wa Mwanza kwa sababu hana data zake wala hakuna ushirikiano na shirika la huko bila kulitaja shirika la ATCL ambalo yeye halijui kama lipo wala ni Airline gani zinafanya kazi TZ.
 
Hapana mkuu wangu haikuhusiana na ATCL kusimamishwa hata kidogo.. Kama ingewezekana basi Precision wanakwenda Mwanza angenambia wanaweza kunipa ticket from TO - London - Dar -Mwanza na kurudi - Kweli nataka kusafiri na niliposoma maelezo yako ilikuwa kama umeniamsha!..

Ni mazungumzo ya muda mrefu nimeongea naye na kanambia UPO ushirikiano mkubwa sana baina na mashirika ya ndege na ndio maana unaona connection zinajulikana hata nje..ndege na flight zinapangwa kutokana na abiria wanaotegemewa na kadhalika pia tukumbuke kuwa kila ndege ina nauli zake wakitumia hata fedha local hivyo ni lazima kuwepo na makubaliano kabla hujabeba/ kusubiri ndege au abiria wa mtu..Anyway story ndefu ya nini wakati swala ni ATCL..

Mifano hiyo yote ya ushirikiano kanipa kutokana na maswali yangu.. Mkuu unajua nikisha simama ktk ubishi na hata nimekutumia wewe kumwambia mbona nimeambiwa inawezekana!..jibu la mwisho haiwezekani isipokuwa naweza kwenda hadi Dar na schedule wanayo lakini hawezi kunihakikishia usafiri wa Mwanza kwa sababu hana data zake wala hakuna ushirikiano na shirika la huko bila kulitaja shirika la ATCL ambalo yeye halijui kama lipo wala ni Airline gani zinafanya kazi TZ.

Mkandara,

Huenda umeoongea na kanjanja, hebu muulize anatumia mtandao gani wa reservations? Galileo au Amadeus? halafu mueleze akutafutie careers/operators katika route ya DAR-MWZ kama hataona hapo basi umeuliza a wrong person.

Pili, unapokata ticket katika route ya DAR-MWZ fare yake inaonekana katika hiyo reservation system kuwa ni kiasi gani. Abiria abiria anaweza kulipa nauli yake hukohuko alipo kwa kutumia currrency inayotumia kwenye nchi ambayo ni equivalent na ile inayooneshwa katika reservation system. Masuala ya kuconvert hufanyika IATA Clearing House baada career ku-bill aliyepokea pesa.
 
Well, Mkuu alichonambia ni kwamba BA itanifikisha Dar.. Mwanza haiwezekani hana connection na nilipotumia maelezo yako ndipo aliponipa hizo habari za franchise, codeshare partners na Allience kati ya mashirika ya ndege hakugusia kabisa IATA kuhusika na uwezekano wangu kufika Mwanza.
Kama nilikuelewa IATA inahusiana na malipo yaani fedha na ndio maana nikasema hiyo clearance ni sawa na benki sio mpangaji wa ushirikiano wa mashirika ya ndege..
Hata hivyo, nitajaribu na Agencies wengine maanake nilizungumza kwa simu na BA wenyewe...sijui wanatumia mtandao gani lakini ofisi yao iko Airport.
 
Zakumi,
Bahati mbaya sana katika nchi yetu kumekuwa na utamaduni wa diagnosis ya matatizo na hatimaye prescription kutolewa na "tume".Sijaelewa hasa mantiki ya utaratibu huu maana ni wazi kabisa kuwa matatizo ya ATC hayahitaji uvae miwani uyaone na kuyaelewa.Major prob ni management period.Kwanini hawaondolewi mara moja ( board na management) its very hard to comprehend.
Kama ulivyosema vema,uendeshaji wa biashara hii kwa miaka hii unahitaji watu wapya wenye mtizamo mpya wa jinsi ya kufanya mambo.Ukiangalia walioko katika kuendesha ATC ni watu wenye fikra na mtizamo wa 1947! wengi wao hawajawahi kuwa good performers mahali popote.If anything wamewahi kuwaangusha sana watanzania. Itakuwa ngumu.

Management, Management, Management

Kuna uwezekano mkubwa matatizo ya uongozi yanatokana na schoolarship zetu na utamaduni tuliokuwa nao.

Katika mji ninaoishi kuna jumuia nyingi za kitanzania. Lakini hakuna hata moja naweza kusema iliyokuwa na mafanikio.

Jumuia nyingi zinaanzishwa na sherehe kubwa na zinapotea bila kuelewa zimepotelea wapi. Na baada ya kupita muda fulani wengine watazifufua na kuziacha tena kufa.

