Gsana
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 4,383
- 1,342
Nilikuwa barabarani jana maeneo ya Mlandizi naendesha gari toka Moro kuja Dar. Nilikamatwa na Trafiki na kosa kubwa ni kwamba niliovertake sehemu mbaya.
Baada ya kuuliza kabila langu alionekana kukereka sana na kusema kwamba mnajifanya bush lawyers, mnajipenda sana na ndio maana mwalimu hakuwapenda.
Kusema kweli alisema mabaya kushambulia kabila langu kadri alivyoweza. Nilidhangaa kosa linatoka barabarani na kuwa kosa la kabila. Nilichukia sana kwa kuwa walikuwepo askari wengine wana bunduki niliogopa kusema lolote nistoe mwanya wa kutekeleza amri ya Pinda.
Hii imekuwa mara nyingi sana kuona kejeli na dharau za Polisi kwa kabila langu...
Haipendezi
kyoma pole sana ila nadhani yule jamaa wa mla ndizi ana chuki binafsi na wahaya, last month nilipita pale wakanikamata eti spidi kubwa, i guess ni mbaba na anavaa nguo za khaki,nadhani ni vehicle inspector, akanizuia akaniambia nikamwone trafiki mwenzie pale pembeni, yule aliyekuwa amekaa kwenye pikipiki ni mdada, na jamaa alikuwa ameshika kitu kile kinachorusha vitu vizito vilivomnasa mwangosi.
nkamuuliza afande mbona hamna kibao cha spidi, akang'aka , kumbe na kibao haukuona nyuma, tunakuandikia na faini ya kutoona kibao,dah nkawa mpole, nikaona isiwe taabu...
Baada ya kuomba leseni akashtuka eti eeh kumbe mhaya eeh. Nyie mna pesa sana ebu lipa faini ya serikali pale...dah nkambembeleza akagoma, eti hamna maelezo wewe lipa tu...
baada ya kubanwa sana,nkwamwambia msinifanyie vile gari nampelekea mwenzenu akacheka sana(uwa sipendi kujitambulisha kwa kazi yangu, mimi kama mimi), wewe uko idara gani?sikupenda kuwa wazi sana nkamwambia mi dreva tu ila nampelekea field force...ile gari ilikuwa mpya haina hata namba, aksema hata kama basi nitoe ya maji maana wamekaa sana juani...akazidi kuwaka sana eti kumbe nyie ndo mnafaidi operation kimbunga!mpaka mnaanza kwenda bandarinilazma nasi tugawane....na maneno kibao... Nyie wahaya mna ela, na dharau juu,si utoe sasa uliyonayo...nkaenda kwenye droo ya gari nkatoa elfu tano....dah jamaa kukunjua akasema ,sasa afande mwandikie faini apo maana anafanya utani, sisi tuko4 tunafanyeje?dah jamaa alinikera mpaka basi...ila kwa kuwa hata mimi sitaki kuwapa mafisadi faida, nkaongeza 5 ili mambo yaishe....
Nkasepa ila kitu kilichonisumbua safari nzima ni kwa nini jamaa alishambulia sana kabila wakati kanikamata mimi kama mimi?KUMBE INAWAPATA WENGI EEH? JAMANI AFANDE WALIOPO JF WAAMBIE WENZENU WAHAYA NI KAMA WATU WENGINE TU , TABIA AU UWEZO WA MTU SIO WA KABILA JAMANI......