Tofautisha mtu na chama au taasisi, yawezekana kabisa kuna mengi yamefanywa na mtu kipindi akiwa ccm lakini kwa sasa ni chadema, sasa utasema alofanya mtu akiwa ccm basi kilifanywa na ccm? jibu ni HAPANA.
Ndo maana tunashindwa kuwaelewa walobaki ccm kama kweli wana uwezo mzuri wa kufikiri au wamekaririshwa tu. Huwa nashindwa kumwelewa mtu anayesimama kwa mavazi ya njano na kijani akatamba kwamba wao ndo wenye nchi.
Ni sawa mkubwa. Tunaweza pia kuangalia dhamana ya kuboresha maisha ya Watanzania ambayo imekuwa mikononi mwa ccm kwa miaka zaidi ya hamsini sasa. Tunapotoa dhamana ya uongozi wa nchi kwa chama, tunategemea ufanisi wa kiwango kikubwa katika nyanja mbali mbali za maendeleo na taswira yake ionekane katika maisha ya Mtanzania.
Angalia hadi sasa ccm imeshindwa kutoa huduma bora za afya kwa Watanzania wanalipa kodi kubwa kila kukicha.
Viwango na ubora wa elimu unasidi kushuka hadi wana standardize matokeo ya mitihani ya taifa halafu wanasingizia watu wamefaulu huku uelewa ukiwa ule ule wa kupanda mikwaju na mibuyu.
Huduma za maji safi na salama imekuwa ndoto hata mijini ambako serikali imetandika mabomba tu lakini kinachopita katika hizo bomba ni siri ya vyura.
Majority hadi leo hawana makazi sahihi.
Tatizo la vifo vya wanawake na wfatoto, achana na wanaume wanaokufa kiume limeendelea kuwa tatizo huku eti takwimu zikisemwa limedhibitiwa.
Kushuka kwa democrasia nchini kunakofanywa makusudi kwa maslahi ya watawala kumekuwa kisu shingoni kwa mtanzania wa kawaida. imebidi aendelee kunyamaz hata anapoona hapawi sawa kwa hofu ya kutendewa yasiyotarajiwa wala kuelezewa.
Raslimali za nchi kuwa mikononi kwa jina la mwa wageni kwa jina la uwekezaji na watu wachache wenye asili ya kiasia na kunaacha uzao wa Watz na tumaini la kuwa kama wahindi wekundu.
Angalia jinsi tasnia ya habari inavyodhibitiwa ili kuwanyima wananchi taarifa sahihi na muhimu ambazo zingewasaidia kupanga na kufanya maamuzi sahihi.
Mgawanyo mbovu wa mapato ya serikali , rushwa, ufisadi na kukosa uwajibikaji katika sekta ya umma, kumejenga wingu jeusi la kutisha katika anga la Tz. Watu wanaishi wakingojea siku zao zifike basi.
Utekelezaji mbovu wa mipango dhaifu ya maendeleo, mipango mibovu na miji na ukosefu wa miundo mbinu sahihi ya technolojia, uzalishaji, usafirishaji, masoko na nishati, ni vyanzo vya mauti kwa wananchi.
Haya na mengine mengi, yanahitaji serikali makini inayoelewa, inayojali na yenye nia za dhati za kuboresha ustawi wa taifa. Siyo ccm iliyoshindwa kwamiaka 50.
Hapa ndipo tunaona kwamba, kama kuna mtu mmoja ni dhaifu, akafanya maamuzi yasiyokubalika, mfumo wa serikali umbane na kurekebisha alipokosea. Kama mfumo nidhaifu, watu wataendelea kujiamulia kufanya kle wanataka, kuchukua maamuzi ya ovy na kuyatelekeza, matokeo yake ndiyo tunakuwa na hawa wanaotukanwa na Sweety Radhia kwamba wamezaliwa kariakoo.
Kumbe kama seriakli ya ccm ingekuwa ni kwa ajli ya wananchi, isingeruhusu hali yoyote, mtu yeyote, taasisi yoyote ama chombo chochote, kutenda kinyume na malengo ya maendeleo hadi kuzalisha tabaka linalosemwa na kuzaliwa kariakoo.
Njia pekee ya kuhakikisha nchi yetu inapiga kasi katika maendeleo ni kuunganisha nguvu za pamoja ili kupata serikali itakayotengeneza mfumo sahihi unaohitajika kwa sasa katika kubadilisha uozo wa serikali ya ccm na kuleta maendeleoa. Yote haya yanayotusumbua yanahusiana moja kwa moja na Serikali dhaifu ambayo ni ya ccm and ndiyo maana tunasema ccm imejenga matabaka ya watu wanaoitwa wamezaliwa kariakoo.