Hotuba ya Rais Kikwete ya mwisho wa mwaka

naumia sana moyoni jinsi ambavyo watu wengi wanazidi kupoteza munkari wa kusikiliza hotuba za mkuu..sijui aje na approach ya Chavez!!??
 
Heri ya mwaka mpya Baba H, siku hizi unapotea sana Mkuu. Kuhusu huyu mhe. wetu mimi nilishaacha kusikiliza hotuba zake baada ya ile aliyoitoa bungeni. Mkulu hayupo serious kabisa.
 
Mwalimu naomba unisaidie hesabu kidogo..



hesabu zangu hazipandi.. where am I messing it up?

Mwanakijiji,

Rudi kwenye hotuba za rais za nyuma juu ya hizi pesa za mabilioni ya JK. NI kwamba hicho ndio kiasi ambacho serikali ilitenga na kuweka kama dhamana. Bank zilishauriwa na zilikuwa na uwezo wa kukopesha zaidi ya hizo pesa (bilioni moja kwa mkoa).

Nilikuwa interested na hiyo scheme na nilisoma hotuba zote husika. Milioni 21 kwa bara ilikuwa ni minimum na wala sio maximum.

Utekelezaji wa huo mpango ulikuwa bomu na hizo pesa hazijasaidia sana. Huwa najiuliza ilikuwaje wawakilishi wa wananchi kama wabunge wakashindwa kusimamia hizo fedha?
 
Hotuba iliyo jaa spinning si hotuba .Mie sitaisoma kwa undani ila nataka kuona aliyo tueleza hadi akapewa kitim yanatendeka
 
Yepi hayatatendeki?. Please yaanishe ,Tuyaone-Tuyajadili. Sio unarusha maneno Tuu?

Mkuu huyajui haya hadi niyaweke hapa tena upya then am out .Huwezi kijadili kaa huna historia sasa .Fuatilia mijadala utayajua mengi .
 
Wana JF,
Rushwa ni Adui mkubwa

Fisadi ni Adui

Katika hitimisho JK amedai hatuna adui?

"...Tunaumaliza mwaka nchi ikiwa na sifa kubwa katika medani ya kimataifa. Uhusiano wetu na mataifa yote duniani ni mzuri. Hatuna adui.
Uelevu wangu, Hatuna adui kutoka nje!

Je hawa maadui wetu wa jamii, wa ndani ya nchi ;-Mafisadi, Wala rushwa, Watoa rushwa-sio maadui tena?
 
Yote tisa kumi ni Kipande hiki..

Tunaumaliza mwaka nchi ikiwa tulivu. Hii inathibitisha kuwa nchi inaweza kuwa tulivu isipokuwa pale ambapo baadhi yetu tutakapokuwa tumeamua kuwa isiwe hivyo. Naomba mwaka 2009 uwe tofauti. Tuache vitendo vya kuchochea ghasia kwa kisingizio chochote kile. Vitendo hivyo havitavumiliwa hata kidogo. Ni vizuri tukaambiana mapema tusije tukalaumiana. Naomba Watanzania wenzangu wote na hasa wanasiasa wenzangu tuyatambue hayo na tujiepushe nayo. Naomba makundi ya kijamii yatambue ukweli huo na waache kuwaendekeza wanasiasa hasidi..

.

Je, maneno haya mazito yanaweza kuwa yametokana na kitu gani haswa!..
 
Mheshimia: Rais inampasa akumbuke kuwa UTULIVU WA NCHI unahitaji kulindwa na pia kutunzwa. na kwa bahati njema imetokea kuwa yeye ndie mwanye jukumu kubwa la kuhakikisha ulinzi na matunzo hayo vinapatikana. Kama Amiri jeshi mkuu atakua tayari kuyatumia majeshi yetu ya ulinzi dhidi ya maadui wa nje ikibdi kufanya hivyo.(Mungu aepushie mbali) Na kwa maadui wa ndani ambao wako wa aina nyingi na hujitokeza kwa sura tofauti, silaha ya kwanza ni kutowaonea haya. pili kuhakikisha sheria zinafuatwa na haki inatekelezwa bila kujali jina, urafiki, cheo cha jana au cha leo. Ni pale haki itakapotendeka tu na ionekane kuwa imetendeka, ndipo AMANI NA UTULIVU vitakapoweza kushamiri. kinyume cha hayo Wananchi hawataacha manung'uniko na malalamiko. Mh:Rais kizaizai cha mafisadi ni mtihani kwako hasa ukizingatia lile BATAMZINGA la Krismasi ya Ufisidi ktk jina na umbo la Rais mstaafu B W MKAPA hatujajua nini kinaendelea kuhusu tuhuma zote zinazo mwandama kiumbe huyo!!!! Inachukuwa na kuhitaji zaidi ya hadithi na methali njema ili kutunza na kulinda AMANI NA UTULIVU nchini. Mh: Rais usiombe bakuli la maji ukanawa kama alivyofanya Herode, yeye alikua na Pilato juu yake wewe ndio Pilato pia. NA haya si kwa uchochezi bali HAKI HAKI HAKI. macho, masikio na akili za Watanzania vinakuangalia wewe RAIS.
 
Spinning spinning JK...
Mhesimiwa nakutakia kila la kheri, miezi iliyobaki ipite haraka kama umande wa asubuhi kwenye jua. Wapishe wengine watufanyie kazi maana ni wazi imekushinda.
 
Haya nimeona Kikwete akiwapongeza TRA..tena yuko mbioni kuwazawadia sijui kitu gani! Labda mimi nakosea lakini sioni mantiki kabisa kutumia T shilingi iliyoshuka thamani kuonyesha makusanyo zaidi ya mwaka wakati ktk mwaka mzima kuna biashara mpya zilizofunguliwa ambazo zimeongeza kipato..
Ukikusanya kodi Tsh.100 toka kwa watu 10 mwaka jana huwezi kutumia ongezeko la ukusanyaji wa kodi..ikiwa zimekusanywa Tsh. 120 (+20) wakati mwaka huu umekusanya hizo kodi toka watu 12..
 
..nilijitahidi sana kusikiliza kwa makini hotuba ya huyu kilaza..lakini i saw and heard nothing new ...nikaishia kulala...nimejaribu hata kuisoma ..and i see it doesnt even worthy kuchangia lolote....no wounder hata thread ya hotuba za jk siku hizi haipati wachangiaji kwa kasi...

remember those days tulikuwa tunakesha kwa walio ngambo..kusubiria....na walio tanzania wanakesha wana post ....siku hizi watu wanaona usanii ndani ya sanaaaaaa!
 
Nafikiri hotuba na utekelezaji ni vitu viwili tofauti na hili la utekelezaji ndio limekuwa tatizo sugu sana basi wito wangu kwa viongozi watekeleze kwa vitendo juu ya usimamizi wa mambo ya msingi ambayo yamekuwa yakipigiwa kelele sana.
 
..nilijitahidi sana kusikiliza kwa makini hotuba ya huyu kilaza..lakini i saw and heard nothing new ...nikaishia kulala...nimejaribu hata kuisoma ..and i see it doesnt even worthy kuchangia lolote....no wounder hata thread ya hotuba za jk siku hizi haipati wachangiaji kwa kasi...

remember those days tulikuwa tunakesha kwa walio ngambo..kusubiria....na walio tanzania wanakesha wana post ....siku hizi watu wanaona usanii ndani ya sanaaaaaa!

Bora umesema wewe.

Sijui kwa nini huwa tunapoteza muda kujadili hotuba za JK wakati tunajua fika hakuna kitu zaidi ya usanii. La muhimu nafikiri ni kuiombea nchi na yeye mwenyewe ili 2010 aachie ngazi. Otherwise TZ itaendelea kuwa maskini kuliko hata Somalia.
 
Rais wetu bwana,

Wakati mwingine yuko sawa wakati mwingine yuko hivi.Cha muhimu hapo alitaka kutuambia alikuw aMbugani kipindi cha Christmas.

Mamabo muhimu kwa nchi hii ni pamoja na Bush kuja Bongo,Kukamatwa kwa mafisadi lilikuwa jambo dogo sana.
 