Nilihamua kufanyia utafiti wa kufa hizi jumuia. Nilichogundua ni kuwa miundo ya jumuia hizi ni sawa kabisa. Kutakuwepo na Mwenyekiti, Makamu, katibu na kamati zenye wenyeviti na makatibu.

Na miundo hii inafanana kabisa na miundo ya jumuia nilizoziona Tanzania nikiwa shuleni au vyuoni. Ni copycat ya TANU/CCM na jumuia zake. Hakuna innovation yoyote.

Kwa maoni yangu binafsi yanayotokea ATC ni-reflection yetu. Kwa miaka mingi tumefananisha siasa na uongozi. Tumefaninisha usemaji wa maneno mengi na utendaji.

Pale tutakapokubali kuwa management ni art yenye kutumia innovation hatutakwenda mbali. Tutaendelea kufanya kazi kwa utamaduni uliopo sasa.
 
Well, Mkuu alichonambia ni kwamba BA itanifikisha Dar.. Mwanza haiwezekani hana connection na nilipotumia maelezo yako ndipo aliponipa hizo habari za franchise, codeshare partners na Allience kati ya mashirika ya ndege hakugusia kabisa IATA kuhusika na uwezekano wangu kufika Mwanza.
Kama nilikuelewa IATA inahusiana na malipo yaani fedha na ndio maana nikasema hiyo clearance ni sawa na benki sio mpangaji wa ushirikiano wa mashirika ya ndege..
Hata hivyo, nitajaribu na Agencies wengine maanake nilizungumza na BA wenyewe...sijui wanatumia mtandao gani lakini ofisi yao iko Airport.

Mkuu Mkandara,

Ninazielewa taratibu zinazotumika katika safari za anga kikamilifu. Ninachangia nikiwa na uzoefu wa kutosha kuweza kuelimishana kupitia katika forum hii. Ninajua siwezi kuwa mchangiaji bora katika masuala yanayohusu utabibu, military nk lakini katika hili ninaweza kuchangia kwa kina.
 
Well, sijasema huna uzoefu, as a fact mimi ndio kabuntas ktk maswala ya ndege na taratibu zake na ndio maana nimeuliza kuhusu usafiri wangu kutoka hapa nilipo kwenda Mwanza baada ya wewe kunambia inawezekana..I had no clue kuwa inawezekana/ haiwezekani zaidi ya experience yangu.
Ushirikiano kati ya mashrika ya ndege upo mkuu usikatae... nachoshindwa kuelewa ni kwa nini kuwepo na Allience, au Partnership kati ya mashirika ikiwa kila ndege inaweza kuchukua abiria wa ndege yoyote maadam ni mwanachama wa IATA..
Pili sidhani kama kuna shrika la Commercial Airline ambalo sii mwanachama wa IATA na likaruhusiwa kufanya kazi, hilo pia ni jipya kwangu..Labda unipe somo wewe kwa nini kuna ushirika wa Allience au Partnership, kisha maelezo ya huyu mama wa BA pia yamechangia kunionyesha kwamba ATCL inaweza kujoin mashirika makubwa ktk kuunda Allience ili kuzidisha ufanisi wa usafiri wa ndege zake na pengine kuongeza soko lake ndani na nje kama mashirika mengineyo i.e Kenya Airways na Ethiopia zinavyofanya..
 
Well, sijasema huna uzoefu, as a fact mimi ndio kabuntas ktk maswala ya ndege na taratibu zake na ndio maana nimeuliza kuhusu usafiri wangu kutoka hapa nilipo kwenda Mwanza baada ya wewe kunambia inawezekana..I had no clue kuwa inawezekana/ haiwezekani zaidi ya experience yangu.
Ushirikiano kati ya mashrika ya ndege upo mkuu usikatae... nachoshindwa kuelewa ni kwa nini kuwepo na Allience, au Partnership kati ya mashirika ikiwa kila ndege inaweza kuchukua abiria wa ndege yoyote maadam ni mwanachama wa IATA..

Hiyo alliance unayoitaja ni kwamba haivunji makubaliano ya jumla ya wanachama wa IATA.

Makubaliano ya aliiance ni specific co-operation agreements ambazo zinafanywa na hayo makampuni, ikiwa ni pamoja na namna gani wanaweza kushare soko, maximum utilization ya equipment zao, sharing of common services etc. Mara nyingi mashirika yanayofanya alliance huwa kwanza yanakuwa katika uwezo sawa wa kushindana katika biashara hiyo. At the sametime huwa wanaona kuwa katika ushindani wao baadhi yao wana advantage katika soko fulani na wengi wana advantage katika soko lingine kwa upande mwingine. Sasa wanachofanya ni kuungana ili kuweza kupunguza gharama au kuepuka hasara katika maeneo fulani.


