Hongera CCM

Mods napendekeza huu uzi ulioletwa na Juliana Shonza ufutwe kwa kuwa umetolewa au kwa kutokuelewa vizuri idadi ya kata ambazo Chadema walishinda kwenye uchaguzi wa kata 26 uliofanyika hivi karibuni na/au umepotoshwa kwa makusudi kwani maelezo yake hayana usahihi...Chadema walishinda kata kumi na sio nane kama alivyoeleza.

Pia napendekeza Juliana Shonza ambaye ni mleta mada apigwe ban kwa kufuata sheria za JF kwa kupotosha jamii kwa taarifa za uongo!!!

Cc Invisible Moderator
 


PUMBA TUPU Juliana Shonza, wapi ndugu yako Mwapamba?Nawaonea huruma sana, poleni sana MALAYA WA KISIASA.
 
Last edited by a moderator:
Chama cha mapinduzi kingekuwa kinauwezo wa kusema baadhi ya wanachama wangeumbuka,maana CHAMA kingewakataa katika majukwaa,ukisoma katiba ya chama cha mapinduzi wachache sana wana sifa ya kuwa wanachama wa chama hiki
*Katiba ya chama mapinduzi nitanukuu
(Toleo la februari 1997) Fungu la kwanza
""Mtu atakayekubaliwa kuingia katika CCM au Kuendelea kuwa Mwanachama,ni yule anayetimiza masharti yafuatayo-
Mosi,kuwa mtu anayeheshimu watu
Pili,kuwa mtu anayefanya juhudi ya kuielewa,kuieleza,kuitetea na kuitekeleza ITIKADI na siasa ya CCM
Tatu,kuwa mtu mwenye kuamini kuwa kazi ni kipimo cha utu,na kuitekeleza imani hiyo kwa vitendo
Nne,kuwa mtu anaependa kushirikiana na wenzake
Tano,Kuwa mtu ambaye siku zote yuko mstari wa mbele katika utekelezaji wa mambo yote ya umma,kulingana na miongozo ya CCM
Sita,kuwa wakati wote ni mfano wa tabia nzuri kwa vitendo vyake na kauli yake,kuwa mwaminifu,na kutokuwa mlevi au mzururaji
Saba,kuwa ama mkulima,mfanyakazi au mwenye shughuli nyingine yoyote halali ya kujitegemea
"VV"
 
Duh! Hivi UDSM kinatoa makapi kiasi hiki?
Hata IGP wa green guards aka mwigulu naye ni mhitimu wa pale, tena first class!

Bi juliana msalimie mwigulu huko mafichoni.
 

Ni sawa mkubwa. Tunaweza pia kuangalia dhamana ya kuboresha maisha ya Watanzania ambayo imekuwa mikononi mwa ccm kwa miaka zaidi ya hamsini sasa. Tunapotoa dhamana ya uongozi wa nchi kwa chama, tunategemea ufanisi wa kiwango kikubwa katika nyanja mbali mbali za maendeleo na taswira yake ionekane katika maisha ya Mtanzania.

Angalia hadi sasa ccm imeshindwa kutoa huduma bora za afya kwa Watanzania wanalipa kodi kubwa kila kukicha.

Viwango na ubora wa elimu unasidi kushuka hadi wana standardize matokeo ya mitihani ya taifa halafu wanasingizia watu wamefaulu huku uelewa ukiwa ule ule wa kupanda mikwaju na mibuyu.

Huduma za maji safi na salama imekuwa ndoto hata mijini ambako serikali imetandika mabomba tu lakini kinachopita katika hizo bomba ni siri ya vyura.

Majority hadi leo hawana makazi sahihi.

Tatizo la vifo vya wanawake na wfatoto, achana na wanaume wanaokufa kiume limeendelea kuwa tatizo huku eti takwimu zikisemwa limedhibitiwa.

Kushuka kwa democrasia nchini kunakofanywa makusudi kwa maslahi ya watawala kumekuwa kisu shingoni kwa mtanzania wa kawaida. imebidi aendelee kunyamaz hata anapoona hapawi sawa kwa hofu ya kutendewa yasiyotarajiwa wala kuelezewa.