Yote tisa kumi ni Kipande hiki..

Tunaumaliza mwaka nchi ikiwa tulivu. Hii inathibitisha kuwa nchi inaweza kuwa tulivu isipokuwa pale ambapo baadhi yetu tutakapokuwa tumeamua kuwa isiwe hivyo. Naomba mwaka 2009 uwe tofauti. Tuache vitendo vya kuchochea ghasia kwa kisingizio chochote kile. Vitendo hivyo havitavumiliwa hata kidogo. Ni vizuri tukaambiana mapema tusije tukalaumiana. Naomba Watanzania wenzangu wote na hasa wanasiasa wenzangu tuyatambue hayo na tujiepushe nayo. Naomba makundi ya kijamii yatambue ukweli huo na waache kuwaendekeza wanasiasa hasidi..

.

Je, maneno haya mazito yanaweza kuwa yametokana na kitu gani haswa!..


Mwaka wa 2008 tunaoumaliza leo ulikuwa mwaka wa aina yake kwa taifa letu na katika historia ya uongozi wangu. Ulikuwa ni mwaka ambao tumepata mafanikio mengi mazuri na mengine ya kihistoria katika nyanja mbalimbali za maisha ya wananchi wa Tanzania na taifa letu. Lakini, pia kulikuwepo na changamoto au matukio machache ambayo yalisababisha baadhi ya watu ndani na nje ya nchi yetu wapate shaka juu ya hatima ya umoja, amani na utulivu wa nchi yetu. Umoja, amani na utulivu ndiyo nguzo kuu na sifa kubwa inayoitofautisha na kutambulisha Tanzania miongoni mwa mataifa barani Afrika.
Ndugu Wananchi;
Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwamba tumeumaliza mwaka huu kwa usalama, amani na utulivu. Tuzidi kumuomba baraka na rehema zake, katika mwaka 2009, ili nchi yetu iendelee kuwa na amani, utulivu na watu wake waishi kwa upendo, umoja, masikilizano, mshikamano na ushirikiano kama ndugu wa taifa moja.
Pamoja na kumuomba Mwenyezi Mungu, hatuna budi kutambua kuwa dhamana ya kuhakikisha kuwa nchi yetu inaendelea kuwa tulivu na yenye amani na upendo miongoni mwa watu wake ni yetu wenyewe. Ni ukweli ulio wazi kuwa katika mwaka huu tunaoumaliza sasa baadhi yetu tumekuwa tunafanya vitendo au kutoa kauli ambazo zilikuwa zinalielekeza taifa kubaya. Tena tulikuwa tunafanya hivyo kwa ajili ya kuendeleza manufaa binafsi ya kisiasa. Ni matumaini yangu kuwa tutajiepusha na mambo hayo katika mwaka 2009. Nawasihi viongozi wenzangu wa kisiasa na wa kijamii tubadilike, tuweke mbele maslahi ya taifa ili tuiepushe nchi yetu na mabalaa ambayo baadhi ya wenzetu yaliwakuta.

Kama hii hotuba aliandikiwa na Januari Makamba, basi ujue imelenga kuzima kelele za kuitaka serikali iwashughulikie mafisadi na hasa wa EPA na zaidi Kagoda. Walengwa wa hotuba hii ni wanasiasa, viongozi wa dini, wamiliki wa vyombo vya habari, wahariri wakorofi na wananchi wachache/

Lakini kama hotuba aliiandika mwe nyewe, basi atakuwa anawalenga wale walioanzisha vita dhidi ya wale wanaopiga vita ufisadi na hii ni pamoja na wale wanaothubutu kubadili vita na kuwataka ASKARI MAHIRI wageuke nyuma na kuanza kurusha risasi upande wao na kuwapa mgogo mafisadi. JK kama hivyo ndivyo nakuunga mkono lakini kama ni kinyume yaani kama na wewe unaungana na wanaotaka kuzima moto wa vita ya ufisadi SIKO PAMOJA NAWE na naamini humu JF na wananchi wengi hawatakuwa pamoja nawe. Kuwa upande wa wananchi wako asilimia 80 waliokupa kura.
 
