Hivi Waganda wana matatizo gani na Kiswahili

Ni kweli ndugu wengi hawajui kiswahili... ni ajali ya kihistoria ikiwa ni pamoja na madhara ya vita Tz waliyopigana kumg'oa Iddi Amin Uganda.Askari wetu walikuwa wanaongea kiswahili lakini pia majambazi na wahalifu wakawa wanaitumia lugha hiyo katika matukio.Hii ikajenga chuki dhidi ya kiswahili ambapo kilionekana ni lugha ya majambazi!

WOS,
Hili jambo la history ni kweli. Ila angalia maneno ya JAFAR hapa chini yanatofautiana kidogo na yako. Pia askari wa Tanzania hawakukaa sana Uganda kiasi kwamba hilo tatizo liwe la muda mrefu. Ni sawa na shangazi yangu alikuwa akisema kuwa walivamiwa na askari wenye PUA kubwa kama domo la bata na walikuwa wakiwaita MA-KUYA. Nilikuja baadaye kugungua walikuwa Wacongo hasa baada ya kumuona Urlus Mabele na pua lake na wap hawasemi KUJA ila KUYA. Ila kwa kuwa walikaa kwa muda mfupi, husikii hata leo hii madhara ya Wacongo kuchukiwa Tanzania.

Usiwalaumu sana Waganda, actually tunatakiwa tuwasaidie kukijua kiswahili. Waganda kutopenda kiswahili kinatokana na historia ya nchi yao. Enzi zile za Idd Amin Dada (RIP), kiswahili kilikuwa kinatumika sana na watu wake wa karibu, hasa hasa Jeshi. Kwa kuwa wanajeshi walikuwa wanyanyasaji, wabakaji na sifa zote mbaya walikuwa nazo, hivyo basi huko mtaani ukiongea kiswahili ulikuwa unatengwa, maana inawezekana 100% wewe ni wa Amin na unahatarisha maisha ya watu. Idd Amin mwenyewe alikijua kiswahili.

Historically, mpaka leo waganda wana kasumba hiyo.

Jafar,
Kuna rafiki yangu mmoja aliniambia juu ya hiyo kesi. Akasema enzi hizo ukisema Kiswahili, basi hata Polisi watakuachia. Jamaa akikuta mnacheza mpira na aseme kiswahili kuwa na yeye anataka kucheza, basi alipewa namba na mmoja wenu kuondoka. Hawa jamaa (askari wa Amini wenye kuvaa mashati ya vitenge) walikuwa WANAOGOPWA sanaana. Sidhani neno WALITENGWA lilikuwepo. Walichotaka wao walipata ila sema hata kama watu walikuwepo nao basi hao watu WALIKUWA WANACHEKA husu USO UMEKUNJAMANA na hofu juu ya kwamba utasema neno jamaa akugeuzie kibao. Hawa jamaa walikuwa kama miung watu, wakifanya watu chochote wanachokitaka.
Ila sasa wameanza kubadilika. Hebu msikie Jose Camelleon, jama ana-rap Mashairi kama hana akili vile..... "alisema yeye halagi UGALI, nikamkimbia na kumuacha KIGALI,........"
 
Ni kweli ndugu wengi hawajui kiswahili... ni ajali ya kihistoria ikiwa ni pamoja na madhara ya vita Tz waliyopigana kumg'oa Iddi Amin Uganda.Askari wetu walikuwa wanaongea kiswahili lakini pia majambazi na wahalifu wakawa wanaitumia lugha hiyo katika matukio.Hii ikajenga chuki dhidi ya kiswahili ambapo kilionekana ni lugha ya majambazi!
Nasikia pia Amin aliitumia sana Jeshini... Ilikuwa Jeshi la Uganda kama hujui kuzungumza Kiswahili, hupati ajira.

