G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Ama kweli Rias Magufuli ana kiburi.
Haiingii akilini anakuja na mipango ambayo kwa namna moja ama nyingine, kwa kiongozi wa nchi ni mipango ya upande mmoja. Alishindwa kuweka mzani wa alipotoka na vitu vyake vs watu aliowaongoza ili ajue afanye nini. Kushindwa kufanya hivyo ni tafsiri kuwa yeye ndiye mpangaji na ni lazima watu wafuate.
Kwanza hii tabia amekuwa nayo kwa miaka mitano iliyopita. Kinachonishangaza ni yeye kuonyesha waziwazi kuwa mwendo ni uleule kwa miaka mitano ama zaidi ijayo. Hii ni hatari sana hasa ukizingatia ishara ambazo zimeanza kujitokeza za kulazimisha ushindi.
Hotuba nzima ya Rias Magufuli imejikita katika kununua ndege na kuongeza kipande cha reli ya kisasa kutoka Dodoma hadi Isaka-Makutopora.
Tuwe wakweli, Rais alipora haki muhimu za wafanyakazi kwa miaka mitano iliyopita na kubebesha mzigo mzito wa kodi kwa watanzania masikini ili kugharamia miradi ambayo mingi ni kama analazimisha ikamilike ndani ya muda mfupi huku akijua athari zake. Kwa jana alipaswa japo kuongea jambo jipya kwa watanzania ambalo linagusa maisha yao moja kwa moja ili ajadiliwe vinywani mwao. Amefeli kabla ya safari ya kampeni.
Mradi wa SGR kwa hesabu zangu mpaka ufike Isaka itagharimu si chini ya trilioni 8. Kwa awamu ya miaka mitano iliyopita mradi umeelea elea tu vipande hadi Morogoro na amefanikiwa tu kulipa trilioni 1.2
Hali hii inanifanya niamini kuwa mabavu anayotumia Magufuli kwenye huu uchaguzi ni ili apate wabunge wote wa CCM na yeye ashinde ili mradi huu ambao nina uhakika ili ukamilike kutoka tarehe ha leo hautachukua chini ya miaka 8! (Ana mpango wa kuongeza muda? Ana mpango wa kupendekeza kodi kandamizi zaidi ili apate fedha?)
Hayo ni yenu watanzania ila kiukweli ukitoka kwako tarehe 28 kwa nia ya kumpigia Rais Magufuli kura basi ni sawa na mtu umetoka kwako na kamba kwa lengo la kuingia porini ili ukajinyonge ufe!
Sisi hapa leo tutaonekana tunapiga porojo ila kiukweli kwa mambo aliyofanya Magufuli basi ukimpigia jura ni aibu juu ha nafsi yako! Nyie sikilizeni wasanii na baadhi ya wafuasi wake ambao wamejitoa kumeza akili za watu ila mjue wanafanya hivyo kwa maslahi yao! Sisi tulimpinga Magufuli mwanzoni kabisa mwa utawala wake kwakuwa tunamjua vyema! Tunaijua akili yake!
Haiingii akilini anakuja na mipango ambayo kwa namna moja ama nyingine, kwa kiongozi wa nchi ni mipango ya upande mmoja. Alishindwa kuweka mzani wa alipotoka na vitu vyake vs watu aliowaongoza ili ajue afanye nini. Kushindwa kufanya hivyo ni tafsiri kuwa yeye ndiye mpangaji na ni lazima watu wafuate.
Kwanza hii tabia amekuwa nayo kwa miaka mitano iliyopita. Kinachonishangaza ni yeye kuonyesha waziwazi kuwa mwendo ni uleule kwa miaka mitano ama zaidi ijayo. Hii ni hatari sana hasa ukizingatia ishara ambazo zimeanza kujitokeza za kulazimisha ushindi.
Hotuba nzima ya Rias Magufuli imejikita katika kununua ndege na kuongeza kipande cha reli ya kisasa kutoka Dodoma hadi Isaka-Makutopora.
Tuwe wakweli, Rais alipora haki muhimu za wafanyakazi kwa miaka mitano iliyopita na kubebesha mzigo mzito wa kodi kwa watanzania masikini ili kugharamia miradi ambayo mingi ni kama analazimisha ikamilike ndani ya muda mfupi huku akijua athari zake. Kwa jana alipaswa japo kuongea jambo jipya kwa watanzania ambalo linagusa maisha yao moja kwa moja ili ajadiliwe vinywani mwao. Amefeli kabla ya safari ya kampeni.
Mradi wa SGR kwa hesabu zangu mpaka ufike Isaka itagharimu si chini ya trilioni 8. Kwa awamu ya miaka mitano iliyopita mradi umeelea elea tu vipande hadi Morogoro na amefanikiwa tu kulipa trilioni 1.2
Hali hii inanifanya niamini kuwa mabavu anayotumia Magufuli kwenye huu uchaguzi ni ili apate wabunge wote wa CCM na yeye ashinde ili mradi huu ambao nina uhakika ili ukamilike kutoka tarehe ha leo hautachukua chini ya miaka 8! (Ana mpango wa kuongeza muda? Ana mpango wa kupendekeza kodi kandamizi zaidi ili apate fedha?)
Hayo ni yenu watanzania ila kiukweli ukitoka kwako tarehe 28 kwa nia ya kumpigia Rais Magufuli kura basi ni sawa na mtu umetoka kwako na kamba kwa lengo la kuingia porini ili ukajinyonge ufe!
Sisi hapa leo tutaonekana tunapiga porojo ila kiukweli kwa mambo aliyofanya Magufuli basi ukimpigia jura ni aibu juu ha nafsi yako! Nyie sikilizeni wasanii na baadhi ya wafuasi wake ambao wamejitoa kumeza akili za watu ila mjue wanafanya hivyo kwa maslahi yao! Sisi tulimpinga Magufuli mwanzoni kabisa mwa utawala wake kwakuwa tunamjua vyema! Tunaijua akili yake!