Pili sidhani kama kuna shrika la Commercial Airline ambalo sii mwanachama wa IATA na likaruhusiwa kufanya kazi, hilo pia ni jipya kwangu..Labda unipe somo wewe kwa nini kuna ushirika wa Allience au Partnership, kisha maelezo ya huyu mama wa BA pia yamechangia kunionyesha kwamba ATCL inaweza kujoin mashirika makubwa ktk kuunda Allience ili kuzidisha ufanisi wa usafiri wa ndege zake na pengine kuongeza soko lake ndani na nje kama mashirika mengineyo i.e Kenya Airways na Ethiopia zinavyofanya..

Si lazima unapofanya biashara ya usafiri wa anga uwe mwanachama wa IATA. Kuna kundi la wasafirishaji huitwa Non-IATA members ambao hufanya biashara kama kawaida. Endapo mmoja kati ya hawa Non-IATA members ameuza na kupokea pesa katika route ambayo ATCL kwa mfano atabeba huyo abiria, basi ATCL itabill moja kwa moja kwenye lile Shirika bila ya kupitia IATA. Unapokuwa member wa IATA kuna advantage nyingi ambazo unaziweza kuzipata ikiwa ni pamoja na kupewa abiria katika njia zako na kupata malipo yake bila ya usumbufu. Vilevile ukiwa member wa IATA ni rahisi ku-share information nyingi zihusuzo aviation. Advantage nyingine ni kuwa IATA huandaa mafunzo mafunzo kwa ajili ya members wake katika ngazi mbalimbali thru out the year. Pia IATA huwakutanisha airlines kujadili mambo tofauti ikiwa ni pamoja na fares, operation regulations na mengine mengi ambayo nikiyataja hapa yatajaza huu ukurasa.

Bottom line ni kuwa you got wrong information from a wrong guy.
Tuendelee kukata ishu mzee.

----------------------------------------------------------------
 
Sawa mkuu,
At the sametime huwa wanaona kuwa katika ushindani wao baadhi yao wana advantage katika soko fulani na wengi wana advantage katika soko lingine kwa upande mwingine. Sasa wanachofanya ni kuungana ili kuweza kupunguza gharama au kuepuka hasara katika maeneo fulani.
1. This is what I'm talking about! - halafu soma hapa Airline alliance - Wikipedia, the free encyclopedia
Si lazima unapofanya biashara ya usafiri wa anga uwe mwanachama wa IATA. Kuna kundi la wasafirishaji huitwa Non-IATA members ambao hufanya biashara kama kawaida
Unaweza kunipa jina la shirika ambalo ni Commercial Airline na sio mwanachama wa IATA..ni ktk kujifunza tu mkuu usiwe na homa ukafikiria labda nafanya utani..SIJUI..
 
Sawa mkuu,

1. This is what I'm talking about! - halafu soma hapa Airline alliance - Wikipedia, the free encyclopedia

Sasa hebu igeukie ATCL ilivyo sasa kama inaweza kufanya alliance na shirika lolote kubwa. Andika ni vitu gani vinaweza kuifanya Airline kubwa kwa sasa kufanya alliance na ATCL. Pia usisahau kuja na data ambayo itathibitisha kuwa hiyo airline ina nafasi gani katika soko la kufanya biashara na ATCL.


Unaweza kunipa jina la shirika ambalo ni Commercial Airline na sio mwanachama wa IATA..ni ktk kujifunza tu mkuu usiwe na homa ukafikiria labda nafanya utani..SIJUI..

Nyavu hizo hapo chini kavue samaki mwenyewe kwa kadri utakavyoweza, unaweza ku-google utakavyo.

Member airlines and non-IATA carriers worldwide. ... Office addresses of IATA Members (including telephone. and facsimile numbers) and a list of the ...
[media]www.geocities.com/anairline/turist.pdf[/media] - 375k - Cached
 
Pundamilia 07,
Mkuu sasa unafanya utani mbona hiyo link inanipeleka kusiko?..
Anyway tazama ile link niliyokupa utaona kwamba kuna mashirika kama Kenya Airways ina Allience ktk Sky Team wakiwa na mashirika mengine makubwa ambayo hawawezi kabisa kushindana..Pia kuna mashirika kibao kama hilo Adria ktk Star Allience limekuwa likifanya kazi kwa hasara na lina ndege 12 tu lipo pamoja na mashirika makubwa..

Bado hatujazungumzia kabisa partnership ambayo utakuta mashirka haya haya yakirudiana ktk Allience tofauti kwa mfano Air Canada na BA..hizo partnership za nini?..yaani hata sielewi mkuu wangu kama IATA ndio kazi yake kuunganisha connections za ndege zote wanachama.