Date::1/2/2009
Kauli ya rais ni vitisho-Wanasiasa
WAHOJI ALITAKA NCHI IWAKE

Na Salim Said
Mwananchi​

SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa onyo kali dhidi ya wanaojihusisha na kuchochea ghasia nchini, akisema "tusije tukalaumiana," wanasiasa wamejibu wakisema kauli hiyo si sahihi na ni ya vitisho ambavyo haviwezi kuwazuia kufanya kazi zao.

Rais Kikwete alitoa onyo hilo juzi wakati wa hotuba yake ya salaam za mwaka mpya alipoonya wale aliowaita wanasiasa hasidi, akisema "tuache vitendo vya kuchochea ghasia kwa kisingizio chochote kile... ni vizuri tukaambiana mapema tusije tukalaumiana".

Lakini kauli yake haijawa nzuri masikioni mwa wanasiasa ambao wanaona kuwa mwaka 2008 ulitawaliwa na vitendo vingi vya kudai haki, ikiwemo migomo na vurugu, wakisema vinathibitisha kuwa nchi haikuwa tulivu kama Rais Kikwete alivyoeleza.

Akizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, kiongozi wa upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohammed (Mbunge) alisema, Rais hakupaswa kutoa kauli hiyo kwa kuwa ni jambo la kawaida katika nchi yoyote kutokea vurugu.

Alisema sheria zilizotungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano na kutiwa saini na rais zipo na kwamba hizo ndizo zinapaswa kutumika kushughulikia wanaosababisha vurugu na si kutoa vitisho tu.

"Nilidhani kuwa rais atasema kuwa ataendelea kusimamia haki na utawala bora katika vitu ambavyo vinalegalega, lakini anatoa vitisho... vitisho ni kinyume kabisa na misingi ya utawala bora," alisema Mohammed.

Alifafanua kwamba kwa kawaida zinapotolewa kauli za vitisho kama hivyo, Watananzania hufikiria kuwa ni wapinzani tu ndio walengwa, lakini ukweli ni kwamba hata chama tawala husababisha vurugu katika baadhi ya maeneo.


"Isiwe kwa wapinzani tu, sheria lazima iwe msumeno kwa kila mtu. Kwa chama tawala na vyama vya upinzani, yaani wanasiasa wote," alisisitiza Mohammed.

Alipinga kauli ya rais kuwa mwaka 2008 ulikuwa tulivu na kuhoji kuwa rais alitaka aone nchi inawaka moto ndio ajue kuwa si tulivu.


Alisema mwaka jana nchi ilitawaliwa na vurugu, migomo na maandamano na ghasia katika sekta mbalimbali nchini Tanzania.

"Mwaka jana hautasahaulika kwa matukio ya migomo na maandamano ya walimu, wanafunzi wa vyuo vikuu na sekondari, wafanyakazi wa Benki ya Makabwela (NMB), wazee wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki na matukio ya ufisadi pamoja na mauaji ya albino. Hii ni amani tu, sijui alikuwa anataka kiashiria gani rais wetu?" alihoji Mohammed.

Hata hivyo, alisema mpasuko wa kisiasa Zanzibar na mfumko wa bidhaa muhimu nchini ambao umesababisha wananchi kutokuwa na amani kwa kukosa mlo wao wa kawaida, yaliutikisa mwaka 2008.

Mohammed alilaumu hotuba ya rais kwa kulifumbia macho suala la ajira kwa Watanzania na kuamua kubaki bubu bila ya kuzungumza chochote kuhusu ahadi hiyo, jambo ambalo alilielezea kuwa ni usaliti kwa wapiga kura.

"Tulitegemea kuwa rais angetuambia katika hotuba yake kuwa ndani ya miaka mitatu ya utawala wake amefanikiwa kutoa ajira ngapi kwa Watanzania lakini hakuligusia kabisa. Huu ni usaliti kwa wapiga kura," alisema Mohammed.

