How Air Tanzania Should be Restructured

Pundamilia07,
Mkuu samahani hapa kidogo nitatofautiana na wewe kuhusiana ubia wetu na KLM..
haiwezekani kuwepo fikra za ubia kati yetu na Uholanzi awamu ya kwanza kwa sababu ulizozisema wewe mwenyewe. isipokuwa labda mkataba wa contract za biashara..


Mkandara nadhani you missed a point, maelezo yangu yalikuwa yanajibu hoja iliyotolewa na Zakumi kwamba KLM walitaka kuingia ubia na ATCL lakini wa-South Africa wakawapa 'watu' fedha ili KLM isipewe nafasi ya kuingia ubia. Ili tuwe kwenye mstari mmoja ni lazima tukanushe kwamba hiyo sentensi ya kwamba KLM walikataliwa kuingia ubia na ATCL. Nikaeleza kuwa KLM walionesha interest wakati wa uongozi wa awamu ya kwanza na nikaelezea pia kuwa kwa wakati ule sera zetu zilkuwa haziruhusu kutokana na utekelezaji wa Azimio la Arusha.
Kimsingi maelezo yangu yalijitosheleza kwani kama hatuweki mambo sawa wasomaji wengi hawatafaidika juu ya historia hii.



Kisha wakati wa awamu ya kwanza hakuna shirika lolote duniani lilikuwa na Ubia na mtu. Ni wakati biashara ya ndege ilipokuwa kubwa kiasi kwamba karibu kila nchi duniani ilikuwa na shirika lake hadi mwaka 1982 mafuta yalipopanda na kufuatiwa economic meltdown wakati wa Reagan ndipo ubia ulipoanza ku save mashrika mengi ya ndege au magari.
Kanma unakumbuka awamu ya kwanza ndege za kigeni zilizokuwa zikija Tanzania zilkuwa zaidi ta mashirika 10, KLM, BA,Swiss, SAS, Aeroflot, Sabena, Alitalia, Air France, Air India, PIA, acha mbali za ndani Afrika na nyingine kibao ambazo zote siwezi kuzitaja zote...mashirika yote haya yalikuwa hayana Ubia na mtu mwingine..

Baadhi ya mashirika ambayo umeyataja (with exceptional ya SABENA ambayo haipo tene) yanasafirisha abiria wao kuja Tanzania bila ya kuhitaji kuleta ndege zao. Utaratibu wa usafirishaji abiria wa ndege upo katika levels tofauti. Airline ya Pakistan inaweza kuuza tiketi ya Karachi - Dar na kumkubeba abiria kutoka Karachi hadi Dubai then kwa njia ya Dubai - Dar career anaweza kuwa Emirates (Si lazima Airline ya Pakistan iwe na ushirikiano wa moja kwa moja na Emirates). taratibu zinazotumika hapo ni zile za IATA.
Kwa hiyo basi kutokuja kwa Ndege zao hakuna maana yeyote zaidi ya mikakati yao ya kuendesha airline hizo kwa ufanisi.


Kwa hiyo, hili swala la Ubia limekuja baadaye na kwa sababu kubwa ya kiuchumi (utandawazi na soko huru) ili kuweza kushindana, pia kutokuwa na mipaka ya biashara kama nilivyoelezea huko nyuma jinsi ATCL inavyoweza kufanya kazi na Emirates kuongeza wateja wakati huo huo wakipunguza misafara kwa kugawana kazi za ndani na nje..

Hili swala la ATCL kufanya kazi na Emirates ndugu yangu siyo kwamba ni suala la ATCL waamue, hapana, kama nilivyoandika hapa awali Emirates ana nguvu sana na soko lake lina uhakika bila hata ya kushirikiana na ATCL. Kimtazamo kama Emirates anahitaji ushirikiano na ATCL hilo angekwisha lifanya siku nyingi ikiwemo kununua hisa za ATCL ambazo kwa Emirates ni pesa ndogo. Lakini kwa vile haihitaji ATCL, basi hata ATCL wakitaka ushirikiano nae, ni yeye Emirates ndiye ataye-dictate terms kwenye mkataba, as a result unaweza usiwe na manufaa kwa ATCL.

Chini ya Ujamaa wa Nyerere ni ndoto kufikiria kwamba Nyerere angeweza kufanya hivyo kwa sababu alikwisha sema hawezi kugeuka jiwe hadi pale tulipopigwa na vumbi la kiuchumi...

Hili nimelieleza kuwa ATC isingeweza kuuza hisa kwa sababu ya sera zilizokuwepo awamu ya kwanza

The bottom line ni kuwa ATCL inahitaji kugeuzwa ili iwe profitable na kuweza kuwavutia wawekezaji wa maana na vilevile iaminike hadi kufikia kukubalika kuwa listed katika soko la hisa ili na akina sisi tununue hisa tufaidike na shirika letu. Viongozi wanaopewa dhamana yakuongoza mashirika yetu halafu wanayapeleka kupata hasara kwa hakika wanawanyima watanzania haki za kuweza kuyamiliki mashirika hayo.
 
Mkuu pundamilia,sijui niseme uliona mbali ,nalisikitikia sana ile kampuni,nafikiri we uliona ulivyokuwa jikoni watu walivyokuwa wanachota..ile kampuni naisikitikia sana hata kabla ya kuondoka nilishauri mengi tu na nini cha kufanya wengi wakajua mi natafuta nafasi
MATUMIZI
uongozi umekuwa na matumizi mengi yasiyo na ridhaa na mengine kwa kutumia,nguvu kutumia pesa za kampuni...

MIKOPO:
Kulikuwa na mikopo ya ajabu ajabu ambayo hata kama atakuja CEO gani na kuwekka manegement chafu..kama hiyo iliyo tanzania atcl nina hakika hata wapewe billion kumi hataweza kufika popote kama mwenyekiti wao wa bodi anavypiga kelele...
kumekuwa na mikopo ya viongozi bila kuangalia uwezekano wa kampuni kufa ama walifikiri hata wakiondoka wataachwa...mfano mmojawapo wa kusikitisha ni

CEO:nakumbuka wakati naondoka alipewa mkopo wa miilioni 100...ambayo mpaka leo hii tuna ushahidi ni millioni kumi tu ndio iliolipwa toka aingiziwe kwenye account yake

DIRECTOR'S
HAWA WAMEJIKOPESHA SH MILLION 80 KILA MMOJA
PASIPOKUJUA IPO SIKU WATAKOSA PESA YA MAFUTA YA NDEGE.....HAWA WAKO 7 ZIDISHA MARA 80 INATOKA NGAPI=

ACHA MATUMIZI MENGINE MACHAFU...NAFIKIRI KWA USHAURI WA MWISHO WAZIRI AAMUE TU KUMSHAURI RAISI AIFUTILIE MBALI HIYO MANAGEMENT NA KUWEKA WAPYA HARAKA KUIKOA ATCL..HAWA WALIOPO HAWANA MPANGO WA KURUSHA NDEGE SI LEO WALA KESHO......

MI NASHANGAA SANAA IWEJEE MTU KAMA CEO ANADAIWA HELA NYINGI HIVYO NA AENDELEE KUKALIA KITI....CHA KUSIKITISHA ANA MADENI YA TICKETI ZA BURE ZAIDI YA MILLIONI 10 BILA KULIPA ...KWA KUTOA DIRECTION WAPEWE HAWA...SASA NAFIKIRI UMEFIKA WAKATI WA KUAMUA SERIKALI KAMA WANAAIITAJI ATCL AMA LA KULIKO KUWAPOTEZEA WATU MUDA WAO.....KUMEKUWA NA MALALAMIKO HATA MIKOPO WANAYOKATWA HAWAIPELEKI SEHEMU HUSIKA..M NAFIKIRI KIONGOZI ATAKAINGIA AJITAHIDI KUWASAIDIA KUJUA YALE MAKATO YALIENDA WAPI......HAIWEZEKANI MTU ANASTAFU AJUI HATA PPF YAKE IKO AMA LAH.....