Raslimali za nchi kuwa mikononi kwa jina la mwa wageni kwa jina la uwekezaji na watu wachache wenye asili ya kiasia na kunaacha uzao wa Watz na tumaini la kuwa kama wahindi wekundu.

Angalia jinsi tasnia ya habari inavyodhibitiwa ili kuwanyima wananchi taarifa sahihi na muhimu ambazo zingewasaidia kupanga na kufanya maamuzi sahihi.

Mgawanyo mbovu wa mapato ya serikali , rushwa, ufisadi na kukosa uwajibikaji katika sekta ya umma, kumejenga wingu jeusi la kutisha katika anga la Tz. Watu wanaishi wakingojea siku zao zifike basi.

Utekelezaji mbovu wa mipango dhaifu ya maendeleo, mipango mibovu na miji na ukosefu wa miundo mbinu sahihi ya technolojia, uzalishaji, usafirishaji, masoko na nishati, ni vyanzo vya mauti kwa wananchi.

Haya na mengine mengi, yanahitaji serikali makini inayoelewa, inayojali na yenye nia za dhati za kuboresha ustawi wa taifa. Siyo ccm iliyoshindwa kwamiaka 50.

Hapa ndipo tunaona kwamba, kama kuna mtu mmoja ni dhaifu, akafanya maamuzi yasiyokubalika, mfumo wa serikali umbane na kurekebisha alipokosea. Kama mfumo nidhaifu, watu wataendelea kujiamulia kufanya kle wanataka, kuchukua maamuzi ya ovy na kuyatelekeza, matokeo yake ndiyo tunakuwa na hawa wanaotukanwa na Sweety Radhia kwamba wamezaliwa kariakoo.

Kumbe kama seriakli ya ccm ingekuwa ni kwa ajli ya wananchi, isingeruhusu hali yoyote, mtu yeyote, taasisi yoyote ama chombo chochote, kutenda kinyume na malengo ya maendeleo hadi kuzalisha tabaka linalosemwa na kuzaliwa kariakoo.

Njia pekee ya kuhakikisha nchi yetu inapiga kasi katika maendeleo ni kuunganisha nguvu za pamoja ili kupata serikali itakayotengeneza mfumo sahihi unaohitajika kwa sasa katika kubadilisha uozo wa serikali ya ccm na kuleta maendeleoa. Yote haya yanayotusumbua yanahusiana moja kwa moja na Serikali dhaifu ambayo ni ya ccm and ndiyo maana tunasema ccm imejenga matabaka ya watu wanaoitwa wamezaliwa kariakoo.
 
Hapo sasa mbuyu kama mchicha kwa chama chao wapi na wapi? hapo kapotoka
 

Thubutu yake amepewa za uso ataenda tena? anyway akienda asisahau kuchukua komedi yake, Mwigulu ni mtaji kwa CDM
 
Juliana shonza, wewe ni mchumia tumbo, mnafiki, zakubimbi na ndumilakuwili. Wewe na Mwampamba ndiyo mnachangia kuibomoa CCM. Hata wana ccm wenyewe wanafahamu ila 'wanawapaisha' kinafiki wakidhani kwamba Chadema itasikitika kuwapoteza, bila kutambua kuwa mmetemwa na Chadema kama makapi tu. Mpo CCM kiushabiki wa kisiasa tu ijapokuwa mnachangia kuibomoa ccm zaidi kuliko kuijenga. Ni watu wenye akili za kuku tu, kama Mwigulu wanaoweza kukubali kuwakumbatia. Shame upon all of you.
 

