Housigeli anataka kuniharibia ndoa yangu jamani

haya mambo ya house girl yamezidi, mie nitakuja kuweka house boy tu kwangu.
 
...yaani nanihii mpaka akasahau chupi? no way bana...huenda kwenye kuanua nguo za maza hauz, chupi yake ikachanganyika nazo..
Mbona mu wepesi wa ku jump kwenye conclusions? :)
Mhh Always an Element of Doubt!
 
...nakweli, mimi ningesema, "...nilidhania chupi yako mama nanihii, nimeiokota nje!" :)
Mbu------------ I salute you man.

Nimeisoma hii kwangu mimi ninaiona kama kitu kidogo sana wala kisipaswe kukuuliza kichwa Mama Kelvin. Mradi si mume anayeshinikiza wala usipate presha.
1. Haya ni matokeo ya kumwachia dada kazi zote hata zile ambazo unapaswa kuzifanya wewe mwenyewe. Kwa namna ulivyoelezea ni kama vile wewe ni mama wa nyumbani au mfanyabiashara ambaye huna budi kutoka nyumbani kwano na si mfanyakazi ambaye umeajiriwa. Nasema hivi kwa kuwa ungekuwa umeajiriwa basi dada asingewezasema kuwa unatoka mchana.

2. Kama wewe ni mfanyabiashara kama nilivyoguess basi jaribu kupangilia safari zako za biashara ambazo zitakupa siku chache za wewe kuwa nyumbani kwako. Na muda huo utakaokuwepo nyumbani jitahidi kuchakarika mama hata kama binti atakuwa amekaa chini wewe chakarika especially vile vya kumtengenezea mume.

Otherwise ni umbeya tu wa watoto wa kike na hasa kama kazoeana sana na watu hapo nyumbani na huyo mama mkwe wala si wa kumlaumu ndivyo walivyo baadhi yao so usijisumbue kumfukuza housegirl wala mama mkwe badilisha ratiba yako kucover yale wanayoyashupalia

Ushukuru MUNGU mumeo yuko upande wako otherwise.............
 
Duh, pole sana dada.
Mimi nakushauri kama unaweza sali sana na hilo pepo likupitilie mbali, muombe bwana Yesu ainusuru ndoa yako, na baada ya hapo wewe sasa jipange upyaaaaaa!!!!!..
Unajuwa wamama wa siku tunajisahau sana katika ndoa zetu, we are taking everything for granted, unadhani ukiolewa ndiyo basi, unajinenepea bila mpango, kutwa kushiriki kwenye kitchen parties, kazi ofisini ni safari saa zoteeeee, hatupiki, hatufui, hatufanyi chochote majumbani mwetu, watoto wetu hatuwalei vizuri tunawaachia hao mahousegeli kuna wamama hata hawalali na watoto wao wakiwa wachanga wanaachwa na mahousegeli jamani ili mradi tu vituko. Tukiwa na kazi nzuri basi tunajiona na kujisikia kuwa tuko sawa na hao waume zetu, hapana inabidi tujirekebishe sana. Siyo wanaume wote wako sawa wengine wanakuangalia tu kama hawajali kumbe wanamaindi kimoyoni.
Hivi mnajuwa kuna wamama wanawaachia mahousegeli kufuwa hadi chupi zao na chupi za waume zao, jikoni wanaingia hata baada ya miezi 2 ndiyo wanafika jikoni, sex mpaka aanze mwanaume sisi kila siku tuko busy na tumechokaaa unadhani mume haoni yote hayo, wamama wengine wachafu na wavivu hata kutandika vitanda vyao hawawezi yote no dada anafanya, jamani waume wana macho nao wanaona, mwisho wa siku si bora ajiolee tu huyo housegeli.
By the way sisemi kama wewe unafanya haya yote ila nahisi kuna sehemu utakuwa ulikosea.
Anyway jipange upyaaaaaaa hujachelewa bado, naamini mume wako anakupendaaa ndiyo maana hata akakueleza yanayoendelea.

Nakutakia mafanikio mema na ujipange upya dada sawa. Muombe Mwenyezi Mungu atakusaidia na akupe nguvu.

Ni mimi Mahengo
 
Dear mama

nina experiance ya vitu hivi niliwahi kuona nyumba moja baba analala na house chumbani na mke wake anajua hilo na wakati wanaenda kulala pamoja mke anajua ila niligundua kwamba yule mwanamke alikuwa anakosa nguvu fulani hivi ya kumwokoa -- hakui haki zake ni nini yeye kama mwanamke na kama mke wa mtu ( wamechukuwana mitaani ) so wengine huwa wanasema ahh hatujaowawna hana haki hizo -- wengine elimu zao na kutojua dunia inakwendaje kazi kukaa ndani tu


Mmhh haya ni kweli?
 
haya mambo ya house girl yamezidi, mie nitakuja kuweka house boy tu kwangu.

Pretty kwenye nyumba ya jirani kuna houseboy kafanya kazi za ndani kama miaka 6 baba wa nyumba akamtilia shaka,akamwambia nataka ujifunze gari kuna rafiki yangu atakukabidhi pick-up ukishajuwa kuendesha.Houseboy akasema baba mi nimeridhika na kazi hii,mzee akajuwa kuna kitu kinaendelea akataka kumtimua,mama akasema ukimtimua nami naondoka jamaa akasema poa tu ondokeni wote.
 
Kuhusu mahousegirl Mama mia nikueleze siri moja aliniambia jamaa ambaye kila kukicha mkewe anafukuza housegirl baada ya kugundua wana uhusiano na mumewe.Aliniambia yeye hupenda harufu orijino na mkewe ni mtu wa masabuni/mapafyumu kibao nikamwambia si umwambie aache kutumia akiwa nyumbani akajibu nimemwambia hasikii.
 
Kuhusu mahousegirl Mama mia nikueleze siri moja aliniambia jamaa ambaye kila kukicha mkewe anafukuza housegirl baada ya kugundua wana uhusiano na mumewe.Aliniambia yeye hupenda harufu orijino na mkewe ni mtu wa masabuni/mapafyumu kibao nikamwambia si umwambie aache kutumia akiwa nyumbani akajibu nimemwambia hasikii.

Mh mnakosaga sababu?!!
 
msaidieni ki ukweli huyo mama mia amekwama ki ukweli kabisa mpeni njia amalize hiyo tabu yake.
 
Dear mama

nina experiance ya vitu hivi niliwahi kuona nyumba moja baba analala na house chumbani na mke wake anajua hilo na wakati wanaenda kulala pamoja mke anajua ila niligundua kwamba yule mwanamke alikuwa anakosa nguvu fulani hivi ya kumwokoa -- hakui haki zake ni nini yeye kama mwanamke na kama mke wa mtu ( wamechukuwana mitaani ) so wengine huwa wanasema ahh hatujaowawna hana haki hizo -- wengine elimu zao na kutojua dunia inakwendaje kazi kukaa ndani tu

Hii hutokea sana tu,kuna jamaa mtaa wa pili ana vijisenti kidogo kaoa kwenye familia masikini basi ndugu kibao wa mkewe wanaishi pale,sasa huyu jamaa akitoka kulewa anachagua leo alale na nani kati ya hao ndugu,huyo mama kwa kujua shida iliyopo kwao na jamaa anavowasaidia mpaka kijijini anaishia kusikitika na kukonda tu.
 
Wakimama pamoja na majukumu mengi ya maisha ni vyema mkatambua wajibu wenu kama mama katika nyumba zenu,mkijisahau sana matatizo kama hayo lazima yatatokea tu!!!!!!

Tunza familia yako hasa mumeo!!!!
 
Hii hutokea sana tu,kuna jamaa mtaa wa pili ana vijisenti kidogo kaoa kwenye familia masikini basi ndugu kibao wa mkewe wanaishi pale,sasa huyu jamaa akitoka kulewa anachagua leo alale na nani kati ya hao ndugu,huyo mama kwa kujua shida iliyopo kwao na jamaa anavowasaidia mpaka kijijini anaishia kusikitika na kukonda tu.

Mmhh jamani huu nao ni uozo uliokithiri,yaani kisa kwetu masikini ndo jamaa afanye hivyo sasa kama ni UKIMWI si familia nzima itaisha jamani,lakini huyo jamaa nae hana akili kabisa hivi haoni aibu kufanya mapenzi na ndugu wa mkewe,nadhani atakuwa na matatizo fulani maana haya mambo ni ya aibu jamani. Bado haiingii akilini kwamba shida za familiya ya mkewe yeye ndo awe amepata chance ya kuendekeza ufuska? huyo ana shida na kama hiyo nyumba ina housegirl siku mama na ndugu zake labda hawapo jamaa atamdandia housegirl.
 
Wakimama pamoja na majukumu mengi ya maisha ni vyema mkatambua wajibu wenu kama mama katika nyumba zenu,mkijisahau sana matatizo kama hayo lazima yatatokea tu!!!!!!

Tunza familia yako hasa mumeo!!!!

Ni kweli kabisa unayoyasema Nyuki,kila mama akitambua wajibu wake katika familia sidhani kama tutalalamika oo housegirl ananiharibia ndoa mara oo jamaa ana nyumba ndogo,hayo hayaatakuwepo kabisa maana ukielewa wajibu wako na ukielewa kuwa wewe ndo mwangalizi wa familia utakuwa umezuia mianya yote ambayo inaweza kuharibu ndoa yako.
 
kila mama akitambua wajibu wake katika familia sidhani kama tutalalamika oo housegirl ananiharibia ndoa.

Nimeangalia akina mama wengi wakisha olewa na akabahatika kuzaa mtoto mmoja basi kwisha kazi anajisahau maana hapo atataka binti wa kazi yeye anaona wajibu wake ni kudo tu na mzee vingine vyote anamwachia binti wa kazi hata kudo kwenyewe kiwango kinashuka anakuwa mzembe zembe flani basi mzee anaona bora abadilishe radha tu.
 
Mmhh jamani huu nao ni uozo uliokithiri,yaani kisa kwetu masikini ndo jamaa afanye hivyo sasa kama ni UKIMWI si familia nzima itaisha jamani,lakini huyo jamaa nae hana akili kabisa hivi haoni aibu kufanya mapenzi na ndugu wa mkewe,nadhani atakuwa na matatizo fulani maana haya mambo ni ya aibu jamani. Bado haiingii akilini kwamba shida za familiya ya mkewe yeye ndo awe amepata chance ya kuendekeza ufuska? huyo ana shida na kama hiyo nyumba ina housegirl siku mama na ndugu zake labda hawapo jamaa atamdandia housegirl.

Kama ndugu hawasalimiki housegirl atapona kweli.Mi nimeona mwanamme anaetembea na binamu wa mkewe na mkewe anafahamu na wanaishi nyumba moja.Kuna mambo mengi sana yaliojoficha majumbani kwetu.
 
Mi naona huyo h/g hana tatizo tatizo ni huyo mama mzima anamshauri mwanae kuvunja ndoa sasa hapo anajenga au anabomoa? Nadhani jibu ni kubomoa sasa ukweli una mme mzuri sana na mheshimu sana kwani mpaka kakufikishia basi anakupenda na kukuthamini kwa hiyo jitaidi kwa muda unaokuwa huru uwe karibu zaidi na mumeo na umfurahishe mpaka ukikosekana sekunde awe anakukumbuka tu. Pia Mkalisheni huyo h/g na kumshauri kwani yeye kutoa hizo habari hajakosea bali ni uelewa mdogo maana mtu aliyempa ni wa nyumbani kwa hiyo yawezekana kwa muda mama aliyokaa ameona ubize wako akamhoji h/g naye akijua ni mama kumficha si rahisi na ikiwezekana huyo house girl asifue nguo za mmeo na ukiwepo upike mwenyewe. Ila kaa na mmeo mjadili hili swala kwanza kwa makini na mshauri awe na msimamo na hata kumwambia mama yake kuwa hakuwa sahihi kumwambia maswala kama hayo na hakuwa sahihi pia kuongea na h/g maswala mazito kama hayo. Jambo la mwisho bila ya mumeo kujua fuatilia mwenendo mzima wa huyo h/g wako.
 
Hakuna sababu ya kumkasilikia mtu yeyote, wewe mama umesahau majukumu yako,

ukiamka asubuhi unajiangalia kwenye kioo, ukiona matongotongo usoni unavunja kioo? hapana ila unajisafisha,

nafikiri umenielewa, hao watu ni vioo vyako, tumia muda huu kujirekebisha, na mumeo anakupenda sana ndio maana kakueleza kila kitu vinginevyo angekula kona kimya kimya.
 
Mahouse girl wanalaumiwa bure, mke ukiwa na excuse nyingi pale mzee anapotaka kufumua jipu lake ujue atatafuta mtaalam mwingine wakati wowote. Kwa kuwa housegirl anavyo vifaa vya kutumbulia jipu mzee atatumia vifaa hivyo kwa sababu anavijua vizuri storage yake na pia ni sehemu ya miliki zake, tena anapatikana kwa urahisi wakati wowote jipu linapoiva. Isitoshe, pengine housegirl atajituma zaidi kufumua jipu kuliko mama ambaye anatumia uzoefu wa uprofessa wake akitumia mbinu zilezile za kale asitake kuwa mbunifu.

Wanawake wengi ndio wanaowatuma waume zao kutafuta tiba mbadala kwa nyodo zao, sasa aende nje kule akarudi na moto wenye kuangamiza familia yote? Mwanamke awe tayari wakati unaofaa na wakati usiofaa kwa usalama wa wote na kumjenga mumewe. Vinginevyo acha hosegirl amsaidie kila kitu.
 
Back
Top Bottom