WAKUU HUU MUDA TUMSHAURI RAISI NANI AMBE ANAWEZA KUONGOZA ATCL..MEANS AWE NA SIFA GANI...

Sweetbaby,

Ni kweli hawa waheshimiwa walijikopesha hiyo mikopo kutoka katika fedha za ATCL?

Kama hivyo ndiyo basi Serikali inapaswa kueleza kadhia hii sambamba na wakati huu ambapo kuna matatizo ya kiuendeshaji hapo ATCL. Kutotoa taarifa juu ya jambo hili itakuwa ni makosa makubwa kwa upande wa serikali. Hata kama hizo pesa walizipata kutoka katika financial institution basi taarifa ni lazima iwekwe wazi.

Ikumbukwe kwamba tayari pesa za serikali zimekwisha pelekwa ATCL na huenda nyingine ziko njia kwenda huko, ni vema hili la kujilopesha likawekwa wazi.
 
Pundamilia07,
Baadhi ya mashirika ambayo umeyataja (with exceptional ya SABENA ambayo haipo tene) yanasafirisha abiria wao kuja Tanzania bila ya kuhitaji kuleta ndege zao. Utaratibu wa usafirishaji abiria wa ndege upo katika levels tofauti. Airline ya Pakistan inaweza kuuza tiketi ya Karachi - Dar na kumkubeba abiria kutoka Karachi hadi Dubai then kwa njia ya Dubai - Dar career anaweza kuwa Emirates (Si lazima Airline ya Pakistan iwe na ushirikiano wa moja kwa moja na Emirates). taratibu zinazotumika hapo ni zile za IATA.
Kwa hiyo basi kutokuja kwa Ndege zao hakuna maana yeyote zaidi ya mikakati yao ya kuendesha airline hizo kwa ufanisi.
Mkuu samahani ni wewe ambaye hukunisoma vizuri..maelezo yako hayo hapo juu ndiyo kitu nalichozungumzia muda wote huko nyuma.. Kisha sio sheria za IATA kubadilihana abiria mkuu hata kidogo ni mikataba baina ya mashirika mawili kuhusu usafirishaji wa Abiria. iwe kuna Ubia ama makubaliano ya contracts..Naelewa fika kwamba mashirika yale yote hayafiki tena Tanzania lakini abiria wake wanakuja na mashirika mengine tofauti na wakati wa Nyerere..Lakini mkuu wangu my point is, huwezi kusafirisha abiria wa shirika fulani wakati fedha imelipwa nchi nyingine ni lazima kuna makubaliano kati ya mashirika mawili jinsi ya kugawana mapato ya msafiri mmoja aliyesafiri kwa ndege mbili za mashrika mawili tofauti..Na sio swala Huo ndio Ubia naozungumzia mimi, na sielewi unaposema Emirates wangekwisha nunua hisa ikiwa ATCL sio public sokoni, hizo hisa watazinunua vipi ikiwa hujapeleka mali yetu sokoni? ..
Mkuu Emirates wanahitaji abiria zaidi toka Tanzania ikiwa kuna uwezekano wa kuvunja masoko ya ndege nyingine zilizobakia..tunaweza kuwa regional (Tanzania) partner wa Emirates with our goals being connection Tanzania and the world, na wanaweza tu kukunua hisa pale tutakapo tangaza kuwa Public soko letu DSE..Kitu muhimu kwao ni soko, vitu kama
Ebu wewe nambie mkuu wangu kam Unaishi Mwanza na unaweza kuapata ticket ya kwenda London bila kuja Dar utaacha kusafiri na ATCL toka Mwanza kuja Dar au Kili na kuunganisha na Emirates?.. Je ni Watanzania wangapi watakao penda kufanya hivyo (air of their choice) badala ya kuja Dar kutafuta ticket za BA, KLM au Swiss Air ambazo hatuna mpango wa kubadilishana nao wasafiri kama ulivyozungumzia hapo juu!
Bila shaka mauzo ya ticket za Emirates zitaongezeka..Emirates hawana haja ya kufahamu ATCL ina mtaji kiasi gani isipokuwa tunaweza vipi kuongeza soko lao nchini.. ATCL itakwenda nchi jirani na kuvuta wasafiri wa Emirates nchi za Asia na Ulaya na pengine hata sisi ATCL kuwa na ndege moja kwenda Dubai kila siku..
Ndivyo mashirika yote yanavyoshirikiana mkuu wangu Ubia unakuja tu kwa kutazama thamani ya soko lililopo, vitu kama Load factor, Revenue, seat miles na kadhalika of which I'm pretty sure tupo juu safi, bearing in mind population yetu na matatizo ya Usafiri mwingine nchini.
Again nitarudia kusema tatizo la ATCL ni UONGOZI mbaya nothing to do with shirika ATCL..soko na mali zake zote ziko safi..Kama vile Tanzania yenye Utajiri mkubwa lakini ndio nchi maskini iloshindikana kutokana na Uongozi mbaya... Potential ipo na ndiyo inawasukuma wawekeshaji kumiminika nchini kwa sababu hatuna tena policies za Ujamaa (mkono wa serikali).. Aliyesubiri kuona Tanzania ikiinuka kwanza would be the looser mkuu wangu..Tanzania itainuliwa na wale walio take risk na ndio watakaofaidika na uwekeshaji wao.. Tukisha pata mabawa tu kila kitu kitakuwa ghali na hakuna tena mwalimu..

Sasa ukifikiria njia ya kuondoka Umaskini huu ni kuuza nchi kwanza badala ya ku deal na main problem utakuwa hujafanya kitu zaidi ya kupoteza kila kitu kama tulivyopoteza madini..Watu walinunua share za Barricks mara tu waliposikia wameshinda mikataba fulani ya machimbo.. kabla hata hawajachimba shimo moja mkuu wangu lakini kila siku zinavyokwenda na utajri kuzidi ndivyo share zake zinavyosidi kuwa ghali kwa wananchi..Hivyo swala la ATCL sio swala la Innovation ni swala la kufuata mfumo uliokuwepo sasa hivi duniani.. mashrika yote unayoyaona ya ndege yalitoka mikononi mwa serikali na kuingia ktk soko huria wakati biahsra ya ndege ilikuwa ikitumba..Watabiri wa wall street hutazama mbele na sio kitu ambacho tayari kinazalisha na risk ni ndogo, faida yake huwa ndogo sana..
Swala la uongozi mbaya ndani ya ATCL ni swala ambalo linaweza kabisa kumalizwa within one month of operating. Wakisha ingia wajuzi wa biashara na kuwekesha fedha zao utaona mwenyewe mabadiliko sehemu zote za uzembe..trust me.

Niliyoaandika kuhusu Nyerere ni kwamba hapakuwepo na makubaliano ya namna hii ndio maana mashirka hayo yote yalileta ndege zao. Sasa uliposema kwamba Ubia kati ya KLM na ATC ulitakiwa toka wakati wa mwalimu ndipo niliposema isingewezekana kabisa kwa sababu mbali na siasa zetu mfumo huo haukuwepo kabisa duniani..sijui kama umenielewa hapo..
 