Waganda wengi wakaona kuwa haina haja ya kuongea kiswahili kwa sababu ni lugha inayotumiwa sana jeshini na si lugha ya kiraiya. Ila sasa mambo yamebadilika sana, japo wapo kweli wanao jitia kuwa hawajui kuongea Kiswahili... Wengi wao sasa wanajitahidi kuongea kwa kweli...!
 
Mmenikumbusha visa viwili vya Waganda na Kiswahili ilitokea nikiwa ughaibuni.

KISA 1:
Siku moja Mganda akaulizwa na mzungu kwamba lugha yake ya taifa ni ipi? akasema kiingereza, duh mzungu akaanza kujiuliza inakuwaje? hiyo ni lugha ya taifa huko uganda. Nami nikiwa pembeni yao, nilimhurumia jamaa alivyojitahidi kujieleza.

Toka siku hiyo akiulizwa lugha yake ni ipi alijibu kuwa ni KISWAHILI. Lakini bado akawa ni mgumu kuongea.

KISA 2:
Tukiwa kwenye sherehe za Waafrika, tukakubaliana tuimbe wimbo wa Taifa kutoka nchi mojawapo. Mwafaka ukawa tuimbe wa Tanzania, Wakenya na wa-Sauzi wakaafiki, shida ikaja Waganda. Kiswahili hawajui, kwa kuwa tyuuni ni moja na bondeni basi wabondeni wakaimba kibondeni, wakenya na watanzania tukaimba kwa kiswahili, Mganga akaona bora aimbe ki-bondeni kuliko kiswahili. Walitushangaza sana, lakini sherehe ilifana, kwani Wazungu walishangaa kwa kuona waafrica tukiimba tyuuni moja, ingawa lugha ni mbili tofauti.

Hivyo ni visa nilivyokutana navyo vya Waganda na Kiswahili. Nawapa pole kwa experience mbaya na lugha hii.

Anyway wakati ukifika wataongea, kama siyo sasa basi vizazi vijavyo, maana nilisikia rais wao anataka kiswahili kifundishwe mashuleni.
 
Jamani hawa wenzetu wanaboa kishenzi! mimi wakati mwingine nashindwa kuwaelewa lengo lao..Ebu fikiria eti wanajifanya hawajui kuongea kiswahili? nani kasema ? Wanyarwanda, wakongo wengi wao ni wazuri wa kuongea hii lugha.Kichekesho huwa nakiona kwa hawa wenzangu tunapokuwa mazingira yanayotukutanisha na wakenya, eti wenyewe hawakijui, na hata mtu akitamka ni kama yule mzungu anaye jifunza kiswahili.
Siyo kama nawataka sana waongee kiswahili lakini nawaonea huruma kwani wanajishahua lakini hawana lugha ya taifa.. ukimuuliza anakwambia kiingereza, na uingereza wasemeje?

Tatizo la kwanza hapa ni umri wa wachangiaji wengi na tatizo la pili ni uvivu wa kutokutaka kuijua vizuri historia ya Uganda. Jina Uganda ilibuniwa na wakoloni kwa sababu ya heshima waliyoupa Ufalme wa Buganda chini ya Kabaka na hata makao yao makuu waliiweka katikati ya Baganda. Kabla ya uhuru, lugha rasmi zilizofundishwa mashuleni zilikuwa Kiingereza na Luganda na ili uweze kuendelea ilibidi ufaulu somo la Luganda - lugha ya kabila la Baganda. Hata baada ya uhuru lugha hii ya Luganda ilifundishwa nchini kote kama kiswahili kilivyofundishwa Tanzania. Kuna wakati hata walifikiria kuifanya kuwa lugha ya taifa lakini kutokana na ushirikiano uliokuwapo baina ya nchi za Afrika Mashariki huo mpango haukufanikiwa. Lugha ya Luganda iliwaunganisha Waganda kama Kiswahili kilivyowaunganisha Watanzania.

