Kule Bungeni Wabunge Wahaya Ndio wanaongoza kwa kuchanganya Lugha (kiswanglish)huku wengine majimbo Yao ni ya vijijini sana wapiga kura wengi hawajui Kingereza lakini wanawalazimisha kununua Kamusi ili wajue mbunge wao kaongea nini Hii kasumba ya kudhani kuzungumza Kingereza ni Usomi inawasumbua sana !wanapaswa watambue Kuwa hiyo lugha ya Mkoloni pale England inazungumzwa na wote hadi Omba omba tena hawajaenda shule ni lugha Yao tu .kumbuka Elimu(taaluma)hupatikani ktk Lugha mbali mbali pasipo kutumia kingereza Wapo wasomi wafaransa wachina warusi wahispania wajeruman nk wana PHD wamesoma kwa Lugha zao na hawajui kingereza na maisha yanaendelea kwao soma kingereza kwa manufaa yako na kimataifa lakini unapokuwa Nyumbani jitahidi kuipenda na kuithamini lugha yako hakika utapendwa na wengi