Naye Gedius Rwiza anaripoti kuwa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), kimeelezea kushangazwa kwake na kauli ya Rais Kikwete ya kuonya dhidi ya wanasiasa na vikundi vya kijamii vitakavyojihusisha na kuchochea ghasia.

Rais wa CWT, Gratian Mukoba alisema wameipokea kwa mshangao kauli hiyo, kwa sababu rais wa nchi anapozungumzia migomo, anajumuisha walimu ambao wamekuwa wakidai haki zao na sio kuchochea migomo.

Mukoba alisema kauli hiyo ya rais inalenga kuwatisha walimu na wafanyakazi wote wanaoidai serikali madai mbalimbali na kwamba, katika matukio yote yaliyotokea mwaka jana hakuna tukio la mgomo ambalo lilikuwa la uchochezi bali yalilenga kudai haki.


Aidha alisema kuwa, pamoja na kauli hiyo wanategemea kufanya mkutano mkuu mwishoni mwa mwezi huu, kufanya majumuisho ya mwenendo mzima wa ulipaji wa madai ya walimu na kuongeza kuwa baada ya kufanya uhakiki huo watatoa tamko dhidi ya serikali.

"Baada ya kufanya uhakiki huo kama madai hayo yatakuwa hayajawa tayari na mimi nasema tusije kulaumiana maana hapa naona ni kama mchezo wa paka na panya," alisema Mukoba.


Walimu waliitisha mgomo nchi nzima wakishinikiza walipwe zaidi ya Sh16 bilioni ikiwa ni malimbikizo ya malipo yao mbalimbali, hata hivyo mgomo huo ulikumbana na vizingiti mbalimbali vya mahakamani, ikiwemo amri isiyo ya kawaida ya kuuzuia mgomo iliyotolewa usiku na jaji wa Mahakama ya Kazi.

Alisema kauli kwamba baadhi ya watu wamekuwa na lengo la kujinufaisha na ghasia hizo, si kweli kwani upande wa walimu ni jambo ambalo liko wazi hadi sasa bado wanapigwa chenga na kushindwa kupata haki zao.

Naye Fidelis Butahe anaripoti kuwa wastaafu wa EAC, ambao waliwahi kuzuia barabara ya Ali Hassan Mwinyi inayotumiwa na vigogo wengi wa serikali katika harakati zao za kudai haki, wameahidi kuendelea na mikakati yao kama hawatalipwa mafao wanayodai kwa zaidi ya miaka 31.

Mjumbe wa Jumuiya hiyo, Ramadhani Makingi alisema kuwa licha ya Rais Kikwete kutoa onyo kwa wanasiasa na vikundi vya kijamii dhidi ya ghasia, hawatakubali kuona haki yao inapotea kwani hadi sasa hawajalipwa mafao yao huku serikali ikiwa imeshatoa tamko kuwa zoezi la malipo hayo limeshafanyika.

"Kama unavyojua hivi sasa suala letu linashughulikiwa na Kamanda (wa kanda maalum ya Dar es salaam, Suleiman) Kova ametuahidi kuwa atalifikisha sehemu husika na atatupatia jibu.

Lakini kama serikali haitakubali kukaa na sisi kujadili malipo yetu na ikiendelea kung’ang’ania msimamo wake kuwa imeshatulipa, hatutasita, tutaendelea na harakati zetu mpaka tutakapohakikisha tumelipwa," alisema Makingi.

Alisema kuwa licha ya rais Kikwete kutoa onyo kwa wanaochochea vurugu, wapo watu wanaodai haki zao kwa hiyo serikali inatakiwa iwaangalie na sio kuwatisha ili washindwe kudai haki zao, akisema vitisho ni kinyume na sheria za haki za binadamu.

"Tulipanga matembezi zaidi ya mara nne tumezuiwa na polisi; tumefukuzwa kutumia uwanja wa Mnazi Mmoja; tumedai malipo yetu tukaambiwa kuwa hatukuwa wafanyakazi wa EAC bali tulikuwa vibarua; wastaafu wengine wanakufa kila siku, lakini hakuna msaada wowote tunaopata.

