WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 970
kuna mahali wamama tunajisahau sana napo ni hapo kwa kumuachia h'gal kila kitu akifanye, mpaka kutandikiwa kitanda jamani, hapana!, QUOTE]
Na je,
ukiwa na h'boy..inakuwaje? Huyo baba bado atamchukua? ( im playing the devil's advocate)
kuna mahali wamama tunajisahau sana napo ni hapo kwa kumuachia h'gal kila kitu akifanye, mpaka kutandikiwa kitanda jamani, hapana!, QUOTE]
Na je,
ukiwa na h'boy..inakuwaje? Huyo baba bado atamchukua? ( im playing the devil's advocate)
WOS, usije kushangaa watu wakakujibu... unauliza ndevu kwa Osama?
kuna mahali wamama tunajisahau sana napo ni hapo kwa kumuachia h'gal kila kitu akifanye, mpaka kutandikiwa kitanda jamani, hapana!, QUOTE]
Na je,
ukiwa na h'boy..inakuwaje? Huyo baba bado atamchukua? ( im playing the devil's advocate)
h'gals/boyz wote kwangu mie kunifanyia usafi room yangu hapana!
nakushauri mfukuze mara moja. kuna ndugu yangu alikuwa na hausi geli toka iringa, alikuwa mdada. akapata safari, akamwacha na mmewe na watoto. housegirl alianza kumwekea dawa yule mbaaba, dingi likaanza kumchukia mkewe aliyemzalia watoto bila kupenda, siku wakamkamata housegirl akiletewa dawa na rafiki yake toka iringa ili ammalize kabisa yule mama mwenye nyumba achukue ndoa. baba likuwa anafanya mapenzi nae kwa nguvu za dawa, akampenda housegirl kuliko mkewe. alipokuja kugundua na dawa imeisha nguvu, alimpeleka hadi polisi, dingi lilitaka kumkatakata vipande kwasababu alikuwa ameshaitesa sana ndoa, ndani kulikuwa kama jehanamu kwa muda mrefu katika ndoa. msichana alifukuzwa kama mbwa, sasa hivi anafanya kazi kwenye mgahawa fulani hapa mtaani. watu hawana hata hamu nae, wanajuta kumfahamu. ukitaka kuwa na house girl, chukua kale kanakomaliza tu shule kule iringa au mikoa mingine,kakianza kuwashwa kidogo tu, mpe zawadi na nauli aende nyumbani akasalimie wazazi moja kwa moja.
ujuzi huwa sio wajuzi, kwasababu wengine ni watoto hata hawana uzoefu.labda kama una lihousegirl likubwa sana ndo linaweza kuwa lilikubuhu. wengi wanakuwa walimaliza lasaba wakaja kuvunjia ungo ndani kwetu. hivyo sio wajuzi,ila wana dawa.
ujuzi huwa sio wajuzi, kwasababu wengine ni watoto hata hawana uzoefu.labda kama una lihousegirl likubwa sana ndo linaweza kuwa lilikubuhu. wengi wanakuwa walimaliza lasaba wakaja kuvunjia ungo ndani kwetu. hivyo sio wajuzi,ila wana dawa.
Nzuri ngoja ninywe kiloba nikushauri.
Masanilo,Brenda,Mwanajamii,Nyamayao,WOS,Mbu,Msanii,Joyceline mnaweza mkaendelea na mjadala mwenzenu huyo jahazi linazama h/g katoa TG kwa baba mwenye nyumba.
Kuwaita wote nadhani sio good idea,house girl awepo kwenye hicho kikao ili iweje?Hapana...ni vyema yeye aongee na mama mkwe pekee na pia cha muhimu zaidi ajirekebishe.Nani kakuambia kwamba laitoa Tig kwa baba mwenye nyumba,soma tena uelewe vizuri.
namshauri huyu mama punguze jazba amuite mama mkwe wake, mume wake na huyo dada wayaongee kwa uwazi bila kuuma uma maneno, halafu kama kuna sehemu alikuwa anakosea kama binadamu na mama mwenye nyumba ahakikishe anaparekebisha, akiona kuna uhusiano kati ya baba na binti amrudishe binti kwa wazazi wake amkabidhi na aeleze.