Mkuu kama ulikuwepo nimechukua muda kusoma mahusiano ya haya mashirika na inanipa picha kabisa kuwa IATA clearing unahusiana zaidi na transaction za malipo within hizi Airline na sio uhusiano kati ya mashirika ktk Usafiri. Na mwisho utaona shirika kama Emirates na Air India hawapo ktk ushirika wa Allience yoyote wakati kuna mashirika madogo sana yamejiunga.
Sasa my conclusion, maadam umekataa kunipa darasa nafikiri kwamba inawezekana kufika Mwanza kwa KLM..Nafanya ku guess tu lakini nadhani inawezekana nikapata ticket ya kwenda Mwanza kwa KLM kwa sababu ya Allience kati yao na Kenya Airways ambayo ina hisa zake Precision Air jambo ambalo halikuwezekana na BA..
Utanisamehe mkuu, kweli nafanya ubishi lakini hii yote inatokana na majibu yako kuwa nje zaidiNa kikubwa zaidi ni imani yangu kwamba ATCL inaweza kabisa kufanya kazi vizuri maadam kuwepo na mikakati madhubuti bila kui underestimate kwa sababu tu ya udhaifu wa viongozi wake wakati Asstes zake tu zinaweza kufikia mabillioni ya fedha ambazo tunaweza kuzipoteza kutokana na uzembe wa kutofikiria mbele..
 
Management, Management, Management

Kuna uwezekano mkubwa matatizo ya uongozi yanatokana na schoolarship zetu na utamaduni tuliokuwa nao.

Katika mji ninaoishi kuna jumuia nyingi za kitanzania. Lakini hakuna hata moja naweza kusema iliyokuwa na mafanikio.

Jumuia nyingi zinaanzishwa na sherehe kubwa na zinapotea bila kuelewa zimepotelea wapi. Na baada ya kupita muda fulani wengine watazifufua na kuziacha tena kufa.

Nilihamua kufanyia utafiti wa kufa hizi jumuia. Nilichogundua ni kuwa miundo ya jumuia hizi ni sawa kabisa. Kutakuwepo na Mwenyekiti, Makamu, katibu na kamati zenye wenyeviti na makatibu.

Na miundo hii inafanana kabisa na miundo ya jumuia nilizoziona Tanzania nikiwa shuleni au vyuoni. Ni copycat ya TANU/CCM na jumuia zake. Hakuna innovation yoyote.

Kwa maoni yangu binafsi yanayotokea ATC ni-reflection yetu. Kwa miaka mingi tumefananisha siasa na uongozi. Tumefaninisha usemaji wa maneno mengi na utendaji.

Pale tutakapokubali kuwa management ni art yenye kutumia innovation hatutakwenda mbali. Tutaendelea kufanya kazi kwa utamaduni uliopo sasa.


Umegusa penyewe haswaaa!!
Si unajua tena ATCL from ATC which was a parastatal..depending heavily on subvention kutoka serikalini.Si unajua pia kuwa parastatals uedeshajaji wake ulivyokuwa? sidhani kama walikuwa wanaelewa kitu kinachoitwa faida/profit au bottomlines.Kwa vile hakukuwa na drastic changes kiutendaji na hata kwenye mindsets za watendaji basi wanabehave kama kampuni ya umma ambapo wanadhani kazi yao ni kuwepo pale, ku enjoy na si kufanya faida.Ni kama mtoto anayenyonya weeeee na mama akamwendekeza... hataacha ziwa! Its high time serikali wateue watu wenye uwezo wenye track record kiutendaji... wawape mamlaka kamili kiutendaji na kiundeshaji - ili management ichukue hatua watakazoona zinafaa ( be it retrenching staff, ) serikali iwape kianzio na baada ya hapo waendeshe shirika katika namna itakayoleta faida. Kadhalika hao watendaji wawajibishwe pale ambapo hawafanyi faida.
 
Pundamilia 07,
Mkuu sasa unafanya utani mbona hiyo link inanipeleka kusiko?..

Anyway kama hiyo link imegoma kukupeleka kule unakotaka google list of Non-IATA Members utaipata bila shaka.

Anyway tazama ile link niliyokupa utaona kwamba kuna mashirika kama Kenya Airways ina Allience ktk Sky Team wakiwa na mashirika mengine makubwa ambayo hawawezi kabisa kushindana..

KLM ina hisa ktk Kenya Airways, Kenya Airways ina hisa ktk Precision Air, sasa unadhani wakati KLM akiuza route ya Amsterdam - Mwanza, route ya Dar-Mwanza ataipa ATCL? haihitaji a rocket science kujua hili. Sehemu ya nauli ya DAR-Mwanza ni ya KLM thru Kenya Airways.

Pia kuna mashirika kibao kama hilo Adria ktk Star Allience limekuwa likifanya kazi kwa hasara na lina ndege 12 tu lipo pamoja na mashirika makubwa..