Nimeshindwa kujizuia, potelea mbali, umeandika hoja za kitoto sana, baadhi yake nimezipaka rangi. Inasikitisha kuona kuwa uwezo wako wa kujenga hoja umeishia hapo.
 
yaani kwa hiki ulichokiandika inaonyesha una upeo mdogo Sana wa kufikiria.
Hata sisi wengine tusiofatilia siasa sana tunajua CCM wamepoteza huu uchaguzi wewe unasema eti wameibuka kidedea???seriously??Kupoteza kata mlizokuwa mnazishikilia ni kuibuka kidedea?
Dada yangu siasa ni science kama science nyingine,inahitaji uwezo wa kufikiria na kudadavua mambo.
Ningekuwa mimi ni wewe ningeandika maneno machache tu
"wana arusha mliotupigia kura tunashukuru kwa kura zenu, tutaendelea kufanya jitihada ili kurudisha imani mliyokuwa nayo kwa CCM"
Nape mwenzio anaujua ukweli ndio maana kakaa kimya hajataka kuongelea lolote. Ila wewe na kiherehere chako unatoka huko unakuja kuandika utumbo hapa. Dada yangu sometimes kukaa kimya ndio JIBU SAHIHI ZAIDI. unajishushia hadhi yako kidogo uliyokuwa nayo.

Wewe na mwenzio Mtela mlikuwa mnapimwa tu ni kiasi gani mnaweza kusaidia chama, ila kwa matokeo haya ambayo mmeshindwa kutoa ushawishi na ushindi hata kwa kituo kimoja inaonyesha kazi yenu ni UTUMBO mtupu na kinachofuata ni kutupwa kama mpira wa kiume unavyotupwa baada ya matumizi (maana hata jinsi unavyoshikwa before matumizi ni tofauti unavyoshikwa baada ya matumizi).

kaa chini jitafakari, hivyo viposho visikupe kiburi. wenzio akina wassira washazeeka washakula vya kutosha.

WATCH OUT!!!!!!
 
Afadhali Shonza ana interest tunazozijua kutoka kwa Mwigulu mzee wa kuovertake,na kina radhia,simiyu yetu n.k,wao interest zao ni zipi ndani ya ccm,nijuzeni tafadhali.

Buku Saba si haba
 
Degree nyingine ni hadi uwe bingwa wa kutanua!
Mleta mada anaamini CCM imepata kura nyingi kuliko mwaka 2010 wakati wapiga kura wa Arusha walikuwa asilimia karibia 20??!
Kama ndivyo, basi CCM inajifia bure!
Halafu ungalileta takwimu zinazoonesha kabla ya chaguzi zote nani alikuwa na kata ngapi na amebakiwa na ngapi!
Vinginevyo ni kuonesha kwamba bodi ya mikopo haikopeshi fedha peke yake ila hata akili!
 
Nashindwa kumwelewa huyu mdada, kati ya cdm na ccm kipi kilianza kama mchicha? kumbe ni kweli shoza alijifukuzisha cdm baada ya kujikuta elimu yake ni ndogo kulinganisha na wenzake, kweli huyu ni bulula kweli.
 
Nashindwa kumwelewa huyu mdada, kati ya cdm na ccm kipi kilianza kama mchicha? kumbe ni kweli shoza alijifukuzisha cdm baada ya kujikuta elimu yake ni ndogo kulinganisha na wenzake, kweli huyu ni bulula kweli.

Kati ya yote ili la CCM kuwa mchicha nimeniacha hoi, mchicha oyeeeeeee haya ndio majembe ya CCM.
 
Kabla ya matokeo kutanganzwa mkatoka NDUKI -- wewe na Kamanda wa Green Guards.sijui mlikimbilia wapi maana dar mmeonekana jana.

Walienda kujifuta machozi chobisi!
Si mnamjua mzee wa vodosho!?
 
Ulijisikiaje siku ulipofukuzwa uanachama wa CHADEMA? bora tuanzie hapo make usomeki kabisa sijui unaandika ukiwa na jazba sijui hasira au ndo jinsi unavyojenga hoja?
 
Mbona uchaguzi ulifanyika kata 26.Umeandika kuwa CCM walishinda kata 16 na CHADEMA kata 8 vipi kata zilizobakia 2 zilichukuliwa na chama gani?.

Huyu binti nikati ya watanzania wanaomiliki makaratasi yanayoitwa degree!
Yeye na mchumi namba moja wanakidhalilisha UDSM!
Ngh!
 
Radhia sweety.....kumbe ukitulia unakua na sweety ideas wakati mwingine...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…