Hizi ni mbegu za mmea gani?

Hizi ni mbegu za mmea gani?

Zinaitwa msikesike.Hilo jina nililisikia huko Mwanza.Tulikuwa tunazichezea kwenye mchanga.Unaweka mafungu ya mchanga kadhaa kisha unaficha mbegu moja kwenye hayo mafungu ya mchanga halafu unamwambia mwenzako achague fungu lenye hiyo mbegu.
 
Habari za mchana mabibi na mabwana jamvini hapa?

Hizi hapa chini ni mbegu za mmea gani na zina kazi gani? Nikiwa mdogo nilikuwa naziona kwa bibi yangu, na alikuwa anazitunza sana.

Sikuwahi kufikiria kuwa ni mbegu za mti, wala sikuwahi kumuuliza kazi yake. Sasa hivi karibuni nikauona huo mmea mahali fulani na mbegu zake hizo, nikagundua kumbe hizo ni mbegu za mme. Bahati mbaya bibi yangu kwa sasa ni marehemu.

Je hizo mbegu ni za mmea wa aina gani na kazi yake ni nini?
Kwa kisukuma tuliziita bhosalozena (shanga za Zena) wanawake walikuwa wanazitoboa na kuzifunga kwenye uzi baadae kiunoni tayari kukuingiza mjini usiku,mmea ulikuwa unatambaa kwenye miti mingine. Umenikumbusha mbaaaaaaali
 
Kwa kisukuma tuliziita bhosalozena (shanga za Zena) wanawake walikuwa wanazitoboa na kuzifunga kwenye uzi tayari kukuingiza mjini usiku,mmea ulikuwa unatambaa kwenye miti mingine. Umenikumbusha mbaaaaaaali


WEWE NDUGU YANGU UNAZIJUA KWELIKWELI KUNA MTU ANASEMA ZINAPATIKANA KWENYE MTI...😀😀😀😀😀😀
 
Zinaitwa msikesike.Hilo jina nililisikia huko Mwanza.Tulikuwa tunazichezea kwenye mchanga.Unaweka mafungu ya mchanga kadhaa kisha unaficha mbegu moja kwenye hayo mafungu ya mchanga halafu unamwambia mwenzako achague fungu lenye hiyo mbegu.
Huu mchezo tuliita kimweku
 
charminglady

HIZO MBEGU ZINATUMIKA SANA NA KUTENGENEZA UREMBO WA SHANGA. ILA, NARUDIA ILA, HIZO MBEGU NI SUMU NA UKIZIONA WEKA MBALI SANA NA WATOTO NA ZINAWEZA KULETA MADHARA HATA KWA WATU WAZIMA PIA. NA SI MTI NI ILE MIMEA YA KAMBA KAMBA INAOTA KWA KASI SANA NA KUJAZANA SEHEMU MOJA KWA KUTAMBAA.

MAJANI YAKE YANAFANANA NA ILE MIMEA UKISHIKA MAJANI YAKE YANASINZIA HIVI. HIVYO USIJARIBU KUWEKA MDOMONI UTADHURIKA.
Ni kweli mkuu kama ulivyosema mti wake ulivyo ila kugusu sumu kidogo sielewi mana hata huko mikoani hua inajiotea yenyewe na sijawahi kusikia wakisema ni sumu
 
Zinaitwa ndilolo. ...ni kama matunda unaloweka kwenye maji ya uvuguvugu then unazinyonya zinatoa ujiuji kama maziwa....pia hutumiwa kutengenezea lotion
 
Mkuu izo mbegu sumu, tena hatari, wanasema ikivunjwa hio mbegu afu ukaila basi within 24 hours-3 or 5 days unaenda kukutana na mungu...... ila ukiila ivi ivi athari yake ni ndogo kwa sababu ya shell yake, lakini utajisikia kuumwa ila sio serious kiivo
 
charminglady

HIZO MBEGU ZINATUMIKA SANA NA KUTENGENEZA UREMBO WA SHANGA. ILA, NARUDIA ILA, HIZO MBEGU NI SUMU NA UKIZIONA WEKA MBALI SANA NA WATOTO NA ZINAWEZA KULETA MADHARA HATA KWA WATU WAZIMA PIA. NA SI MTI NI ILE MIMEA YA KAMBA KAMBA INAOTA KWA KASI SANA NA KUJAZANA SEHEMU MOJA KWA KUTAMBAA.

MAJANI YAKE YANAFANANA NA ILE MIMEA UKISHIKA MAJANI YAKE YANASINZIA HIVI. HIVYO USIJARIBU KUWEKA MDOMONI UTADHURIKA.
BABUU ACHA KUWAZUGA WATU HAKUNA MADHARA KWA MTU ATAKAE MEZA HIZZO MBEGU, KWA KIFUPI HIZO MBEGU KWA KULE KWETU KIGOMA ZINA FAHAMIKA KWA JINA LA (MTURUTURU) TUME YACHEZEA SANA ENZI HIZO TUKIWA WADOGO NA NIME YAMEZA MNO HAYO MATURUTURU WALA ATA SIKUWAHI KUDHURIKA KIAFYA....
 
Habari za mchana mabibi na mabwana jamvini hapa?

Hizi hapa chini ni mbegu za mmea gani na zina kazi gani? Nikiwa mdogo nilikuwa naziona kwa bibi yangu, na alikuwa anazitunza sana.

Sikuwahi kufikiria kuwa ni mbegu za mti, wala sikuwahi kumuuliza kazi yake. Sasa hivi karibuni nikauona huo mmea mahali fulani na mbegu zake hizo, nikagundua kumbe hizo ni mbegu za mme. Bahati mbaya bibi yangu kwa sasa ni marehemu.

Je hizo mbegu ni za mmea wa aina gani na kazi yake ni nini?
Busalu zena
 
charminglady

HIZO MBEGU ZINATUMIKA SANA NA KUTENGENEZA UREMBO WA SHANGA. ILA, NARUDIA ILA, HIZO MBEGU NI SUMU NA UKIZIONA WEKA MBALI SANA NA WATOTO NA ZINAWEZA KULETA MADHARA HATA KWA WATU WAZIMA PIA. NA SI MTI NI ILE MIMEA YA KAMBA KAMBA INAOTA KWA KASI SANA NA KUJAZANA SEHEMU MOJA KWA KUTAMBAA.

MAJANI YAKE YANAFANANA NA ILE MIMEA UKISHIKA MAJANI YAKE YANASINZIA HIVI. HIVYO USIJARIBU KUWEKA MDOMONI UTADHURIKA.
Sio kweli kabisa ni uzushi mkubwa sana kama ni kifo naona mimi nipo kabulini
 
Wanaosema hizi mbegu ni sumu si kweli, siwezi kuwaita WAONGO kwa Sababu ndio walivyosoma kwenye mnazoziita Link!!

Lakini hizi mbegu binafsi nimemeza sana tu utotoni nikiaminishwa kuwa ni kinga ya macho(red eyes).

Na kweli ule ugojwa sijawahi umwaga!! Labda ni kwa imani tu lakini sikuwahi kuumwa!! Tunaoishi nnje ya mji hapa Dsm tunaweza kuziona kwenye vijiporipori!!

Mpaka sasa nikizifumaniaga nameza tu kwa kuwa hzina madhara yyte na bado naamini ni kinga ya macho!!
 
Hizo mbegu zamani zilitumika kama dawa ya waliovimba Macho na kua mekundu,unameza 2 kutwa kwa muda wa siku 3 (Sikushauri kumeza hizi dawa kwa miaka hii)

Kuna watu walikua na imani eti kama akijifukiza ubani anachanganya na hizi mbegu,eti ni kama ulinzi dhidi ya watu wenye vijicho (yaani kujilinda na wale watu wenye jicho la husuda)
 
Nazifahamu kwa jina la fiwi, zamani tulikuwa tunachezea tuu, sasa labda tukuulize wewe bibi yako alikuwa anazitumia kwa shughuli gani?? Mana umesema alikuwa anazitumia sana.
 
Zinaitwa msikesike.Hilo jina nililisikia huko Mwanza.Tulikuwa tunazichezea kwenye mchanga.Unaweka mafungu ya mchanga kadhaa kisha unaficha mbegu moja kwenye hayo mafungu ya mchanga halafu unamwambia mwenzako achague fungu lenye hiyo mbegu.
Duh! Umenikumbusha mbali sana me nilizimeza miaka ya 2000 mpaka leo sijaugua macho
 
Zinaitwa Sipo, ukimeza mbegu hizo ni kinga ya ugonjwa wa macho!!
Yaani hutaumwa na macho(red eyes) tena!!
Yapo hata mimi nazifahamu kwa jina la sipo (kwa mikoa ya Pwani) .Nilishazimeza sana utotoni na hazina madhara kama watu wanvyosema kwa imani kwamba zina kinga dhidi ya mahonjwa ya macho.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Back
Top Bottom