Hivi vijana wengine mnaharakisha nini kuoa?

Hivi vijana wengine mnaharakisha nini kuoa?

shosti ameyavaa mapenzi vibaya na huyo mtoto wa shamba kajua kua huyu mtoto nimpindue vipi,na anavyo elekea huyu mtoto anapewa mpaka aseme mwenyewe basi......

Sasa huyu ni kumpa live na mumeo pia wakufundwa mweeee ndoa si kukojozana ni zaidi
 
Bila shaka huyo kijana ni MUHAYA maana ndo wanaendekeza sana mambo ya NGONO na kuoana bila mpangilio kwa kutegemea misaada toka kwa ndugu na jamaa. Zaidi huyo dada atakuwa kampa MFEREJI MARINGO WA MAJI TAKA
(DAWASCO) aka TIGO ndo maana kijana hasikii lolote

kalye mpali ya nyoko"'"
 
Mkuu sikufichi sijalala hata kidogo tangu jana mpaka sasa,inshallah ntafanya hivyo na pia namsubiri Dad aje nimsikilize nini tufanye yani nikizubaa mtoto namkosa,naona ananitoka kwenye himaya yangu hivi hivi ......
na angalau yule mzazi wa binti angesema basi njoo tujadili ananijibu pumba ndio nimerowa nimajiiiiiiii...

Kweli tena, tena kuhusu istikhara mwambie Mzee ndo amshauri, ukimshauri wewe anaweza sali bila udhu...(natania)

Pole sana, yani usikubali binti aingie, atawasambaratisha familia nzima...Kama wazazi hawana busara wanajibu hivyo kabla hata ya Posa, akiolewa jee? Wanajiamini nini?
 
ah haha hahaaa hahaaaa...............atakuwa kaoshwa break zake na machicha ya nazi huyu kijana, mwisho wa siku yakawekwa kwenye kisosi then binti anajipakulia ka candle light dina, lolest

Ha ha ha ha na kweli loh awez fanya maamuzi magumu hivyo
 
Ishu yako ngumu lakini rahisi mkubalie lakini mpe masharti akiweza utamruhusu aoe mwambie alishe familia yenu kwa wiki 3 bila nyinyi kutoa hata shilingi akiweza basi yupo tayari kuoa akishindwa basi asubiri mda bado.
Mkuu mimi staki kumwambia atulishe hata mlo mmoja,najua wazi hawezi kua miaka21 yuko chuo mwaka wa2 kula kulala,ada ya shule na matumizi yote natoa mimi sasa wale wanaosema Mtoto akililia wembe mpe kwangu siukubali,sababu he is my son siwezi kumuona anapata tabu nikamuangalia sasa afadhali nikatae mapema kuliko kumpa huo wembe kwasababau ukisha mkata huwezi kujua utamkata mpaka moyo afe au utakata mfupa abaki kilema..
 
Mkuu sikufichi sijalala hata kidogo tangu jana mpaka sasa,inshallah ntafanya hivyo na pia namsubiri Dad aje nimsikilize nini tufanye yani nikizubaa mtoto namkosa,naona ananitoka kwenye himaya yangu hivi hivi ......
na angalau yule mzazi wa binti angesema basi njoo tujadili ananijibu pumba ndio nimerowa nimajiiiiiiii...

Yani huyu unamkosa kabisa na kinacho baki sasa hivi anaweza kukwambia hataki kuendelea na shule tena! Hakika jiandae kisaikolojia maana nina hakika ukikataa hii ndoa atakwambia na shule ataki lakini wewe usije kukibali kuingia kwenye mtego wa kumpa baraka za kuoa au kufanikisha yeye kuoa wakati hata hajiwezi kabisa.... Huyu ameshatengenezwa kabisa..daa yani amekuwa zuzu kabisa
 
Mkuu mimi staki kumwambia atulishe hata mlo mmoja,najua wazi hawezi kua miaka21 yuko chuo mwaka wa2 kula kulala,ada ya shule na matumizi yote natoa mimi sasa wale wanaosema Mtoto akililia wembe mpe kwangu siukubali,sababu he is my son siwezi kumuona anapata tabu nikamuangalia sasa afadhali nikatae mapema kuliko kumpa huo wembe kwasababau ukisha mkata huwezi kujua utamkata mpaka moyo afe au utakata mfupa abaki kilema..

