Hivi wahaya tumewakosea nini Polisi?

Hivi wahaya tumewakosea nini Polisi?

Haohao kina NANI:shocked:!!???? Ningekutana na wewe ningekurusha kichurachura na kukuimbisha "Jua lile literemkee Mama" mpaka ungeomba umwite Mukama au mama mkwe wako aje kukuombea msamaha. Senene mkubwa wee:shocked:..
Hahahaha, muraaa umeniacha hoi
 
Polisi nao wanakuwa kama mbaazi iliyokosa maua ikasingizia jua,sasa hayo yote yalikuwa ya nini ya rabi ...waambie wakiweza walifute hili kabila.
 
Polisi nao wanakuwa kama mbaazi iliyokosa maua ikasingizia jua,sasa hayo yote yalikuwa ya nini ya rabi ...waambie wakiweza walifute hili kabila.


Watz kwanini tumekuwa watu wa kuchukiana na kufuatiliana kana kwamba baadhi ni watz na wengine ni wakenya ama wasudani hivi kiasi hiki?
 
Tutake Radhi mkuu tafadhali. Ni sawa na kusema MAJAMBAZI yote ni Wachaga au MA.LAYA wote ni WAHAYA. Jenerolaizesheni sio nzuri.

Radhi ya nini mkuu Borat69? sundoka amesema polisi wengi ni Wakurya; hajasema kuwa Wakurya wote ni polisi. Wala sioni tatizo hapa. Ni kweli kuwa polisi wengi ni akina mura.
 
Last edited by a moderator:
Radhi ya nini mkuu Borat69? sundoka amesema polisi wengi ni Wakurya; hajasema kuwa Wakurya wote ni polisi. Wala sioni tatizo hapa. Ni kweli kuwa polisi wengi ni akina mura.
Mkuu Iselamagazi,
Nimeguswa sehemu nyeti na Hilo. Ndio maana nimeombwa atutake Radhi.
 
Mkuu siku ukisimamishwa na polisi kabla ya yote we weka simu ianze kurekodi, unajua nje hivi vijimakosa vya kijingajinga hua vinawekwa sana kwenye media na watu wanapelekwa court daily vinapungua, hapa kavunja sheria kabisa na hii inaweza kumkosesha hata kazi, mapolisi bongo hawajisomi kabisa, labda sababu mafunzo ni ya fasta au wanapewa mshahara kidogo.
 
Hahahaha, muraaa umeniacha hoi
Haahaaahaaaa......Umeikumbuka enzi za Kombania nini mkuu Piper? Jamaa yangu mmoja alikuja kwenye mafunzo na kitambi....Afande Mwijarubi akamwambia unakuja na kitambi unafikiri hapa umekuja kuchuma mapapai...kuruta ruka Kama chura Maji huku unaimba jua literemkee mama. Jamaa alitoa machozi baada ya raundi kadhaa...
 
Nilikuwa barabarani jana maeneo ya Mlandizi naendesha gari toka Moro kuja Dar. Nilikamatwa na Trafiki na kosa kubwa ni kwamba niliovertake sehemu mbaya.

Baada ya kuuliza kabila langu alionekana kukereka sana na kusema kwamba mnajifanya bush lawyers, mnajipenda sana na ndio maana mwalimu hakuwapenda.

Kusema kweli alisema mabaya kushambulia kabila langu kadri alivyoweza. Nilidhangaa kosa linatoka barabarani na kuwa kosa la kabila. Nilichukia sana kwa kuwa walikuwepo askari wengine wana bunduki niliogopa kusema lolote nistoe mwanya wa kutekeleza amri ya Pinda.

Hii imekuwa mara nyingi sana kuona kejeli na dharau za Polisi kwa kabila langu...