Sasa hapo tukiandamana au kudai mafao yetu utatuambia kuwa tunachochea vurugu wakati ni wazi kuwa madai yetu hayasikilizwi," alisema Makingi.

Licha ya Kikwete kuhusisha baadhi ya vurugu hizo kuwa zinachochewa na wanasiasa, lakini hakuweka bayana vitendo hivyo vya uchochezi vilifanywa na watu gani.

Wastaafu hao mpaka sasa wameshafanya matukio makubwa manne. Julai 26 na Septemba 4 mwaka jana waliandamana mpaka Ikulu, Oktoba 17 walijazana nje ya ofisi za Wizara ya Fedha na Uchumi kwa nia ya kuzungumza na Naibu Waziri wa Wizara hiyo juu ya mafao yao.

Hatua yao ya nne, ambayo ilisababisha viongozi nane wa Jumuiya hiyo kukamatwa na kufunguliwa mashitaka ya kukusanyika bila kuwa na kibali, waliifanya Oktoba 29 baada ya kukaa katikati ya Barabara ya Ali Hassan Mwinyi na Umoja wa Mataifa kuanzia alfajiri na kusababisha msongamano mkubwa wa magari jijini Dar es Salaam.
 
sishangai kuona kauli kama hizi. Miaka nenda miaka rudi ya utawala wa JK hatujaona matunda ya uongozi wake. Serikali yake imekosa mwelekeo. Na kama kawaida ya CCM huwa wanatafuta wanyoinge. Na kawaida yao wanyonge wao ni wapinzani wa visiwani. Tunakaribia kura haya anzeni kazi mabingwa.
 
Dar cuts growth forecasts for 2008 and 2009

Posted Friday, January 2 2009 at 11:47
THE EAST AFRICAN​

Tanzania has cut its 2008 and 2009 growth forecasts as the global economic slowdown hits exports in east Africa's second biggest economy and postponed plans to issue a sovereign bond, the country's president said.

Known for its relative stability in the region, Tanzania's economy depends largely on mining, agriculture and tourists visiting its wildlife parks and beach resorts. It has been touted as one of the more appealing frontier markets.

"Because of the negative effects of the global economy slowing down, it is projected we will not achieve our 2008 economic growth projections, as well as those of 2009," President Jakaya Kikwete said in a speech marking the end of 2008, seen by Reuters on Friday.

"It is projected that the economy will grow at 7.7 percent instead of 7.8 percent (in 2008), and 7.3 percent instead of 8 percent in 2009," Kikwete said.

Tanzania, like many countries worldwide, has not been spared by the global financial turmoil that has reined in growth and hit commodity prices and sectors such as tourism.

In June 2008, the east African nation of 40 million people had projected its economy would grow by 8.1 percent in 2009, and accelerate to 9.2 in 2011. It grew by 7.1 percent in 2007.


Kikwete said the financial downturn had forced the country to postpone plans to issue a Eurobond to fund improvements to infrastructure, which is seen as a constraint on development.

"The international financial turmoil has forced us to postpone our plans to raise funds using sovereign bonds to build our major roads. It is my hope that when conditions improve we will examine this plan afresh," he said.

In October, Tanzania said it expected to have a sovereign credit rating by March this year and was planning to issue a Eurobond for more than $500 million.

Tanzania is among Africa's main aid recipients. It received $336 million in debt relief from the International Monetary Fund under the Highly Indebted Poor Countries programme.

But with interest in emerging markets collapsing as Western investors dump any perceived risk from their portfolios and with Western governments forced to spend billions saving their banks, Tanzania is bound to feel a pinch from the economic crisis.

Kikwete said the country's national park authorities had reported a slowdown of between 7 percent and 18 percent in tourist arrivals and earnings.
"The drop in our export sales and the drop in tourist arrivals will harm our economy, and our foreign exchange earnings will fall and lower our ability to buy imports."

Tanzania's Tourist Board had projected the sector would earn $1.2 billion in 2008, from 750,000 to 800,000 visitors. In 2009, it was expected to earn $1.35 billion from 950,000 visitors.

Kikwete said the global economic downturn had also led some businesses to postpone investment in the country.
 
Back
Top Bottom