Jeshi letu la Polisi wanafanya kazi kwa bidii na utii sana, hakika tuna Jeshi la Polisi linalofuata sheria na taratibu za nchi yetu, tena kwa kukupa taarifa mapema kuwa usifanye jambo fulani, na ukifanya ndio unapata adhabu, huu ni uzalendo wa hali ya juu wa Jeshi letu.
Majeshi mengine ya Polisi nchi za wenzetu, wala taarifa hupewi, unashangaa umekamatwa na kupigwa vibaya na kuumizwa au hata kuuawa, na hupewi taarifa ya awali hata kidogo, ila Jeshi letu la Polisi, wanasema kabisa mapema, usifanye hiki na kile, na ukiacha kufanya, wala hawakugusi kabisa, Chadema watukutu na kujifanya jeuri sana, hivi kweli unaweza
kushindana na Jeshi la Polisi? Nadhani wamepata funzo, kwani amani tulio nayo inafaa ilindwe kwa hali na mali.