Kwanza, biashara ya ndege siwaachii wazee. Nitawatafuta vijana wa miaka 30 -37 waliowahi kuwa marubani na wenye MBAs au Menejimenti digrii yoyote.

Ningeligawa shirika katika:
i. Uchukuzi mizigo
-ndani ya nchi
-kati ya nchi za Afrika Mashariki
-na nchi za nje
ii. Usafirishaji watu
-ndani ya nchi
-kati ya nchi za Afrika Mashariki
-na nchi za nje

Ningelianza biashara ya ndani na kuhakikisha magazeti, barua, fedha na vifurushi, vyakula, nguo na bidhaa nyingine vinafika katika asilimia 75 ya Tanzania asubuhi saa 12 siku ifuatayo.

Kisha ningelianza kusafirisha mizigo toka na kwenda nchi jirani.

Halafu ningezipa boost EPZ marehemu zilizopo mipakani kwa kuhakikisha kuna dege moja kubwa toka China, Malaysia, Korea, Japan kwenda na kuja Tanzania kila wiki.

Ninaamini mapato kutoka sehemu hizi yatanisaidia kuhakikisha kuwa vijidegee vya Precision sijui Community ninavipa overtime kila siku kwa maana ningelivuta kila Mtanzania mwenye kipato kiwe kidogo namna gani kutamani kusafiri kwa divisheni ya ATC Nafuu Services!

Ningelianzisha divisheni ya helikopta za kivita na kuzigeuza kuwa za usafiri na uchukuzi ambazo Barack Obama atazifuta kazi akiingia Ikulu ya Marekani.
 
Akili,
Kwanza, biashara ya ndege siwaachii wazee. Nitawatafuta vijana wa miaka 30 -37 waliowahi kuwa marubani na wenye MBAs au Menejimenti digrii yoyote
Duh! sasa wewe mkuu wangu umeniacha nje kabisa!.. yaani unafikiria rubani mwenye MBA anaweza kuwa rubani mzuri kuliko yule ambaye hakusomea digriii au sio..
Hivi kweli unaamini kabisa mtu mwenye digrii ya MBA ni dereva mzuri wa gari kuliko yule ambaye hana digrii!.. au una maanisha kitu gani!
 
Pundamilia07,

Mkuu samahani ni wewe ambaye hukunisoma vizuri..maelezo yako hayo hapo juu ndiyo kitu nalichozungumzia muda wote huko nyuma.. Kisha sio sheria za IATA kubadilihana abiria mkuu hata kidogo ni mikataba baina ya mashirika mawili kuhusu usafirishaji wa Abiria. iwe kuna Ubia ama makubaliano ya contracts..

Unaelewa nini kuhusu IATA Clearing House (ICH) na inavyofanyakazi? (jibu lako lirejee pia katika maelezo yako hapo juu)

Naelewa fika kwamba mashirika yale yote hayafiki tena Tanzania lakini abiria wake wanakuja na mashirika mengine tofauti na wakati wa Nyerere..Lakini mkuu wangu my point is, huwezi kusafirisha abiria wa shirika fulani wakati fedha imelipwa nchi nyingine ni lazima kuna makubaliano kati ya mashirika mawili jinsi ya kugawana mapato ya msafiri mmoja aliyesafiri kwa ndege mbili za mashrika mawili tofauti..

Hii sehemu itajibiwa na maelezo utakayoyatoa juu ya ufahamu wa IATA Clearing House

Na sio swala Huo ndio Ubia naozungumzia mimi, na sielewi unaposema Emirates wangekwisha nunua hisa ikiwa ATCL sio public sokoni, hizo hisa watazinunua vipi ikiwa hujapeleka mali yetu sokoni? ..

South African Airways walinunua hisa za ATCL, je walizinunua kutoka kwenye soko la hisa?


Mkuu Emirates wanahitaji abiria zaidi toka Tanzania ikiwa kuna uwezekano wa kuvunja masoko ya ndege nyingine zilizobakia..tunaweza kuwa regional (Tanzania) partner wa Emirates with our goals being connection Tanzania and the world, na wanaweza tu kukunua hisa pale tutakapo tangaza kuwa Public soko letu DSE..Kitu muhimu kwao ni soko, vitu kama
Ebu wewe nambie mkuu wangu kam Unaishi Mwanza na unaweza kuapata ticket ya kwenda London bila kuja Dar utaacha kusafiri na ATCL toka Mwanza kuja Dar au Kili na kuunganisha na Emirates?.. Je ni Watanzania wangapi watakao penda kufanya hivyo (air of their choice) badala ya kuja Dar kutafuta ticket za BA, KLM au Swiss Air ambazo hatuna mpango wa kubadilishana nao wasafiri kama ulivyozungumzia hapo juu!
Bila shaka mauzo ya ticket za Emirates zitaongezeka..Emirates hawana haja ya kufahamu ATCL ina mtaji kiasi gani isipokuwa tunaweza vipi kuongeza soko lao nchini.. ATCL itakwenda nchi jirani na kuvuta wasafiri wa Emirates nchi za Asia na Ulaya na pengine hata sisi ATCL kuwa na ndege moja kwenda Dubai kila siku..
Ndivyo mashirika yote yanavyoshirikiana mkuu wangu Ubia unakuja tu kwa kutazama thamani ya soko lililopo, vitu kama Load factor, Revenue, seat miles na kadhalika of which I'm pretty sure tupo juu safi, bearing in mind population yetu na matatizo ya Usafiri mwingine nchini.
Again nitarudia kusema tatizo la ATCL ni UONGOZI mbaya nothing to do with shirika ATCL..soko na mali zake zote ziko safi..Kama vile Tanzania yenye Utajiri mkubwa lakini ndio nchi maskini iloshindikana kutokana na Uongozi mbaya... Potential ipo na ndiyo inawasukuma wawekeshaji kumiminika nchini kwa sababu hatuna tena policies za Ujamaa (mkono wa serikali).. Aliyesubiri kuona Tanzania ikiinuka kwanza would be the looser mkuu wangu..Tanzania itainuliwa na wale walio take risk na ndio watakaofaidika na uwekeshaji wao.. Tukisha pata mabawa tu kila kitu kitakuwa ghali na hakuna tena mwalimu..

Sasa ukifikiria njia ya kuondoka Umaskini huu ni kuuza nchi kwanza badala ya ku deal na main problem utakuwa hujafanya kitu zaidi ya kupoteza kila kitu kama tulivyopoteza madini..Watu walinunua share za Barricks mara tu waliposikia wameshinda mikataba fulani ya machimbo.. kabla hata hawajachimba shimo moja mkuu wangu lakini kila siku zinavyokwenda na utajri kuzidi ndivyo share zake zinavyosidi kuwa ghali kwa wananchi..Hivyo swala la ATCL sio swala la Innovation ni swala la kufuata mfumo uliokuwepo sasa hivi duniani.. mashrika yote unayoyaona ya ndege yalitoka mikononi mwa serikali na kuingia ktk soko huria wakati biahsra ya ndege ilikuwa ikitumba..Watabiri wa wall street hutazama mbele na sio kitu ambacho tayari kinazalisha na risk ni ndogo, faida yake huwa ndogo sana..
Swala la uongozi mbaya ndani ya ATCL ni swala ambalo linaweza kabisa kumalizwa within one month of operating. Wakisha ingia wajuzi wa biashara na kuwekesha fedha zao utaona mwenyewe mabadiliko sehemu zote za uzembe..trust me.

