Binti
Juliana Shonza najua hii thread umeianzisha kwa maelekezo ya bosi wako. Pamoja na hayo na kwa faida ya vilaza wa hesabu wenzako hapo lumumba ngoja nikusaidie kufanya hesabu ya darasa la kwanza. Kwa akili yako ndogo unashindwa kujua kwamba kama ccm ilishinda kata 16 na Chadema imeshinda kata 8 basi jumla ya kata zilizofanya uchaguzi ni 24 (16+8=24!hesabu ya darasa la kwanza hii)sasa sijui kata 2 umezipeleka wapi!!??
Jumla ya kata zilizopaswa kufanya uchaguzi tarehe 16/06/2013 ni kata 26.
Kata zilizofanya uchaguzi tarehe hiyo 16/06 zilikuwa kata 22 (baada ya policcm kulipua bomu mkutano wa Chadema na hivyo NEC kuahirisha uchaguzi katika kata 4 za Arusha).
Katika kata 22 zilizofanya uchaguzi awali ccm ilishinda kata 16 na Chadema ikashinda kata 6 (Chadema ilirudisha mikononi kata zake 2 na kuchukua 4 kutoka kwenu ccm).
Katika uchaguzi uliofanyika Arusha juzi tarehe 14/07/2014 Chadema imewagaragaza vibaya ccm kwa kujinyakulia kata zote 4.
Kwa ujumla msimamo wa ushindi wa kata kwa ujumla ni kwamba Chadema 10 ccm 16. Lakini pia kwa uwiano wa wingi wa kura Chadema ina 46% huku ccm ikiwa na 49%. Sasa nataka uanzie hapo uniambie kama ccm imeongeza idadi ya wapiga kura toka 2010 au imeporomoka? sitarajii kwamba mhitimu wa Chuo Kikuu cha Dsm unaweza kushindwa hata kuunga unga hesabu ndogo kama hizi, unless uniambie hiyo degree uliipata kwa mlango wa dharura.