Nashukuru sana mkuu,mimi bado sina ofisi maana ndo nime anza natamani niki pata mtaji nianze process za kusajili kampuni ya usafi ili niweze kupata soko pia katika taasisi ambako kwa sasa siwezi kufika.
Pia kuhusu hiyo 30,000 ni faida yangu maana matumizi ya dawa si makubwa hii dawa ina tumika kidogo sana naweza tumia Lita 3 tu kwa nyumba nzima ikiwa ni pamoja na Tiles na kama ni masink tu ni chini ya hapo pia dawa natengeneza mwenyewe kwa gharama ndogo tofauti na kununua.
Kuhusu gharama za uendeshaji sana sana kwa sasa ni nauli , chakula kabla ya kazi na baada ya kazi pamoja na dawa ndo vinavyo nigharimu.
Kuhusu Imani kwa wateja inatokana na aina ya mtu nnaye kutana naye na asiye weza kuni amini namuuzia dawa akiona matokeo yake ana nitafuta nimfanyie kazi.