Niliyoaandika kuhusu Nyerere ni kwamba hapakuwepo na makubaliano ya namna hii ndio maana mashirka hayo yote yalileta ndege zao. Sasa uliposema kwamba Ubia kati ya KLM na ATC ulitakiwa toka wakati wa mwalimu ndipo niliposema isingewezekana kabisa kwa sababu mbali na siasa zetu mfumo huo haukuwepo kabisa duniani..sijui kama umenielewa hapo..

Haya ya Emirates kuingia ubia na ATCL, ah kwangu mimi sioni uwezekano wa Emirates kufanya hivyo kwa sasa kwani tayari wana-dominate soko na hakuna threat ya aina yeyote.

Tuendelee kukata issue
 
Last edited:
Haya ya Emirates kuingia ubia na ATCL, ah kwangu mimi sioni uwezekano wa Emirates kufanya hivyo kwa sasa kwani tayari wana-dominate soko na hakuna threat ya aina yeyote.

Tuendelee kukata issue

Pundamilia07:

Unasema kuwa sheria za wakati ule zilizuia KLM kuchukua ATC. Naomba unieleze kama Tipper lilikuwa ilikuwa chini ya serikali ya Tanzania au Italy walikuwa na hisa pia. Vilevile naomba data za Tanzania Investment Bank. je serikali ya Tanzania ilikuwa na 100% au Ujerumani ilikuwa na hisa pia?

Kama makampuni hayo yalikuwa hayamilikiwi na serikali kwa 100%. Kwanini sisi tulichukua mzigo wa 100% katika kitu tusicho na expertise nacho?
 
Pundamilia07:

Unasema kuwa sheria za wakati ule zilizuia KLM kuchukua ATC. Naomba unieleze kama Tipper lilikuwa ilikuwa chini ya serikali ya Tanzania au Italy walikuwa na hisa pia. Vilevile naomba data za Tanzania Investment Bank. je serikali ya Tanzania ilikuwa na 100% au Ujerumani ilikuwa na hisa pia?

Kama makampuni hayo yalikuwa hayamilikiwi na serikali kwa 100%. Kwanini sisi tulichukua mzigo wa 100% katika kitu tusicho na expertise nacho?

Nadhani iko haja ya kujikumbusha juu ya TIPER na TIB kama ambavyo umeelezea japokuwa si hayo mashirika mawili tu uliyoyataja. Kuna zaidi ya hayo just few to mention NHC, TFC nk.

Tofauti ya ATC na hayo mashirika uliyoyataja ni kwamba yalianzishwa kama sehemu ya msaada baina ya serikali ya Tanzania na nchi husika. Hata serikali ya Uholanzi ilikwishafanya jambo kama hilo pale ilipotoa msaada wa kumalizia Jengo ambalo lingelikuwa ofisi mpya za East African Airways ambalo sasa linaitwa ATC House yalipo makao makuu ya ATCL. Jengo hilo lilimaliziwa na waholanzi na pia ndiyo waliojenga Kilimanjaro Aircraft Maitenance Facility pale KIA.

Kwa case ya ATC shirika hilo lilianzishwa moja kwa moja na serikali na haikuwa ni mradi wa msaada kama ilivyokuwa hayo mashirika mengine uliyoyataja.

Kuhusu swali lako la kwani serikali ilichukua mzigo wa mia kwa mia katika kitu tusicho na expertise nacho, hapo nadhani unakosa kuirejea historia ya kuanzishwa ATC.

ATC ilianzishwa mara tu baada ya iliyokuwa Jumuiya Afrika Mashariki kuvunjika. Tanzania kama ilivyokuwa nchi nyingine za Kenya na Uganda ilikuwa inategemea usafiri wa anga kupitia East African Airways. tanzania kama nchi mshiriki ilikuwa na wataalam wengi tu kuanzia marubani, mafundi (Akina Michael Shirima), watalaam wa uendeshaji, wataalam wa masoko na mauzo, wataalam wa Ground handling & cargo etc etc.
Kwa hiyo serikali ilikuwa na jukumu la kuzikusanya hizo resources ili ziweze kufanya kazi kwa manufaa ya watanzania wote, ndipo Marehemu Jaji Yahya Rubama alipopewa kazi ya kusimamia ATC inazaliwa na kufanya kazi.

haya ni kwa ufupi lakini ATC ina historia ndefu na ya kutukuka kwa upande wa wafanyakazi waliowahi kuwepo hapo na wale waliopo.
 
Pundamilia 07,
Duh, mkuu wangu kazi kweli kweli kukufahamisha nachojaribu kusema..Mkuu navyofahamu mimi IATA clearing House inafanya kazi kama benki vile yaani nyie mna makubaliano yenu kwanza na transaction za kubadilishana malipo wanafanya wao..Lakini sio IATA inayopanga Ubia wa mashirika husika. Ni jukumu lenu kuunda huo ushirikiano, kama vile mimi leo hii bill zangu zinapitia Benki moja kwa moja na pia malipo yangu kupitia benki moja kwa moja lakini sio benki iliyoweka mkataba wangu na kampuni ya simu, cable na hata ajira yangu...

Tukirudi ktk swala la Tipper na mengineyo ninavyofahamu mimi au niseme kuelewa kwangu ni mkataba under contract uliofikiwa baina ya serikali yenu na nchi hizo zilipotupa mikopo ya kuunda miundombinu hiyo. Na serikali za nchi hizo ziliweka mashirika ya kusimamia ujenzi na uendeshaji wa mashirika hayo kama ilivyo TAZARA lakini serikali ya China haina hisa ndani ya shirika hilo..Tulifanya hivyo hata ktk mashamba ya katani, kahawa na kadhalika na nakumbuka mwalimu wakati wa Azimio la Arusha alianza kuwatimua baadhi wazungu tukashika wenyewe wafujaji.. tukaua kilimo na mashirika mengine mengi tu lakini kama hawa jamaa wangekuwa na ubia ndani nina hakika kesi zile zingekwenda UN..kama tulivyopelekwa ktk mkataba wa Citywater..
Kuhusu KLM kuingia Ubia umetumia South Africa nadhani hatuelewani hapa. Nachozungumzia ni wakati wa Nyerere kwanza na pili Emirates wasingeweza kununua share ATC kama South Africa kwa sababu Ubia huo ulikuwa kwa tender na sio soko huru. Hivyo ilitegemnea sisi tutamchagua nani..kama ilivyokuwa Richmond au mashirika mengineyo..

Tunarudi palepale tu kuwa Ushirikiano wetu na Emirates sio lazima wao wanunue share kwetu ila inawezekana kukawepo na partnership kutokana na soko tulilokuwa nalo sisi..Muhimu hapa kwa Emirates ni Umiliki wa chombo hiki na soko letu kwao sio hali ya chombo ATCL kwa sababu hatuwambii wanunue ATCL..
Kivutio kikubwa kinaweza kuwa tukienda public na kuunda upya management yenye mwelekeo..Na zaidi ya hapo Emirates wanaweza sana kutusaidia ktk kupanga malengo mapya, mfumo mpya wa utawala, mafunzo na kadhalika.. haya yote yanawezekana kabisa..
Mkuu wangu hapa kwetu Air Canada ni mbovu kupindukia yaani unachefua roho na Uongozi wake ni mbaya ajabu lakini wanashirikiana na BA vizuri tu.. Kuna wakati shirika lilianza kufirisika, ilibakia kidogo wamuuzie Mchina sijui Mjapan lakini serikali ikaingilia kati wakaweka stimulus ndani kuokoa jahazi, wakabadilisha hata management nzima na mambo kibao wakati huo huo BA haikuwa na tatizo hata moja na walikuwa wakingiza faida..Sikusikia BA wakijiuliza kuingia ubia huo na Air Canada ambayo ilikuwa ktk hali mbaya sana kuongozi na hata service zake ni mbovu hadi leo hii..
 
forget to partner with Emirates

they can codeshare - that means TC will put its code on EK flights in and out of DAR

or Interline - this is the new way. if you interline if other airlines such as BA and EK, you can sell one ticket from TC destination such Mwanza to LHR where TC does not serve

so the flight from MWANZA to LONDON will be on on ticket.

and most important things Emirates will introduce to DAR is daily Boeing 777 - 300 ER which has a capacity of maximum 442 pax effectively from 29 of march where summer timetable starts. Emirates will almost doubled their capacity from their current flight Airbus 330 - 200 which has capacity of 250.

this proved that there is huge opportunity out of DAR.
 
