wametuzidi shida, nenda Kenya kama hukukomaa siku hiohio, hakuna ardhi, ajira, n.k. ubepari na matabaka umefanya klila mtu a-struggle
Na huyu rais wao inaonekana amezungukwa na wachapa kazi
Umeongea point mkuu,Nyerere alichokosea ni kuondoa Unyapara, ndiyo maana kila siku watu wanakacha kufanya kazi badala yake wanadai Haki wasio ifanyia kazi kila siku migomo na uvivu.
Lakini Kenya waliendelea kutumikishwa na wazungu baada ya Uhuru wao sisi tuliboronga kwenye Azimio la Arusha kwa kutaifisha mashirika na kurundika watumishi wengi wasio na sifa. Ndugu Naization iliingia hapo tujirekebishe hatujachelewa.
nimewahi kufanya kazi na wa kenya........wapo hivi....kila kazi wanayofanya ana hakikisha boss wake anajua amefanya nini tofauti na job description yake.....atahakikisha kuonyesha kuna kitu tofauti amefanya na boss AJUE,,,ila mbongo anaweza kufanya hicho kitu na akauchuna maisha yakaendelea......mfano,,,,anaweza kuja kazini mpaka juma pili akija afanye kazi kidogo au aje azuge tu,,,lkn management ita notice kua kuna bwn fulani hua anakuja kazini mpaka juma pili......kwa kifupi wanajua siasa za kazi.....waliwahi kunisumbua nikawashtukia nikala nao sahani moja wakasepa na kuniachia ofisi.....nikahama company nyingine nikaanza kutumia style yao....mambo safi kabisa....
Watanzania acheni kujidharau, si kweli kwamba Wakenya wametuzidi kwa kila kitu. Watanzania tupo mbele katika nyanja mbalimbali, Tatizo mtoa mada na wachangiaji wengine wamesha jidharau mbele ya Wakenya, na hiki kitu hata kama mimi ningekuwa Mkenya ningefurahia sana. Rise up watanzania wenzangu, tuna vitu vingi tu vya kujuvunia, na siku zote, there is still a room for improvement hata kwa wakenya pia, kuna baadhi ya mambo wanajifunza kutoka kwetu Watanzania , na sio kweli kwamba tupo chini kiasi hicho. Pia ni lazima tuangalie tofauti ya sera za kuichumi tulizorithi huko nyuma toka nchi zetu zipate uhuru hadi sasa. Na nina uhakika, kwa kasi na rasilimali tulizonazo Watazaniam, si muda mrefu tutawapita Wakenya katika maendeleo na hasa katika maeneo ya ukuaji wa uchumi. Tunachohitaji Watanzania ni uongozi mzuri utakao tuongezea kasi ya maendeleo kufikia nchi ya ahadi.
Ila nimeona mtoa mada amechomekea na ka-udini kidogo si vizuri,swala la Mahakama ya Kadhi katika Katiba halikubaliki. Kila nchi ina misingi yake, hatuwezi ku copy mambo ya nchi nyingine, ndio maana tukaitwa Watanzania, sis tupo 'unique'
Ukikutana nao nje ya nchi wana confidence za kufa mtu. wakiwa kwao hawataki longo longo na kama hawaelewani watapigana mikwaju kisha wanadeliver
Tazama KTN au KBC picha ziko clear, news zimetulia, watangazaji wametulia
Soma gazeti la NATION au Standard...huwezi fananisha na lile gazeti la Michuzi (daily nyuz) au lile la copy and paste (guardian)
sisi tuna watu wengi zaidi, rasili mali nyingi zaidi, wanasiasa wengi zaidi, vyama vya siasa vingi zaidi, magazeti mengi zaidi, JF ndio zaidi, cabinet yetu kubwa kuliko ya kwao, katiba yao (na mahakama ya kadhi ndani) ndio walipitisha, sasa kwa nini hawa wana deliver na sisi hatuna kitu?
I've tried to hate them lakini nimeshindwa, cant hate their ambition esp based on their national interest.
Halafu wao kujenga li Superhighway kama hili ili iweje?
ahh sisi hata kuthubutu tunashindwa sijui kwa nini
![]()
![]()
![]()
![]()
![]()
![]()
![]()
![]()