Watawala wote wa Uganda pamoja na kuwa hawakuwa Baganda waliongea Luganda fluently kama Baganda. Marehemu Obote, mlangi, ili akubalike ilibidi aoe Baganda na pamoja na kuchaguliwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Uganda baada ya uhuru, Kabaka mfalme wa Buganda aliendelea kuwa "parallel head of state" mpaka Obote alipompindua. Idi Amin, mnubi kutoka Sudan, wengi wa wake zake walikuwa Baganda na hata yeye aliongea Luganda vizuri zaidi kuliko kiswahili. Katiba ya kwanza Uganda iliandikwa kwa lugha mbili - kiingereza na Luganda. Kwa Waganda lugha ya kiswahili ni lugha ngeni kama Kiarabu au Kihindi - fikirieni kama hivi sasa ingetolewa hoja ya kututaka sote tujifunze na kuongea Kiarabu ama Kihindi !!.
 
Ni kweli ndugu wengi hawajui kiswahili... ni ajali ya kihistoria ikiwa ni pamoja na madhara ya vita Tz waliyopigana kumg'oa Iddi Amin Uganda.Askari wetu walikuwa wanaongea kiswahili lakini pia majambazi na wahalifu wakawa wanaitumia lugha hiyo katika matukio.Hii ikajenga chuki dhidi ya kiswahili ambapo kilionekana ni lugha ya majambazi!


Waingereza Walitesa sana watu africa kote pamoja na Uganda na-kingereza kiltumika sana kuchapwaviboko, makofi, namatusi na mateso yote yalifanyika kutumia lugha ya kingereza lakini bado waganda wanji-proud kuzungumza kingereza.

tatizo la waganda bado wanacolonised attitude, hawapendi mambo yao, bado hawajamaa nimalumbukeni, wasisingizie etikiswaili kilitumika kiujambazi. I don't buy this.
 
Watawala wote wa Uganda pamoja na kuwa hawakuwa Baganda waliongea Luganda fluently kama Baganda. Marehemu Obote, mlangi, ili akubalike ilibidi aoe Baganda na pamoja na kuchaguliwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Uganda baada ya uhuru, Kabaka mfalme wa Buganda aliendelea kuwa "parallel head of state" mpaka Obote alipompindua. Idi Amin, mnubi kutoka Sudan, wengi wa wake zake walikuwa Baganda na hata yeye aliongea Luganda vizuri zaidi kuliko kiswahili. Katiba ya kwanza Uganda iliandikwa kwa lugha mbili - kiingereza na Luganda. Kwa Waganda lugha ya kiswahili ni lugha ngeni kama Kiarabu au Kihindi - fikirieni kama hivi sasa ingetolewa hoja ya kututaka sote tujifunze na kuongea Kiarabu ama Kihindi !!.
Siamini kama ugeni wa Kiswahili kwa Waganda utaulinganisha na Kiarabu au Kihindi. Hii ni kwa sababu kiswahili ni lugha ya kibantu kama kilivyo Kiganda (Luganda) na lugha nyingi za huko uganda. kwa mantiki hiyo kiswahili si lugha ngeni na tofauti sana na kiganda. Kwa mantiki hiyo si ngeni kama unavyotaka kutusadikisha. Wangeweza kujifunza kiswahili kirahisi zaidi kuliko Kiarabu na Kihindi.

Pili, kati ya Kiingereza na Kiswahili ipi lugha ngeni zaidi kwao. Naamini kiingereza! Lakini pamoja na ugeni huo wanaendelea kujifunza wao na watoto wao kwa bidii kweli hata kama lafudhi inaendelea kuwazingua. Ipi lugha rahisi kwao kujifunza: kiingereza ua kiswahili?

Wale jamaa bwana ukweli unabaki palepale: wana majivuno sana. Ni hilo tu. Mengine kama yapo ni nyongeza. Lakini ni kubwa ni majivuno.
 
