Tumain
JF-Expert Member
- Jun 28, 2009
- 3,154
- 70
MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), Dk. Edward Hoseah, amemtupia lawama Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), Elieza Feleshi, akisema amekalia kesi 60 za vigogo.
Dk. Hoseah aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akihojiwa na waandishi wa habari muda mfupi baada ya sherehe za maadhimisho ya Siku ya Maadili kitaifa, zilizofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.
Ingekuwa kila mtu anatoa maamuzi yake, ningekuwa mimi ningesema kuwa kila mtu asimamie kesi zake, kwa sasa nina kesi 60 kwa DPP, hata hivyo suala hilo kamuulizeni DPP zaidi, alisema bila kuwataja vigogo hao.
Source: Tanzania daima
Dk. Hoseah aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akihojiwa na waandishi wa habari muda mfupi baada ya sherehe za maadhimisho ya Siku ya Maadili kitaifa, zilizofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.
Ingekuwa kila mtu anatoa maamuzi yake, ningekuwa mimi ningesema kuwa kila mtu asimamie kesi zake, kwa sasa nina kesi 60 kwa DPP, hata hivyo suala hilo kamuulizeni DPP zaidi, alisema bila kuwataja vigogo hao.
Source: Tanzania daima