Pundamilia 07,
Duh, mkuu wangu kazi kweli kweli kukufahamisha nachojaribu kusema..Mkuu navyofahamu mimi IATA clearing House inafanya kazi kama benki vile yaani nyie mna makubaliano yenu kwanza na transaction za kubadilishana malipo wanafanya wao..Lakini sio IATA inayopanga Ubia wa mashirika husika. Ni jukumu lenu kuunda huo ushirikiano, kama vile mimi leo hii bill zangu zinapitia Benki moja kwa moja na pia malipo yangu kupitia benki moja kwa moja lakini sio benki iliyoweka mkataba wangu na kampuni ya simu, cable na hata ajira yangu...

No, sasa nadhani nikueleze jinsi gani IATA Clearing House inavyofanyakazi. Member Airlines wana makubaliano ya ujumla juu ya kufanya transactions zao either katika mauzo ya passenger tickets au cargo. As long as Airline ni Member wa IATA basi career akibeba passenger aliyenunua tiketi kwa moja ya members wa IATA bila ya kujali jambo lolote IATA Clearing House itapelekewa jukumu la ku-deal na transaction hiyo. Kwenye kufanya transactions hapa hakuhitaji mkataba wa Airline kwa Airline tayari wote wanatekeleza makubaliano ya pamoja ambayo yalikwisahafikiwa.

Tukirudi ktk swala la Tipper na mengineyo ninavyofahamu mimi au niseme kuelewa kwangu ni mkataba under contract uliofikiwa baina ya serikali yenu na nchi hizo zilipotupa mikopo ya kuunda miundombinu hiyo. Na serikali za nchi hizo ziliweka mashirika ya kusimamia ujenzi na uendeshaji wa mashirika hayo kama ilivyo TAZARA lakini serikali ya China haina hisa ndani ya shirika hilo..

Nadhani hapa kama umenielewa vizuri nilikuwa ninajibu swali lako la TIPER na TIB na nikasema kuwa hiyo miradi ilianzishwa kama sehemu ya misaada, kwahiyo mkataba mnapokubaliana inabidi kutekeleza yale yote yaliyomo ndani ya mkataba ule. endapo mkataba umesema kuwa mradi huu pamoja na mambo mengi utatoa mafunzo kwa wazalendo ndani ya miaka mitano halafu wageni wataondoka...hapo ni lazima kuwa wazalendo watachukua nafasi, sasa kama wameharibu hilo ni swala jingine kwani hatuwezi kuwa na wataalam wa kigeni ambao watakaa hapa daima milele. Tatizo la kuongozi hasa kwenye menejimenti za mashirika ya umma lina historia ndefu ambayo wengi tunafahamu japokuwa bado hasa sijasoma tafiti ambayo imeanisha kwa kina kujua hasa sehemu sugu ni zipi. hii ni changamoto kwa wanazuoni wanaweza kutuletea tafiti zao ninaamini tafiti zipo na labda nyingine zimekaliwa kama kawaida yetu sisi waafrika ndivyo tulivyo.


Tulifanya hivyo hata ktk mashamba ya katani, kahawa na kadhalika na nakumbuka mwalimu wakati wa Azimio la Arusha alianza kuwatimua baadhi wazungu tukashika wenyewe wafujaji.. tukaua kilimo na mashirika mengine mengi tu lakini kama hawa jamaa wangekuwa na ubia ndani nina hakika kesi zile zingekwenda UN..

Hapa kilichotokea yalikuwa ni mabadiliko ya umiliki kwani mashamba kama ambavyo umesema yalikuwa yanamilikiwa na wazungu au kwa kifupi yalikuwa yakimilikiwa na watu binafsi. Kwahiyo kimsingi wale watu binafsi walikuwa wakilenga zaidi kilimo kama biashara nyingine yeyote na walitimiza yote ya kufanya biashara ikiwemo kulipa mishahara kulingana na production. Lakini tulipoyachukua kwa maana ya serikali ilipoyachukua mashamba hayo tukatengeneza mfumo tofauti kabisa ambao haukuwa na tija au haukujali suala la kilimo kama ni sehemu ya biashara. Tukaaza kulipa mishahara na huduma nyinginezo bila ya kujali uwezo wa kuzalisha. ufujaji wa mali ulikuwa mkubwa kwa vile hakukuwa na mtu ambaye hasa anauchungu na mali ile ya 'umma' hatimaye tukaporomoka.

Hata hivyo siwezi kuwalaumu sana hao waliofanya hivyo kwani wakati nchi yetu ilipoanza kujitawala ndani ya miaka 10 serikali ilitaka kuhakikisha kila sehemu ya uongozi wa Tanzania inashikiliwa na watanzania na wakati huohuo nchi haikuwa na wataalam wa kutosha wakuweza kufanya yote hayo. Matokeo yake ni kwamba kuongoza taasisi kama benki haikujali kuwa uwe mtu wa taalauma gani, ukiwa mwalimu inatosha kuongoza benki. Kama nilivyosema kuwa siwezi kuwalaumu hao waliopewa nafasi hizo kwani ndiyo waliokuwepo na tulikuwa tunataka kwenda mbele. Kwa makosa hayo kitu kikubwa cha kufanya ni kwamba tusiendelee kuyarudia makosa ambayo hatuna sababu ya kuyarudia kwa wakati huu, mfano mzuri ni uongozi wa ATCL.


kama tulivyopelekwa ktk mkataba wa Citywater..
Kuhusu KLM kuingia Ubia umetumia South Africa nadhani hatuelewani hapa. Nachozungumzia ni wakati wa Nyerere kwanza na pili Emirates wasingeweza kununua share ATC kama South Africa kwa sababu Ubia huo ulikuwa kwa tender na sio soko huru. Hivyo ilitegemnea sisi tutamchagua nani..kama ilivyokuwa Richmond au mashirika mengineyo..


Mkandara,

Mimi ninaamini kuwa wewe ni mmoja kati ya wale wanaofuatilia mambo yanavyokwenda hapa Tanzania. Tumekuwa wote tukisoma kuwa serikali iko katika hatua nzuri za mazungumzo na kampuni ya China juu ya kuichukua ATCL. Je hapo kuna soko la hisa au ilitangazwa tender?
Kama nilivyoandika huko nyuma yeyote ambaye anaitaka ATCL kwa sasa hivi ndiye atakaye dictate terms, serikali iko tayari kufanya lolote iwezalo kumpatia yule ambaye ataonesha dhamira ya kweli ya kuichukua ATCL. Kumbuka kuwa pamoja na SAA kuwa hisa 49% lakini serikali ilikubali kuwa na idadi sawa ya wajumbe katika bodi ya wakurugenzi na kukubali Mwenyekiti japo atatoka Tanzania, lakini lazima wamthibitishe wao (SAA) na awe 'neutral'. kana kwamba haitoshi serikali mwenye hisa zaidi ya SAA ikakubali kuipatia SAA menejimenti ya ATCL bila ya hata kuwepo mtanzania ndani yake. Ninachotaka kusema kuwa wenye kutaka ndiyo wanaojuwa nini chakufanya, sisi tunaitikia tu.