Kuna mtu niliona amemshauri aondoke aondoke aende wapi? yeye ni mwanamke anatakiwa awe strong apiganie nyumba yake na penzi lake, bora mume hana tatizo hao wengine wasikunyime usingizi
Ila ukumbuke responsibilities zako as a wife.
WomenofSubstanc;430077]
Na je,
ukiwa na h'boy..inakuwaje? Huyo baba bado atamchukua? ( im playing the devil's advocate)
Housigeli anataka kuniharibia ndoa
Anti/kaka jamii
habari yako. Nategemea mzima wa afya na hutasita kunisaidia kunipa ushauri unaonifaa. Mimi ni mwanamke mwenye watoto wawili. Tangu nimeolewa miaka sita iliyopita, nimekuwa na msichana wangu wa kazi mmoja ambaye nimempenda sana hasa kwa kuwalea vizuri watoto wangu na kuwa mwepesi wa kazi. Kutokana na kuishi vizuri na housigeli huyu, amekuwa kama mtoto wa nyumbani na hata ndugu zangu na wa mume wangu wanampenda sana na wamemzoea kupita kiasi.
Tatizo hili la kuwazoea ndugu wa mume wangu sasa naona linataka kuharibu ndoa yangu kwani huyu msichana ameanza tabia mbaya na amemweleza mkwe wangu kuwa mimi situlii nyumbani na sina muda wa kumshughulikia mume wangu kwani kazi zote anafanya yeye, mimi kazi yangu kusafiri na kushinda kazini. Huyu mama mkwe wangu kusikia hayo, amekuja juu na sasa anamshinikiza mume wangu aniache eti nashindwa kuhudumia nyumba na badala yake amuoe housigeli. Mume wangu ameshtuka na amenieleza kila kitu hali iliyonikasirisha sana.
Sasa naomba ushauri wako kwani mama mkwe bado yupo kwangu, je, nifanyeje kabla hajaondoka kurudi kwake? Mama Kelvin Tabata, Dar es Salaam. Mama Kelvin pole sana kwani inaonekana huyo mama mkwe wako hajaelimika vya kutosha. Uzuri wa mwanamke haupimwi kwa kazi za nyumbani pekee, bali kuna mambo mengi na mkwe wako anapaswa kutambua kuwa wewe unafanya kazi hivyo huwezi kukaa nyumbani muda wote na ndiyo sababu ukatafuta msaidizi.
Lakini pia ni vyema ukiwa nyumbani ufanye kazi zilizopo ikiwamo kumpikia mumeo na kumhudumia ipasavyo. Usiwe na hasira za haraka kwa msichana wako wa kazi kwani inawezekana aliulizwa kimtego naye akajibu vizuri tu lakini mkweo akawasilisha kwa mumeo vibaya. Nadhani mumeo pia anapaswa amweleze mama yake kwa upole kuwa wewe unafanya kazi na huwezi kufanya kazi zote za nyumbani. Pia amweleze kuwa huyo msichana wa kazi kamwe hawezi kuwa mke wa mtoto wake.
Naamini mtoto wake akimwelimisha na akawa na msimamo, mama mkwe wako ataelewa au hata kama hataelewa, atashindwa kuendelea kusisitiza anachotaka. Ni vyema pia ukakaa na mshichana wako na kumhoji ilikuwaje hata wakazungumza hayo na mkweo na ukiona kama alichokonolewa basi mtahadharishe akae mbali na mama mkwe na asiwe mwepesi kueleza mambo ya ndani ya nyumba kwa mkweo.
Hata hivyo fanya uchunguzi wako kwa siri na ukiona msichana wako anapalilia ili aolewe yeye, basi ni vyema ukatafuta msichana mwingine wa kazi na huyo kumwondoa ili asije kuharibu ndoa yako. Haina haja kugombana na mtu yoyote kwani naamini huyo mkweo ataondoka na nyinyi mtaendelea na maisha yenu. Pia jifunze kuvumilia kwani wakwe wengine uelewa wao ni mdogo.
Huyo House girl sio anataka kuharibu ndoa, bali anataka kuitengeneza. Inaelekea mama ulishachukulia mambo mengi for granted. Kwa sababu h.girl anafanya kazi vizuri ukabweteka na kusahau baadhi ya majukumu yako nyumbani. Chunguza vema unaweza kukuta kuwa hakusaidii kuosha nguo za mzee tu, bali na mengne mengi anakusaidia