Hapo inategemea kimkakati Adria ni potential kiasi gani kwa Star Alliance.


Bado hatujazungumzia kabisa partnership ambayo utakuta mashirka haya haya yakirudiana ktk Allience tofauti kwa mfano Air Canada na BA..hizo partnership za nini?..yaani hata sielewi mkuu wangu kama IATA ndio kazi yake kuunganisha connections za ndege zote wanachama.

Go to website ya IATA utaweza kujifunza mengi na kufaidika jinsi IATA inavyofanya kazi zake na wanachama wake.

Mkuu kama ulikuwepo nimechukua muda kusoma mahusiano ya haya mashirika na inanipa picha kabisa kuwa IATA clearing unahusiana zaidi na transaction za malipo within hizi Airline na sio uhusiano kati ya mashirika ktk Usafiri.

IATA Clearing House ni kitengo tu ndani ya IATA kinachoshughulikia transactions zinazofanywa na wanachama wake. IATA yenyewe inahusika na mambo mengi sana kama nilivyokupa mfano hapo juu.

Na mwisho utaona shirika kama Emirates na Air India hawapo ktk ushirika wa Allience yoyote wakati kuna mashirika madogo sana yamejiunga.
Sasa my conclusion, maadam umekataa kunipa darasa nafikiri kwamba inawezekana kufika Mwanza kwa KLM..Nafanya ku guess tu lakini nadhani inawezekana nikapata ticket ya kwenda Mwanza kwa KLM kwa sababu ya Allience kati yao na Kenya Airways ambayo ina hisa zake Precision Air jambo ambalo halikuwezekana na BA..

Maelezo yangu niliyokupa ndiyo hayo yanayotumika hadi dakika hii ninavyoandika

Unaweza kukata ticket kutoka London hadi Mwanza na tikiti yako itaonekana kama hivi:
LHR-DAR career BA
DAR-MWZ career TC
ATCL na BA hawahitaji kuwa na makubaliano yeyote maalum katika hili as long as wao ni IATA Members.


Utanisamehe mkuu, kweli nafanya ubishi lakini hii yote inatokana na majibu yako kuwa nje zaidiNa kikubwa zaidi ni imani yangu kwamba ATCL inaweza kabisa kufanya kazi vizuri maadam kuwepo na mikakati madhubuti bila kui underestimate kwa sababu tu ya udhaifu wa viongozi wake wakati Asstes zake tu zinaweza kufikia mabillioni ya fedha ambazo tunaweza kuzipoteza kutokana na uzembe wa kutofikiria mbele..

Nimekusamehe, najua ubishi wako unatokana labda na uwezo wako mwenyewe binafsi wakuelewa mambo kwa haraka. Lakini ninaamini utakwenda katika website ya IATA na kujifunza zaidi.

Pili, as of today ATCL ni kama haina assets kwani it's technically bankrupty. Kama hawawezi kuwa-bailed out assets zao zitauzwa kufidia madeni

---------------------------------------------------
 
Pili, as of today ATCL ni kama haina assets kwani it's technically bankrupty. Kama hawawezi kuwa-bailed out assets zao zitauzwa kufidia madeni
Sawa mkuu nimekusikia...Anyway tuachane na haya hayana mpango mkuu wangu.. ATCL iwezeshwe kujitegemea..
My 2 cent...iwekwe ktk soko letu DSE, hata kama kwa kuanzia share zikiuzwa Tsh500 au 1000 kwa share blaa! blaa! blaa! wawekeshaji wapo I'm sure na zitakuja panda baadaye kwani soko lipo hakuna haja ya kuambiwa zaidi.
Swala la Emerites au Gulf Air ni gumu tu upande wetu sisi kwani nijuavyo mashrika makubwa hupenda kuyameza mashirika madogo ili wapate kushindana sehemu husika..
KLM, Kenya Airways na Precision Air ni tishio kwa mashirika mengine na ili yapate kushindana inabidi nayo yafikirie njia mpya za kutawala soko la East Africa.
Kwa hiyo tunaweza kujenga ushirikiano wa aina fumani na mashirika makubwa ambayo yanaweza sana kutusaidia ktk vifaa na taaluma nyingine zinazoendana na biashara hiyo..Ni imani yangu hili linawezekana.
Pili, kabla ya yote haya serikali imwage stimulus ktk bajeti yake kuokoa shirika..Uuzaji ticket ufanywe na ofisi za mashirika ya Tourism Agents badala ya ofisi za ATCL.
ATCL technically haikuwepo, tuliingia bankrupt toka siku ATC tulipoamua kujiunga na SA.
 