Tunarudi palepale tu kuwa Ushirikiano wetu na Emirates sio lazima wao wanunue share kwetu ila inawezekana kukawepo na partnership kutokana na soko tulilokuwa nalo sisi..Muhimu hapa kwa Emirates ni Umiliki wa chombo hiki na soko letu kwao sio hali ya chombo ATCL kwa sababu hatuwambii wanunue ATCL..
Kivutio kikubwa kinaweza kuwa tukienda public na kuunda upya management yenye mwelekeo..Na zaidi ya hapo Emirates wanaweza sana kutusaidia ktk kupanga malengo mapya, mfumo mpya wa utawala, mafunzo na kadhalika.. haya yote yanawezekana kabisa..
Mkuu wangu hapa kwetu Air Canada ni mbovu kupindukia yaani unachefua roho na Uongozi wake ni mbaya ajabu lakini wanashirikiana na BA vizuri tu.. Kuna wakati shirika lilianza kufirisika, ilibakia kidogo wamuuzie Mchina sijui Mjapan lakini serikali ikaingilia kati wakaweka stimulus ndani kuokoa jahazi, wakabadilisha hata management nzima na mambo kibao wakati huo huo BA haikuwa na tatizo hata moja na walikuwa wakingiza faida..Sikusikia BA wakijiuliza kuingia ubia huo na Air Canada ambayo ilikuwa ktk hali mbaya sana kuongozi na hata service zake ni mbovu hadi leo hii..

Believe me, kuwa Emirates hawahitaji mshirika katika route ya Dar - Dubai kwani market share yao iko juu. Kinachotakiwa ni kwa ATCL iangalie kutafuta nafasi yake katika route hiyo na jambo hili litahitaji kufanyika utafiti wa hali ya juu na wala si vinginevyo. Moja ya yale ambayo unaweza kuyafanya kama ATCL inataka kwenda Dubai ni lazima 'umpigie magoti' Emirates umwombe unachotaka na hapo unaweza ukashirikiana nae lakini yeye ndiye atakaye command makubaliano. Huo ni ukweli Gulf Air aliyekuwa na nguvu sana alikimbizwa na Emirates, yuko wapi OmanAir?. What Emirates did, alinunua frequent flyers wa Gulf Air na ku-double mileages zao na wengine kuwapa Gold Card, na kuleta equipment ya kisasa kabisa katika soko la Dunia, sasa ikifikia hapo tena unataka nini zaidi ya kukubali atakalosema. Endapo utakubali analotaka Emirates basi ujue pia uwe tayari kukubali hata yale ambayo hayana maslahi kwa taifa na hii ndiyo abia ya mikataba kuna ku-gain na ku-lose ili mkubaliane.
 
Last edited:
Tanzania ianzishe kampuni mpya ambayo haina madeni na inasera mpya. ATC ifungwe na hii itakuwa njia rahisi.
 
Kufa ATC haifi....inasubiriwa kuanza tena kwa nguvu mpya....mapendekezo ya tume yatatoa mwelekeo wa hali ya mbeleni.Hopefully mapendekezo yanayotolewa hapa JF yataonwa na kuchagiza kitakachoamuliwa.
 
Pundamilia07,
Mkuu labda nichukulie kwamba unajua unachokizungumza lakini hadi hapa inaonyesha tunatoka ktk mada na kuanza kuijadili IATA..
Kifupi mkuu, Hivi unaweza kunambia mtu anaweza kukata ticket London BA ambaye ni member wa IATA na kuja hadi Mwanza kwa kuchukua connection Dar na ATCL ambaye pia ni member wa IATA kwa ticket moja alokata London?..kama inawezekana naomba somo na kama Haiwezekani naomba somo pia na hii (hai) ndicho nachozungumzia mimi ili kuiwezesha ATCL.

Swala hapa mkuu wangu ni jinsi gani ATCL should be restructured, bilichotazama mimi ni uwezo wa ATCL kufungua ukurasa mpya wa biashara na mifano yote ya Ubia na ushirikiano kama vile Kenya Airways na Precision..Ni swala la wewe kufikiria kwa nini Precision imeweka ushirikiano na Kenya Airways ikiwa kila member wa IATA anatakiwa kubeba abiria wa mtu mwingine wao watamaliza mahesabu ya malipo!..

Swala la mashamba, mkuu pia nimezungumzia Azimio la Arusha kama chanzo cha mabadiliko nchini haikuwa swala la Utaifishaji.. mfano, mashamba ya sukari Kilombero tuliingia mkataba na serikali ya Kiholanzi kuayendesha mashamba yale lakini hayakuwa yao toka mwanzo..sizungumzii nani aliyenyan'ganywa mashamba hayo kabla serikali haijawaweka Waholanzi..Azimio la Arusha halisisitizi tu Kutaifisha mkuu wangu isipokuwa pia kumwezesha Mtanzania kuendesha uchumi wa nchi yake, hivyo tulipowafukuza Waholanzi kutoka Kilombero halikuwa swlaa la kufaifisha isipokuwa kuwaweka wazalendo wananchi ktk utawasla wa mashamba hayo..hivyo kuuvunja mkataba ambao serikali ilikuwa iki own 100% ya mashamba hayo..

Mwisho swala la Emirates unakosa kitu muhimu sana nachozungumzia hapa..Lee hapo juu kazungumza exacctly nachosema mimi kuwa soko la Abiria Tanzania sio Dar.. wewe unatazama Emirates na Dar hakuna aliyesema tunataka ushirikiano nao kwa ajili ya safari za nje kuja Dar isipokuwa ni sisi tunaweza kuwaletea wasafiri wengi toka mikoani ambao ni zaidi ya asilimia 70 ya wasafiri wote waendao nchi za nje..Kwa hiyo sisi tunachotazama ni kuijenga ATCL ktk safari za ndani na nchi jirani kwanza.. lakini hatuwezi kufanya hivyo bila kupata mshirika ambaye ana uwezo wa kwenda nchi za nje kwa hiyo tunachotazama sio kutoka Mwanza kuja Dar tu bali msafiri huyo aweze kutoka Mwanza hadi Dubai kwa ticket moja ya ATCL au kutoka Dubai hadi Mwanza kwa ticket moja ya Emirates..Bila shaka navyofahamu mimi hii ndio sababu Precision wameungana na Kenya Airways au Zambia na Swiss Air, nje ya hapo sioni sababu..
 
Kufa ATC haifi....inasubiriwa kuanza tena kwa nguvu mpya....mapendekezo ya tume yatatoa mwelekeo wa hali ya mbeleni.Hopefully mapendekezo yanayotolewa hapa JF yataonwa na kuchagiza kitakachoamuliwa.


WoS:

Kuna jamaa yangu, baba yake alipostaafu kutoka serikani basi akaanzisha biashara zake. Katika biashara yake akaleta mambo yake ya kiserikalini. Akachukua chumba kimoja na kukifanya ofisi. Akaajiri watumishi wa kufanyia kazi na kuwalipa mishahara. Mradi wake ulikuwa ni ng'ombe wa maziwa wawili tu na bustani. Auchukua muda mradi mzima ukawa finito.

