Hivi vazi la taifa limekwenda wapi?

Hivi vazi la taifa limekwenda wapi?

Ndugu wana JF,

Nimeona niwaulize swali hili labda mnaweza kunisaidia kujua!

kama sijakosea, mwaka jana kulikuwa na mradi uliotambulishwa kwetu wenye lengo la kukusanya maoni na design mbalimbali ya vazi la taifa! Kwangu mm sikuona maana yake kwa mantiki ya vvipaumbele hivyo kwangu mimi niliuona huu mradi kama justification ya matumizi ya hela bila mpangilio ukizingatia umasikini uliopo miongoni mwa wananchi na sasa hivi nchi ilivyo na deni kubwa. Zile fedha zingetumika kwenye miradi ya kupunguza umaskini miongoni mwa Watanzania.

Swali langu pia mnisaidie kujua kama limekamilika au ndo ishu ya "katiba mpya" imeifunika?

Tujadili!
 
Hich ni kisurisuri na kimepita, mara zote wezi wanakuwa wajanja sana wanapoandaa jinsi nzuri ya kujipatia kipato pindi wanapotaka kuwahadaa wananchi kwa maelezo mazuri. Wzi mtupu!
:nimekataa:nimekataa:nimekataa
 
Watanzania wengi wakati mwingine naona hawana kazi hivi vazi la taifa halipo? ANGALIENI NGAO YA TAIFA YA BIBI NA BWANA mböna mnakuwa watu wa ajabu sana
 
vi, hoja na mchakato wa vazi la taifa umefikia wapi? What is the status...?[/SIZE]

Mimi naona watu nasubiri tume ya kuchakachua katiba imalize. Wewe naweza kusema vazi iwe mgolole ya masai kumbe katiba imesema ni suruali fupi na hijabu nyeusi na hakuna ruhusa kujadilli.!

Kwa hiyo chakachueni kwaza katiba halafu tujue yapi mnabakiza wananchi iseme!.
 
Hapo ni njia tu ya watu kula pesa, halina mantiki hilo vazi wala halina msaada. Izo pesa za kufanyia mchakato wangeenda hata kuchimbia visima.
 
wee kweli akili imeganda, hivi kuhoji mambo ya msingi yanayotumia pesa ya umma ni ushabiki? kumbe ndo maana CCM wanatuibia sana aiseee....
sawa mimi imeganda lakini wewe akili yako ni tope zito lenye maji machafu!
una uelewa finyu sana wewe sijui elimu yako uliacha shule ukiwa darasa la nne?
ushabiki huwa watu wanashangilia kitu kikiwa hot ila kikienda likizo basi washabiki wanakaa kimya wanasubiri jambo jipya! hivyo ndivyo ilivyokuwa kwetu watu walilishabikia saana lilivyopotea hakuna aliyehoji lolote
 
Zamani hatukuwa nalo hilo vazi leo wanalipana posho kulitafuta wakati utambulisho mwingine wetu wa kitaifa kama lugha ya kiswahili tunaviona vya kuja,mlima k'jaro,serengeti na vivutio vingi vimetushinda eti vazi la taifa wizi mtupuuu!
 
Saiv tumeshachelewa kupata vazi la taifa ilikua lije tangu ulipopatikana uhuru,kipindi hicho watu wengi walikua wajinga sasa kila mmoja ataleta hoja yake
 
sawa mimi imeganda lakini wewe akili yako ni tope zito lenye maji machafu!
una uelewa finyu sana wewe sijui elimu yako uliacha shule ukiwa darasa la nne?
ushabiki huwa watu wanashangilia kitu kikiwa hot ila kikienda likizo basi washabiki wanakaa kimya wanasubiri jambo jipya! hivyo ndivyo ilivyokuwa kwetu watu walilishabikia saana lilivyopotea hakuna aliyehoji lolote
Kwa hiyo na wewe ni shabiki tuu? Acha watu wahoji maana kuna pesa nyingi zilitengwa kwa shughuli hiyo na hakuna feedback
 
Wadau natumaini wote mnafahamu jinsi mchakato wa vazi la Taifa ulivyoanza hapa kati ukapotea juzi tunaambiwa na Mkurugenzi wa Utamaduni (Prof. Mwansoko) kuwa mchakato unaendelea kwa kusubiri kujadiliwa na Makatibu Wakuu na baadae Baraza la Mawaziri, lakini najiuliza hivi kweli serikali kweli ipo serious na hili jambo? wakishapitisha vazi la taifa je viongozi watakuwa tayari kutumia/kuvaa hilo vazi na kuachana na european Suits? na kuvaa Batik, Khanga na Vitenge. je watasaidia viwanda vya ndani kuzalisha bidhaa za ubora za hata kushindana na viwanda vya nje? Mi nashauri pia wasiishie kwenye vazi la taifa waweke msisitizo wa kutumia vitu vinavyozalishwa ndani kama Samani/furniture zinazotengenezwa hapa ili kukuza uchumi wa nchi yetu na kuzalisha ajira nyingi zaidi hususani kwa vijana.
 
Hawa jamaa walitoa sana mapovu karibia kujaza pipa kuhusu eti kuwa na vazi la taifa , uhuni mtupu wakati utandawazi umeshatuathiri siku nyingi ..sasa naweza kusema vazi lao wangewapa punda kimya kimya wawe wanavaa kipindi wanasafirisha madawa ya kulevya na sio kutuletea promo za kihuni watanzania hatuna time na ndio maana hakuna hata mtu anataka kuwa na hii kitu baada wao kupiga kimya!
 
bado wanatafakari waje na style ipi ya vazi la ndani walishamaliza la nje
 
Back
Top Bottom