Umegusa penyewe haswaaa!!
Si unajua tena ATCL from ATC which was a parastatal..depending heavily on subvention kutoka serikalini.Si unajua pia kuwa parastatals uedeshajaji wake ulivyokuwa? sidhani kama walikuwa wanaelewa kitu kinachoitwa faida/profit au bottomlines.Kwa vile hakukuwa na drastic changes kiutendaji na hata kwenye mindsets za watendaji basi wanabehave kama kampuni ya umma ambapo wanadhani kazi yao ni kuwepo pale, ku enjoy na si kufanya faida.Ni kama mtoto anayenyonya weeeee na mama akamwendekeza... hataacha ziwa! Its high time serikali wateue watu wenye uwezo wenye track record kiutendaji... wawape mamlaka kamili kiutendaji na kiundeshaji - ili management ichukue hatua watakazoona zinafaa ( be it retrenching staff, ) serikali iwape kianzio na baada ya hapo waendeshe shirika katika namna itakayoleta faida. Kadhalika hao watendaji wawajibishwe pale ambapo hawafanyi faida.

WoS:

Nakumbuka miaka si mingi iliyopita wabunge fulani walitembelea Ethiopia. Baada ya kuona uwanja mzuri, tayari nao wakataka Tanzania iwe na state of the art Airport.

Nadhani na hiki ndio kitu kinachotusumbua. Tukiona mwenzetu kafanya vizuri, hatutaki kuelewa siri ya mafanikio yake bali tunataka kupata vitu vizuri.

Ujenzi wa uwanja wa ndege wa Addis Ababa umekwenda sambasamba na ukuaji wa shirika lao la ndege.

Kwa mfano wakati Ethiopia hiko kwenye civil war kwa miaka mingi na wakati mwingine vita vilikuwa ndani ya Addis Ababa, Ethiopia Airline iliweza ku-weather matatizo yote. Shughuli zote zilihamishwa nje ya nchi, ndege zikawa zina-operate kutoka Dubai na nyingine Europe.

Sidhani kama Tanzania kuna managers ambao wanaweza kufanya entities wanazoongoza kuwa resilient kiasi hicho.
 
CEO:nakumbuka wakati naondoka alipewa mkopo wa miilioni 100...ambayo mpaka leo hii tuna ushahidi ni millioni kumi tu ndio iliolipwa toka aingiziwe kwenye account yake

DIRECTOR'S
HAWA WAMEJIKOPESHA SH MILLION 80 KILA MMOJA PASIPOKUJUA IPO SIKU WATAKOSA PESA YA MAFUTA YA NDEGE.....HAWA WAKO 7 ZIDISHA MARA 80 INATOKA NGAPI=

...

Hivi benki zimewekwa za nini mpaka watu wakopeshane hela zote hizi zikiwa za shirika....nadhani huu ulikuwa ni uchumaji watu walijiandalia wakijua kuwa shirika halina muda mrefu.
 
Sawa mkuu nimekusikia...Anyway tuachane na haya hayana mpango mkuu wangu.. ATCL iwezeshwe kujitegemea..
My 2 cent...iwekwe ktk soko letu DSE, hata kama kwa kuanzia share zikiuzwa Tsh500 au 1000 kwa share blaa! blaa! blaa! wawekeshaji wapo I'm sure na zitakuja panda baadaye kwani soko lipo hakuna haja ya kuambiwa zaidi.

Mkuu Mkandara,

Ukitaka kuorodhesha kampuni katika soko la hisa ni lazima liwe na sifa ambazo tayari zimekwishawekwa kwa ajili ya kuuza hisa hizo. Naamini kabisa DSE hawawezi kupokea kampuni ambayo mahesabu yake yanaonesha hasara ili wauze hisa.
Lengo kuu la wanunua hisa ni kupata faida katika uwekezaji wao, haingii akilini mwangu ninatoa fedha na kununua hisa za ATCL ili iweje? ukiwekeza katika kampuni ambayo inapata hasara maanake na wewe umekula hasara huwezi kupata gawio (dividends) katika njia yeyote ile.
Kanuni za kuuza hisa katika masoko kama hayo pia zinawalinda wanunuzi dhidi ya hasara ambazo wanaweza kuzipata. Makampuni yote yanayotaka kuuza hisa ni lazima yatangaze taarifa zao za fedha na ziwe wazi kwa public. Yeyote atakaye jaribu kutoa taarifa za uongo juu ya kampuni ili watu wanunue hisa atakuwa ametenda kosa la jinai. Ukipata nafasi soma ile kesi ya Enron.


Swala la Emerites au Gulf Air ni gumu tu upande wetu sisi kwani nijuavyo mashrika makubwa hupenda kuyameza mashirika madogo ili wapate kushindana sehemu husika..