Mambo yote ya tume uliyoleta hapa yamefanyika mara nyingi sana katika nchi hile yetu ya mababu. Lakini matokeo ni yaleyale. Ninaweza ku-bet na wewe, katika kipindi cha miaka mitano, shida za ATC zinatakuwa ni zilezile.

Mentality za watendaji wetu ni kama za baba wa jamaa yangu. wanafikiri kuwa kila kitu kikishakuwa katika nafasi yake basi mafanikio yatatelemka kama chakula cha wana waIsrael.

Kama hawatakuwa na model inatakayo-sustain growth na itayo-address kundi la wateja, hakuna kitakachofanyika. Mpaka sasa mashirika ya kiserikali hayajuhi wateja gani wanatakiwa na jinsi gani ya ku-sustain growth. Siku zote wakiona Ethiopia Airline, wanasema na sisi tuanzishe la kwetu.

Katika posti yangu moja nimesema hawa jamaa wanatakiwa kuiga Southwest Airline (period). Na wateja wawe local.
 
Zakumi,
Bahati mbaya sana katika nchi yetu kumekuwa na utamaduni wa diagnosis ya matatizo na hatimaye prescription kutolewa na "tume".Sijaelewa hasa mantiki ya utaratibu huu maana ni wazi kabisa kuwa matatizo ya ATC hayahitaji uvae miwani uyaone na kuyaelewa.Major prob ni management period.Kwanini hawaondolewi mara moja ( board na management) its very hard to comprehend.
Kama ulivyosema vema,uendeshaji wa biashara hii kwa miaka hii unahitaji watu wapya wenye mtizamo mpya wa jinsi ya kufanya mambo.Ukiangalia walioko katika kuendesha ATC ni watu wenye fikra na mtizamo wa 1947! wengi wao hawajawahi kuwa good performers mahali popote.If anything wamewahi kuwaangusha sana watanzania. Itakuwa ngumu.
 
Pundamilia07,
Mkuu labda nichukulie kwamba unajua unachokizungumza lakini hadi hapa inaonyesha tunatoka ktk mada na kuanza kuijadili IATA..

Mkuu Mkandara,

Unajua wakati mwingine tunapojadili basi hoja za nyongeza hujutokeza ambazo huboresha ile hoja mama, hili ni jambo la kawaida inaonesha afya njema ya majadiliano mapana na ya kina.


Kifupi mkuu, Hivi unaweza kunambia mtu anaweza kukata ticket London BA ambaye ni member wa IATA na kuja hadi Mwanza kwa kuchukua connection Dar na ATCL ambaye pia ni member wa IATA kwa ticket moja alokata London?..kama inawezekana naomba somo na kama Haiwezekani naomba somo pia na hii (hai) ndicho nachozungumzia mimi ili kuiwezesha ATCL.

Hilo unaloliulizia kwamba abiria anaweza kukata tiketi London - Mwanza ni possible na linafanyika wakati wote. Utaratibu unakuwa kama hivi:
Route ya LHR (London Heathrow) - DAR career anakuwa British Airways
Route ya DAR-MWZ career anakuwa ATCL
Malipo kwa safari nzima abiria anamlipa British Airways (endapo Alikata tiketi katika ofisi za British Airways).
Wakati Abiria anapofika Dar na ku-connect safari yake kwenda Mwanza atatoa coupon inayoonesha route ya DAR - MWANZA na ATCL watampatia boarding pass kwa safari hiyo.
Kitakachofuata ni ATCL kuipeleka ile coupon waliyoichukua kwa abiria in exchange of the boarding pass to IATA Clearing House ambapo portion ya ATCL itatolewa katika ile nauli nzima ambayo British Airways aliipokea.

Utaratibu huu hauhitaji makubaliano maalum kati ya Airline na Airline kama ambavyo nimeeleza hapo awali isipokuwa ni makubaliano ya pamoja. ATCL imekuwa ikisafirisha abiria wanaunganisha safari zao kwa aina hii tangu mwaka 1977 hadi iliposimamishwa hivi karibuni.



Swala hapa mkuu wangu ni jinsi gani ATCL should be restructured, bilichotazama mimi ni uwezo wa ATCL kufungua ukurasa mpya wa biashara na mifano yote ya Ubia na ushirikiano kama vile Kenya Airways na Precision..Ni swala la wewe kufikiria kwa nini Precision imeweka ushirikiano na Kenya Airways ikiwa kila member wa IATA anatakiwa kubeba abiria wa mtu mwingine wao watamaliza mahesabu ya malipo!..

Mkuu Mkandara,

Suala la Precision Air na Kenya Airways nadhani nilielezee kidogo kwa faida yako na wasomaji wengine.

Precision Air ni sehemu ya Kenya Airways. Kenya Airways wanamiliki 49% ya hisa zote za Precision Air. Chief Executive Officer wa Precision Air ni Mkenya from Kenya Airways. Kwahiyo ushirikiano wa Kenya Airways na Precision Air unafuata a rule of thumb. Maamuzi yeyote yatakayoiathiri Kenya Airways ni part and parcel ya Precison Air. Katika Financial Statements za Kenya Airways Precision Air inakuwa report kama sehemu ya investment za Kenya Airways.

Je ni kwanini Kenya Airways alinunua hisa za precision Air?

Wakati ATCL ilipokuwa katika mchakato wa kuuza hisa 49% kwa strategic partner Kenya Airways ilikuwa ni miongoni mwa mashirika ya ndege yaliyojitokeza ku-bid. Lakini wakati zimesalia dakika kama siyo masaa kuutangazwa nani ameshinda mchakato ule, Kenya Airways walijitoa baada ya SAA kuvujisha siri kuwa wao tayari wame-bid USD 20mil dhidi ya USD 6mil za Kenya Airways.
Nia kubwa ya Kenya Airways kutaka kununua hisa za ATCL haikutofautiana sana ile ya SAA kwani from DAR to Nairobi ni mwendo wa takribani saa moja na ushee hivi, kwa maana hiyo basi Kenya Airways isingependelea kujenga Hub mahali karibu kabisa na Nairobi.
Aidha Kenya ilikuwa inaitaka ATCL ili kumweka mbali mshindani wake SAA mbali na soko la Afrika ya Mashariki.
Baada ya Kenya Airways kuikosa ATCL na kuona tayari mshindani wake amekiwsha ingia katika ardhi ya Afrika Mashariki, alicholifanya ni ku-propose kwa Precision Air wamuuzie hisa 49% ili apate kuingia kwenye ardhi ya Tanzania ambane hasimu wake SAA asitanuke zaidi na kuleta madhara, ikiwemo kutoifanya DAR kuwa Hub ya SAA.
Kenya Airways ilikuwa nirahisi kuipata Precision Air kwani kuingia kwa SAA katika soko la Tanzania kulihatarisha kuwepo kwa Precision Air. Lengo kubwa la SAA ni kuiondoa ATC kwa hiyo lengo dogo obvious wangehakikisha kuwa Precision ndiyo inakuwa ya kwanza kufunga virago. Kwa kuzingatia hali hiyo ya kitisho Precision Air iliona the only shield to put before SAA ni kuwakaribisha Kenya Airways.
Kwani nini Kenya Airways bado wapo na Precision Air?
Endapo itathibitika kuwa ATCL ndiyo imekufa moja kwa moja, basi interest za Kenya Airways ndani ya Precision Air pia zitabadilika na huenda ndiyo unaweza kuwa mwisho wa Precision Air kwani lengo kuu la Kenya Airways ni kutawala soko la Afrika masharaiki ikibidi kwa 99%. Na ambacho wanaweza kukifanya Kenya Airways wataanzisha kampuni ambayo itakuwa ni feeder kwa East Africa kwa ajili ya Ndege zake.
Hii ndiyo mtazamo wa Kenya Airways.