Tatizo la kwanza hapa ni umri wa wachangiaji wengi na tatizo la pili ni uvivu wa kutokutaka kuijua vizuri historia ya Uganda. Jina Uganda ilibuniwa na wakoloni kwa sababu ya heshima waliyoupa Ufalme wa Buganda chini ya Kabaka na hata makao yao makuu waliiweka katikati ya Baganda. Kabla ya uhuru, lugha rasmi zilizofundishwa mashuleni zilikuwa Kiingereza na Luganda na ili uweze kuendelea ilibidi ufaulu somo la Luganda - lugha ya kabila la Baganda. Hata baada ya uhuru lugha hii ya Luganda ilifundishwa nchini kote kama kiswahili kilivyofundishwa Tanzania. Kuna wakati hata walifikiria kuifanya kuwa lugha ya taifa lakini kutokana na ushirikiano uliokuwapo baina ya nchi za Afrika Mashariki huo mpango haukufanikiwa. Lugha ya Luganda iliwaunganisha Waganda kama Kiswahili kilivyowaunganisha Watanzania.

Watawala wote wa Uganda pamoja na kuwa hawakuwa Baganda waliongea Luganda fluently kama Baganda. Marehemu Obote, mlangi, ili akubalike ilibidi aoe Baganda na pamoja na kuchaguliwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Uganda baada ya uhuru, Kabaka mfalme wa Buganda aliendelea kuwa "parallel head of state" mpaka Obote alipompindua. Idi Amin, mnubi kutoka Sudan, wengi wa wake zake walikuwa Baganda na hata yeye aliongea Luganda vizuri zaidi kuliko kiswahili. Katiba ya kwanza Uganda iliandikwa kwa lugha mbili - kiingereza na Luganda. Kwa Waganda lugha ya kiswahili ni lugha ngeni kama Kiarabu au Kihindi - fikirieni kama hivi sasa ingetolewa hoja ya kututaka sote tujifunze na kuongea Kiarabu ama Kihindi !!.

Unachanganya mambo. Luganda hakijawahi kuwa lugha ya taifa ya Uganda ingawa waingereza walikibeba sana. Hapakuwa na kitu kama parallel head of state kati ya Obote na Mutesa. Mutesa alikuwa ceremonial President ( alichaguliwa na bunge) na Obote, executive President. Obote alijpojitangaza kuwa rais badala ya Mutesa, wabaganda wakatangaza kujitoa katika federation ya Uganda. Obote akashambulia makazi ya Mutesa na kumfanya akimbilie uingereza. Mwaka 1967, bunge likabadilisha katiba na kufuta federation na kuanzisha ofisi ya executive President ambayo Obote akaikwaa.

Wabaganda ni asilimia takriban 17 ya watu wote Uganda. Kuna makabila mengi zaidi ya hao wabaganda. Au unataka kuniambia waacholi, wabunyoro, walango (kabila la Obote) n.k. wote wanaongea kiluganda? Kisingizio kuwa lugha ya kiswahili ni ngeni au ilitumiwa na askari wa Amin does not hold water. Ni ulimbukeni wao unaowasumbua. Na tunavyozidi kuwabembeleza ndivyo wanavyozidi kujisikia. Hatuwahitaji kama vile wasivyotuhitaji. waongee kiswahili, wasiongee ni juu yao. Ili mradi hawa-insult our intelligence kwa visingizio visivyo na maana!

Amandla......
 
Mhhh,
wewe fundi mchundo kweli ulikimbia umande? Asante kwa historia Mhandisi anayejificha kwa jina la Fundi Mchundo :)
 
Unachanganya mambo. Luganda hakijawahi kuwa lugha ya taifa ya Uganda ingawa waingereza walikibeba sana. Hapakuwa na kitu kama parallel head of state kati ya Obote na Mutesa. Mutesa alikuwa ceremonial President ( alichaguliwa na bunge) na Obote, executive President. Obote alijpojitangaza kuwa rais badala ya Mutesa, wabaganda wakatangaza kujitoa katika federation ya Uganda. Obote akashambulia makazi ya Mutesa na kumfanya akimbilie uingereza. Mwaka 1967, bunge likabadilisha katiba na kufuta federation na kuanzisha ofisi ya executive President ambayo Obote akaikwaa.