Kama ambavyo nilisema hapo awali kuwa hawa wakubwa wanaweza kutaka kushirikia na wewe endapo tu wataona kuna threat. KLM waliona tayari Kenya Airways ni potential katika soko la Afrika Mashariki, na vilevile walikuwa na changamoto za kushindania soko na British Airways, Air France na kadhalika. Kwa hiyo KLM aliona katika Afrika Mashariki mpango wake wa kushindania soko na Airlines zingine za Ulaya ni kununua Kenya Airways ili aweze kukuza soko la Afrika Mashariki na kujiweka on the safe side dhidi ya washindani wengine. Ndiyo maana hata leo hii tumeona kukuwa kwa soko la KLM katika njia ya Amsterdam - Dar.
Kwa upande wa Emirates wao wa tayari wananguvu sana katika soko la DAR - Dubai na hawahitaji kumshirikisha mtu unless kunatokea threat dhidi yao. Ukitaka kushirikiana na Emirates kwa sasa hasa nikiiangalia ATCL, labda iwe feeder wa Emirates na hapo usitegemee growth ya ATCL tena.
Lakini wanaweza kutest mapigo ya Emirates kwa kuomba ushirikiano na Qatar halafu tuone nini kitatokea, je Emirates will cut Dar - Dubai fare to 50% for one year ili washindani wake wapate hasara?

Nakumbuka wakati SAA imeingia ubia na ATCL ilikosea kwa kufunga ofisi za ATCL pale Chester House, Nairobi. Kenya Airways walipata video ya siku ambayo bango la ATCL linaondolewa kutoka kwenye ofisi zile na kuitangazia Public kuwa ATCL is no longer operating DAR - Nairobi Route. Kana kwamba haitoshi Kenya Airways ili cut fare ambayo iliifanya ATCL ipate hasara kubwa na hatimaye kujiondoa kwenye route hiyo kabla ya Kenya Airways kurudisha nauli mpya.

Kwahiyo Mkuu, mbinu katika biashara hii ni nyingi sana mwenye nguvu anaweza kukuziba pumzi hadi unakata roho.

ATCL inachotakiwa kufanya kufanya utafiti wa kutosha wa kujua ni ipi nafasi yake sasa hivi katika soko la usafiri wa anga hapa Tanzania.


KLM, Kenya Airways na Precision Air ni tishio kwa mashirika mengine na ili yapate kushindana inabidi nayo yafikirie njia mpya za kutawala soko la East Africa.

Ni wazi kabisa hao jamaa hawalali, hizi kauli zinazosema kuwa serikali ina mpango wa kusaidia ATCL wao si habari njema sana, kwani wanatamani wasikie serikali ikitangaza kuwa kuanzia leo ATCL haipo tena. Hata hivyo juhudi za serikali za kuikoa ATCL pia ndiyo zinazoifanya Precision Air iendelee kuwepo leo na kutoa mchango mkubwa katika sekta ya anga ikiwa ni pamoja na kuwapatia utaalam wazalendo. Kama ATCL haitakuwepo uwepo wa Precision utakuwa ni wa mashaka, na huenda jeuri ya wakenya tutaiona kwa kuingiza ajira ya wakenya katika kila kona ya Precision Air.

Kwa hiyo tunaweza kujenga ushirikiano wa aina fumani na mashirika makubwa ambayo yanaweza sana kutusaidia ktk vifaa na taaluma nyingine zinazoendana na biashara hiyo..Ni imani yangu hili linawezekana.

Hapa mkuu, nadhani tunaelewa msaada maana yake ni
nini. Anayekusaidia anataka kuona je atafaidikaje zaidi kuliko wewe unayepewa msaada huo. Tukae chini tuangalie jinsi ya kujenga uwezo ili tuwe attractive hata ikibidi kushirikiana na mtu mwingine basi tuwe na 'kasauti' kidogo.


Pili, kabla ya yote haya serikali imwage stimulus ktk bajeti yake kuokoa shirika..Uuzaji ticket ufanywe na ofisi za mashirika ya Tourism Agents badala ya ofisi za ATCL.
ATCL technically haikuwepo, tuliingia bankrupt toka siku ATC tulipoamua kujiunga na SA.

Hili suala la kuuza tiketi ni la kimkakati litategemea menejimenti husika itakavyoona inafaa. Lakini sioni tatizo kwa ATCL isiuze tiketi zake itegemee Agent. Ulimwengu wa kuuza tiketi umebadilika, tiketi zinauzwa kupitia kwenye internet. Kwahiyo tuishauri ATCL iboreshe huduma zake ili hata kwenye duka la jirani tu hapa la vyakula mtaani kwetu tuweze kufanya mipango ya safari. (Nasema hivi kwa kuamini kuwa si wote watanzania wenye access ya internet. Mwenye duka hapo mpemba au mchaga kama ana internet anaweza kukufanyia booking na ukalipa online)

---------------------------------------------
 
Last edited:
WoS:

Nakumbuka miaka si mingi iliyopita wabunge fulani walitembelea Ethiopia. Baada ya kuona uwanja mzuri, tayari nao wakataka Tanzania iwe na state of the art Airport.