Swala la mashamba, mkuu pia nimezungumzia Azimio la Arusha kama chanzo cha mabadiliko nchini haikuwa swala la Utaifishaji.. mfano, mashamba ya sukari Kilombero tuliingia mkataba na serikali ya Kiholanzi kuayendesha mashamba yale lakini hayakuwa yao toka mwanzo..sizungumzii nani aliyenyan'ganywa mashamba hayo kabla serikali haijawaweka Waholanzi..Azimio la Arusha halisisitizi tu Kutaifisha mkuu wangu isipokuwa pia kumwezesha Mtanzania kuendesha uchumi wa nchi yake, hivyo tulipowafukuza Waholanzi kutoka Kilombero halikuwa swlaa la kufaifisha isipokuwa kuwaweka wazalendo wananchi ktk utawasla wa mashamba hayo..hivyo kuuvunja mkataba ambao serikali ilikuwa iki own 100% ya mashamba hayo..

Mwisho swala la Emirates unakosa kitu muhimu sana nachozungumzia hapa..Lee hapo juu kazungumza exacctly nachosema mimi kuwa soko la Abiria Tanzania sio Dar.. wewe unatazama Emirates na Dar hakuna aliyesema tunataka ushirikiano nao kwa ajili ya safari za nje kuja Dar isipokuwa ni sisi tunaweza kuwaletea wasafiri wengi toka mikoani ambao ni zaidi ya asilimia 70 ya wasafiri wote waendao nchi za nje..Kwa hiyo sisi tunachotazama ni kuijenga ATCL ktk safari za ndani na nchi jirani kwanza.. lakini hatuwezi kufanya hivyo bila kupata mshirika ambaye ana uwezo wa kwenda nchi za nje kwa hiyo tunachotazama sio kutoka Mwanza kuja Dar tu bali msafiri huyo aweze kutoka Mwanza hadi Dubai kwa ticket moja ya ATCL au kutoka Dubai hadi Mwanza kwa ticket moja ya Emirates..Bila shaka navyofahamu mimi hii ndio sababu Precision wameungana na Kenya Airways au Zambia na Swiss Air, nje ya hapo sioni sababu..

Mkuu Mkandara,

Kwanza nadhani itabidi uthibitishe usahihi wa takwimu zako hasa pale ulipotoa takwimu ya 70%. Siwezi kuikataa ama kuikubali data hiyo unless iko supported na takwimu sahihi.

Lakini hata hivyo ukiangalia maandiko yako kwa makini sidhani kama abiria wote wanaoanzia safari Dar kutoka sehemu zingine wanaletwa DAR na Foreign Airlines. Ni wazi kuwa ATCL au Precision Air ndiyo wanaowaleta kutoka huko wanakotoka. Kwa maana hiyo basi ni wajibu wa ATCL kibiashara kukamata soko la ndani kwa asilimia kubwa ili iweze kuwa na nguvu ya zaidi bila ya kutegemea kufanya ushirikiano na Foreign Airline yeyote katika kumiliki soko lake la ndani.
Pamoja hayo ikumbukwe kuwa siyo wasafiri wote wanaotoka nje ya mkoa wa Dar es Salaam wanatumia usafiri wa ndege kutoka huko makwao.


That's why nilisema kuwa Emirates hana shida yeyote na soko la Tanzania kwani there;s no any threat what so ever. Sioni ni kwani Emirates afanye hivyo unless kama nilivyoandika hapo awali kuwa labda ATCL inaweza kutaka ushirikiano lakini haitakuwa na sauti wa nguvu kubwa katika negotiation kati yao, trust me!


Tuendelee kukata ishu mzee!

------------------------------------------------------------
 
Kufa ATC haifi....inasubiriwa kuanza tena kwa nguvu mpya....mapendekezo ya tume yatatoa mwelekeo wa hali ya mbeleni.Hopefully mapendekezo yanayotolewa hapa JF yataonwa na kuchagiza kitakachoamuliwa.

Unadhanin watakuja na opendekezo gani jipya litakaloiokoa ATCL? nakuhakikishia hata kama mapendekezo yakiwa mazuri, utekelezaji utakuwa hovyo na matojkeo yake yanaweza kuwa mabaya kuliko tunayoyaona hivi sasa. Hivi ni tatizo gani la ATCL ambalo halijulikani? Kuna haja ya kuunda tume kutafuta ufumbuzi kuhusu katatizo ya ATCL? WIZI MTUPU
 
Pundamilia07,
Mkuu yote sawa...nimepiga simu ofisi ya British Airways hapa wamenambia wana issue ticket ONLY to Dar - Tanzania..siwezi kufikishwa Mwanza kwa sababu hakuna member wa timu yao anayekwenda huko...
Kwa maelezo zaidi kuhusiana na connection kanambia wanaweza tu kunisafirisha ikiwa kuna mashirika ambayo ni franchise yao, ni codeshare partners wao pia kikubwa zaidi ni member wa network ya ushirikiano (Airlines Allience) ambayo shirika linatakiwa kuwa member au subsidiary wake kunifikisha Mwanza..Sasa sielewi kinachoendelea kama kanifunga kamba sijui lakini majibu yake ndio hayo siwezi kupata ticket moja hadi Mwanza - Tanzania.

Mkuu, hizo hesabu za asilimia 70 ya wasafiri wa ndege kwenda nje unafikira nimetunga!..Hata hivyo haiusiani kabisa na ATCL isipokuwa ni hesabu ambayo nimeipata toka chombo cha serikali hivyo siwezi kuiweka kama unavyodai kwa sababu sikuipata toka site fulani..
Nachokuomba chukulia kuwa ni kweli na jaribu kuangalia jinsi gani ATCL inaweza kufanya kazi zaidi kwa kushirikiana na mashirka kama Emirates kwa sababu nilizoandika mwanzoni..USHIRIKIANO . Iwe kwa kununua hisa, iwe kwa Ubia, iwe kujiunga na Allience yote kwangu ni sawa maadam tunaweza kusafirisha abiria wetu toka Mwanza< Bukoba moja kwa moja kwenda nje with a connection Dar au Kili..

Mkuu wangu Mashrika yote makubwa duniani mbali na ku run international flights yana mashirika madogo yanayo run ndani ya nchi zao iwe Uingereza, France, Japan au America na kuna ushirikiano kmkubwa kati ya shirika mama (International) pamoja na hilo la ndani (Local).. huwezi kuchukua Air Canada kuja Toronto au Vancouver ukaunganisha na shirika lolote la ndani ati maadam kuna ndege inakwenda huko..

Hata hivyo, tumeongea vya kutosha na ushauri wangu kwa serikali yetu ni kuliokoa shirika hili lakini badala ya kuliwekea regulations, wakati umefika sisi tuondoe hizo regulations ambazo hazihusiani kabisa na business Policies zaidi ya kuwepo mkono wa serikali ndani ya Uongozi wa chombo hicho..ATCL iwe huru (public private company) na viongozi wake WAPYA wapewe nguvu ya kuwa Responsible na Accountable..
 
Back
Top Bottom