Wabaganda ni asilimia takriban 17 ya watu wote Uganda. Kuna makabila mengi zaidi ya hao wabaganda. Au unataka kuniambia waacholi, wabunyoro, walango (kabila la Obote) n.k. wote wanaongea kiluganda? Kisingizio kuwa lugha ya kiswahili ni ngeni au ilitumiwa na askari wa Amin does not hold water. Ni ulimbukeni wao unaowasumbua. Na tunavyozidi kuwabembeleza ndivyo wanavyozidi kujisikia. Hatuwahitaji kama vile wasivyotuhitaji. waongee kiswahili, wasiongee ni juu yao. Ili mradi hawa-insult our intelligence kwa visingizio visivyo na maana!

Amandla......

Fundi Mchundo hakuna popote niliposema Luganda iliwahi kuwa lugha ya taifa Uganda - nilichosema ni kuwa iliwahi kupendekezwa.

Pili nimesema wakoloni ndiyo walibuni jina Uganga kutokana na Kingdom of Buganda. Hebu fikiria kama kwa mfano Tanganyika ingeitwa Sukumaland.

Tatu nilisema kuwa lugha ya Uganda ilitumika kama official language mashuleni na kama hukufaulu katika mtihani, nafasi yako ya kuendelea ilikuwa finyu. Ndio maana waliosoma hadi vyuo vya juu enzi hizo waliongea Luganda fluently hadi Wa-Acholi unaowataja.

Nne pamoja na kuwepo makabila mengine, Luganda iliweza kuwaunganisha Waganda kwa sababu iliongelewa na asilimia kubwa ya Waganda (over 10m) kusini hadi kaskazini, mashariki hadi magharibi.

Tano nimesema kuwa kwa sababu tayari walikuwa na lugha iliyoenea sehemu nyingi za nchi hiyo hawakuona umuhimu wa kuongea kiswahili.

Nilipata bahati ya kuishi Uganda kwenye miaka ya nyuma na sehemu nyingi ili ueleweke ilibidi ujue Luganda. Watanzania wengi waliokuwa Uganda kwa namna moja ma nyingine walijifunza Luganda na si hizo lugha zingine unazozitaja.

Kitendo cha Obote kumshambulia Kabaka kiliwatia uchungu sana Baganda. Ndio maana kitu cha kwanza alichofanya Idi Amin baada ya kutwaa madaraka ilikuwa ni kurudisha imani ya Baganda kwa kuipa heshima Kingdom of Buganda kwa kumrudisha mjukuu wa Kabaka. Hii iliwafurahisha sana Baganda kiasi cha kumkubali huyo dikteta hadi siku alipomwua Kiwanuka aliyekuwa Jaji Mkuu.

Museveni ambaye pia si Baganda naye alikuja kutumia mbinu hiyo hiyo alipotwaa madaraka ili akubalike- Uganda bila Buganda ? - sijui.
 
Ni kweli ndugu wengi hawajui kiswahili... ni ajali ya kihistoria ikiwa ni pamoja na madhara ya vita Tz waliyopigana kumg'oa Iddi Amin Uganda.Askari wetu walikuwa wanaongea kiswahili lakini pia majambazi na wahalifu wakawa wanaitumia lugha hiyo katika matukio.Hii ikajenga chuki dhidi ya kiswahili ambapo kilionekana ni lugha ya majambazi!

Hii sababu hata mimi nimeambiwa na Waganda wenyewe, nikawaonea huruma sana. Kimsingi naungana na wachangiaji wenzangu, kwamba hatulazimiki kuishi kwa matakwa ya historia, kwani ulimwengu unabadilika sana sasa.
Nakumbuka kuna wakati rafiki yangu mmoja toka Uganda alikuwa anajisikia vibaya sana pale ambapo mimi m'bongo, Wanyarwanda, Wakenya na Wakongo tulipokuwa tunaongea Kiswahili na kufurahi, kiasi kwamba akajiona kama anatengwa.
Wanatia huruma sana, wanahitaji kubadilika!
 