Usikubaliane na huu msemo wa Wembe maana kwenye hili hauna maana yeyote kabisa..huyu mtoto akiharibikiwa kwa wewe kukubali hii ndoa utajilaumu sana usikubali kabisa
 
Kwanza pole n masahibu, Mwambie huyo kjn akuelekeze anapoishi huyo msichana kwa nia nzuri 2 then nenda kaonane n huyo binti n kumueleza unavyoona ww ukiona akupi ushirikiano kwa unalotaka unaweza waingia wazazi wake ili mshauriane n kote ukiona bilabila nawa mikono yako miwili n uwaache nadhani Mungu atakusimamia kama una nia njema.
 
aisee mamito pole sana kwa hayo

cha kufanya hebu tafuta wazee na ukoo wenu mkae mjadili na mmumwambie maisha ya ndoa yalivyo asidhani ni pipi kwenye ndoa kuna mengi ataweazaje kumlea mtoto wa watu huku hana kitu yaani ajishughulishi yeye mwenyewe ni mtegemezi kwenu ongeeni naye uenda kashalishwa ukubwa anataka kulenga na nazi yake nzima sijui kama ataiweza huyo

kingine nendeni kwa watumishi wa Mungu yaani mchungaji wako wewe na mumeo na huyo kijana akapate ushauri toka kule asiharakishe kuoa kwani kupo ataoa tu cha muhimu ajipange maisha kwanza na namna atakavyoweza kukaa na binti wa wa watu aisidhani kuoa ni masuala ya kitandani tu la hasha ni masuala mbalimbali ya maisha yako huko atuulize siye tuliopo kwenye ndoa tutamwambia mambo yakoje.
 
Amekua mbishi wala siamini kama ndio yeye ...........
Kweli kulea ni kazi,najua uchungu uupatao ila lazima ujue sisi vijana ndivyo tulivyo, nnavyoona kashaonjeshwa kitu kitamu na mtoto kadata, hapo huna jinsi simama kama mlezi na uwe na msimamo katika hili swala!! lakin mbona inaonyesha mzee kama hajigusi? jua kwamba wewe ni msaidizi wa mzee, kaa nae kwanza umweleweshe maana si picha nzuri ikiwa mzee anasema OK then wewe unapinga, kazana wewe na mzee wote muwe na msimamo mmoja kama mnakataa mkatae wote na kama mnakubali mkubali wote!!! alafu kingine, mjitahidi (hasa mzee) kuwa karibu nae hasa kumwelimisha na kumshauri maswala ya maisha na kumskiliza nini anataka.

By the way futa machozi pole sana.
 
Hivi huko kwenye vyuo vikuu wanafundishwa nini? Maana binadamu wa kwanza kujenga na kusomesha watu ngazi ya chuo kikuu ilikuwa ni kuwajengea uwezo wa kufikiri kwa mantiki (to reason). Haijalishi anasoma nini kama hawezi kuresoan basi hajaelimika. Endelea na msimamo huo huo, dhamira yako njema Mungu anaiona.
 
Hivi huko kwenye vyuo vikuu wanafundishwa nini? Maana binadamu wa kwanza kujenga na kusomesha watu ngazi ya chuo kikuu ilikuwa ni kuwajengea uwezo wa kufikiri kwa mantiki (to reason). Haijalishi anasoma nini kama hawezi kuresoan basi hajaelimika. Endelea na msimamo huo huo, dhamira yako njema Mungu anaiona.

Ahsante...
 
Kweli kulea ni kazi,najua uchungu uupatao ila lazima ujue sisi vijana ndivyo tulivyo, nnavyoona kashaonjeshwa kitu kitamu na mtoto kadata, hapo huna jinsi simama kama mlezi na uwe na msimamo katika hili swala!! lakin mbona inaonyesha mzee kama hajigusi? jua kwamba wewe ni msaidizi wa mzee, kaa nae kwanza umweleweshe maana si picha nzuri ikiwa mzee anasema OK then wewe unapinga, kazana wewe na mzee wote muwe na msimamo mmoja kama mnakataa mkatae wote na kama mnakubali mkubali wote!!! alafu kingine, mjitahidi (hasa mzee) kuwa karibu nae hasa kumwelimisha na kumshauri maswala ya maisha na kumskiliza nini anataka.

By the way futa machozi pole sana.
Ahsante kwakunipa nguvu,unajua kila nyumba ina raha zake na ina dhiki zake,mumewangu nisimtoe Shukrani ananipenda ananisikiliza ila ikifika kwenye msawala kama haya anakua mtu wa hasira sana mara anasema mwache kama hakusikii dunia itamfunza sasa hapo ujue ndio amesha maliza na hataki kurudia tena hiyo story, sasa ndio mapungufu yake inabidi nimkubali alivyo,sasa hili nilazima nisimame kisawasawa...
 
Back
Top Bottom