Dr Adam Francis
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 711
- 1,165
Leo natamani kupata maoni ya makada wenzangu wa Chama Cha Mapinduzi, waliopo humu jukwaani.
Kuna ubaya gani wa kuwapa CHADEMA reforms wanazozitaka ili washiriki uchaguzi bila manung'uniko?
Mm binafsi sijapata kusikia mtu hata mmoja, ndani na nje ya CCM akisema hivi, reform hii inayodaiwa na CHADEMA ubaya wake ni huu, na reform ile ubaya wake ni ule! Ninachokisikia ni muda hautoshi kana kwamba CHADEMA wameanza kudai reforms zao leo.
Kwenye uchaguzi huu, CCM itakuwa na mtaji wa kura 13milioni za kuanzia za wanachama wake, na kura yangu ikiwepo, mafanikio ya ilani 2020-2025 ya kuyanadi, Sh. 86 bilioni kwaajili ya kampeni, mabalozi wenye hamasa waliowezeshwa baiskeli, watendaji wa CCM kata wenye hamasa waliowezeshwa pikipiki, mabasi ya kisasa n.k. Chama gani kitatushinda?
Mm nadhani, kutokuwapa CHADEMA reforms wanazozitaka sio sawa. Inaleta imani kuwa CCM inategemea madhaifu ya sheria zetu kushinda chaguzi badala ya nguvu yake ya kisiasa na imani ya wananchi.
CCM ni kubwa sana, ushindi wake kwenye uchaguzi hauwezi kuhatarishwa na reforms wanazozitaka CHADEMA. Tuwape reforms, tuwashinde uchaguzi, tutakuwa tumewaziba midomo.
View: https://vm.tiktok.com/ZMALV8XcR/
Kuna ubaya gani wa kuwapa CHADEMA reforms wanazozitaka ili washiriki uchaguzi bila manung'uniko?
Mm binafsi sijapata kusikia mtu hata mmoja, ndani na nje ya CCM akisema hivi, reform hii inayodaiwa na CHADEMA ubaya wake ni huu, na reform ile ubaya wake ni ule! Ninachokisikia ni muda hautoshi kana kwamba CHADEMA wameanza kudai reforms zao leo.
Kwenye uchaguzi huu, CCM itakuwa na mtaji wa kura 13milioni za kuanzia za wanachama wake, na kura yangu ikiwepo, mafanikio ya ilani 2020-2025 ya kuyanadi, Sh. 86 bilioni kwaajili ya kampeni, mabalozi wenye hamasa waliowezeshwa baiskeli, watendaji wa CCM kata wenye hamasa waliowezeshwa pikipiki, mabasi ya kisasa n.k. Chama gani kitatushinda?
Mm nadhani, kutokuwapa CHADEMA reforms wanazozitaka sio sawa. Inaleta imani kuwa CCM inategemea madhaifu ya sheria zetu kushinda chaguzi badala ya nguvu yake ya kisiasa na imani ya wananchi.
CCM ni kubwa sana, ushindi wake kwenye uchaguzi hauwezi kuhatarishwa na reforms wanazozitaka CHADEMA. Tuwape reforms, tuwashinde uchaguzi, tutakuwa tumewaziba midomo.
View: https://vm.tiktok.com/ZMALV8XcR/