Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,463
- 39,929
Pamoja na kutoa pole na rambirambi, ni lazima tujiulize tutaendelea mpaka kulini kwa kutegemea rehema za Mungu? Sitoshangaa leo tutaambiwa katika Hotuba ya Rais kuwa haya yalikuwa ni mapenzi ya Mungu na ya kuwa wanaunda tume kuchunguza kitu gani kilisababisha na wananchi wasiwe na wasiwasi hali ni shwari na halikuwa tukio la kighaidi..
Katika wazimu wetu tutasema Amen.. na kusahau kabisa mlolongo wa kutojiandaa na majanga ambao serikali ya CCM imeuendeleza kwa miaka kadhaa sasa na kutuacha tuishi kwa bahati!
Jana, tumeikwepa risasi! Huko mbeleni (na itakuwa hivyo kwani majanga yataendelea kutokea hata kama tunaombea yasitokee, ndiyo kanuni ya ulimwengu!) tutakuja kulia kama tulivyolia kwenye MV. Bukoba na Bahi! (wengine wanajiuliza "Bahi?"! wameshasahau!
I have more to say.. listen..
[mp3]http://mwanakijiji.podomatic.com/enclosure/2009-04-29T23_41_36-07_00.mp3[/mp3]
Update: Nasikia hadi hivi sasa waliokufa wamefikia 10:
Pili: Mabomu yaliripuka wakati yakihamishwa-mengine yalikuwa yapelekwe Shinyanga na mengine yalikuwa yanaandaliwa kwa ajili ya safari ya Darfur pamoja na kikosi cha kulinda amani kutoka TZ.
Lakini jeshi halitaki kusema kulikuwa na askari wangapi ndani ya ghala wakati mlipuko unatokea(thanks MN) - Isomeke yawezekana watu wengi zaidi wamefariki kuliko idadi ya awali kama nilivyodokeza katika taarifa yangu ya awali kwenye main thread.