Haipendezi
Hivi mtu anaweza kutokea amekusimamisha halafu aanze kuongea hayo maaaneno bila kuwa na chanzo wewe ndio tatizo inaonekana umefika ukaanza kuleta maneno maneno yasiyo kuwa na msingi ndani ya office ya mtu
1.mbona wengine tunasimamishwa na tunalipa faini bila kuambiwa kuwa maneno hayo wakati mimi ni mhaya
2. umefanya kosa changia serikari ili wafanyakazi walipwe na tuinue uchumi wa nchi yetu
3.ukidharauliwa na msukuma mmoja ndio tuseme wote wasukuma wana matatizo
wangapi wanakufanyia dharau huko mtaani lakini huji JF kuongea nyie ndio mnafanya kazi iwe ngumu kwa askari wetu wakati wana kazi ngumu kweli
 
Halafu unakuja humu kulalamika!!??:shocked:. Hiyo sababu ya wewe kuwa Muhaya na kuchukiwa na Polisi ni UONGO NA UZANDIKI MKUBWA. Na hapo unapomsingizia Mzee Wetu Baba wa Taifa....Kama hakuwapenda ungefika hapo ulipo mpaka unaweza kuendesha gari na kuandika Utumbo JF!!?? Acha Umburula wewe Bwenga.
...siku zote jitahidi kuelewa nini hasa kilichomo ndani ya mada, kwa hayo matusi uliyotoa ya kumshambulia mleta hoja yanathibitisha dhairi kuwa uwezo wako wa kudadafua na kuchanganua mambo kutiliwa mashaka.
 
Polisi nao wanakuwa kama mbaazi iliyokosa maua ikasingizia jua,sasa hayo yote yalikuwa ya nini ya rabi ...waambie wakiweza walifute hili kabila.

Ndugu yangu ukimsoma vizuri mleta sredi unapata picha kwanini traffic alikasirika,mleta sredi anakiri alikua ana overtake sehemu mbaya. Sasa inaonekana alianzisha ubishi na mkwara. Traffic akakomaa,akamwandikia notification. Sasa wakati anauliza particulars zake ambako unaulizwa na kabila lako ndipo akathibitisha kwamba ni walee......!
 
Tusiseme ukabila umeisha Tanzania. Utasikia wanasema eti Mhaya, MMchaga na Mmnyakyusa hawawezi kuwa rais hapa Tz. Mawazo ya kibaguzi ya wazi wazi kabisa
 
...siku zote jitahidi kuelewa nini hasa kilichomo ndani ya mada, kwa hayo matusi uliyotoa ya kumshambulia mleta hoja yanathibitisha dhairi kuwa uwezo wako wa kudadafua na kuchanganua mambo kutiliwa mashaka.
Wewe nae UMEROGWA na nani Jamaniii!!!!??:shocked:. Huyu mleta mada ni Mtani wangu. Na hayo matusi unayosema nimeyatoa hizo ni salamu kutoka kwa Mkurya kwenda kwa Muhaya. Acha kuvalia Kanga mdundiko wa Mtaa wa pili.
 
Waitu,
Polisi mbona ni watani zako omwami Mbuli? Umesahau kuwa polisi na gesh ndio porofesheno kuu ya wale wajukuu zenu wa pande za kanda maalumu?

Ungezungumza nao kama mtani wao mungeelewana tu, usiogope bunduki zao zile ni vifaa vya kazi kama vile nyie kina nshomire mnavyotumia hizo kalamu kuwekea saini kwenye madokomenti.

Shumaramu waitu.[/QUOTE
mmmm! Wangambila stupid mbele ya waifu
 
Nilikuwa barabarani jana maeneo ya Mlandizi naendesha gari toka Moro kuja Dar. Nilikamatwa na Trafiki na kosa kubwa ni kwamba niliovertake sehemu mbaya.

Baada ya kuuliza kabila langu alionekana kukereka sana na kusema kwamba mnajifanya bush lawyers, mnajipenda sana na ndio maana mwalimu hakuwapenda.

Kusema kweli alisema mabaya kushambulia kabila langu kadri alivyoweza. Nilidhangaa kosa linatoka barabarani na kuwa kosa la kabila. Nilichukia sana kwa kuwa walikuwepo askari wengine wana bunduki niliogopa kusema lolote nistoe mwanya wa kutekeleza amri ya Pinda.

Hii imekuwa mara nyingi sana kuona kejeli na dharau za Polisi kwa kabila langu...

Haipendezi

kwani mkubwa neno overtake halina msamiati au neno la kiswahili mimi nadhani mbwembwe nyingi labda hata kabla hajapata taarifa za kumjulisha wewe ni mhaya ulianza kwa misamiati ya kiingereza mingi sana na ikamchosha hata mimi sikulelewa mwanzoni kuoveratake ni nini......tena kwakuwa askari wetu ni wasomi wakakwazika.
 
Back
Top Bottom