Hivi ndivyo Lowassa alishiriki Richmond

TUsisahu kitu kimoja hapa...mwakyembe anasema kuna mambo walificha kulinda heshima ya serikali..wasiwasi wangu hili scandal ni la serikali nzima ya JK....mana kama kuna vitu vilifichwa kulinda heshima ya serikali, ni vitu gani hivyo wakati vilivyotolewa tu vilitosha waziri mkuu kujiuzulu? vingetolewa na hivyo vilivyofichwa? nadhani JK angejiuzulu...pole sana Lowasa, umetolewa kafala ilhali mlikuwa wengi hata na swaiba wako JK...we hukumbuki wakati wa mjadala mkali, JK alipotoka ziara ya marekani alithibitisha kukutana na wamiliki wa kampuni ya RICHMOND, lakini baadae akina mwakyembe wanasema Richmond ni kampuni hewa!..., Mbona Kamati ya Mwakyembe haikumuhoji Rais kujua hao aliokutana nao Marekani na kuzungumza nao ni akina nani?...Pole sana EL......mlikuwa wengi, lakini ilikuwa zamu yako.

Kinachonishangaza ni hiki cha Wabunge na kamati za Bunge kudai kuwa wanafanya mambo mengine kwa kuinusuru Serikali au kulinda heshima ya Serikali.

Sasa najiuliza, wao kama mhimili wa Tatu wa Serikali kwa mujibu wa Katiba, inakuwaje wnaonea haya makosa ya Serikali kwa gharama za jasho na kodi za Mwananchi wa Tanzania?

Leo hii wanapigana vikumbo Bungeni kuilaumu Serikali kuwanyanyasa na kuwakosea heshima kwa kuhojiwa na TAKUKURU, lakini wao ni wepesi kuionea huruma Serikali Kuu na kuilindia heshima!

Huu ni unafiki na mbaya zaidi ni undumilakuwili ambako kunafikia kulifanya Bunge letu lionekane kama ni wapiga mhuri kwa matakwa ya Serikali Kuu na Chama kinachotawala na zaidi ni kuwa Bunge letu bado halijawa huru na kua na uwezo wa kuidhibiti Serikali.

Nikisema kuwa Wapiganaji wanapigania nini au kuhoji kelele za kung'ang'ania koo moja na simfumo mzima mbovui wa kiutendaji, naambiwa sina akili au nikae kimya!

Ndio maana leo hii Pinda na Sitta wanatishana, ndio maana mwaka jana na juzi Lowassa na Sitta walitishana na ni kutokana na Bunge kushindwa kuwajibika na kujilinda kwa kutumia Katiba kwa kuogopa mkao wa Kikao cha Chama.

Leo hii isingekuwa Wahisani kuhoji kilichotokea Dodoma wakati wa kikao cha mwishi cha NEC ambacho kilimsulubisha Sitta, Serikali na CCM wasingetoa kauli za kujisahihisha au kusema Spika wa Bunge (ambaye Kikatiba ni mhimili mkuu na mtu mwenye hadhi yake) hakuwekwa kwenye kikaango na kudiriki kuwasuta Wabunge wake wenyewe kwa kushindwa kulizungumzia suala la taratibu za Kibunge ndani ya Bunge.

Hata hili suala la posho za Wabunge kwenye vikao au wao kuwa ni wajumbe wa bodi na kupata posho mara mbili ni mtego ambap Wabunge wenyewe wamejiwekea na wanaanza kunaswa kama Paya.

Ikiwa Spika anadiriki kudai eti kupewa Posho ya ziada ni Utamaduni wa Kitanzania na hivyo kuihalalisha na ukikimbuka zile kauli zake za kusema Wananchi wakihongwa na Mafisadi wapokee hongo, je unadhani Spika na Bunge wana heshima gani tena au uwezo gani kuidhibiti Serikali?

Kwa nini Mwakyembe aseme waliilindia Heshima Serikali lakini wakamkaba koo Waziri Mkuu? je Waziri Mkuu si Serikali na Kiongozi Mkuu wa Serikali Bungeni?
 
Mkandara,

..hapana. Richmond waliingia nchini wakati wa utawala wa Mkapa na walisaini Memorandum of Understang[MOU] na serikali kwamba watakusanya funds within 18 months kwa ajili ya ujenzi wa bomba la mafuta la Dar--Mwanza.

..sasa miezi 18 ilipita na hawa Richmond hawakuonekana kabisa. serikali ikaona kwamba jamaa ni wababaishaji kwa hiyo ikawaandikia barua ya kufuta MOU. barua ya serikali kufuta MOU iliandikwa na Bashir Mrindoko ambaye ni Kamishna wa Nishati ktk wizara ya Nishati na Madini. barua hiyo nadhani iko kama kiambatanisho ktk ripoti ya Dr.Mwakyembe.

..actually, Mwakyembe amependekeza Bashir Mrindoko achukuliwe hatua kwasababu hakumshauri vizuri Katibu Mkuu Arthur Mwakapugi kuhusu uwezo wa kifedha wa kampuni ya Richmond.

..baada ya serikali kufuta MOU kati yake na Richmond, sasa ndiyo Kikwete amepata hao wawekezaji toka Qatar kujenga hilo bomba la mafuta.

Kwa nini Serikali ilimnyang'anya Elisante Muro huu mradi wa bomba la Mafuta?
 
FMES,

Unajifanya umesahau uhuni waliofanyiwa Salim na Maelcela 2005 na chama chako cha CCM?was it that long that you can not remember kuwa kampeni chafu ndani ya chama chako iliyompa madaraka Kikwete ndiyo iliwapakazia kina Salim na Malecela unazi na tuhuma zisizo na msingi?

Ushahidi wa Meremeta, sisi tumeuweka hapa ndani wazi kwa kila mtu na tumeupeleka Serikalini ufanyiwe kazi, je wako huo wa Richmond umeshauweka wazi hadharani au uko mkobani?

- Una maana kama ule uhuni aliofanyiwa Zitto kule Chadema, au wa CCM tu? Yaani umeshasahau kwamba siasa ni mchezo mchafu tayari?

- Unasema ushahidi wa Meremeta, umeipa serikali ipi hiyo ya USA au bongo? Eti unategemea serikali ya bongo ifanye nini na ushahidi dhidi yake? Mkuu vipi mbona miguvu ya hoja badala ya hoja?

Respect.

FMEs!
 
Nchi hii inaelekea pabaya! Na watu kama Lowassa ndio wamejipanga kuwa "Urais" ni lazima hata iweje. Eeh sasa akiwa ndio mwenye last saying mambo yatakuwaje? Issue ya Kiwira itakuwa "cha mtoto" utafika wakati mtu atanunua Magereza halafu atawapangisha wafungwa! Si ulaji bwana na wafungwa kibao!
 
Wasafishaji hawajui, ila sabuni inayomfaa Lowasa na nduguze ni mahakama tu, kwakuwa kuna mkubwa zaidi yake ktk ishu hii, sijui itakuwaje?
 
Mkandara,

..hapana. Richmond waliingia nchini wakati wa utawala wa Mkapa na walisaini Memorandum of Understang[MOU] na serikali kwamba watakusanya funds within 18 months kwa ajili ya ujenzi wa bomba la mafuta la Dar--Mwanza.

..sasa miezi 18 ilipita na hawa Richmond hawakuonekana kabisa. serikali ikaona kwamba jamaa ni wababaishaji kwa hiyo ikawaandikia barua ya kufuta MOU. barua ya serikali kufuta MOU iliandikwa na Bashir Mrindoko ambaye ni Kamishna wa Nishati ktk wizara ya Nishati na Madini. barua hiyo nadhani iko kama kiambatanisho ktk ripoti ya Dr.Mwakyembe.

..actually, Mwakyembe amependekeza Bashir Mrindoko achukuliwe hatua kwasababu hakumshauri vizuri Katibu Mkuu Arthur Mwakapugi kuhusu uwezo wa kifedha wa kampuni ya Richmond.

..baada ya serikali kufuta MOU kati yake na Richmond, sasa ndiyo Kikwete amepata hao wawekezaji toka Qatar kujenga hilo bomba la mafuta.
Shukran kwa ufafanuzi..That's why I love JF kwa sababu unaweza kuunganisha vitu vingi sana kutokana na maelezo ya watu..Ebu nisaidie moja hapa, wakati Richmond wakiweka mkataba wa MoU, nani alikuwa waziri wa nishati na nani alikuwa behind the first deal... naona picha inazidi kupanuka kwani nataka kujua hawa Richmond waliingiuaje nchini na kwa gear gani?
 
Shukran kwa ufafanuzi..That's why I love JF kwa sababu unaweza kuunganisha vitu vingi sana kutokana na maelezo ya watu..Ebu nisaidie moja hapa, wakati Richmond wakiweka mkataba wa MoU, nani alikuwa waziri wa nishati na nani alikuwa behind the first deal... naona picha inazidi kupanuka kwani nataka kujua hawa Richmond waliingiuaje nchini na kwa gear gani?

Kwa kuongezea;
  1. Mbona aliyekuwa Balozi wetu US, Balozi Andrew Daraja haongelewi kabisa kwenye haya yote wakati aliwahi kuwatembelea Richmond kabla ya wao kupewa kazi TZ.
  2. Je alipokuwa anakutana nao alikuwa anamuwakilisha nani na aliishauri nini serikali kuhusiana na hawa Richmond?
 
الحق والسلطة التقديرية لبيع بك قميصا وكيتنغه​
 
الحق والسلطة التقديرية لبيع بك قميصا وكيتنغه
 
الحق والسلطة التقديرية لبيع بك قميصا وكيتنغه
السلام عليكم
 
hili jipya kaka..............tujuze zaidi
Kwa kuongezea;
  1. Mbona aliyekuwa Balozi wetu US, Balozi Andrew Daraja haongelewi kabisa kwenye haya yote wakati aliwahi kuwatembelea Richmond kabla ya wao kupewa kazi TZ.
  2. Je alipokuwa anakutana nao alikuwa anamuwakilisha nani na aliishauri nini serikali kuhusiana na hawa Richmond?
 

headline_bullet.jpg
Nyaraka zaonyesha kila hatua aliweka mikono yake
headline_bullet.jpg
Uthibitisho wa kuibeba Richmond watolewa peupe
headline_bullet.jpg
Kumbe ndiye aliipora Tanesco kazi ya kusaka mzabuni
headline_bullet.jpg
Wizara ya Nishari na Madini ilisubiri maamuzi yake .
and "The case is closed"
 
kumbe ushahidi ulikuwepo? sasa Leo mbona mnasema hakuna? mnayuchanganya nyie vijana wa ufipa
 
Mbona hizi mada za Lowassa zimekuwa nyingi sana leo? Kuna mtu kafufuka nini??
 
Hamna ni kuweka tu kumbukumbu sawa kwamba sio kila anachokisema member humu ni cha kutilia maanani sana
 
Mbona hizi mada za Lowassa zimekuwa nyingi sana leo? Kuna mtu kafufuka nini??
Wanajaribu kupunguza kasi ya anguko linalowaendea kwa kasi ili kuwazuia vipofu kuona uchumi ukididimia na viwanda kuota mbawa!! Watazua sana na kufukia vichwa ardhini huku maumbile yakibaki juu hadharani!!!

Kadri upepo utakavyovyuma ndivyo tutavyoendelea kuona nyeti za kuku - in Lembeli voice
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom