Hivi Wakenya wametushinda nini?

Hivi Wakenya wametushinda nini?

na sasa wana treni ya kwenda kasi..si bado tunataabika na treni za zamani na barabara zisizo na mbele wala nyuma

Hili la treni ya kwenda kasi uzushi hakuna kitu kama hiko, kwasasa
 
Uongozi wa JF uliamua kuihamisha from jukwaa la siasa kulinda CCM
 
wametushinda maariifa na Uthubutu. Pia elimu yetu ni BUTU si kwa Ukanda wa Afrika mashariki tu bali duniani.
 
Wakenya wako very much practice oriented and that's why they do deliver. Sisi wabongo tuko very much theoretical oriented and we don't deliver. Tuna mipango mingo sana mizuri lakini imeishia kwenye makabrasha na mafaili inazidi kujaa vumbi bila utekelezaji wowote. We're not committed hatuko serious. Hara maofisini kwa mfano utendaji kazi wetu sio wa kuleta tija and we don't have to expect changes from this point of view. Kenyans know what they want
 
Wakenya wametufundisha tuache umbumbumbu Wa kukariri tuwe sharp na tujiongeze.
 
Mi nimefanya kazi sana na wakenya hata wao wengi tu wavivu. Uvivu ni tabia ya mtu binafsi. WAkenya wengi ni vilaza ukija kwenye Technical point of view. Ila watanzania hawana tabia ya kujisifu.
Hawajisifu ila asilimia kubwa ni wazito mno.
Mfano: Mkuu Wa mkoa Wa morogoro alitumbuliwa na PhD yake alafu hajiongezi anatoa tamko la kulilia ajira inayotokana na kuteuliwa.
Huyo ni mfano Wa mindset ya watanzania asilimia 80.
 
Majibu ni rahisi sana yanaanzia kwenye historia, jamii yetu, mila na desturi.

Uswahili wa tanzania umechangia kwa kiasi kikubwa kuwa na tabia za kipwani na kimwinyi ambapo watu hawajitumi sana hii inachangiwa na influence kubwa ya desturi za kiarabu katika jamii ya kiswahili na tanzania kwa ujumla au hata jamii ya kiswahili kenya kama mombasa.

Pili Tanzania ilikuwa na mfumo wa ujamaa ambao ni wa kusaidiana, kutegemea serikali zaidi na ambao umefanya watu kutokujituma zaidi tofauti na mfumo wa kibepari wa survival for the fittest uliopo kenya.

Zaidi resources nyingi kama ardhi kubwa, madini, bahari imefanya tanzania kulala usingizi kuamini kila kitu kipo wakati kenya hawan resourve sana kwa hivyo msingi wao ni kufanya kazi na viwanya (service economy) ambapo imepelekea kuifanya kuwa nchi bora afrika kwa mambo mengi.

Kingine na pengine kikubwa ni ubora wa elimu ya kenya na pia idadi ya wakenya wenye elimu ni jambo walliwapita watanzania kwa umbali sana.

Pia tusisahau influence ya ukoloni wa uingereza tofauti na tanzania ambapp kilikuwa na wajerumani pamoja na waingereza ambapo kwa njia moja au nyingine imechangia kudestabilise mfumo wa sasa.

Mwisho ni viongozi waliotawala nchi hizi baada ya waasisi hao pia wamekuwa na mchango mkubwa wa nchi hizi zilipo.

Kuna suala la diaspora pia. Kenya ni kati ya nchi zenye diaspora wengi nje ya africa. Tafiti zinaonyesha mchango wa diaspora kwa kutuma pesa na investment ni mkubwa kuliko say wawekezaji uchwara wa kiasia tulionao.

Lakini kwa miaka 15 ijayo tanzania ikiboresha elimu na kujikita kwenye viwanda basi ina nfasi kubwa ya kuwa taifa kiongozi afrika mashariki mbele ya kenya.

Mawazo huru...naipenda kenya kama nchi ya pili baada ya tz
 
Ukikutana nao nje ya nchi wana confidence za kufa mtu. wakiwa kwao hawataki longo longo na kama hawaelewani watapigana mikwaju kisha wanadeliver

Tazama KTN au KBC picha ziko clear, news zimetulia, watangazaji wametulia

Soma gazeti la NATION au Standard...huwezi fananisha na lile gazeti la Michuzi (daily nyuz) au lile la copy and paste (guardian)

sisi tuna watu wengi zaidi, rasili mali nyingi zaidi, wanasiasa wengi zaidi, vyama vya siasa vingi zaidi, magazeti mengi zaidi, JF ndio zaidi, cabinet yetu kubwa kuliko ya kwao, katiba yao (na mahakama ya kadhi ndani) ndio walipitisha, sasa kwa nini hawa wana deliver na sisi hatuna kitu?

I've tried to hate them lakini nimeshindwa, cant hate their ambition esp based on their national interest.