Nadhani na hiki ndio kitu kinachotusumbua. Tukiona mwenzetu kafanya vizuri, hatutaki kuelewa siri ya mafanikio yake bali tunataka kupata vitu vizuri.

Ujenzi wa uwanja wa ndege wa Addis Ababa umekwenda sambasamba na ukuaji wa shirika lao la ndege.

Kwa mfano wakati Ethiopia hiko kwenye civil war kwa miaka mingi na wakati mwingine vita vilikuwa ndani ya Addis Ababa, Ethiopia Airline iliweza ku-weather matatizo yote. Shughuli zote zilihamishwa nje ya nchi, ndege zikawa zina-operate kutoka Dubai na nyingine Europe.

Sidhani kama Tanzania kuna managers ambao wanaweza kufanya entities wanazoongoza kuwa resilient kiasi hicho.

Za10,
Inasikitisha kwelikweli..... mambo ya ad hoc siku zote hayawezi kuleta manufaa wala kuwa sustainable......
unazungumzia miaka ya nyuma... halafu kama ni kuwa na state- of -the -art airport Addis, its a recent development licha ya kwamba ET ina zaidi ya miaka 100 toka iazishwe na bado inadunda.Mimi nimejaribu kuangalia hata viwanja vyetu vya ndege... utaona kabisa hakuna sense of planning for the future..DIA ilivyojengwa in the early 80s ndio imebakia hivyohivyo na inazidi kuminywaminywa kwa kuongezewa ugly structures kila kukicha... vijibadana na vikontena kila mahali...( na wahusika kila leo unawasikia wanasafiri nje ya nchi kwenda kujifunza..sijui wanajifunza nini na wanakuja ku apply vipi!)..

Angalia uwanja wa Zanzibar..hapo tena ni shughuli! Kinachoshangaza ni kwamba pamoja na kusikia kuna mipango ya kuupanua.... kuna watu wanajenga tena si ujenzi mdogo..karibu kabisa na airport...hii maana yake sijui ni nini.... au ndo mbinu za kuja kudai compensation hefty?
Anyway coming back to our national carrier.... may be a divine intervention will salvage the situation.Tusubiri tuone.
 
Nakubaliana kwa kiasi kikubwa na haya yote; lakini kwanza ningeona serikali iuze hisa za ATCL kwa Watanzania au mashirika ya kitanzania ili iendeshwe kibiashara na umiliki uwe mikononi mwa watu wanaojali faida inayotokana na huduma nzuri.

Naam!

Laiti kama maneno haya yangepewa uzito unaostahili, tungeondoka kwenye huu ujima haraka kuliko njia nyingine yeyote. Kama walivosema wenzangu, tatizo siyo fedha, tatizo ni uendeshaji...

Kuuza hisa kwa Makampuni na Watanzania binafsi kutakaribisha mchakato wa kuondoa udhaifu huo wa uendeshaji, haraka! Na KUPE huyu ataacha kuendelea kutunyonya damu yetu kidogo tuliyobakia nayo. Siyo hivyo tu, muda si mrefu faida itaanza kuonekana, na Hazina kupitia TRA wataanza kujumlisha, siyo kutoa!

Neema kwa Watanzania itaanza kuonekana, badala ya laana!!!!
 
Tatizo la ATCL sio kukosa mtaji na wala sio kukosa wateja, tanzania kuna route ambazo bado zina abiria wengi sana kama wakuwa serious. Kitu cha msingi ni Raisi wetu haachane na wazee wake waliozoea kula pesa za mashirika ya umma.

Anatakiwa kuchagua vijana ambao wana new drive katika operation management, makata amesoma operation mara ya mwisho wakati challenge za operations kwa tanzania zikiwa ni kubeba abiria bila kujari mambo mengine.

Tunatakiwa kuwa na mtu anayejua jinsi ya kubalance costs, time and quality wakati akiacha quality na time videtermine costs. Vinginevyo hilo shirika halitasimama lenyewe hata siku moja maana wanachojua ni kukusanya mapesa wa abiria bila kujari kama ndege itasafiri au haipo na kama haipo abiria anakaa wapi anakuwa compesated vipi kwa muda aliokosa ndege.

Mfano mzuri ni mkurugenzi wa KCB tanzania he is just a young man but doing well in business compared to wazee tuliozoea kuwaona wakiongoza mashirika kumbe ndio wanayamaliza
 
Back
Top Bottom