Inabidi wabadilike kwa kweli. Pamoja na kuelewa kwamba kuna historia inayohusisha kiswahili na mambo yasiyo mema kwao, wanapaswa kuwa na mtazamo chanya. Kwangu mimi nalichukulia kwa jinsi hii; kujifunza lugha nyingi kwa kadri ya uwezo wako ni kwa manufaa yako katika ulimwengu huu wa utandawazi. Wenzao wa Kenya wanajitahidi kuibia ibia Kiswahili na kujichanganya Tanzania, kwa Waganda wanakuwa na wakati mgumu, maana hata Watanzania wenyewe wanakuwa na kama kuwashangaa, wakiwaona kama watu wenye dharau.
Kimsingi suala la kujichanganya ni zuri sana, mfano mzuri ni Bw Ssebo wa East Africa Radio/Tv. Jamaa huwa ananifurahisha sana, kajifunza Kiswahili akiwa anasoma sheria pale Mlimani, na sasa yuko fluent na amedaka kazi hapa hapa Tanzania.
Maisha yanaendelea.


Wala usikwazike, labda tu uwashauri nao wakipe kipaumbele.


Hakika.
Lakini Kipaumbele kitatokana na mahitaji ya Waganda wenyewe, kama wanaona Kiswahili hakiwafai basi huenda wakaacha hali kama ilivyo, kwa gharama zao!


Tatizo la sumu ya ubaguzi ni kuwa haina mipaka. Ukishakuwa bigot basi utabaki hivyo hivyo.

Amandla........

Duh!
Jf tuna mambo sana.
 
Hawa jamaa wanasema kiswahili kwao ni kwa rude people. Ukiwa unaongea kiswahili it is termed as rude person. Thats why mara nyingi huongelewa tu askari na wanajeshi.
 
Waende zao kule hawan issue! Dharau tu! Ila sehemu wakiwa na shida wanaongea
 
Mag3,

Hapo zamani ilikuwa ukienda Mbeya bila kujua kinyakyusa hauoni ndani. Makabila yenye mji kama wasafwa walilazimika kutumia kinyakyusa na hata wakati mwingine kujiita wanyakyusa! Lakini kutumika kwa kinyakyusa hakukuwa na maana kuwa kimekubalika bali ilikuwa ni lugha ya wenye nguvu na wengine walilazimika kuitumia. Nguvu ya wanyakyusa ilipopungua, lugha ya nyingine zikaanza kutamba na makabila mengine kudai utambulishi zaidi. Leo hii sidhani kama kuna mswafa atakae jivunia kuitwa mnyakyusa.

Maana yangu ni kuwa kutumika kwa kiluganda na makabila mengine hakuwezi kutafsiriwa kuwa ni kukubalika. Kama ingekuwa hivyo, basi kiluganda kingefanywa lugha ya taifa ya Uganda. Mimi siamini kuwa pingamizi la kukifanya kiluganda kuwa lugha ya taifa lilitoka nje ya Uganda na si ndani ya Uganda kama ulivyosema. Mbona hata mimi nimewahi kukutana na wa-uganda wasio waganda na wengi wao walikuwa na usongo na waganda. Hawa, pamoja na kuzungumza kiluganda wasingekubali aslani lugha hiyo kufanywa ya taifa. Nimesikia mahojiano yakifanyika Gulu na lugha iliyotumika ni kiswahili ( kibovu lakini kiswahili na si kiluganda). Tatizo ni pale tunapowafanya hawa misguided fools wachache wakiganda kuwa mfano wa raia wote wa Uganda. Kama vile wanyakyusa waklivyojidanganya kuwa Mbeya yote ni yao.

Miaka ya nyuma ni wakenya wachache waliotaka kusema kiswahili. Nao waliona ni lugha ya wasioendelea na kuendekeza lugha zao za asili na kiingereza. Leo wakenya wako mstari wa mbele katika kuendeleza matumizi ya kiswahili. Wakati mwingine kiswahili chao ni fasaha kuliko cha kwetu.