Halafu wao kujenga li Superhighway kama hili ili iweje?

ahh sisi hata kuthubutu tunashindwa sijui kwa nini
17222619748_1b69229090_b.jpg

15829023643_e4d746c237_b.jpg

17384406106_a6e6de9f6c_b.jpg

7293527580_6750ff3295_b.jpg

11072537_1036594563035763_5241949039730488886_n.jpg

10922767_977705588928824_6489992242201783296_n.jpg

11255259_1070521696309716_3735786793160014247_n.jpg

11218850_1070517392976813_6774185895852903247_n.jpg
Watz walio Nchi za nje wanasifika kwa ufanyaji kazi uliotukuka.mfano madaktari watz walioko Botswana.Tabu yetu humu nchini ni tunanyimana Mishahara na kuwapendelea wageni halafu tunalalamika kuwa watanzania ni wavivu.
 
Ujamaa ulikuwa na faida nyingi sana kuliko unavyofikiri wewe. Hata kiswahili ni lugha inayotuunganisha. Tatizo hapa ni watu kukosa uzalendo. Hasa nyie mnaoenda nje ya nchi hamkumbuki nyumbani.
Moja ya faida ya ujamaa kwa nchi zilizofanikiwa. enzi za ujamaa ilikuwa ni uzalendo na utaifa kwa watu wote.

Ukisema ujamaa ulikuwa na faida myingi sana ila hakuna uzalendo ni wazi kuwa haukuwa na faida yoyote ile na ndiyo maana ulikufa na hatujaambulia kitu na tukarudia matapishi ya mfumo wa waloloni.

ujamaa umeturudisha nyuma tena hatua nyingi sana. Maana tulianza mbio za Marathon na kuishia kati kati na baadaye kuanza upya mbio hizo huku Kenya wakiukata upepo karibu na kumaliza mbio. Na umetacha kuwa watu wasio na uthubutu na waoga wasiojiamini wala wasiojua haki zao.
 
Wakenya wametuzidi katika kila sekta. Kijamii, kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Kiuchumi
Kenya ndiyo nchi yenye uchumi mkubwa EAC. Fedha yao ndiyo yenye nguvu na inaimarika kila uchao huwezi linganisha. na Tsh.

soko lao la hisa lina makampuni mengi tena ya kwao wenyewe ambayo hata huku DSE yamekuwa listed eg NMG, KCB etc

sekta ya viwanda imepiga hatua kubwa kuliko Tz mfano Tz imekuwa soko kubwa kwa bidhaa zao.

sekta ya nishati wamepiga hatua kubwa, umeme kwao upo wa uhakika kuliko Tz, pia matumizi yao ni makubwa kuliko Tz ambayo ndo kwanza ina migao mingi na bado kuna giza vijijini.

Wakenya wana optimal utilization of resources kwa maendeleo yao sio kama Tz ina enough arable land ambayo bado haitumiwi.

Kijamii
jamii ya wakenya imeelimika kwa kupata elimu tena yenye bora huwezi linganisha na Tz schools hazina miundombinu bora kwa wanafunzi.

Japo ukabila unawatafuna na hivi sasa wanapambana na magaidi wa al shabab.

Wakenya wameweza kuiwakilisha nchi yao vyema kupitia michezo ya riadha, rugby etc Tz bado ipo nyuma kimichezo wala haijawahi fanya vizuri kimichezo.

Jamii ya wakenya wameweza kutangaza vivutio vyao vizuri hati wanapata sifa kuwa na vivutio vizuri ikiwa Tz imebarikiwa kuwa na vivutio vingi ila havijulikani duniani
 
Wao haweleti siasa kwenye kila jambo na sio waongeaji sana
 
Kwa uzoefu wangu, wakenya wana tabia pia ya kujielewa na kujiamini. Niliwahi kushiriki kwenye interview ya kutafuta Chief Executive wa shirika moja la Tanzania ambalo lilitangaza hiyo nafasi kimataifa. Katika watu walioitwa kwenye interview walikuwepo watanzania, wakenya na mataifa mengine. Kulikuwa na swali moja ambalo kila mtu aliulizwa. Nalo lilikuwa unataka tukulipe kiasi gani ukipata nafasi hii?.

Kilichonisikitisha walikuwepo watanzania wenye elimu kubwa (eg PhD) na sifa zote lakini walishindwa kujibu swali hili.

Swali lingine lilikuwa kuwa kwanini tukuajiri wewe na sio wenzako? Nalo watanzania wakachemsha.

Matokeo yake akaajiriwa raia wa kigeni ambaye wala hakuwa mzuri sana ila alionyesha kujiamini na kujielewa.

Inabidi tuanze kuangalia namn ya kuwajenga vijana kwa elimu nzuri, kujielewa na kujiamini. Unaweza kuwa na sifa zote lakini hujielewi wala kujiamini. Hili tatizo liko mpaka kwenye michezo.
 
kweli bado tunasafari ndefu ya kufika siku zote mtu anayejisifu kwa kila anachojisifu ujue hakiwezi kukifanya kwa ustadi na sikila mpango lazima utimie kwa muda unaotaka wewe kenya is nothing to us even they tried to battle with us they will never win
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom