Wakuu,
Hili swali ni zuri sana na ni kipimo tosha cha kujua ni kwa namna gani binadamu tunafikiri (wakati mwingine) kama mashine (mfano wa compyuta).
Ijapokuwa kuna ambao wamejaribu kulijibu swali hili lakini wengi wamejibu haraka bila ya kufikiri sana.
Sababu inayofanya tutoe majibu kwa swali kama hili inategemeana na nini tunajua kuwa ni 'ukweli' katika 'subconscious level' (ROM) zetu baada ya 'conscious level' (RAM) kukosa majibu ya haraka.
Ni kama mtu anakuuliza kama umewahi kufika mahali fulani. Kitu cha kwanza kitakachokuja akilini ni kutafuta katika 'conscious level' ya akili yako kuhusiana na eneo uliloulizwa. Ukilipata, basi utajibu ilhali ukiliona eneo hilo katika akili yako. Kama hukulipata katika 'conscious level' huenda kulitafuta katika 'subconscious level'. Huko nako kama jibu lipo litaletwa katika 'consious level'. Utaratibu huu wa kutafuta kutoka 'subconscious level' na kuleta katika 'conscious level' huchukua muda; sekunde, nusu dakika hata wiki. kama halikupatikana katika 'conscious level', basi kutegemeana na nini unajua kuwa ndiyo 'ukweli' wa eneo tajwa, utaanza kutengeneza picha ya eneo husika hata kama hujawahi kufika. Ukishatengeneza picha, italetwa katika 'conscious level' na hatimaje jibu hutolewa.
Mwisho; swali la mtoa mada halina jibu la moja kwa moja sababu linategemea vitu vingi; nini maana ya mapenzi, malezi, mazingira aliyokulia na anayoishi mhusika na pia nini kinatafsiriwa kama ni 'ukweli' juu ya namna sahihi ya kuishi katika 'subconscious level' ya mhusika.
Tafakari.