Hakuna mtu anayedai kuwa Buganda si sehemu ya Uganda. Ninachosema ni kuwa Uganda si Buganda peke yake. Lakini wao kama vile wenzao wa Quebec, Catalonia, Zanzibar n.k. ni lazima wakumbuke kuwa wao ni sehemu ya taifa na si vinginevyo.

Amandla.......
 
Kuna hali ya kufikiri kwamba Waganda hawapendi na hawajui kiswahili lakini mimi naona hii ni 'Generelazation'. Kuna aina mbili ya waganda ambao hapendi Kiswahili.

1) Wasomi ambao hasa wengi wao wamezaliwa mjini. Hawa ndio wenye "stigma" na Kiswahili. Kwao ni lugha ya Kishenzi kwa sababu eti wanajeshi na majambazi wanatumia lugha hii ya manyanyaso. Maneno kama "panda gari", "fungua mlango" na " lala chini" yanatumiwa na wanajeshi na majambazi hivyo watu waliosoma wanaona Kiswahili ni lugha ya kutisha tisha hivi. Hawakipendi Kiswahili! Wale ambao hawajasoma sana wanazungumza kiswahili bila kuwa na "stigma".

2) Katika Uganda kuna kabila kubwa la "Baganda". Hawa ni watu ambao wanajipenda sana na mila zao, Lugha yao na Kabbaka (mfalme) wao ni bora kuliko chochote. Mgogoro kati ya Kabbaka Sir Edward Mutesa na Milton Obote miaka ya 1960 ulianzia kwa bunge la "Baganda" (sio Uganda) kutoa azimio la kumtaka Waziri Mkuu (wakati huo Obote) aondoe serikali yake mjini Kampala maana ni Ardhi ya Baganda. Wakati huo Sir Edward Mutesa alikuwa ni "Titular President". Ugonvi ukatokea na Kabbaka Mutesa akakimbia nchi na kufia uhamishoni. Ukiacha Kiigereza Baganda hawataki lugha zaidi ya Luganda.

Ukienda Kasikazini kule Acholi na West Nile wanazungumza Kiswahili. Mashariki mwa nchi sehemu za Soroti, Tororo, Bugisu na kwingineko Kiswahili kinatumika sana. Vile vile wafanya biashara karibu wote wazungumza kiswahili hata kama sio kwa ufasaha maana bila hivyo itakuwa vigumu maana wakongo, warundi na wanyarwanda hawajui kiingereza na wanaenda Uganda kufanya biashara.

Mwisho East African Radio na EATV pamoja na ITV( ikiwemo na wasanii) vimefanya kazi kubwa ya kugeuza "mind set" ya Waganda wasomi kuhusu Kiswahili. Sasa hivi wasomi wengi wana shauku ya kujua Kiswahili na pole pole wanaanza kubadilika. Itachukua muda lakini pole pole watajua.
 
Kuna hali ya kufikiri kwamba Waganda hawapendi na hawajui kiswahili lakini mimi naona hii ni 'Generelazation'. Kuna aina mbili ya waganda ambao hapendi Kiswahili.

1) Wasomi ambao hasa wengi wao wamezaliwa mjini. Hawa ndio wenye "stigma" na Kiswahili. Kwao ni lugha ya Kishenzi kwa sababu eti wanajeshi na majambazi wanatumia lugha hii ya manyanyaso. Maneno kama "panda gari", "fungua mlango" na " lala chini" yanatumiwa na wanajeshi na majambazi hivyo watu waliosoma wanaona Kiswahili ni lugha ya kutisha tisha hivi. Hawakipendi Kiswahili! Wale ambao hawajasoma sana wanazungumza kiswahili bila kuwa na "stigma".

2) Katika Uganda kuna kabila kubwa la "Baganda". Hawa ni watu ambao wanajipenda sana na mila zao, Lugha yao na Kabbaka (mfalme) wao ni bora kuliko chochote. Mgogoro kati ya Kabbaka Sir Edward Mutesa na Milton Obote miaka ya 1960 ulianzia kwa bunge la "Baganda" (sio Uganda) kutoa azimio la kumtaka Waziri Mkuu (wakati huo Obote) aondoe serikali yake mjini Kampala maana ni Ardhi ya Baganda. Wakati huo Sir Edward Mutesa alikuwa ni "Titular President". Ugonvi ukatokea na Kabbaka Mutesa akakimbia nchi na kufia uhamishoni. Ukiacha Kiigereza Baganda hawataki lugha zaidi ya Luganda.

Ukienda Kasikazini kule Acholi na West Nile wanazungumza Kiswahili. Mashariki mwa nchi sehemu za Soroti, Tororo, Bugisu na kwingineko Kiswahili kinatumika sana. Vile vile wafanya biashara karibu wote wazungumza kiswahili hata kama sio kwa ufasaha maana bila hivyo itakuwa vigumu maana wakongo, warundi na wanyarwanda hawajui kiingereza na wanaenda Uganda kufanya biashara.

Mwisho East African Radio na EATV pamoja na ITV( ikiwemo na wasanii) vimefanya kazi kubwa ya kugeuza "mind set" ya Waganda wasomi kuhusu Kiswahili. Sasa hivi wasomi wengi wana shauku ya kujua Kiswahili na pole pole wanaanza kubadilika. Itachukua muda lakini pole pole watajua.

Ubarikiwe, Mkuu, kwa kutuweka sawa.

Amandla......
 
inanikumbusha msemo mmoja unaosema " Kiswahili was born in Zanzibar, grew up in Tanzania, got sick in Kenya and died in Uganda". Si ajabu msemo huu unawafanya wawe hivyo. Kwao kiswahili ni lugha ya wanajeshi kwani kilsambaa sana wakati majeshi ya Tanzania yako huko vitani na kulinda amani.

Ni mategemeo yangu kuwa East African Community itasaidia kukua na kushaminri kwa kiswahili huko Uganda.
 
Mag3,

Hapo zamani ilikuwa ukienda Mbeya bila kujua kinyakyusa hauoni ndani. Makabila yenye mji kama wasafwa walilazimika kutumia kinyakyusa na hata wakati mwingine kujiita wanyakyusa! Lakini kutumika kwa kinyakyusa hakukuwa na maana kuwa kimekubalika bali ilikuwa ni lugha ya wenye nguvu na wengine walilazimika kuitumia. Nguvu ya wanyakyusa ilipopungua, lugha ya nyingine zikaanza kutamba na makabila mengine kudai utambulishi zaidi. Leo hii sidhani kama kuna mswafa atakae jivunia kuitwa mnyakyusa.

Duh Mwanangu Fundi umenikumbusha mbali sana hiyo notion hapo juu!
Unajua shule ziliwahi sana kule Tukuyu kuliko maeneo mengi ya mkoa wa Mbeya, kuliko Uporoto kwa Wasafwa, ama Senjele kwa Wanyiha, ama Sange kwa Wandali, ama Kambi Katoto kwa Wabungu, ama Igalako na Utengule kwa Wasangu, kwa hiyo zile clerical jobs nyingi zilidakwa na Wanyakyusa wasomi enzi hizo. Sasa kwa kuwa mabosi walikuwa ni Wanyaki, now you know what to do ili upate kazi, ama uwe mmoja wao upate kazi, au uwe kinyume nao na ukose kazi! Na huu ndo ukweli halisi wa wakati huo kwa mkoa wa Mbeya na maeneo mengine, najua inakera na sana na inauma lakini ndivyo ilivyokuwa mpaka hapa majuzi wakati shule zilipoanza kusambaa Usafwani!
Nisingependa kuingia ndani sana kwa suala hili kwa sababu nitaonekana mkabila (kama ilivyo kwenye ile mada nyingine ya ukabila Ikulu n.k.)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom